TFF yatoa maamuzi sakata la Ramadhani Singano 'Messi' na timu yake Simba

TFF yatoa maamuzi sakata la Ramadhani Singano 'Messi' na timu yake Simba

Ku forge document ni koza la JINAI, na anaye shiriki katika kuficha kosa ni mkosaji, POLISI waingilie hili swala, huyu aliyefanya haya aadhibiwe kwa mujibu wa sheria za nchi.
malinzi, toa maelezo je katibu kafanya kwa baraka za TFF kuharalisha kosa, au kafanya kama Mwesigwa. Tusiendekeze huu upuuzi, nina imani aliye forge hakuwa na baraka za klabu ya Simba. Hivyo aadhibiwe kama yeye. Mnakumbuka kisa cha aliyekuwa katibu wa Yanga Mr Makongoro?
 
Last edited by a moderator:
Ku forge document ni koza la JINAI, na anaye shiriki katika kuficha kosa ni mkosaji, POLISI waingilie hili swala, huyu aliyefanya haya aadhibiwe kwa mujibu wa sheria za nchi.
malinzi, toa maelezo je katibu kafanya kwa baraka za TFF kuharalisha kosa, au kafanya kama Mwesigwa. Tusiendekeze huu upuuzi, nina imani aliye forge hakuwa na baraka za klabu ya Simba. Hivyo aadhibiwe kama yeye. Mnakumbuka kisa cha aliyekuwa katibu wa Yanga Mr Makongoro?

Mkuu tatizo ninaloliona hapa ni kutoelewa implications za sakata hili. Wengi wanang'ang'ania Singano aachwe huru aende atakako. Hili ni sawa. Lakini kuna jambo serious limejificha ndani ya hili sakata zima. KUGUSHI NYARAKA. Hii ni jinai na TFF haina mamlaka ya kuhukumu hili. Nashangaa kuona TFF wanaweza kukaa na pande mbili zinazotuhumiana kugushi nyaraka na kufanya usuluhishi. Hii ni aibu kubwa.

Kimsingi hili ni suala la kipolisi. Nilitarajia polisi waingilie kati bila hata kusubiri kuletewa kwani tayari limeshakuwa wazi kupitia vyombo vya habari. Hapa hakuna kukwepa, ni lazima sheria za nchi zifuatwe. Kama ilivyofanyika kwa Chuji, ndivyo inavyotakiwa kufanywa sasa.

Hii ni aibu kwa Jamal Malinzi NA TFF yake. Aibu kubwa
 
Last edited by a moderator:
Najiuliza tu. Eti wakae wakajadili. Je wasipokubaliana?
 
Tatizo watu mna vichwa vigumu. Ishu sio mkataba uliopo Simba au kwa Messi, ishu ni mkataba uliopo TFF. Kama mkataba wa Messi ndio ungekuwepo TFF, angeshakuwa huru zamani sana na Yanga wangeshampa milioni 70

Wewe ndiye mwenye kichwa kigumu kama jiwe. Endapo TFF wanao mkataba halali wangeamuaje kuwa wakajadili mkataba mpya? Weka unazi pembeni ili ujadili uzi huu ukiwa neutral kama Makoye Matale.
 
Last edited by a moderator:
We jamaa una akili sana,kwa maana hiyo simba ndio wamefoji mkataba

Simba wamefoji mkataba lakini TFF imeamua kuficha aibu hiyo kwa kudai 'hakuna mshindi' lakini wakakae wajadili mkataba mpya. Endapo TFF wange declare kuwa Simba wamefoji repercussion yake ni kubwa mno kwani wangekuwa wamembip Kova moja kwa moja naye angekamata wote waliotajwa na TFF.
 
Hivi zile kadi nne za njano ziliishia wap?
 
Ku forge document ni koza la JINAI, na anaye shiriki katika kuficha kosa ni mkosaji, POLISI waingilie hili swala, huyu aliyefanya haya aadhibiwe...
. Tusiendekeze huu upuuzi, nina imani aliye forge hakuwa na baraka za klabu ya Simba.
Muendelee na msimamo huu huu hata kama itakuja kugundulika kwamba aliyefoji mkataba ni Messi. Isitokee kwamba kama ni Messi ndiye aliyefoji basi muanze kutetea kwamba aah sijui dogo asamehewe, hapana, sheria iwe msumeno. Itakuwa jambo la kiungwana kama hamtapotea kwenye uzi huu.
 
Muendelee na msimamo huu huu hata kama itakuja kugundulika kwamba aliyefoji mkataba ni Messi. Isitokee kwamba kama ni Messi ndiye aliyefoji basi muanze kutetea kwamba aah sijui dogo asamehewe, hapana, sheria iwe msumeno. Itakuwa jambo la kiungwana kama hamtapotea kwenye uzi huu.

In fact kwa msimamo wa Simba, kisheria ni kuwa Mwesigwa anasatahili kushitakiwa pia, kwani nia yake ni kuficha mharifu.
 
Muendelee na msimamo huu huu hata kama itakuja kugundulika kwamba aliyefoji mkataba ni Messi. Isitokee kwamba kama ni Messi ndiye aliyefoji basi muanze kutetea kwamba aah sijui dogo asamehewe, hapana, sheria iwe msumeno. Itakuwa jambo la kiungwana kama hamtapotea kwenye uzi huu.

Singano hana ubavu wa kufoji mkataba na angekuwa yeye ndio kafoji tayari angekuwa ameshafungiwa na TFF.Ukweli wa mkataba huu wanaujua kina Rage na Mzee Kinesi
 
Kweli mwisho wa ubaya aibu. Singano ana vielelezo vya hatari. Dogo hakukurupuka.
 
... Labda nikuulize kwa nini huyo Messi hana mkataba original? Kwa kawaida inapashwa ziwe original 3 kwa case kazi hizi. Kila party yaani Simba na Messi wanakuwa na original copy na TFF wanapeleka original copy vile vile. Na je aliyepeleka huo mkataba TFF ni mchezaji au ni Simba? Kama ni Simba waliupeleka, basi wanayo nafasi kubwa kwamba walipeleka huo ambao upo forged. Kuondoa huo utata ili suala lingekwenda polisi ili wahusishe wataalamu wa miandiko ili kubaini nani mwenye mkataba halali kati ya Simba na Messi. Huu mtindo wa forgery inabidi utafutiwe dawa.
Angalau wewe umenena, ila kwa kuongezea ni kwamba mkataba ule uliopo TFF ndio wa kuuzingatia zaidi katika kuuchunguza. Sahihi na dole gumba vichunguzwe kama sio vya Messi.
Mimi ninachoona hadi sasa ni kwamba hii mikataba haijaghushiwa, hakuna aliyefoji hapo, isipokuwa inaelekea Messi alisaini copy tatu akiamini zinafanana kumbe labda alichezewa akili akasaini copy moja ya mkataba wa miaka miwili (ikabaki kwake) na baada ya hapo akasaini bila kuchunguza copy nyingine mbili za mikataba ya miaka mitatu (ya Simba na TFF). Sasa hapo kama hali ni hiyo, hana ujanja, ni uzembe wake tu. Hata polisi wakichunguza watakuta sahihi na dole gumba ni la Messi, na kibao kinaweza kumgeukia yeye pamoja na kwamba Simba hawakumfanyia uungwana. Lakini mbele ya sheria, maandishi yana nguvu kuliko uungwana!
 
Angalau wewe umenena, ila kwa kuongezea ni kwamba mkataba ule uliopo TFF ndio wa kuuzingatia zaidi katika kuuchunguza. Sahihi na dole gumba vichunguzwe kama sio vya Messi.
Mimi ninachoona hadi sasa ni kwamba hii mikataba haijaghushiwa, hakuna aliyefoji hapo, isipokuwa inaelekea Messi alisaini copy tatu akiamini zinafanana kumbe labda alichezewa akili akasaini copy moja ya mkataba wa miaka miwili (ikabaki kwake) na baada ya hapo akasaini bila kuchunguza copy nyingine mbili za mikataba ya miaka mitatu (ya Simba na TFF). Sasa hapo kama hali ni hiyo, hana ujanja, ni uzembe wake tu. Hata polisi wakichunguza watakuta sahihi na dole gumba ni la Messi, na kibao kinaweza kumgeukia yeye pamoja na kwamba Simba hawakumfanyia uungwana. Lakini mbele ya sheria, maandishi yana nguvu kuliko uungwana!

Ni kweli mkuu kuna uwezekano kwamba hicho ndicho kilichofanyika. Watu wengi uwa ni wavivu wa kusoma, hivyo akiisha uona huo wa kwanza una miaka 2 anadhani na hiyo mingine iko hivyo hivyo na kusaini bila kusoma kila kitu. Matokeo yake anasaini wa miaka 3 wakati copy anayopewa yeye ni wa miaka miwili. All in all huu ni uhuni pia ambao klabu kubwa kama ya Simba hawaapashwi kuufanya. Bahati mbaya huwezi kumlazimisha mchezaji abaki na wewe kwa ujanja kama huu. anaweza kubaki kuwa mchezaji wa Simba kwa mwaka mmoja zaidi with zero contribution sasa sijui hiyo itaisaidia vipi club ya Simba.

Tiba
 
Kweli mwisho wa ubaya aibu. Singano ana vielelezo vya hatari. Dogo hakukurupuka.


Kwa comment hii inaonyesha wewe tayari umeshachukua upande. Tayari una matokeo kabla ya kuingia uwanjani.
Umeamua kesi kwa kusikiliza maelezo ya mlalamikaji, na kwa kuwa tayari uko partial kwake huna sababu ya kusikiliza utetezi wa mlalamikiwa!

Wengine sisi tumejifunza kusikiliza pande zinazohusika na kupitia vielelezo husika kabla ya kufanya hitimisho. Kwa namna hii tutabishana milele.
 
Kwa comment hii inaonyesha wewe tayari umeshachukua upande. Tayari una matokeo kabla ya kuingia uwanjani.
Umeamua kesi kwa kusikiliza maelezo ya mlalamikaji, na kwa kuwa tayari uko partial kwake huna sababu ya kusikiliza utetezi wa mlalamikiwa!

Wengine sisi tumejifunza kusikiliza pande zinazohusika na kupitia vielelezo husika kabla ya kufanya hitimisho. Kwa namna hii tutabishana milele.

Sihitaji upande mimi. Ni kwamba sipendi kupaka mafuta kwa mgongo wa chupa. Kuna video hapa jukwaani ikionyesha ushahidi alionao Messi. Crystal clear. Sihitaji kumfurahisha mtu hapa, haki itendeke, basi. Otherwise tuendelee na desturi ya wabongo ya kusafishana.
 
Angalau wewe umenena, ila kwa kuongezea ni kwamba mkataba ule uliopo TFF ndio wa kuuzingatia zaidi katika kuuchunguza. Sahihi na dole gumba vichunguzwe kama sio vya Messi.
Mimi ninachoona hadi sasa ni kwamba hii mikataba haijaghushiwa, hakuna aliyefoji hapo, isipokuwa inaelekea Messi alisaini copy tatu akiamini zinafanana kumbe labda alichezewa akili akasaini copy moja ya mkataba wa miaka miwili (ikabaki kwake) na baada ya hapo akasaini bila kuchunguza copy nyingine mbili za mikataba ya miaka mitatu (ya Simba na TFF). Sasa hapo kama hali ni hiyo, hana ujanja, ni uzembe wake tu. Hata polisi wakichunguza watakuta sahihi na dole gumba ni la Messi, na kibao kinaweza kumgeukia yeye pamoja na kwamba Simba hawakumfanyia uungwana. Lakini mbele ya sheria, maandishi yana nguvu kuliko uungwana!

Toka nianze kulisoma hili sakata sijawahi kukutana na post niliyoiunga mkono kama hii. Ila ukijibu hili swali utakuwa umemaliza kiu yangu.

Katika hizo copy tatu alizosaini, sasa kwanini yeye hana original yake badala yake ana photocopy yake?
 
Leo hii ndio siku ambayo sakata la Ramadhan Singano a.k.a Messi lilikua linasikilizwa kwenye ofisi za TFF ambapo pande mbili zilikutana chini ya TFF.

Baada ya kikao kirefu muafaka uliofikiwa chini ya TFF ni kwamba kuvunjwa kwa mikataba yote miwili ambayo inatofautiana. So, kikao kimeamua kwamba mkataba wa alionao Messi uvunjwe na mkataba walionao Simba uvunjwe waingie makubaliano mapya. Upande wa Singano haujakubaliana na maamuzi hayo kwasababu unamtaka yeye akubaliane na Simba tena.

Lakini kwa mujibu wake ni kwamba anatakiwa kuwa huru kama mkataba umevunjwa na sio kukubaliana upya na Simba. Singano anataka kuwa mchezaji huru ndio aamue mwenyewe kama kuongea na Simba au club nyingine.

Chanzo: Shaffih dauda

Messi akirogwa kujaza mkataba na simba katika mazingira haya atajutia uwamuzi wake huo, yafuatayo yanaweza kumtokea 1 kusugua benchi sana 2 kulaumiwa kila timu inapofanya vibaya wakati Messi akiwa mchezaji siku hiyo, ataambiwa ameuza mechi au amecheza chini ya kiwango
 
Toka nianze kulisoma hili sakata sijawahi kukutana na post niliyoiunga mkono kama hii. Ila ukijibu hili swali utakuwa umemaliza kiu yangu.

Katika hizo copy tatu alizosaini, sasa kwanini yeye hana original yake badala yake ana photocopy yake?
Nikiwa katika muendelezo wa hisia zangu tu za jinsi mchezo ulivyofanyika, bado naona ni uzembe huo huo wa Messi. Ukisikia maelezo yake katika ile video clip anayoelezea sakata hili, Messi anasema alipewa mkataba wake wiki moja baada ya kusaini. Hii ina maana alipokabidhiwa kitita wala hakuwa na haja tena na mambo ya 'makaratasi', aliona amemaliza. Nahisi Simba walitoa photocopy ya hiyo nakala yake moja wakampa naye akaridhika tu, halafu original japo ni wa miaka miwili, hawakumpa. Naomba ieleweke kuwa hayo ninahisi tu
 
Back
Top Bottom