Tetesi: Jack Tuyisenge atua nchini kumalizana na Mo Dewji

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
53,868
Reaction score
121,001

Ule mtambo wa mabao wa Gor Mahia pacha wa Meddie Kagere inasemekana ametua Bongo kumalizana na bosi wa Wana-robo fainali-CAF Championship Simba SC.

Tuyisenge ambaye anawaniwa pia na AS Vita ameonyesha nia ya kukipiga Msimbazi kilichobaki na kuweka sawa maslahi ya pange zote mbili.

Naitakia kila la kheri chama langu. Hakika Tuyisenge na Kambole kutoka ZESCO wakinaswa kule mbele kazi itakuwa imeisha
 
Mkude na Kotei hawatoshi mkuu?Kwa beki nakubaliana na wewe, Wawa na Juko watafute timu zingine
Juuko aende ila wawa simba wajifikirie mara 2 mbili, ukimtoa nyoni wawa ni beki bora zaidi ssc.. Ni mpambanaji, kiongozi, muhamasishaji, muanzilishi mzuri wa mashambulizi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo la timu za bongo zikianza kuishambulia timu moja kuchukua wachezaji wake ni hapo hapo. Wakati yanga ilipokuwa kwenye peak akili zao zilikuwa zimbabwe hasa platnum tuu , huu ugojwa simba wameambukizwa. Kama ana hela pale AS VITa kuna mitambo ambayo sii ya dunia hii ina speed na vipawa
 
mnabeba vizee kila siku mwisho itakuwa timu ya maveterani
Hata kagere,Boko na Okwi mlisema ni wazee lkn angalia shughuli yao kwa mpira wa bongo ukisema u deal na umri ni kudanganyana wachezaji wengi wana umri mdogo kwenye makaratasi ila sio kweli na hii ni karibu nchi nyingi za Ki Africa swala la umri hawazingatii tofauti na wenzetu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kamwene gongo wazi
 
Simba hii ni azam tupu,haya kuna manula,nyoni,kapombe,bocco,mmh!!

Sent from my TECNO CA6 using JamiiForums mobile app
 
Rekodi zake zipo vip huko kenys? Isijekuwa msimu mzima hajafikisha hta goli kumi halafu mnampapatia

Sent using Jamii Forums mobile app
Kiufupi ndio kinara aliyeipeleka Gor Mahia robo fainali kama ilivyo kwa Kagere hapo Simba,CAFCC yeye ni miongoni mwa wafungaji bora na ameingia kwenye CAFCC Best XI kama forward.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…