TFF na wadau wa michezo, tunafeli wapi?

TFF na wadau wa michezo, tunafeli wapi?

MTAZAMO

JF-Expert Member
Joined
Feb 8, 2011
Posts
19,675
Reaction score
33,583
Wakuu,

Baada ya kuangalia game ya Kongo DRC vs Uganda imenipa tafakari kubwa sana. Ilikuwa game ya viwango ambayo hata kama Taifa Stars tungeingia na akina Samatta ingekuwa aibu.

Kwanini pamoja na ligi yetu kuwa bora kwa udhamini kuongezeka by far kulinganisha hizi nchi jirani lakini bado hatuzalishi wachezaji bora? Uganda wamechukua wachezaji wengi wa Vipers lakini uwezo wao ni mkubwa mno hata kuwadhibiti Wakongo.

Hapa Tanzania timu zetu zote kubwa bila International players pengine hata ubingwa wa ndani ungekuwa rehani. Kipi hakiwekwi wazi kinachokwamisha kupata quality players. Imagine ilifikia hatua Nyoni na Yondani waliombwa wasistaafu timu ya Taifa kutokana na uhaba wa mabeki wa kati kipi kile!

Issues za sports academy imesemwa sana ila hata hizi zilizopo zinakwama wapi? Zimetoa wachezaji competitive enough kama mfano kwa Taifa? Ndio wapo ila kawaida! Simba imehangaika kutafuta kiungo mkabaji na locally hakuna mchezaji bora aliyewafaa wa kumpiku walau Erasto Nyoni! Yanga pale wamemsajili Mudathir lakini bado bila Bangala na yule mganda hawatoboi. Why?

Nafikiri Serikali ikubali kurudisha mashindano ya shule za msingi na sekondari kuanzia ngazi ya wilaya hadi Taifa. Hizi gharama wasikwepe tena ipitishwe bungeni. Watoto karibia wote wapo huko mashuleni, hakuna mbadala wa kupata vipaji zaidi ya huko.

Wadau wa michezo hasa watangazaji pia watengeneze ajenda zitazosaidia michezo badala ya vipindi vyao kutawala trending Issues tena gossips. Ni aibu nchi kuwa na michuano mbadala tegemeo kama Ndondo cup tena juhudi za mtu binafsi badala ya mikakati ya kitaifa.

Sasa Wakongo, wazambia n.k wanakimbilia Tanzania ambako ushindani wa local players upo chini sana. Hatuandai wachezaji bora, hatuna mikakati ya kuandaa makocha bora alafu kesho Taifa Stars ikicheza tunahamasishana kutegemea miujiza!

Tubadilike...
 
Ulozi wachezaji wa hizi timu zetu wanaweka mbele ulozi kulogana badala waige mazuri miongoni mwao wao kwa wao..mfano Fei mchezaji mzuri mzawa wamemloga akili zikamruka...

Viongozi nao wanawaza matumbo yao tuu hakuna mwenye uchungu na soka letu..
 
Nafikiri Serikali ikubali kurudisha mashindano ya shule za msingi na sekondari kuanzia ngazi ya wilaya hadi Taifa. Hizi gharama wasikwepe tena ipitishwe bungeni. Watoto karibia
Unaangalia Citizen TV inaonesha Mechi za CHAN, unaangalia UBC nayo inaonesha mechi hizo, unakuja TBC inaonesha maendeleo ya awamu ya 6, hapa kuna kukuza soka?? TBC wanapaswa kujua kuwa ni haki ya wananchi kupata habari, ikiwa ni pamoja na kuangalia michuano ya kimataifa..wajifunze Kenya na Uganda
 
Unaangalia Citizen TV inaonesha Mechi za CHAN, unaangalia UBC nayo inaonesha mechi hizo, unakuja TBC inaonesha maendeleo ya awamu ya 6, hapa kuna kukuza soka?? TBC wanapaswa kujua kuwa ni haki ya wananchi kupata habari, ikiwa ni pamoja na kuangalia michuano ya kimataifa..wajifunze Kenya na Uganda
Nimeshangaa pia, hii michuano inatoa somo kubwa sana sana. Umeangalia game ya Mozambique vs Libya? Hapo hakuna international players ila mpira unapigwa mkubwa mno! Unaogopa kama tungeshiriki [emoji50]

Sent from my SM-A315F using JamiiForums mobile app
 
Leo tuna watoto hata wa juzi wanaenda kumaliza elimu ya msingi hawajawahi kushuhudia interschool competitions! Seriously? Uliza mwanao kama una mtoto! Tunasubiri nini kuanza?

Sent from my SM-A315F using JamiiForums mobile app
 
Topic za Morrison aisumbua Yanga ndio trending kila sehemu tunashindwa kujadiliana vitu basics kabisa.

Mara ngapi tunaona mahojiano na viongozi wa TFF kuelezea mipango ya soka kwa vijana? Mipango yao huko nyuma imefeli wapi? Timu za vijana kwenye club zetu kubwa zipo imara? Zina basics infrastructure? Kuna kanuni za kubana hizi timu zetu?

Sent from my SM-A315F using JamiiForums mobile app
 
Wakuu,

Baada ya kuangalia game ya Kongo DRC vs Uganda imenipa tafakari kubwa sana. Ilikuwa game ya viwango ambayo hata kama Taifa Stars tungeingia na akina Samatta ingekuwa aibu.

Kwanini pamoja na ligi yetu kuwa bora kwa udhamini kuongezeka by far kulinganisha hizi nchi jirani lakini bado hatuzalishi wachezaji bora? Uganda wamechukua wachezaji wengi wa Vipers lakini uwezo wao ni mkubwa mno hata kuwadhibiti Wakongo.

Hapa Tanzania timu zetu zote kubwa bila International players pengine hata ubingwa wa ndani ungekuwa rehani. Kipi hakiwekwi wazi kinachokwamisha kupata quality players. Imagine ilifikia hatua Nyoni na Yondani waliombwa wasistaafu timu ya Taifa kutokana na uhaba wa mabeki wa kati kipi kile!

Issues za sports academy imesemwa sana ila hata hizi zilizopo zinakwama wapi? Zimetoa wachezaji competitive enough kama mfano kwa Taifa? Ndio wapo ila kawaida! Simba imehangaika kutafuta kiungo mkabaji na locally hakuna mchezaji bora aliyewafaa wa kumpiku walau Erasto Nyoni! Yanga pale wamemsajili Mudathir lakini bado bila Bangala na yule mganda hawatoboi. Why?

Nafikiri Serikali ikubali kurudisha mashindano ya shule za msingi na sekondari kuanzia ngazi ya wilaya hadi Taifa. Hizi gharama wasikwepe tena ipitishwe bungeni. Watoto karibia wote wapo huko mashuleni, hakuna mbadala wa kupata vipaji zaidi ya huko.

Wadau wa michezo hasa watangazaji pia watengeneze ajenda zitazosaidia michezo badala ya vipindi vyao kutawala trending Issues tena gossips. Ni aibu nchi kuwa na michuano mbadala tegemeo kama Ndondo cup tena juhudi za mtu binafsi badala ya mikakati ya kitaifa.

Sasa Wakongo, wazambia n.k wanakimbilia Tanzania ambako ushindani wa local players upo chini sana. Hatuandai wachezaji bora, hatuna mikakati ya kuandaa makocha bora alafu kesho Taifa Stars ikicheza tunahamasishana kutegemea miujiza!

Tubadilike...
Watanzania hawako serious.

Mfano mzuri ni wewe mwenyewe kushindwa kujua hata matatizo yanayotukwamisha hadi uje kulia lia hapa Jf.
 
Serikali kama mdau mkubwa wa michezo haijafanya vya kutosha kuimarisha na kuendeleza michezo,

Nb: hivi viwanja vya mpira vinavyo milikiwa na ccm wali vijenga? Na Kama hawaku vijenga wali vipataje?

Hawa jamaa ni moja ya sababu ya kuzorotesha mpira hapa Tanzania, mchezo unaweza kuahirishwa au kusogezwa mbele eti kisa Wana ratiba ya mkutano uwanjani, na wakimaliza mkutano uwanja unakua hovyo haufai kabisa
 
Tuanzishe sports academ tena je hzi zilizopo ambazo nyengne zimekuwa zinatumiwa na hawa ndugu zetu wazee wa ngada?
Soka la tanzania kigezo chake ni pesa anaecheza apate fweza awe na kiwango au hana na anaewekeza apate fweza hata timu iwe na -ve/+ve performance hayo mengine kwetu hayapo
 
Kwanza kabisa tunaanza kufelishwa na TFF, hili ndio tatizo namba moja la mpira wetu, hapa tusidanganyane, hatuwezi kuongozwa na watu wasiojielewa, lazima nasi na mpira wetu tutakuwa hatueleweki tu.
 
Serikali kama mdau mkubwa wa michezo haijafanya vya kutosha kuimarisha na kuendeleza michezo,

Nb: hivi viwanja vya mpira vinavyo milikiwa na ccm wali vijenga? Na Kama hawaku vijenga wali vipataje?

Hawa jamaa ni moja ya sababu ya kuzorotesha mpira hapa Tanzania, mchezo unaweza kuahirishwa au kusogezwa mbele eti kisa Wana ratiba ya mkutano uwanjani, na wakimaliza mkutano uwanja unakua hovyo haufai kabisa
Wewe umemaliza kila kitu. Mchawi ni Siri Kali. Tutazunguuuka mwisho tutagotea hapo.
 
Back
Top Bottom