TFF Imeingia kwenye mtego wa Simba na Yanga

TFF Imeingia kwenye mtego wa Simba na Yanga

french

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2017
Posts
3,572
Reaction score
3,726
Nasema mpaka sasa TFF ishajiingiza kwenye mtego wa Simba na Yanga na kujinasua itakuwa ngumu sana. Lineman aliyeshindwa kung'amua offside ya kagere amefungiwa miaka 3. Offside hii ilikuwa ngumu sana kuiona kitaalamu inaitwa just offside. Baada ya hapo simba kuna mechi walicheza wakanyimwa goli la wazi kabisa.

Sikumbuki kama refa alipewa adhabu yoyote. Watu wanasubiri kwa hamu adhabu ya marefa waliompa goli Bocco, mechi ya Yanga na Mtibwa, na mechi ya leo ambapo offside zilizotolewa kwa Simba karibia 4 pamoja na ile ya goli hazikuwa offside. Watu wamekaa kimya wakisubiri hao waamuzi pia wafungiwe miaka 3 au zaidi. Maana aliyetoa goli la just offside amefungiwa miaka 3.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom