Bila bila
JF-Expert Member
- Dec 20, 2016
- 22,168
- 39,118
Niko uwanja wa Kambarage Shinyanga naangalia mechi kati ya Stand United na Mtibwa. Kuna tukio limetokea kwenye mechi hii dakika ya 7 labda niliweke hapa wajuzi Wa sheria za mpira mlijadili. Mchezaji Wa Mtibwa kafanya faulo mita kama kumi kutoka kwenye box la 18 la upande wake. Refa akapuliza filimbi na kuhesabu hatua 10 toka kwenye mpira na kuwaamuru wachezaji Wa Mtibwa waweke ukuta. Wao wakahesabu hatua 8 wakaweka ukuta wao tofauti na alipowaelekeza Refa. Hata walipoelekezwa waligoma na ukatokea ubishi kati yao na Refa kama dk 4 nzima. Ili kumaliza ubishi Refa akawaacha walipoweka ukuta akarudisha mpira nyuma hatua 2 na faulo ikapigwa. Je, kwa waamuzi kama hawa wanaogomewa na wachezaji na wao kulazimika kufuata maamuzi ya wachezaji tutegemee nini mechi ya ligi kuu inachezeshwa kama chandimu?