TFF kufungia Viwanja wakati ligi imeanza ni sawa?

Frank Wanjiru

JF-Expert Member
Joined
Apr 12, 2012
Posts
22,719
Reaction score
40,739
Nimeshangaa leo kusikia kuwa TFF imevifungia baadhi ya Viwanja kwa visitumike kwenye matches za ligi kuu Tanzania,kama vile Jamhuri Morogoro na Ushirika Moshi. Je TFF walikuwa wapi muda wote huo kuvifungia kabla ligi haijaanza,au ndio mwendelezo wa ule ubabaishaji wa Soka la Bongo?
 
Watu waliposema Karia hana maana yoyote hapo TFF watu walidhani Yanga ndio wanamwandama. Ligi imechelewa kuisha, viwanja havijakaguliwa mpaka ligi inaanza, maandalizi ngao ya hisani ni sifuri, afu unasikia mtu kapita bila kupingwa. Inabidi Serikali zitafute nanna ya kupambana na rushwa kwenye vyama vya michezo.
 
Bodi hii ya ligi inaongozwa na msanii sijui Kasongo, kabla ya ligi walikagua viwanja wakavipitisha kwa sababu azam wanaonyesha mpira live tumeshuhudia uwanja wa dodoma na karume mara haufai hii inaonyesha kuna watu walipewa pesa wakatia mfukoni wala hawakwenda kufanya ukaguzi.
Hivi vitu waandishi wa michezo wangekuwa wanavipigia kelele labda wangeshituka ila waandishi wenyewe wamekalia umbeyaumbeya tu.
 
Baada ya vodacom kushindwa kuendelea kudhamini ligi kuna mdhamini mwingine kapatikana?
 
Wenye viwanja ni wajibu wao kuhakikisha wakati wote vinakidhi viwango vya ubora. Ukaguzi na kufungwa vinaweza vikafanywa wakati wowote.

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
 
Uwanja unafungiwa muda wowote ukionekana haufai
Uwanja unahitaji matunzo kama kufyeka nyasi nk
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…