Tetesi za Makamba kuwania uenyekiti wa AU na kuwaunga mkono Gen Z kimemponza kutimuliwa uwaziri?

Tetesi za Makamba kuwania uenyekiti wa AU na kuwaunga mkono Gen Z kimemponza kutimuliwa uwaziri?

Ileje

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2011
Posts
9,524
Reaction score
13,682
Moja ya makosa makubwa aliyofanya January Makamba ni kutaka kuwania kuwa Mwenyekiti wa African Union huku akifahamu fika kuwa nafasi hiyo inawaniwa na Raila Odinga ambaye anaungwa mkono na Rais Ruto wa Kenya.

Itakumbukwa kuwa Rais Ruto alimshawishi Odinga kuwania nafasi hiyo ili kuimarisha utawala wake ambao unatishiwa na uwepo wa Odinga kama kiongozi wa upinzani. Aidha uwepo wa Odinga ni tishio kwa Rais Ruto katika uchaguzi Mkuu ujao wa 2027 hivyo kumlazimisha Ruto kumpigia Odinga kampeni katika nchi zote za Afrika ya Mashariki kumuunga mkono. Tanzania tayari iliwisha kubali kumuunga mkono Odinga katika adhma yake ya kuwa Mwenyekiti wa AU kwa hiyo kitendo cha Makamba kutaka kuwania nafasi hiyo kinaonyesha ni utovu wa nidhamu kwa Rais Samia.

Kosa la pili la Makamba ni kuwaunga mkono Gen Z katika harakati zao za kumng'oa Rais Ruto madarakani. Makamba alionyesha kuwaunga mkono Gen alipokwenda Jijini Nairobi kuweka jiwe la msingi katika jengo la kitega uchumi la Tanzania na kushangiliwa kwa vifijo na vijana waliokuwa wanaandamana.

Makamba mara nyingi amekuwa haridhiki na nafasi anazopewa na viongozi wake wakiwemo Magufuli na sasa Samia na kutaka kuwania urais wa nchi mwenyewe.

PIA SOMA
- Kuelekea 2025 - Uteuzi na Utenguzi: Nape, January na Byabato out! Jerry Silaa ahamishiwa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari
 
Duuh kwa hiyo ana akili za panzi hawezi kumsoma hata boss wake!

Kweli mtaka yote kwa pupa hukosa yote!
 
Tanzania Begins Work on 22-Storey Twin Towers in Nairobi
The office complex in Upper Hill will be known as Tanzania Towers.

Updated on
July 1, 2024
By
Hellen Ndaiga

1721671298509.png

An impression of Tanzania Towers in Upper Hill, Nairobi. PHOTO | COURTESY
Tanzania has launched the long-delayed construction of its office complex in Nairobi, aiming to reduce rental costs for its chancery and embassy staff housing.

The project, announced in 2014, is being implemented by the National Social Security Fund (NSSF) as part of Tanzania’s plan to involve its pension funds in implementing projects for the country’s foreign embassies.

Apart from hosting the Tanzanian embassy, a portion of the 22-storey twin towers complex—at the junction of Mara and Hill roads in Upper Hill—will be reserved for business offices.

Dubbed Tanzania Towers, the office complex, initially proposed as a 26-storey building named Umoja House will help Kenya’s neighbour earn foreign exchange.

“The Tanzania Towers will save the government rental expenses for the chancery and embassy staff housing,” Tanzania’s foreign affairs minister January Makamba said during the groundbreaking event on Tuesday, June 18
 
Hakuna kitu hapo, ni hisia zako tu.
Kama waliweza kuteuliwa maana yake wangeweza kutumbuliwa pia. Ni siasa za CCM tu.
 
Moja ya makosa makubwa aliyofanya January Makamba ni kutaka kuwania kuwa Mwenyekiti wa African Union huku akifahamu fika kuwa nafasi hiyo inawaniwa na Raila Odinga ambaye anaungwa mkono na Rais Ruto wa Kenya...
Acheni ujuaji, we unayajua makosa ya Makamba kuliko Mama? Haya tutajie makosa ya Naibu wake. Vijana punguzeni ujuaji. Makamba makosa yake ni mazito.
 
Back
Top Bottom