Ten years now, tasnia ya movie imekosa mbadala wa Kanumba nchini

Ten years now, tasnia ya movie imekosa mbadala wa Kanumba nchini

6 Pack

JF-Expert Member
Joined
Apr 17, 2022
Posts
2,819
Reaction score
5,996
Vipi wakuu, kwema huko mitaani.

Ebwana inasikitisha kuona nchi kubwa kama TZ, iliyosheheni watu wenye vipaji mbali mbali vya uigizaji, anakosekana mtu wa kuziba pengo aliloacha hayati Kanumba.

Mwanzo mwanzo Rey alikuja na mikwara ya kujifanya kuwa yeye ndo mwenye uwezo wa kuliziba na kulifunga kabisa pengo hilo, lakini baada ya miaka miwili ya mikwara tukaja kuona jamaa chali, kaangukia kichwa huku miguu ikiwa juu.

Wakaja wengine ambao nimewasahau mpaka majina, lkn na wao wakaangukia pua na kidevu.
Hakika jamaa alikuwa amebarikiwa kipaji cha pekee kabisa. Laiti angekuwa hai leo hii basi Tanzania tungekuwa na mastaa wakubwa sana walioshindikana Afrika mashariki ambao ni Kanumba na Diamond.

Bora kwenye mziki kidogo Diamond anapata chalenge ya kufukuziwa na kina Kiba, Harmoniza nk, lkn kwa Kanumba pamoja na kufariki ila amekosa hata wa kumsogelea karibu yake achilia mbali kuziba pengo lake.

Wakuu toeni ushauri nini kifanyike ili apatikane wa kusimama nafasi ya hayati Kanumba, maana kwa upande wa comedy naona Joti kafanikiwa kuziba pengo la mzee Majuto.
 
Hakuna Tasnia iliokosa mtu, sema utandawazi umebadilisha mambo, hata huko majuu hakuna movie zina kiki kama kipindi cha kina Rambo na Jack chain,
Now kila mtu ni celebrate kila mtu ni actor na comedian, hata angekuepo angepotea vile vile.
 
Hakuna Tasnia iliokosa mtu, sema utandawazi umebadilisha mambo, hata huko majuu hakuna movie zina kiki kama kipindi cha kina Rambo na Jack chain,
Now kila mtu ni celebrate kila mtu ni actor na comedian, hata angekuepo angepotea vile vile.
Sizani kama angepotea kama unavyofikiria. Labda unambie pengine angekuwa ameshaachana na maswala ya kuigiza movie. Kanumba alikuwa ni Diamond wa sasa, ambapo pamoja na utandawazi ila kumshusha sio rahisi.
 
Bongo movie haina jipya zaidi ni kuigiza mapenzi tu,tasnia imejaa vilaza na wadangaji wasio jua lolote zaidi kujiona uzuri wa sura,umbo ndo kigezo Cha kuwa muigiza.

Tasnia imekosa ubunifu kabisa mfano ulio hai ni huu Director Vincent Kigosi,producer Vincent Kigosi, Editor Vincent Kigosi, cameraman Vincent Kigosi only kwenye Bongo movie ujinga huu huwezi kuta kwenye serious company za uzalishaji movie.

Elimu waigiza wengi ni vilaza walio kimbia shule hawana abc kuhusu Elimu ya filamu licha kwamba tuna chuo kinatoa Elimu hii wapo wapo tu,ukitaka kuthibitisha hili angalia wanavyo andika subtitles tu kwenye movies zao shida tupu unaishia kucheka tu.

Bajeti hakuna uwekezaji wa kutosha wa rasilimali pesa kwenye tasnia hivyo kufanya tasnia kukosa uhalisia wa matendo mfano mtu anapandwa na hasira kwenye scene anashindwa kuvunja hata glass ya maji ya uhai[emoji1787][emoji1787], muingizaji anajifanya tajili mkubwa na pesa nyingi alafu anaendesha ist huu si upuuzi nani aangalie huu ujinga

View attachment 2353639
 
Kifo cha bongo movie kilitokana na msambazaji Steps entertainment kujitoa kwenye tasnia, naamini akipatikana msambazaji mzuri na serikali kusimamia ipasavyo pirates watasimama tena
Ok mkuu nafikiri ulichoandika kinaendana na uhalisia.
 
Bongo movie haina jipya zaidi ni kuigiza mapenzi tu,tasnia imejaa vilaza na wadangaji wasio jua lolote zaidi kujiona uzuri wa sura,umbo ndo kigezo Cha kuwa muigiza.

Tasnia imekosa ubunifu kabisa mfano ulio hai ni huu Director Vincent Kigosi,producer Vincent Kigosi, Editor Vincent Kigosi, cameraman Vincent Kigosi only kwenye Bongo movie ujinga huu huwezi kuta kwenye serious company za uzalishaji movie.

Elimu waigiza wengi ni vilaza walio kimbia shule hawana abc kuhusu Elimu ya filamu licha kwamba tuna chuo kinatoa Elimu hii wapo wapo tu,ukitaka kuthibitisha hili angalia wanavyo andika subtitles tu kwenye movies zao shida tupu unaishia kucheka tu.

Bajeti hakuna uwekezaji wa kutosha wa rasilimali pesa kwenye tasnia hivyo kufanya tasnia kukosa uhalisia wa matendo mfano mtu anapandwa na hasira kwenye scene anashindwa kuvunja hata glass ya maji ya uhai[emoji1787][emoji1787], muingizaji anajifanya tajili mkubwa na pesa nyingi alafu anaendesha ist huu si upuuzi nani aangalie huu ujinga

View attachment 2353639
Kweli waigizaji wengi wa bongo wanatia aibu 🤣🤣🤣
 
Bongo Muvi ya sasa inasubiria tu kampeni za uchaguzi ziwadie ili wakatumike kuwapigia ccm debe kwa ujira kiduchu! Baada ya hapo, wanapigika tena kwa miaka 5!

Ubunifu 0! Miaka nenda style yao ya kuigiza ni ile ile.
😂😂😂😂
 
Vipi wakuu, kwema huko mitaani.

Ebwana inasikitisha kuona nchi kubwa kama TZ, iliyosheheni watu wenye vipaji mbali mbali vya uigizaji, anakosekana mtu wa kuziba pengo aliloacha hayati Kanumba.

Mwanzo mwanzo Rey alikuja na mikwara ya kujifanya kuwa yeye ndo mwenye uwezo wa kuliziba na kulifunga kabisa pengo hilo, lakini baada ya miaka miwili ya mikwara tukaja kuona jamaa chali, kaangukia kichwa huku miguu ikiwa juu.

Wakaja wengine ambao nimewasahau mpaka majina, lkn na wao wakaangukia pua na kidevu.
Hakika jamaa alikuwa amebarikiwa kipaji cha pekee kabisa. Laiti angekuwa hai leo hii basi Tanzania tungekuwa na mastaa wakubwa sana walioshindikana Afrika mashariki ambao ni Kanumba na Diamond.

Bora kwenye mziki kidogo Diamond anapata chalenge ya kufukuziwa na kina Kiba, Harmoniza nk, lkn kwa Kanumba pamoja na kufariki ila amekosa hata wa kumsogelea karibu yake achilia mbali kuziba pengo lake.

Wakuu toeni ushauri nini kifanyike ili apatikane wa kusimama nafasi ya hayati Kanumba, maana kwa upande wa comedy naona Joti kafanikiwa kuziba pengo la mzee Majuto.
Tatizo kwa sasahivi wanaochukuliwa kuigiza hawana vipaji muvi hazina mvuto kama zamani tumehamia kwenye miziki.
 
Back
Top Bottom