TFF hongereni kwa Kumfungia Shaffih Dauda aliyewaambieni Ukweli na Kumuacha Haji Manara aliyehatarisha Usalama wa Taifa na Kuuchafua Mpira

TFF hongereni kwa Kumfungia Shaffih Dauda aliyewaambieni Ukweli na Kumuacha Haji Manara aliyehatarisha Usalama wa Taifa na Kuuchafua Mpira

MINOCYCLINE

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2015
Posts
8,018
Reaction score
16,802
Endeleeni tu Kumchekea huyo Msemaji wa Yanga SC Haji Manara na Upuuzi wake, ila ipo Siku mtatukumbuka tunaowaonya 24/7 kwa Madhara makubwa ambayo yatatokana nae huku mkimuogopa au mkiogopa kwakuwa kuna baadhi yenu mlifaidika mno Kibinafsi na Pesa za GSM.
 
Endeleeni tu Kumchekea huyo Msemaji wa Yanga SC Haji Manara na Upuuzi wake, ila ipo Siku mtatukumbuka tunaowaonya 24/7 kwa Madhara makubwa ambayo yatatokana nae huku mkimuogopa au mkiogopa kwakuwa kuna baadhi yenu mlifaidika mno Kibinafsi na Pesa za GSM.
Haji Manara kafanyaje kwani?
 
Haji Manara kafanyaje kwani?
Anazionya timu zikicheza na timu fulani ziwe makini maana hiyo timu huwa inapuliza sumu vyumbani, hiyo kazi ya kupuliza sumu itakuwa alikuwa akiifanya yeye kipindi cha nyuma
 
Wenye Akili Kubwa mnatushangaza sana yaani Matukio mengine mnayatolea Matamko upesi sana ila sijui kwanini hili la GSM Kujitoa katika Udhamini Mwenza wa Ligi Kuu ya NBC nanyi kama TFF mnachelewa kulitole Tamko wakati Wao ( GSM ) walishatoa lao na tumewaelewa kwa Kiasi chao.

au mnaogopa Kuwajibu ( kutoa Tamko ) Kuwajibu kwakuwa mnajua baadhi yenu mtaumbuka kwani pamoja na kwamba mpaka Udhamini wao Ulisainiwa hadi hivi juzi walipojitoa Vilabu havikupata Fedha zao ila nyie Waandamizi Watano ( nawahifadhi ) wa TFF mmekuwa mkipokea mno Pesa zao Kinyume na Utaratibu?

Tuliwaonya mapema kuhusu GSM ila mkatuona hatunazo ( Mazuzu ) na baada ya kujua Udhaifu wenu wa Tamaa na Upigaji hapo TFF jamaa ( GSM ) wakatumia Akili Kubwa Kuwarubuni ili muwakubali kisha mkiwa nao wawafanyie Umafia huo, wawasome, wajue Siri zenu na wakijotoa waanze kuanika Hadharani Madudu kusudi Mkakati wao wa Kuwachafua kwa Jamii ( Public ) ukamilike na umeshakamilika.

Na nasikia Watu wa GSM wanasubiri kwa hamu zote reaction ( response ) yenu kuhusiana na kule ( huko ) kujitoa Kwao kama Mdhamini Mwenza wa NBC Premier League ili kama nanyi mkiwajibu kwa Kuwasema, Kuwalaumu na Kuwashutumu basi na Wao warejee na Bomu lenu la mwisho ambalo naambiwa litawaacheni Uchi TFF nzima na Wadau ( Wananchi ) hawatowaelewa na huenda hata ukaathiri Udhamini huu Mkuu wa NBC.

TFF mmeshikwa patamu sana na GSM.
 
Haji Manara kafanyaje kwani?
Aliandika kwenye ukurasa wake maneno hayo hapo chini.
JamiiForums1852755857.jpg
 
Mightier nakubali sana nyuzi zako inaonesha jinsi gani ulivyo critical thinker, mchambuzi ,mfatiliaji na mpenzi wa soka...na si soka tu hata katika masuala mengine muhimu ya nchi.

Ni wapuuzi tu ndio wanakuchukia ila wasomi na wenye akili wanakuelewa. Nikiingia JF kitu cha kwanza ni kutafuta nyuzi zako mpya nijue nini kinaendelea nchini Tanzania. Ni aina ya mtu ambae kitu kikiwa cheusi unasema tu ni cheusi na kikiwa cheupe unasema cheupe huna unafiki wa kujipendekeza pendekeza. Hongera sana mkuu.

Ningependa JF wangekuwa na category ya hall of fame...kutambua baadhi ya member wao waliotoa michango na maoni makubwa kwa maendeleo ya nchi katika sekta mbalimbali.
 
rungu hili alilo kutana nalo Dauda linge mtandika na yule mzee wa 'chupli chupli' lingekuwa na manufaa sana kwa taifa hili change ki soka..
 
Back
Top Bottom