Ileje
JF-Expert Member
- Dec 20, 2011
- 9,524
- 13,682
Moja ya makosa makubwa aliyofanya January Makamba ni kutaka kuwania kuwa Mwenyekiti wa African Union huku akifahamu fika kuwa nafasi hiyo inawaniwa na Raila Odinga ambaye anaungwa mkono na Rais Ruto wa Kenya.
Itakumbukwa kuwa Rais Ruto alimshawishi Odinga kuwania nafasi hiyo ili kuimarisha utawala wake ambao unatishiwa na uwepo wa Odinga kama kiongozi wa upinzani. Aidha uwepo wa Odinga ni tishio kwa Rais Ruto katika uchaguzi Mkuu ujao wa 2027 hivyo kumlazimisha Ruto kumpigia Odinga kampeni katika nchi zote za Afrika ya Mashariki kumuunga mkono. Tanzania tayari iliwisha kubali kumuunga mkono Odinga katika adhma yake ya kuwa Mwenyekiti wa AU kwa hiyo kitendo cha Makamba kutaka kuwania nafasi hiyo kinaonyesha ni utovu wa nidhamu kwa Rais Samia.
Kosa la pili la Makamba ni kuwaunga mkono Gen Z katika harakati zao za kumng'oa Rais Ruto madarakani. Makamba alionyesha kuwaunga mkono Gen alipokwenda Jijini Nairobi kuweka jiwe la msingi katika jengo la kitega uchumi la Tanzania na kushangiliwa kwa vifijo na vijana waliokuwa wanaandamana.
Makamba mara nyingi amekuwa haridhiki na nafasi anazopewa na viongozi wake wakiwemo Magufuli na sasa Samia na kutaka kuwania urais wa nchi mwenyewe.
PIA SOMA
- Kuelekea 2025 - Uteuzi na Utenguzi: Nape, January na Byabato out! Jerry Silaa ahamishiwa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari
Itakumbukwa kuwa Rais Ruto alimshawishi Odinga kuwania nafasi hiyo ili kuimarisha utawala wake ambao unatishiwa na uwepo wa Odinga kama kiongozi wa upinzani. Aidha uwepo wa Odinga ni tishio kwa Rais Ruto katika uchaguzi Mkuu ujao wa 2027 hivyo kumlazimisha Ruto kumpigia Odinga kampeni katika nchi zote za Afrika ya Mashariki kumuunga mkono. Tanzania tayari iliwisha kubali kumuunga mkono Odinga katika adhma yake ya kuwa Mwenyekiti wa AU kwa hiyo kitendo cha Makamba kutaka kuwania nafasi hiyo kinaonyesha ni utovu wa nidhamu kwa Rais Samia.
Kosa la pili la Makamba ni kuwaunga mkono Gen Z katika harakati zao za kumng'oa Rais Ruto madarakani. Makamba alionyesha kuwaunga mkono Gen alipokwenda Jijini Nairobi kuweka jiwe la msingi katika jengo la kitega uchumi la Tanzania na kushangiliwa kwa vifijo na vijana waliokuwa wanaandamana.
Makamba mara nyingi amekuwa haridhiki na nafasi anazopewa na viongozi wake wakiwemo Magufuli na sasa Samia na kutaka kuwania urais wa nchi mwenyewe.
PIA SOMA
- Kuelekea 2025 - Uteuzi na Utenguzi: Nape, January na Byabato out! Jerry Silaa ahamishiwa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari