TFF yawafungia viongozi wa Yanga SC miaka 3 kwa kukaidi maamuzi ya Serikali na Shirikisho hilo

TFF yawafungia viongozi wa Yanga SC miaka 3 kwa kukaidi maamuzi ya Serikali na Shirikisho hilo

Ghazwat

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2015
Posts
23,718
Reaction score
66,267
Shirikisho la soka nchini TFF kupitia Kamati ya Maadili, limewafungia Mwenyekiti wa matawi ya klabu ya Yanga, Bakili Makele na Katibu wa matawi ya klabu hiyo Boaz Ikupilika kujihusisha na soka kwa kipindi cha miaka mitatu kwa kukaidi maamuzi ya Serikali na Shirikisho hilo.

Maamuzi hayo yametolewa leo na Mwenyekiti wa Kamati ya Maadili, Hamidu Mbwezeleni katika mkutano na wanahabari uliofanyika katika ofisi za Shirikisho hilo Ilala jijini Dar es salaam.

Viongozi hao wanadaiwa kupinga maagizo ya Serikali na TFF ya kufanya uchaguzi wa kujaza nafasi ambazo ziko wazi ndani ya klabu ya Yanga.

Pamoja na adhabu hiyo waliopewa, pia wanatakiwa kulipa faini ya shilingi milioni mbili kwa kila mmoja.

Hivi karibuni Kamati ya uchaguzi ya Shirikisho la soka ya TFF kupitia Mwenyekiti wake Malangwe Mchungahela ilitangaza tarehe ya uchaguzi wa klabu ya Yanga ambayo ni Januari 13, 2019 na kuagiza klabu hiyo kuanza mchakato wa kutoa fomu za wagombea mara moja.

Nafasi zinazogombewa katika klabu hiyo ni nafasi ya Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti na Wajumbe wanne wa Kamati ya Utendaji.

IMG_20181113_155503.jpeg
 
Unamjua Mwenyekiti wa kamati ya maadili mwanasheria Hamidu Mbwezeleni?
Ni Yanga wa kutupwa.Wamekaidi maagizo lazima waadhibiwe. Walipofungiwa wengine kama Ndumbaro aliyefungiwa maisha mlishangilia. Leo kibao kimegeuka wale wale wamekuwa wabaya.
 
Lakini pamoja na hilo, embu angalia Walipewa siku 60 kwa Simba na Yanga kufanya uchaguzi..Lakini Simba walitimiza na Yanga kuna nafasi inatakiwa ijazwe kwa kuwa ziko wazi

Kama Yanga wanamtaka Manji wafuate utaratibu, achukue fomu agombee Uenyekiti tena, kwani alijiuzulu na nafasi yake akachukua Kaimu Mwenyekiti Clement Sanga, sasa hapo kosa la TFF au Serikali liko wapi mkuu

Yaani Manji arudi kienyeji kwanini?
Ila hii tff ni kufungia tu
 
Lakini pamoja na hilo, embu angalia Walipewa siku 60 kwa Simba na Yanga kufanya uchaguzi..Lakini Simba walitimiza na Yanga kuna nafasi inatakiwa ijazwe kwa kuwa ziko wazi

Kama Yanga wanamtaka Manji wafuate utaratibu, achukue fomu kwani alijiuzulu na nafasi yake akachukua Kaimu Mwenyekiti Clement Sanga, sasa hapo kosa la TFF au Serikali liko wapi mkuu

Yaani Manji arudi kienyeji kwanini?
Mwenye shida ni manji kwa nn hajitokezi ajitokeze akachukue form la sivyo tunasimama na Akilimali tu [emoji6]
 
Yanga wanatuzalilisha sana Watanzania, Manji hataki mnambembeleza nimeona mpaka Mhe Mkuchika ameingia Katika mtego huu.. Yanga yenye wanachama zaidi ya milioni moja lakini inashindwa kupata wa kuziba pengo ilo
 
Adhabu kali sana hii, kuwafungia miaka 3 na faini ya 2M? Hizi ni adhabu za kukomoana tu!
 
Nimeisifu sana hii TFF ya Wallec karia. Yaani sijaona watu wajinga km mashabiki wa yanga wanaomtaka Manji. Kilichonisikitisha mpaka mkuchika analeta siasa za akina Lipumba kwenye mpira!?? Yaani mtu alijiudhuru eti na kurudi arudi kienyeji kwa maombi tu ya watu wenye njaa!??

Halafu huu ni udhaifu wa kijinga kabisaa,hivi kumng'ang'ania Manji maana yake bila Manji hakuna yanga!?? Hii ina maana ikitokea Manji Mungu akamchukua na yanga itakufa!?? Manji akachukue form,ashindane na wenziye akina akilimali. Akigoma Mzee akilimali atakuwa mgombea pekee na hatufanya uchaguzi, atapitishwa tu..
 
Kwa nini Clement Sanga alifutwa uenyekiti wa bodi ya ligi?????TFF walisema Sanga sio mwenyekiti wa Yanga ...baada ya Manji kukataliwa na wanachama maombi yake ya kujiuzuru right!!!!sasa hao hao TFF hawamtambui Manji kama ni mwenyekiti wa Yanga..Mkizidi kukomaa Yanga tutaenda mahakamani Tanzania tufungiwe hata kama tutaqualify AFCON
 
Kwa nini Clement Sanga alifutwa uenyekiti wa bodi ya ligi?????TFF walisema Sanga sio mwenyekiti wa Yanga ...baada ya Manji kukataliwa na wanachama maombi yake ya kujiuzuru right!!!!sasa hao hao TFF hawamtambui Manji kama ni mwenyekiti wa Yanga..Mkizidi kukomaa Yanga tutaenda mahakamani Tanzania tufungiwe hata kama tutaqualify AFCON
Hii tff ya Kingese imejaa mbumbumbu watupu wakisikia Manji wanapagawa
 
Lakini pamoja na hilo, embu angalia Walipewa siku 60 kwa Simba na Yanga kufanya uchaguzi..Lakini Simba walitimiza na Yanga kuna nafasi inatakiwa ijazwe kwa kuwa ziko wazi

Kama Yanga wanamtaka Manji wafuate utaratibu, achukue fomu agombee Uenyekiti tena, kwani alijiuzulu na nafasi yake akachukua Kaimu Mwenyekiti Clement Sanga, sasa hapo kosa la TFF au Serikali liko wapi mkuu

Yaani Manji arudi kienyeji kwanini?

Wanaogopa kuita uchaguzi kwasababu Manji anaweza asishinde.
 
Back
Top Bottom