TFF na hatma ya mpira wa miguu Tanzania

Carica_papaya

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2018
Posts
767
Reaction score
1,272
Wakuu naomba kuuliza. Hivi TFF hawaoni madudu yanayoendelea katika League ya Mpira wa Miguu Tanzania?
Timu zinapewa ushindi kwa makosa ya wazi.

Wachezaji kuwa offside. Muda wa nyongeza kuzidishwa ili kufanikisha ushindi wa timu husika. Hii ni hatari kwa Mustakabali wa mpira wa Tanzania.

Madhara yake:
1. Kuua soka la ushindani
2. Kuwakatisha tamaa mashabiki wa mpira kutohudhuria kwa wingi uwanjani
3. Waamuzi wetu (Referees) kutoaminiwa katika mechi za kimataifa

Suluhu:
1. PCCB kuchunguza tuhuma hizi kama kuna michezo michafu inahusika kuzinufaisha baadhi ya timu
2. BMT kuingilia kati
 
Simba sport club ni janga la taifa kwa maendeleo ya mpira wa nchi wa hii!
 
sasa ikawaje ikawa kona, kama haikuvuka laini ingekuwa sio gori basi lkn ikaenda kuwa kona
Ndio tumshangae mshika kibendera kwanini aweke kona wakati mpira haukutoka nje. Na baada ya metacha kuutema ule mpira maamuzi ya refarii wa kati ilikuwa ni goal kick, wachezaji wa Lipuli wakapaniki kuwa lilikuwa ni goal na sio goal kick. Baada ya hiyo taharuki, refa wa kati akabidi mfate mshika kibendera amsikilize maamuzi yake kwa alichokiona cha ajabu mshika kibendera ndio kazua taharuki zaidi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
HIO SIMU ZENU WAKONYO HAZINA TOFAUTI NA HAO MAREFAA
 
Picha imekuwa doctored..ni rahisi kabisa kwa mtaalamu kuliona hili...doctoring ni kosa la jinai leteni original hapa...
Wewe mwenye original ndio ulete, sio uagize uletewe halafu useme tena si original
 
Nawaza hapo kona ilitokeaje daaa [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Tanzania Football Federation inaongozwa na raia wa Somalia na Burundi. Tuanze kurekebisha hilo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…