TFF, Bodi ya ligi sasa Muda umefika wakutizama makosa ya uwanjani kwa Runinga!

KakaKiiza

JF-Expert Member
Joined
Feb 16, 2010
Posts
11,794
Reaction score
9,075
Niwaombe TFF BODI YA LIGI,WADHANI, sasa wakati umefika wakutoka gizani nakuendesha ligi kitaalamu tumeona mambo mengi ya hovyo yakifanyika uwanjani kwasababu ambazo naweza kuziita za kizembe au za hira waamzi wamekuwa ni chanzo cha matatizo haya ya kupoka haki za timu.

Leo mchezo wa Kati Yanga na Biashara ule ni uhuni wa waamzi, ila zikiwepo luninga zakutizama marudio hii itasaidia kumaliza migogoro isiyo ya lazima.

TFF futilia hili tuboreshe ligi yetu.

Asanteni
 
Mkuu mm sio uto ila ile ilikua penat halali kabsaaaa jifunze kukubali matokeo kama legend CR7 akifungwa uwa anasema ((NO EXCUSE makosa ni yetu wachezaji) hakuna wakumlaumu)

Sent from my Infinix X612 using JamiiForums mobile app
 
Mara nyingi hakuna timu inayobebwa nachokiona hizi timu ndogo kwenye ligi wachezaji sikuzote wanakuwa na presha kubw wanavyokuwa wanacheza na yanga na simba wanakamia Sana gem matokeo yake ndio hayo
ushindi unakuwa unapatikana kwa magoli ya penati
 
Nadhani umeficha kitu lengo la hii thread ni nini? Mimi bado sijaelewa umekusudia nini maana hujawa transparent kuwa wazi basi, maana Jana kuna matukio mawili makubwa moja la penalty lingine ni tukio la kukataliwa goli la 3 la Yanga hebu funguka
 
Yaan mashabiki wa mikia kwa kulalamika umesahau na sisi ile game na prison Ntabanzokiza alivyochezewa faulo ndani ya 18 lkn hatukupiga kelele sana kwahyo ile penat yetu ya cku ile tumepewa leo we tulia tu point tushachukua kwahyo hata uongee vp haibadilishi kitu
 
MAKOLO hawataki yanga ashinde ........kila mech yanga akishnda basi wanaibua vikwazo


Tulien dawa iwaingie
 
Unapata presha bure kushabikia mpira wa bongo...kama hauna moyo wa chuma usitazame kabisa soka la bongo, sikiliza tu redioni
 
makolo mlitaka yule mkurya amuue kabisaa moloko ndiyo mkubali kuwa ile ni penati halali, yaaani kijana wa watu kasukumwa na kupigwa darugaa zito lakini makolo bado mnasema ile siyo penati??????
 
Mimi siwezi zungumza chochote maana ata marudio ya azam yamelikata tukio la penalty. sina wakika alisukumwa au hakusukumwa
 
Nadhani umeficha kitu lengo la hii thread ni nini? Mimi bado sijaelewa umekusudia nini maana hujawa transparent kuwa wazi basi, maana Jana kuna matukio mawili makubwa moja la penalty lingine ni tukio la kukataliwa goli la 3 la Yanga hebu funguka
Kwani hiyo inaondoa alichokiomba huyu mdau? Kama goli ni halali kwa nini alikatae? Kama penalty si halali kwa nini aliikubali ? Yaani huenda at the same time ameipa timu pinzani matokeo na ameinyima haki yake ya ushindi mnono zaidi
Maana si sahihi kwa timu kufunga magoli halali yakataliwe hii si kwa Yanga wala simba timu zote zinatakiwa kushinda,kushindwa au kupata sare kihalali si kwa kuonewa au kwa makosa ya waamuzi wasio na weledi au waliokosa sapoti ya kutosha kutekeleza majukumu yao vema eg technology

Maana hili jambo likilelewa tu na kuonekana liko sawa tu kisa timu unayoishabikia imepata matokeo chanya ipo siku watu watakuja kuuana au kuimizana viwanjani.
 
Tatizo watu wanaangalia gemu wakiwa na mahaba au chuki na timu fulani.

Ile ni clear penalty

Na lile goli la Makambo siyo halali coz mfungaji alipoka mpira kwa golikipa
 
Makolo walitaka kuibebesha Biashara gunia la misumari ambalo wao walishindwa kulibeba.

Mlishindwa kuifunga Yanga mnataka Biashara awatimizie hilo jukumu?
 
Kila mmoja ashinde mechi zake kwa mbinu zozote. Hakuna makasiriko hapa. Vita ni vita muraaaa
 
Unazungumzia tff na bodi ipi ya ligi, mpaka leo mwamuzi wa namungo na yanga mpaka leo bado hajaadhibiwa wakati alifanya makosa ya wazi. Hawashituki hawaitwi kwenye mashindano makubwa kwa sababu wamezoea vibahasha.
 
Naomba kuuliza. Kufunga VAR kwenye mechi moja ni TSH ngapi?

Tukisema tutumia marudio ya Azam TV, nayo ni ubabaishaji tu. Kuna muda Azam TV hawana uwezo wa kurudia tukio katika angle zote. Wanarudia kwa upande mmoja tu. Sijui wanatumia camera moja uwanjani.

Wazungu waliona wafunge VAR, ili kupunguza kelele kwa sababu watu wamewekeza hela zao kwenye mpira.

Mwanzoni mashabiki wakawa wanasema VAR itamaliza ladha ya mpira, lakini ladha haijaisha, zaidi VAR imekuwa mkombozi wa maamuzi huko England.

Sasa, huku bongo TFF wataanza kutumia VAR lini? Mbona kama TFF kwa sasa wanapata hela nyingi? au ndio kusema viongozi wa Tanzania hawana muda wa kujali mambo yenye faida kwa umma, bali wao wanajali matumbo yao?

Bila VAR kelele hazitaisha katika ligi ya bongo, kwa sababu mpira umekuwa wa kasi na ushindani mkubwa, hivyo marefa wanashindwa kukimbizana na purukushani za uwanjani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…