kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 13,778
- 14,214
Ukweli ni kuwa mkubwa hakosei. Rais wa TFF ni mtu mkubwa sana kwenye mpira wetu Tanzania. Ndiye kioo Cha mpira wetu kwasasa, yaani kama ni ukatoliki yeye ndiye wa kanisa nchini na kama ni uislamu yeye ndiye Mufti wetu, haifai atokee mtu yeyote miongoni mwetu akamdhihaki hata kwa kutania TU akiwa anafuraha au ana hasira ya kitu chochote kinachohusu mpira wetu wa miguu.
Ni kweli Yanga ni kubwa kuliko coastal Union, mwenendo wa matokeo ya mechi Ile ya final ya Azam ulikuwa unaiduwaza Yanga kabla ya Yanga kupindua matokeo dakika za mwisho za mechi na kuibuka mabingwa. Furaha ya kupindua matokeo iliwafurahisha wadau wengi wa Yanga kiasi Cha kuwageuza wendawazimu (euphoric) wa muda kiasi Cha kujisahau kuwa Kuna maisha baada ya Ile mechi. Haji Manara alikuwa miongoni mwa wadau hao waliozidisha furaha na uendawazimu wa mpira siku ile kiasi Cha kwenda kukabiliana na kiongozi/Kadinali/mufti wake kwenye mpira, haikuwa sawa hata kama rais nae alionekana kufurahia mafanikio ya coastal Union kama mdau wa coastal Union pengine na Simba.
Binafsi ninamuona Manara kama mtu aliyeingizwa mtegoni na Ile comeback ya Yanga iliyopatikana kwa miujiza na bahati TU badala ya ubora wa kikosi.
Watalaam wa afya ya akili Wana kitu wanachokiita pre-morbid personality, yaani tabia ya mtu kabla ya kupata tatizo/kuugua. Haji maisha yake ameyawekeza zaidi kwenye soccer kiasi Cha kupitiliza, hivyo ufahamu wake na mahaba yake kwenye mpira ni makubwa zaidi kuliko watu wengi.
Mpira ndicho kitu pekee kinachofidia ulemavu wake alionao, na Kuna walemavu wengine kama yeye ambao wanapata nguvu zao kwa kumtazama Manara na kazi zake na mafanikio yake kama mlemavu mwenzao (role model)
Hivyo, kwa maslahi mapana ya mpira, Manara, walemavu na hata wadau wa mpira, nataka kuamini kuwa Haji amejifunza kutokana na kosa lake, ndio maana amekuwa akiomba radhi kila mtu baada ya pale.
TFF itakuwa imara sana kitaifa na kimataifa kama itaamua kumsamehe Manara badala ya kumfungia miaka 2 na kulipwa 20m na mlemavu. Haji hawezi kusukuma mkokoteni juani kama wengine. Ukimgungia mpira atafanya kitu gani kingine?
Ni mawazo yangu TU kama mdau wa mpira.
Ni kweli Yanga ni kubwa kuliko coastal Union, mwenendo wa matokeo ya mechi Ile ya final ya Azam ulikuwa unaiduwaza Yanga kabla ya Yanga kupindua matokeo dakika za mwisho za mechi na kuibuka mabingwa. Furaha ya kupindua matokeo iliwafurahisha wadau wengi wa Yanga kiasi Cha kuwageuza wendawazimu (euphoric) wa muda kiasi Cha kujisahau kuwa Kuna maisha baada ya Ile mechi. Haji Manara alikuwa miongoni mwa wadau hao waliozidisha furaha na uendawazimu wa mpira siku ile kiasi Cha kwenda kukabiliana na kiongozi/Kadinali/mufti wake kwenye mpira, haikuwa sawa hata kama rais nae alionekana kufurahia mafanikio ya coastal Union kama mdau wa coastal Union pengine na Simba.
Binafsi ninamuona Manara kama mtu aliyeingizwa mtegoni na Ile comeback ya Yanga iliyopatikana kwa miujiza na bahati TU badala ya ubora wa kikosi.
Watalaam wa afya ya akili Wana kitu wanachokiita pre-morbid personality, yaani tabia ya mtu kabla ya kupata tatizo/kuugua. Haji maisha yake ameyawekeza zaidi kwenye soccer kiasi Cha kupitiliza, hivyo ufahamu wake na mahaba yake kwenye mpira ni makubwa zaidi kuliko watu wengi.
Mpira ndicho kitu pekee kinachofidia ulemavu wake alionao, na Kuna walemavu wengine kama yeye ambao wanapata nguvu zao kwa kumtazama Manara na kazi zake na mafanikio yake kama mlemavu mwenzao (role model)
Hivyo, kwa maslahi mapana ya mpira, Manara, walemavu na hata wadau wa mpira, nataka kuamini kuwa Haji amejifunza kutokana na kosa lake, ndio maana amekuwa akiomba radhi kila mtu baada ya pale.
TFF itakuwa imara sana kitaifa na kimataifa kama itaamua kumsamehe Manara badala ya kumfungia miaka 2 na kulipwa 20m na mlemavu. Haji hawezi kusukuma mkokoteni juani kama wengine. Ukimgungia mpira atafanya kitu gani kingine?
Ni mawazo yangu TU kama mdau wa mpira.