TFF yarudisha kombe la FA (FA CUP) rasmi, AZAM MEDIA yadhamini kwa Billion 3.3

brave one

JF-Expert Member
Joined
Feb 5, 2013
Posts
4,879
Reaction score
7,386
Shirikisho la soka nchi limefanikiwa kuingia mkataba wa miaka 4 na azam media wenye thamani ya tsh bil 3.3 kwa ajili ya mashindano ya kombe la shilikisho. Mashindano hayo yataendeshwa kwa njia ya mtoano , huku timu 64 zikitarajiwa kushiriki mashindano hayo, timu 16 za ligi kuu, timu 24 za ligi daraja la 1 na timu 24 za ligi daraja la 2, timu za ligi kuu zitaanzia raundi ya 2 ambayo itajumuisha timu 32, timu mwenyeji itakuwa inapata tsh. mil 1 kwa ajili za maandalizi huku timu ya ugenini itakuwa inapata tsh. mil 3 kwa ajili ya maandalizi hii ni kwa kila mechi, timu zitakazo fanikiwa kufika fainali zitakuwa zimecheza mechi 7(Mechi zitachezwa kwa mfumo wa nyumbani na ugenini kasoro mechi ya fainali tu), bingwa wa mashindano haya atapata zawadi ya tsh. mil 50 na atapata nafasi za kuiwakilisha nchi kwenye mashindano ya kombe la shilikisho barani africa.. Hongereni sana TFF kwa hili mnastahili pongezi

=========================

Chanzo: Binzubeiry
 
kwa hili TFF hongereni sana cha msingi wekeni usimamizi imara, huko ndo mtavipata vipaji na sio kuendelea na maboresho ...
 
Mathalani ktk Vpl na Fa kote bingwa akawa Azam,Simba au Yanga je ataiwakilisha nchi ktk makombe yote mawili yaan champions na shirikisho au ni vipi???



Mwenye uelewa anieleweshe
 
duh! kwa mwendo huu kuna timu naiona hapa kupåndå ndege kwendå kushiriki måshindåno yå kimåtåiffå itakuwa stori wåtabaki kuyåsikiliziå kwenye redio nå kuyåonå kwenye luninga tu


#team wåmchångåni fc#
 
Mathalani ktk Vpl na Fa kote bingwa akawa Azam,Simba au Yanga je ataiwakilisha nchi ktk makombe yote mawili yaan champions na shirikisho au ni vipi???



Mwenye uelewa anieleweshe
Mathalani timu ya wananchi dar young africans amekuwa bingwa wa makombe yote mawili yaani bingwa wa ligi kuu Tanzania bara na bingwa wa kombe la Azam sports federation cup (Asfc) basi mshindi wapili wa kombe la shirikisho ataiwakilisha tz katika mashindano ya kombe la shirikisho barani Afrika.
Nadhani nimeeleweka vya kutosha.
 
TFF kwanini wameliita FA Cup?

FA nijuavyo ni Football Association.

Kwanini wasiliite FF Cup?

Tanzania ni Football Federation,

FF ndiyo sahihi.
 

Nimekupata mkuu mkolaj,
Kumbe ataenda kushiriki kwa hisani ya Yanga
 
TFF kwanini wameliita FA Cup?

FA nijuavyo ni Football Association.

Kwanini wasiliite FF Cup?

Tanzania ni Football Federation,

FF ndiyo sahihi.

Bibie nimekupenda bure kwa kuwakwako kwenye Michezo, Hata hivyo kuna point unaikosa hapa.

Kwasasa kombe hili linaitwa KOMBE LA SHIRIKISHO LA MIGUU TANZANIA. yaani TANZANIA FOOTBALL FEDERATION CUP.

Hapo awali ndio lilikuwa likiitwa FA cup kwakuwa TFF hapo awali ilikuwa ikijiita TFA (Tanzania Football Association)

Najua humkubali Malinzi, ila mpongeze kwa hili. Halafu hivi we ni Fan wa club gani hapa nchini? Hop isijekuwa Yanga kwasababu ya rangi ya jezi wanayovaa?

BACK TANGANYIKA
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…