MBIO ZA UTORO ZA THABO BESTER ZAISHIA SAKAFUNI TANZANIA
Waziri Ronald Ozzy Lamola wa wizara ya katiba na vyuo vya mafunzo (magereza) Afrika ya Kusini athiibithisha kukamatwa Thabo Bester nchini Tanzania na tayari mipango ya mchakato wa kisheria ili Thabo Bester awe deported kurudishwa Tanzania imeanza.
Thabo Bester akiwa na mpenzi wake wa kike Dr Nandipha Magudumana pamoja na raia mwingine wa Mozambique wamekamatwa mkoani Arusha wakiwa na hati kadhaa za kusafiria amesema Mh. Bheki Cele waziri wa Polisi wa Afrika ya Kusini.
Mbali ya kutoroka toka jela moja yenye ulinzi mkali Afrika ya Kusini alikokuwa akitumikia kesi za mauaji na ubakaji Thabo Bester pia alikuwa anaendesha biashara za kitapeli za udalali wa majumba na magari ya kifahari kwa kushirikiana girlfriend wake Dr Nandipha Magudumana.
Picha : Jela ya ulinzi mkali ya Mangaung ya Bloemfontein Afrika ya Kusini alipotoroka Thabo Bester mwaka 2022.
Dr. Nandipha Magudumana aliweza wakati mmoja kufanikisha Thabo Bester kuongea kupitia mtandao wa Zoom akiwa ktk chumba cha ulinzi wa juu jela na mkurugenzi wa kampuni moja iliyopo jijini New York Marekani inayomilikiwa na bilionea Tom Motsepe.
Mkurugezi huyo alichukua hatua za tahadhari na kuomba huduma za makachero binafsi / private detective kuweza kumchunguza mtu aliyeongea naye ni nani ktk zoom ndipo alipobaini anaongea na mhalifu aliye jela nchini Afrika ya Kusini akitumikia kifungo kirefu hivyo mkurugenzi huyo kuachana naye mazungumzo ya biashara alizokuwa akizinadi pengine kwa uhakika zingekuwa haramu na za kitapeli....
Dr. Nandipha Magudumana ni msichana msomi wa elimu ya juu, ana digrii mbili za fani ya utabibu na sayansi ya Afya ambazo ni Bachelor of Health Sciences (BHSc) in Biomedical Sciences na Bachelor of Medicine and Bachelor of Surgery (MBChB), toka chuo kikuu tajwa cha University of the Witwatersrand, Johannesburg almaaruf
Wits cha nchini Afrika ya Kusini.
Baada ya unaosemekana mwili wa Thabo Bester kugundulika ukiwa umeungua vibaya kiasi cha kutotambulika kati selo ya jela maarufu yenye ulinzi mkali huko Bloemfontein nchini Afrika ya Kusini, Dr. Nandipha Magudumana alitayarisha ombi la affidavit la kupewa mwili wa aliyekuwa mpenzi wake ili ukafanyiwe maziko Soweto.
Lakini katika hali ya kushangaza baadaye Thabo Bester alionekana akiwa ameongozana na Dr. Nandipha Magudumana wakifanya shopping ktk supermarket moja karibu na walipopana jumba la kifahari la kodi mbaya lililopo Sandton mitaa ya matajiri kilometa moja toka makazi ya Rais Cyril Ramaphosa, na ndipo uchunguzi kuhusu 'kifo' cha Thabo Bester ulipoanza tena.
Picha : Jumba la kifahari alilokodisha tapeli Dr. Nandipha Magudumana kupata muonekano wa kufanikisha madili ya kutapeli ya udalali wa magari na majumba ya kifahari
Uchunguzi huo kwa kutumia picha za CCTV zilizowachukua wapenzi hao supermarket na pia kutaka kufahamu kwa kina vinasaba DNA vya mwili ulio uliungua vibaya jela ulikuwa ni wa nani, ulifikaje vipi ktk selo ya jela na kuzua taharuki kuwa jambazi sugu Thabo Bester ametoroka jela akiwa hai .. hatimaye wapenzi hao wawili katika uhalifu na wakiongozana na jamaa mmoja Zakaria Alberto raia wa Mozambique kunaswa nchini Tanzania.
Thabo Bester | Lamola says Bester and Magudumana were arrested in Tanzania on Friday night