Thamani za hivi vilabu hazitofautiani sana, wapenzi wake huongezeka au kupungua kulinga na matokeo uwanjani kwa kipindi husika. Kiuhalisia wapenzi wa hivi vilabu ni nusu kwa nusu hivyo basi Simba hawatakiwi kupewa dau kubwa kuliko Yanga. Bahati mbaya inasemekana Yanga ameingizwa cha kike , dau la Simba ni kubwa zaidi na wamefanya kutangaza la Yanga mapema ili kuwaziba mdomo wanajangwani pale dau la Simba litakapotangazwa.
Azam Azam Azam.... Nimewaita mara tatu, mkiwapa dau kubwa Simba sisi wanaYanga tutahamia DSTV. Nasikia DSTV wanataka kupindua meza maana soko lao Tanzania linazidi kudhoofika.
Nawakumbusha tu, kiboko yenu Manji anarudi. Najua mnakumbuka vyema alivyowagomea zile milioni mia zenu. Mkileta unazi tunawakimbia.
Azam Azam Azam.... Nimewaita mara tatu, mkiwapa dau kubwa Simba sisi wanaYanga tutahamia DSTV. Nasikia DSTV wanataka kupindua meza maana soko lao Tanzania linazidi kudhoofika.
Nawakumbusha tu, kiboko yenu Manji anarudi. Najua mnakumbuka vyema alivyowagomea zile milioni mia zenu. Mkileta unazi tunawakimbia.