Tetesi "Taarifa Zinazopotosha Kuhusu Ununuzi wa Magari ya CCM"

Tetesi "Taarifa Zinazopotosha Kuhusu Ununuzi wa Magari ya CCM"

PendoLyimo

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2014
Posts
969
Reaction score
1,055
Katika siku za hivi karibuni, kumezuka taarifa za kupotosha kuhusu ununuzi wa magari na Chama Cha Mapinduzi (CCM), zikidai kuwa CCM imenunua magari kwa bei ya juu sana. Taarifa hizo zimeambatanishwa na picha ambazo zimebadilishwa na kuwekewa maandishi ya uongo kwa lengo la kuichafua CCM.

Picha zinazozagaa kwenye mitandao zimechukuliwa kutoka kwenye tovuti ya TopGear Nederland, na kwa makusudi zimeongezwa maandiko ya kupotosha ili kutoa taswira ya uwongo kwa wananchi. Ukweli ni kwamba, hakuna ushahidi wowote wa kiushahidi unaothibitisha madai hayo, na ni wazi kuwa picha hiyo ya kwanza ni sehemu ya propaganda za kuichafua CCM.

Kwa ukweli na uadilifu, tunatoa wito kwa wananchi kuchukua tahadhari dhidi ya habari za uongo zinazozagaa mitandaoni na kuzitafakari kabla ya kuzisambaza. CCM inaheshimu misingi ya uwazi na uwajibikaji, na hatutaruhusu upotoshaji wa aina hii kuathiri imani ya wananchi kwa chama.
 

Attachments

  • WhatsApp Image 2024-10-17 at 4.18.37 AM (1).jpeg
    WhatsApp Image 2024-10-17 at 4.18.37 AM (1).jpeg
    68.6 KB · Views: 7
  • WhatsApp Image 2024-10-17 at 4.18.37 AM.jpeg
    WhatsApp Image 2024-10-17 at 4.18.37 AM.jpeg
    71 KB · Views: 8
Katika siku za hivi karibuni, kumezuka taarifa za kupotosha kuhusu ununuzi wa magari na Chama Cha Mapinduzi (CCM), zikidai kuwa CCM imenunua magari kwa bei ya juu sana. Taarifa hizo zimeambatanishwa na picha ambazo zimebadilishwa na kuwekewa maandishi ya uongo kwa lengo la kuichafua CCM.

Picha zinazozagaa kwenye mitandao zimechukuliwa kutoka kwenye tovuti ya TopGear Nederland, na kwa makusudi zimeongezwa maandiko ya kupotosha ili kutoa taswira ya uwongo kwa wananchi. Ukweli ni kwamba, hakuna ushahidi wowote wa kiushahidi unaothibitisha madai hayo, na ni wazi kuwa picha hiyo ya kwanza ni sehemu ya propaganda za kuichafua CCM.

Kwa ukweli na uadilifu, tunatoa wito kwa wananchi kuchukua tahadhari dhidi ya habari za uongo zinazozagaa mitandaoni na kuzitafakari kabla ya kuzisambaza. CCM inaheshimu misingi ya uwazi na uwajibikaji, na hatutaruhusu upotoshaji wa aina hii kuathiri imani ya wananchi kwa chama.
SIo tu tahadhari toa ushahidi wadhati kuthibitisha kama taarifa haina ukweli,ninavyo fahamu sisi ni watanzania na sisi ni waafrika na zaidi wana siii hasa,hivyo yafaa tutoke nje kuthibitisha kweli kumekucha,licha ya kuambiwa na mwana ccm mwana sii hasa.
 
SIo tu tahadhari toa ushahidi wadhati kuthibitisha kama taarifa haina ukweli,ninavyo fahamu sisi ni watanzania na sisi ni waafrika na zaidi wana siii hasa,hivyo yafaa tutoke nje kuthibitisha kweli kumekucha,licha ya kuambiwa na mwana ccm mwana sii hasa.

..ruzuku ya Ccm ni BILIONI ngapi kwa mwezi?
 
..ruzuku ya Ccm ni BILIONI ngapi kwa mwezi?
Hata kama ingekuwa trillion ngapi sehemu kubwa ni ya wizi.Kwanini ya wizi?Wangeruhusu chaguzi huru bila hujuma kwa vyama pinzani halafu wangeangalia ruzuku yao kwa mujibu wa sheria na kanuni ingekuwa kiasi gani?
 
Jinga kabisa hawa. Yaani sisi kule kajujumere hatuna hata madawati na vituo vya afya, halafu wenyewe wananunua mav8 tu

..tayari wana ma-V8 yaliyonunuliwa enzi za Komred Bashiru na Polepole.
 
Hata kama ingekuwa trillion ngapi sehemu kubwa ni ya wizi.Kwanini ya wizi?Wangeruhusu chaguzi huru bila hujuma kwa vyama pinzani halafu wangeangalia ruzuku yao kwa mujibu wa sheria na kanuni ingekuwa kiasi gani?
duu! kweli watabiri wapo, umejuaje kama uchaguzi utakuwa sio wa huru ??
 
Back
Top Bottom