TFF Pigeni marufuku wachezaji ligi kuu kushiriki ndondo Cup

Window7

JF-Expert Member
Joined
Sep 17, 2013
Posts
4,098
Reaction score
3,038
Imekua kawaida kwa wachezaji wengi wa ligi kuu hapa Tanzania kushiriki ligi za ndondo mitaani. Hili suala linadhoofisha vipaji vyao bila wao kujua lakini pia kunyima fursa vipaji vingine kuibuka.

Nimeshangaa kusikia wachezaji kama Maguli na Chanongo kushiriki ndondo Cup.

TFF chukueni maamuzi juu ya hili.

Cc Mh Jamali Malinzi
 
Unashangaa kuwa Maguli na Chanongo wanacheza Ndondo cup! Subiri mwakani timu yao mikia fc nayo itashiriki, hiyo ndiyo level yao.
 
Wengine ndio time zao za miyaa jamani sasa mnataka wasiwakilishe.....
 
ila huu ni ujinga.. wachezaji hawajitambui kabisa..

hivi mchezaji wa ligi kuu unacheza ndondo ukiumia nani anakutibia??
 
Acha wivu wewe kila sehemu duniani kuna utamaduni wake haijalishi hata kama soka ni lile lile..

Inatakiwa ujue kwenye soka hakuna unachokipata zaidi ya burudani na hiyo ndio burudani na hawa wachezaji wametoka huku huku mtaani na sisi ndio tuliowakuza mpaka kufika huko tena kwa gharama zetu ambazo mara nyingi hatuzidai

Dirk Kuyt ameshawai kukiri kwamba hata yeye mwenyewe alikuwa anacheza ndondo huko kwao wakati anaichezea Liverpool sembuse Maguri

U know nothing na Kama ujui soka na utamaduni wake bora unyamaze usituletee hadithi za panya na paka (simbayanga)
 
Mkuu kwa mishahara gani wanayolipwa bongo?,waache watafute fweza ya mboga...
 
Unashangaa kuwa Maguli na Chanongo wanacheza Ndondo cup! Subiri mwakani timu yao mikia fc nayo itashiriki, hiyo ndiyo level yao.
Naweka kumbukumbu sawia.. Maguri na Chanongo ni wachezaji wa Stand United, na si Simba S.C.
Kutoka Bondeni hadi Ndondo! Pamoja na kwamba Mikia FC haichezi kama timu, wachezaji wake wanacheza Ndondo.
Wachezaji gani wa Mnyama wanaocheza Ndondo?
 
Ndondo inaua kipaji utakuta mpira unaupigia mahesabu utue kwenye mguu mara utasikia umechange direction umekuja wa ugoko.
 
kwa maelezo haya,sina shaka wewe ni mbumbumbu fc
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…