TFF, VODACOM, STAR T.V walipanga kuihujumu Yanga?



Kaka kipindua kwa heshima na taadhima nakuomba ubadili hiyo AVATAR kwani wengine huwa inatukosesha hata hamu ya kula.Natumaini kuwa ombi langu utalifanyia kazi.
 
yebo yebo nao ni wahapa hapa miaka miwil mfululizo wamekutana na timu mbovu CAF lakini wamekuwa wanatoka mapema mwakani sijuoi itakuwa vipi kwa ubingwa wa kupanga matokeo
 

TFF, Vodacom na Simba wamumbuka kama NEC ilivyoumbuka kwenye uchaguzi uchaguzi 2010.
 
jamani jamani simba wenu huyo je anang'ata kumbe simba wenyewe simba koko, khokhohooo na mbweka umbeya
 
Kaka kipindua kwa heshima na taadhima nakuomba ubadili hiyo AVATAR kwani wengine huwa inatukosesha hata hamu ya kula.Natumaini kuwa ombi langu utalifanyia kazi.

ntalifanyia kazi!
 

Mkuu, naomba nikupongeze kwa kutwaa ubingwa, najua mlifanya kazi kubwa wakati sisi tulipojisahau na kuamini kuwa tayari tumeshakuwa mabingwa. Sisi tutajilaumu kwa kuteleza, hasa katika mechi na Azam, tulikuwa ovyo na kupoteza mechi kama vile hatukuwa na kiu ya ubingwa.

Nadhani ukisoma hiyo post namba 14, jamaa yupo sahihi.Ni wewe tu kukubaliana naye au kutokubaliana naye, hakibadiliki kitu kwa vile hata baada ya mechi ya Mwanza yanga walikuwa mabingwa na wakapewa kombe. Hongera.Kwa wengine wetu kama kombe lingepelekwa Mwanza,pia tungeamini ni mpango vilevile kwa sababu kule kulikuwa na mechi ya kuamua bingwa na timu A yanga walikuwa wanacheza na kikosi chao cha pili.
 
TFF wanapenda mzaha sana,unakumbuka sakata la nyimbo za taifa kutopigwa?hapa napo anahitajika mtu wa kuwajibishwa!
 


Wanashangaza sana watu hawa,asante kwa kuliona.
 
tukiweka ushabiki pembeni utakuja kugundua kuwa wenye majukumu wanapenda vitu vya kulipua lipua kwa sababu hakuna mtu wa kuwawajibisha so ndio maana hakuna ufanisi.
miafrica ndio tulivyo-Nyani Ngabu

Shukrani kwa kuliona hilo mtani.
 

Kuna wakati huwa nazikubali sana kazi zako,bravo.
 
yaani huu ndio utetezi wenu!kwa nini kote yasikae makombe feki?au kwa nini isichaguliwe siku ya kukabidhi kombe?yaani matatizo ya kiufundi yanatokea mwanza(makao makuu ya star t.v) halafu dar matangazo yanaendelea!!huu ni mpango!

Shangaa hapo sasa.!!!!!!!!!!!!??????
 
Kaka kipindua kwa heshima na taadhima nakuomba ubadili hiyo AVATAR kwani wengine huwa inatukosesha hata hamu ya kula.Natumaini kuwa ombi langu utalifanyia kazi.

Dah!! Kumbe na wewe umeliona hilo, kwa kweli hii avatar inakera sana...
 
mimi nipo kijijini, kwa wenzangu ambao mpo mjini naomba mnijuze tu lile tambala kubwa lilokuwa limewekwa mtaa msimazi lenye maandishi ya Simba bingwa 2011 bado lipo? na ile order ya kanga na tshirt ambazo zimeshachapishwa atauziwa nani?
 
mimi nipo kijijini, kwa wenzangu ambao mpo mjini naomba mnijuze tu lile tambala kubwa lilokuwa limewekwa mtaa msimazi lenye maandishi ya Simba bingwa 2011 bado lipo? na ile order ya kanga na tshirt ambazo zimeshachapishwa atauziwa nani?

Watarecycle.
 

Fanya utafiti kabla ya kukurupuka ...TFF ilishatangaza kuwa kwa kuwa mshindi wa mwaka huu angekuwa simba ama Yanga na kwa kuwa mshindi alikuwa akabidhiwe kombe lake siku ileile...basi TFF iliandaa makombe mawili..la zamani lilipelekwa uwanja wa taifa Dar, na jipya lilipelekwa kirumba ili timu yoyote itakayoibuka kidedea iweze kukabidhiwa kombe lake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…