TFF mnalitufanyia utapeli wa VAR wapenzi wa soka mnasingizia vibali wakati huko Mauritania VAR imeanza kutumika

OMOYOGWANE

JF-Expert Member
Joined
Dec 30, 2016
Posts
4,701
Reaction score
11,920
Wakuu,

Leo VAR imeanza kutumika huko Mauritania kwenye ligi yao

Sisi huku licha ya uzinduzi kufanyika na ligi kuanza
TFF wanasingizia vibali kutoka CAF na FIFA.

Huu ni utapeli wa mchana kweupe.

Tutegemee maumivu zaidi mpaka msimu unaisha

==================

UPDATES

Tumepigwa
 
Mauritania waliomba mapema,na walipitia taratibu kama ambazo sisi tunazipitia hivi sasa,kwa taarifa yako,kuna mafunzo yanaendelea kwa marefa wetu jinsi ya kuitumia,baada ya hapo maofisa wa fifa watakuja kukagua hivyo vifaa na uelewa wa marefa,wakithibitisha ndipo tutaruhusiwa kuvitumia,tuwe wavumilivu
 
Hii tasrifa yako mkuu chanzo chake ni kipi
 
Swali fikirishi hizo VAR ziko ngapi kwa maana zinatosha kutumika kwenye viwanja tofauti je ni mtambo wa kubebwa bebwa kama vile kamera? Popote ukapelekwa
 
Kwa mafanikio ya Karia kwa tff nadhani 2030 apewe nchi
 
Swali fikirishi hizo VAR ziko ngapi kwa maana zinatosha kutumika kwenye viwanja tofauti je ni mtambo wa kubebwa bebwa kama vile kamera? Popote ukapelekwa
Zipo mpaka mobile VAR mkuu mmiliki wake ni Azam alishanunua anazo
 
Huu utapeli niliuona mapema wengi hamkunielewa haya sasa waliinunua ya nini kama ilikua haitoshelezi mpaka wakaizundua kwa mbwembwe kwa kumtumia waziri mkuu
 
Wewe kama ni kariakoo ulikuwa ushatapeliwa mchana kweupe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…