TFF mchezaji wa 13 Simba?

TFF mchezaji wa 13 Simba?

TFF wasipoangalia Yanga watalifikisha suala hili FIFA kwa sababu upo ushahidi WA wazi kuwa TFF ya Karia ina fanya kazi kwa maagizo ya serikali maana walikikiri kwa vinywa vyao wenyewe kuwa wanatii maagizo ya BMT. Hebu tujiulize wao Kama TFF kwa nini walimtambua Manji lakini wamelazimishwa na serikali kutomtambua kinyume na sheria za FIFA na CAF Hawaoni Kama wana hatarisha ushiriki WA timu yao kipenzi Simba kwenye mashindano ya CAF hata ikiitoa Nkana?
sio FIFA tu lakini linaweza pia kuchukua sura ya kisiasa
 
Mambo ya ngoswe yaachiwe ngoswe wenyewe waamue. TFF waisaidie yanga kumlipa Kakolanya arudi kikosini akaidakie club ili iendelee kufanya vizuri kwenye ligi na sio kuisaidia kufanya uchaguzi unaosababisha vurugu kwenye club



Tff ndo ilimsajiri Beno akaichezee yanga au ,hueleweki
 
Kwasasa huo ndio msaada pekee Yanga inahitaji na sio kusaidiwa kufanya uchaguzi.

Wawasaidie kifedha au hivi huyo beno nae anawatu wanamtegemea ndomana anaona mpira ndo ajira yake mlipeni fedha yake
 
Wawasaidie kifedha au hivi huyo beno nae anawatu wanamtegemea ndomana anaona mpira ndo ajira yake mlipeni fedha yake
Aaaa! Beno nae hasomi alama za nyakati, kazi yake ya ugolikipa ni kazi takatifu haitaki vitendo kama hivyo alivyofanya.
Hakuna timu makini duniani itapenda golikipa mwenye historia ya tabia kama hiyo ya kugoma anapokuwa na shida hasa ya kifedha. Hii ina maana kuwa golikipa kama Beno ana uwezo wa kuchukua fedha kutoka timu pinzani na kuiuza mechi.

Aliyemshauri Beno kufanya hivyo alikosea sana kupita kiasi. Beno hataaminika pahala popote duniani kucheza kama golikipa, maana hawatajua akikasirishwa na uongozi atachukuwa hatua gani kama sehemu suluhisho ya shida yake.
 
Aaaa! Beno nae hasomi alama za nyakati, kazi yake ya ugolikipa ni kazi takatifu haitaki vitendo kama hivyo alivyofanya.
Hakuna timu makini duniani itapenda golikipa mwenye historia ya tabia kama hiyo ya kugoma anapokuwa na shida hasa ya kifedha. Hii ina maana kuwa golikipa kama Beno ana uwezo wa kuchukua fedha kutoka timu pinzani na kuiuza mechi.

Aliyemshauri Beno kufanya hivyo alikosea sana kupita kiasi. Beno hataaminika pahala popote duniani kucheza kama golikipa, maana hawatajua akikasirishwa na uongozi atachukuwa hatua gani kama sehemu suluhisho ya shida yake.

Kwani Beno alisajiliwa yanga kwa mahaba Na timu au alichagua mpira ndo kazi yake

Acheni kuleta hoja mbovu mpeni kijana wa watu haki yake
 
Kama tff sio mmiliki wa Yanga inawashwa na nini kutomtambua Manji kama mwenyekiti halali wa Yanga? Yanga haijawahi kulalamika kukosa mwenyekiti bali inalalamika kukosa pesa za kulipa wachezaji. Kama tff ina huruma na yanga ianzie Kwanza na haki za wachezaji wanaopiga miayo Kwa njaa. Sheria gani hiyo inayomlenga mtu mmoja Tu?
Hizo zote ni mbwembwe na malalamiko yasiyo ya msingi. Kama suala la uchaguzi lipo kisheria, sisi Yanga hatuna budi kufanya uchaguzi. Mengineyo ni udumavu wa ufahamu na mihemuko ya ushabiki tu. Tufanyeni uchaguzi kama uko kisheria mambo yapute.
 
Mbona tff na bmt hawaongelei sheria kuhusu sababu na namna mwenyekiti wa Yanga alivyopata msukosuko ulisababisha ajiuzulu?
Diluted brain!!!

Unatuaibisha wana Yanga wenzako! Unawapa watu njia ya kutufedhuli kwa akili za namna hii. Natafuta namna ya kujificha humu jukwaani nashindwa kwa upupu wako.
 
Kwani Beno alisajiliwa yanga kwa mahaba Na timu au alichagua mpira ndo kazi yake

Acheni kuleta hoja mbovu mpeni kijana wa watu haki yake
Nani hataki kumlipa Beno? Yanga haina hela, sababu za hili hata Beno anazifahamu
 
Back
Top Bottom