TFF msizuge nyie ndiyo mmemuomba msamaha Manara, CAF wangewabomoa

njaakalihatari

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2019
Posts
4,081
Reaction score
8,671
Manara the greatest, the brightest, kijana mstarabu mwenye elimu yake nchi hii yaani degree mbili za south africa na china hajawahi kushindwa vita

Hii ni kwa sababu ana upako wa Mungu yaani ni mpakwa mafuta, wapo waliojaribu kushindana naye waliufyata wenyewe

Barbara sasa hivi ana migogoro kila kukicha, Mo dewji kafunga kiwanda Tanga, Daud bashite kaufyata,January makamba alipigwa dongo moja twiter hajaiunua mdomo tena,Shaffih dauda alinusurika makonde pale hotelini kinshasa ashukuru Marehemu Hans pope alimuokoa, kitenge, prisca hao walikuwa pole mbele ya gwiji hilo linalojua soka ndani na nje

Hapo sijataja simba ambayo ishapoteza makombe baada ya gwiji kuondoka bila kusahau Malinzi aliyethubutu kumfungia gwiji miezi 12 kujihusisha na soka matokeo yake alienda jela bila kusahau ccm-dsm waliomsingizia gwiji kutapeli magari wakamvua cheo cha katibu mwenezi wakaishia kupelekewa pumzi ya moto uchaguzi wa 2015 na ukawa

Gwiji leo limeomba radhi lakini ni zuga tu TFF ndiyo walienda kwake wakuu wa shrikisho wakampigia magoti ila wakaomba sana afanye alivyofanya leo ili ionekane yeye ndiye kaomba radhi

Bahati yenu sana mngemgusa mngetambua Motsepe ni nani hata huo mkutano wa CAf Arusha ungeyeyeyuka maana juzi mmeonyeshewa action ndooogo ya kutangaziwa fainali ya super league ni dar es salaam ghafla ikarudiswa morroco si mnajua Motsepe alikasirika kusikia mnamsumbua manara?

Jamaa afrika inamfatilia kwa karibu sana kaipa simba makombe mfululizo na kuifanya ijulikane afrika na kwa sasa yanga anaenda kuipa kombe la afrika, CAF wanataka wamtumie kulileta kombe la dunia kwenye bara hili la giza lenye vioja na vihoja

Sasa karia ukome kabisa siyo kila mtu wa kumchezea chezea nchi hii , shauri zako cha kufanya zuga tu na faini ya laki tatu yaishe
 
Kama ni hivyo Haji ni mbabe.
ila ajue hizi timu za Kariakoo hazina maana sana unazipambania mpaka unapigana mwisho wa siku timu ikianza kufanya vibaya wanakwambia unauza mechi hawakutaki wanataka uondoke.
 
Haji Manara plz fungua akaunti kwa jina lako mkui
 
yani uombe msamaha live alafu uje utunishe misuli nyuma ya keyboard.
 
KARIA SIYO MJINGA kapoteza game la berkane na waydad baada tu ya kutoa press release kwamba gwiji anafikishwa kamati ya nidhamu akijaribu kumfungia anajua moto wa CAF utamshukia vibaya mnoo, full kujichekesha sasa hivi



 
Tujamaa dizain (design) ya mleta mada ndo mtaji wa biko, tatu mzuka, mchongo pesa, mshindi millionaire n.k.

Vijana fulani hivi wale ambao wako radhi kuingia barabarani kuandamana kisa mwanasiasa fulani hivi amewashawishi lakini yeye (mwanasiasa) haonekani barabarani.

Vijana fulani hivi wako radhi kuvua shati kupigana kumtetea Diamond platnums wakati hawalipwi wala hawafaidiki na mziki wa diamond.

Vijana fulani hivi..sijui nisemeje!!!

Hiyo 9,...10 utakuta mleta mada nae ana demu!!!!!!!!
 
okay ushaandika point au huo ni utangulizi tu?
 
Yaani zamwamwa fulani hivi..
 
Ama kweli Manara ni kiboko ya nchi hii!

mpaka tff waufyata!
 
Yanga kuna vilaza wengi sana ukitaka kuamini muulize mtu yeyote aliyekuwepo arusha kwenye final ya azam sports.
 
Kuna mtu alikua na mtu taasisi moja, mtu akaanzisha ugomvi na mtu, baadaye mtu kamkimbia mtu kakimbilia taasisi nyingine. Anatokea mtu nje ya taasisi ya mtu aliyeikimbiliaa taasisi hiyo anaaminisha watu, mtu huyo hagusiki.

Ni hadithi ya kufikirika tu.
 
Kuna mtu alikua na mtu taasisi moja, mtu akaanzisha ugomvi na mtu, baadaye mtu kamkimbia mtu kakimbilia taasisi nyingine. Anatokea mtu nje ya taasisi ya mtu aliyeikimbiliaa taasisi hiyo anaaminisha watu, mtu huyo hagusiki.

Ni hadithi ya kufikirika tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…