TFF na Bodi ya ligi nafikiri mmeona Suma JKT walivyowapiga mashabiki kwa sababu ya mipangilio mibovu ya kuingia iliyopangwa Getini

Afisa usalama aliye letwa na CAF kusimamia mchezo huo ndie aliye sababisha matatizo yote. Yeye ndiye aliyekua na mamlaka ya milango kufunguliwa mapema...
Hakuna watu wa kumshauri huyo afsa usalama na kumwambia namna gani mashabiki wanapata kero
 
Kweli kabisa mkuu upo sahihi [emoji123]
 
Serikali ndo chanzo cha haya yote.

Rais Hasani ndo chanzo cha haya yote, yeye alikuwa kawekeza kwenye kujitukuza
 
Naskia mmepigwa ngwala balaa
Na wewe unajiita ni GT,furaha ya kusikia watanzania wenzako wamepigwa na wapumbavu wa suma!,sasa mmoja wapo aliyeumizwa ni ndugu yako, may be hili litakufanya utumie akili
 
Afisa usalama anayeletwa na CAF ndiye kiongozi wa maswala yote ya kiusalama katika uwanja wa mpira wa miguu.

Walio Baki hawana maamuzi zaidi ya kushauri tu, na ripoti yake baada ya mchezo ndio inayo pewa kipaumbele na CAF.

Bodi ya Ligi au Tff hawana nguvu zaidi ya kushauri kama wenyeji nini kifanyike, Vikundi vyenu vya ulinzi vitabaki na
Jukumu la ulinzi na usalama.

Utaratibu wote wa kuingia uwanjani na mambo mengine yahusuyo mchezo mamlaka anayo Afisa wa CAF.
 
Afisa usalama anayeletwa na CAF ndiye kiongozi wa maswala yote ya kiusalama katika uwanja wa mpira wa miguu.
Walio Baki hawana maamuzi zaidi ya kushauri tu...
Kama anapokea ushauri ilibidi watu (walinzi wetu) wamshauri hali inavyokua pale getini kipindi Cha mechi kubwa Kama hizi.
 
Afisa usalama anayeletwa na CAF ndiye kiongozi wa maswala yote ya kiusalama katika uwanja wa mpira wa miguu.
Walio Baki hawana maamuzi zaidi ya kushauri tu...
Lengo sio kubishana ila ni kupeana more informations ili kukuza uelewa wetu

 
Na wewe unajiita ni GT,furaha ya kusikia watanzania wenzako wamepigwa na wapumbavu wa suma!,sasa mmoja wapo aliyeumizwa ni ndugu yako, may be hili litakufanya utumie akili
Kaka umejuaje kuwa nimefurahi? Mi nimeandika nilichokisikia tu
 
Issue sio bure ,issue ni mpangilio mbovu wa kuingia kiwanjani, mara kadhaa pale hata mechi za Simba na Yanga, watu wanasukumana na kuvunja geti kwa same issues.
Ndiyo maana mimi sipendi kwenda uwanja.
 
Sasa hawa TFF na bodi ya league si wangempa ushauri tangu mwanzo, kwan huyo Afsa angekataa??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…