Sijasema mahali popote kuwa nilitaka anifurahishe mimi, na wala sijasema amfurahishe mtu yeyote, nimesema atueleze na kutufafanualia kifungu hicho cha sheria kinasema nini maana ndio fani yake halafu atuambie ni kwa namna gani jambo alilofanya Kikwete limekivunja ama halijavunja hicho kifungu cha hiyo sheria. Hakuna nililosema zaidi ya hapo, sasa hapa ......ly! uliyosema nitakuwa mimi au ni wewe? Umepewa akili na fikra za kufikiri lakini unakimbilia kuongelea mambo bila kuangalia kwa undani nini maana yake. Ni watu ka ninyi msiotaka kufikiri ndio mnarudisha nyuma maendeleo ya hii nchi tunayoipenda. Ushauri wa bure, soma, tafakari halafu andika. Umasikini wa kufikiri ni mbaya kuliko aina yoyote ya umasikini hata kama umejaa hela za ufisadi. Ni kansa inayomaliza Taifa hili, ni kansa iliyowakamata wengi, ni kansa inayomaliza heshima ya wanasheria maana hawajielewi hata wako wapi. Ni kansa inayomfanya mru atoe majibu mepesi hata kama yanahusu jambo linalohitaji umakini wa hali ya juu. Ni kansa inayomfanya mtu aseme " amelitupilia mbali pingamizi" bila kueleza kwa kigezo na misingi ipi.