Teuzi za wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi zilizofanywa na Mo Dewji na Mangungu zinadhihirisha tatizo la Simba liko wapi

Teuzi za wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi zilizofanywa na Mo Dewji na Mangungu zinadhihirisha tatizo la Simba liko wapi

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Baadhi yetu tumepiga sana kelele kuonyesha kuwa tatizo kubwa la Simba ni ukosefu wa mfumo thabiti wa uongozi unaowezesha timu kuendeshwa kwa ukaribu na umakini. Simba haina management imara, bali management ipo kama jina tu ila haina watu na waliopo hawana meno ya kutenda majukumu yao. Chukulia mfano cheo kikubwa kama cha CEO, ukiangalia mamlaka aliyonayo unaona hayaendani na cheo hicho.

Jana nimesoma Mwenyekiti wa Klabu Mangungu kamteua Kailima aliyewahi kuwa Tume ya Uchaguzi kuwa Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi. Ukiachana na ukakasi kutokana na historia za utendaji wake kisiasa, Wanasimba wengi hawajawahi kumsikia huyu mtu akijishughulisha na mambo ya mpira, leo hii anapewa ujumbe wa Bodi ambayo kimsingi ndiyo inayoendesha timu.

Wajumbe wengi walioteuliwa na pande zote mbili hata wale waliojiuzulu wana majukumu mengi ya Kiserikali. Hata kama wanaweza kuwa na mapenzi na Simba, nina uhakika ni kazi sana kuwakutanisha hawa watu kutokana na muingiliano wa ratiba zao. Muda wanapata wapi hawa kushughulikia mambo ya mipira? Simba haitakiwi kuwa "pet project" ya Mo, Mangungu wala Wajumbe wa Bodi, inatakiwa kuwa kipaumbele chao wanapoamka hadi wanapolala.

Simba inatakiwa kupanua na kuimarisha Timu yake ya Management, iwe na idara za kutosha na Wakurugenzi wa Idara hizo ndiyo waunde Bodi ya Wakurugenzi. Hawa Wakurugenzi wawe waajiriwa rasmi wa Simba na wapatikane kwa kupitia mchakato rasmi wa ajira na wafanye kazi full time katika idara zao.

Hawa wanasiasa wanaoteuliwa wapelekwe huko kwenye Friends of Simba au ile Executive Network au Baraza la Ushauri. Timu imekuwa na muundo wa ajabu ajabu ndiyo maana kila mtu amekuwa kambale.
 
Unazifahamu kazi za Board of Directors.

Ungesema CEO hafai kuwa Kailima sawa. Lakini bodi inahitaji wajumbe wenye taaluma mbalimbali katika nyanja mbalimbali. Ndio maana ndani ya bodi utakuta kuna kamati. Mfano kamati ya usajili itahusisha moja kwa moja wajumbe wenye ueledi na wacheza mpira.
 
Umeandika vizur....kumbe Simba shida yao wanachanganya viongozi wa siasa na mpira.....
.....kumbe huenda mangungu ni mwanasiasa alafu pale Simba anatuektia
Ni mwanasiasa halafu kibaya zaidi hata siasa yenyewe imemshinda. Ndiyo hao kina Kingwangala wanataka wakimbilie Simba baada ya siasa kuwashinda.
 
Unazifahamu kazi za Board of Directors.

Ungesema CEO hafai kuwa Kailima sawa. Lakini bodi inahitaji wajumbe wenye taaluma mbalimbali katika nyanja mbalimbali. Ndio maana ndani ya bodi utakuta kuna kamati. Mfano kamati ya usajili itahusisha moja kwa moja wajumbe wenye ueledi na wacheza mpira.
Nitajie hao wajumbe wa kamati ya usajili. Bosi wa ATCL anafanya nini kwenye bodi ya Simba na unadhani mtu kama huyo ana muda wa kufuatilia habari za kila siku za timu? Ndiyo maana taasisi za serikali zina ufanisi mdogo maana watu wamerundikiwa mavyeo wakati kuna watu kibao hawana kazi.

Elewa ninachokisema. Bodi ingekuwa inafanya kazi kama Bodi zingine za Wakurugenzi ambazo huwa zina kazi ya kuisimamia Management na kuhakiki utendaji wake isingekuwa na shida maana Bodi nyingi wanaweza kukutana hata mara 3 au 4 tu kwa mwaka ila Bodi ya Simba ndiyo inayoendesha shughuli za kila siku za Simba.
 
Nitajie hao wajumbe wa kamati ya usajili. Bosi wa ATCL anafanya nini kwenye bodi ya Simba na unadhani mtu kama huyo ana muda wa kufuatilia habari za kila siku za timu? Ndiyo maana taasisi za serikali zina ufanisi mdogo maana watu wamerundikiwa mavyeo wakati kuna watu kibao hawana kazi.

Elewa ninachokisema. Bodi ingekuwa inafanya kazi kama Bodi zingine za Wakurugenzi ambazo huwa zina kazi ya kuisimamia Management na kuhakiki utendaji wake isingekuwa na shida maana Bodi nyingi wanaweza kukutana hata mara 3 au 4 tu kwa mwaka ila Bodi ya Simba ndiyo inayoendesha shughuli za kila siku za Simba.
Kwani board ya Simba kazi yake ni kusajili? Sio kweli kuna kamati, kazi ya board ni kusimamia mejementi. Hata Simba kamati ipo.
 
Kwani board ya Simba kazi yake ni kusajili? Sio kweli kuna kamati, kazi ya board ni kusimamia mejementi. Hata Simba kamati ipo.
Muulize huyo aliyesema mambo ya usajili, sijayasema mimi. Nimewahi kumsikia Mangungu, Salim Abdallah na wengine wakisema Bodi ya Simba ndiyo inayoendesha timu, haya siyo maneno yangu.

Ukifikiria vizuri utagundua kwenye muundo sahihi wa uongozi hata kamati ya usajili isingehitajika maana kama una management inayojitosheleza kila idara, una ripoti ya benchi la ufundi na una usimamizi wa Bodi, kwa nini tena uunde kamati ya usajili? Hii ni miundo ya kisiasa iliyopitwa na wakati matokeo yake hatujui nani wa kumbebesha zigo la lawama pale usajili mbovu unapofanyika.
 
Muulize huyo aliyesema mambo ya usajili, sijayasema mimi. Nimewahi kumsikia Mangungu, Salim Abdallah na wengine wakisema Bodi ya Simba ndiyo inayoendesha timu, haya siyo maneno yangu.

Ukifikiria vizuri utagundua kwenye muundo sahihi wa uongozi hata kamati ya usajili isingehitajika maana kama una management inayojitosheleza kila idara, una ripoti ya benchi la ufundi na una usimamizi wa Bodi, kwa nini tena uunde kamati ya usajili? Hii ni miundo ya kisiasa iliyopitwa na wakati.
Simba walituaminishwa club inaenda kuendesha kisasa baada ya mfumo kubadilika, mpaka Sasa haina mkurugenzi wa ufundi badala yake usajili unaofanywa na kamati.
 
Baadhi yetu tumepiga sana kelele kuonyesha kuwa tatizo kubwa la Simba ni ukosefu wa mfumo thabiti wa uongozi unaowezesha timu kuendeshwa kwa ukaribu na umakini. Simba haina management imara, bali management ipo kama jina tu ila haina watu na waliopo hawana meno ya kutenda majukumu yao. Chukulia mfano cheo kikubwa kama cha CEO, ukiangalia mamlaka aliyonayo unaona hayaendani na cheo hicho.

Jana nimesoma Mwenyekiti wa Klabu Mangungu kamteua Kailima aliyewahi kuwa Tume ya Uchaguzi kuwa Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi. Ukiachana na ukakasi kutokana na historia za utendaji wake kisiasa, Wanasimba wengi hawajawahi kumsikia huyu mtu akijishughulisha na mambo ya mpira, leo hii anapewa ujumbe wa Bodi ambayo kimsingi ndiyo inayoendesha timu.

Wajumbe wengi walioteuliwa na pande zote mbili hata wale waliojiuzulu wana majukumu mengi ya Kiserikali. Hata kama wanaweza kuwa na mapenzi na Simba, nina uhakika ni kazi sana kuwakutanisha hawa watu kutokana na muingiliano wa ratiba zao. Muda wanapata wapi hawa kushughulikia mambo ya mipira? Simba haitakiwi kuwa "pet project" ya Mo, Mangungu wala Wajumbe wa Bodi, inatakiwa kuwa kipaumbele chao wanapoamka hadi wanapolala.

Simba inatakiwa kupanua na kuimarisha Timu yake ya Management, iwe na idara za kutosha na Wakurugenzi wa Idara hizo ndiyo waunde Bodi ya Wakurugenzi. Hawa Wakurugenzi wawe waajiriwa rasmi wa Simba na wapatikane kwa kupitia mchakato rasmi wa ajira na wafanye kazi full time katika idara zao.

Hawa wanasiasa wanaoteuliwa wapelekwe huko kwenye Friends of Simba au ile Executive Network au Baraza la Ushauri. Timu imekuwa na muundo wa ajabu ajabu ndiyo maana kila mtu amekuwa kambale.
Kailima Bado ni Mkurugenzi wa tume huru ya uchaguzi
 
Unazifahamu kazi za Board of Directors.

Ungesema CEO hafai kuwa Kailima sawa. Lakini bodi inahitaji wajumbe wenye taaluma mbalimbali katika nyanja mbalimbali. Ndio maana ndani ya bodi utakuta kuna kamati. Mfano kamati ya usajili itahusisha moja kwa moja wajumbe wenye ueledi na wacheza mpira.
Usisahau wawe na vyombo pia ili wasiwe wapiga mizinga Klabuni.
 
Baadhi yetu tumepiga sana kelele kuonyesha kuwa tatizo kubwa la Simba ni ukosefu wa mfumo thabiti wa uongozi unaowezesha timu kuendeshwa kwa ukaribu na umakini. Simba haina management imara, bali management ipo kama jina tu ila haina watu na waliopo hawana meno ya kutenda majukumu yao. Chukulia mfano cheo kikubwa kama cha CEO, ukiangalia mamlaka aliyonayo unaona hayaendani na cheo hicho.

Jana nimesoma Mwenyekiti wa Klabu Mangungu kamteua Kailima aliyewahi kuwa Tume ya Uchaguzi kuwa Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi. Ukiachana na ukakasi kutokana na historia za utendaji wake kisiasa, Wanasimba wengi hawajawahi kumsikia huyu mtu akijishughulisha na mambo ya mpira, leo hii anapewa ujumbe wa Bodi ambayo kimsingi ndiyo inayoendesha timu.

Wajumbe wengi walioteuliwa na pande zote mbili hata wale waliojiuzulu wana majukumu mengi ya Kiserikali. Hata kama wanaweza kuwa na mapenzi na Simba, nina uhakika ni kazi sana kuwakutanisha hawa watu kutokana na muingiliano wa ratiba zao. Muda wanapata wapi hawa kushughulikia mambo ya mipira? Simba haitakiwi kuwa "pet project" ya Mo, Mangungu wala Wajumbe wa Bodi, inatakiwa kuwa kipaumbele chao wanapoamka hadi wanapolala.

Simba inatakiwa kupanua na kuimarisha Timu yake ya Management, iwe na idara za kutosha na Wakurugenzi wa Idara hizo ndiyo waunde Bodi ya Wakurugenzi. Hawa Wakurugenzi wawe waajiriwa rasmi wa Simba na wapatikane kwa kupitia mchakato rasmi wa ajira na wafanye kazi full time katika idara zao.

Hawa wanasiasa wanaoteuliwa wapelekwe huko kwenye Friends of Simba au ile Executive Network au Baraza la Ushauri. Timu imekuwa na muundo wa ajabu ajabu ndiyo maana kila mtu amekuwa kambale.
Hiyo inaitwa organization chart, (muundo wa uongozi)
 
Back
Top Bottom