Thabo Bester maarufu 'Mbakaji wa Facebook' na Dkt. Nandipha Magudumana wakamatiwa Arusha Tanzania. Wafahamu kwa undani wapenzi hawa

Thabo Bester maarufu 'Mbakaji wa Facebook' na Dkt. Nandipha Magudumana wakamatiwa Arusha Tanzania. Wafahamu kwa undani wapenzi hawa

Kwa sababu taasisi zao ziko corrupt

Ova
Basi Kama kweli Serekali ya South inamtaka Mfungwa wao,bas na sisi watukamatie lile jizi alilosema Mama kua limekopa pesa kibao kwenye Bank zetu 5 na likakimbilia huko South,ili tubadilishane nao na hakuna kuwapa Mfungwa wao bure, au watulipe kwa hiyo kazi iliowashinda wao sisi tumeiweza!!
 
Basi Kama kweli Serekali ya South inamtaka Mfungwa wao,bas na sisi watukamatie lile jizi alilosema Mama kua limekopa pesa kibao kwenye Bank zetu 5 na likakimbilia huko South,ili tubadilishane nao na hakuna kuwapa Mfungwa wao bure, au watulipe kwa hiyo kazi iliowashinda wao sisi tumeiweza!!
Gupta family ya huko S/Africa unaifahamu?
 
Ila mambo mengine bwana basi tu nchi ya south Africa raia wake Wana shida nadhani ni mental problem Kuna vitu vinafanyika kweny ile nchi mpaka unabakia unashangaaa yani, Sasa ndo wamekuja kudakiwa bongo land wao walijuwa wako salama
Yawezekana, hata mimi huwa naona kila mkazi wa Dar hayuko sawa kiakili, sijui ni jua lile.
 
View attachment 2581457

Jeshi la polisi Tanzania limewakamata mbakaji maarufu wa Afrika Kusini, Thabo
Bester, na mpenzi wake Dokta Nandipa Magudumana.

Stori ikoje?

2000s Thabo Bester alikuwa anabaka, kupora vitu, na kuwauwa wanawake ambao alikuwa anawatongoza kupitia mitandao ya kijamii. Alikua anaangalia wenye magari na vitu vya thamani.

2012 akafungwa miaka 50 gerezani.

2013 Nandipha ambaye ni daktari wa watoto aliolewa na bwana Oscar Magudumana na wakazaa watoto wawili. Wakatengana bila kupeana talaka; wakati huo dokta alikuwa kashazama penzini na mhuni Bester anayeny** debe gerezani. Yaani walianza mahusiano akiwa bado kwenye ndoa.

Kulingana na ripoti, Bester alikuwa akiwasiliana na Dk Nandipha akiwa bado gerezani. Mrembo akasuka mpango wa kutafuta mahali pa kujificha akitoroka gerezani.

2020, Septemba, Mrembo huyo alikodi nyumba kupitia kampuni ya 4Tune Property Smiths; mkataba ukawa na majina yake na mumewe Bester (ila jina likaandikwa lingine na kazi ikawa ni mtaalamu anayefanya kazi ulaya). Kodi ilikuwa ni Tshs Milioni 5 kwa mwezi (R 4000).

2021 Mei, Kakake Dk. Nandipha, Nkosinathi Sekeleni, alimtuhumu kwa kumsaliti mumewe na kulala na mbakaji Bester. akamtuhumu pia kuwa anatakatisha fedha za Bester kupitia kampuni yake ya Optimum Medical Solutions. Dokta akafungua kesi mahakamani ya kuharibiwa jina na kutishiwa kuuwawa na kaka yake.

2022, Mei, ulitokea moto gerezani na Bester akajumuishwa kuwa mmoja ya waliochomwa vibaya na kufariki.

Dokta Nandipha alienda kudai mabaki ya Bester ayazike akiwa kama "mke wake wa sheria ya kimila".

2022, Juni, kuna watu waliwatonya Polisi Afrika Kusini kuwa mfungwa aliyedhaniwa kuwa amefia kwenye moto gerezani yuko anafanya shopping ya nguo akiwa na dokta Nandipha. Msako ndio ukaanza.

2022, Mwishoni, Nandipa alinunua gari la kifahari la Tshs milioni 170 na akaliendesha mpaka mpaka wa Zimbabwe kisha akalitelekeza huko.

2023, Aprili, Thabo Bester, Dokta Nandipa Magudumana pamoja na mwingine ambaye inasemekana ni mfanyakazi wa dokta wakakamatwa Tanzania wakitoroka.
------------
Mapenzi.


Huyo jamaa alizaliwa baada ya mama yake kubakwa akiwa na miaka 17. Hajwahi kumjua baba yake ni nani. Mama mtu alimtelekeza kwa bibi akiwa mdogo. Jamaa naye alibakwa mara nyingi utotoni na ukubwani.
 
Hii hollywood lazima waiweke kwenye filamu
Ilikua rahisi kumkamata huyo Mchizi kwa sababu ya Demu wake, Demu ake alikua anaacha alama!

Huyo jamaa alikua ana Pesa, na ndo ambazo Demu alizitumia kumtoa Gerezani!

Sasa hapa Broemfontein, kasababisha Msala kwa Askari jela, 2 wameshakanatwa kwa kukutwa wanaendesha Magari ya bei mbaya tofauti na Mshahara wao!

Ndo hao walikua Zamu siku wanaruhusu Gari la kubeba Taka liingie mpaka Gerezani! (Ndo lililomtorosha Mtuhumiwa)

Wamempiga mtu Kiberiti, wakaunguza Selo, ili mtu mmoja hivi mharifu aweze kutoka.
 
Bongo Muvi wangekuwa na jicho la kuona mbali, wangechangamkia hii kesi kwa kutengeneza muvi kali na ya kusisimua sana kuhusiana na hili sakata la Dokta na jamaa yake mbakaji.

Muhimu tu polisi na magereza, watoe ushirikiano kwenye ishu ya majengo yao, na pia kutoa wataalam wa kusaidia hiyo muvi.

Ila kwa bahati mbaya ndiyo hivyo tena! Muda huu watakuwa wanasubiria tu 2025 ifike, ili watumiwe na ccm kwenye kampeni za uchaguzi mkuu kwa malipo kiduchu.
 
Bongo Muvi wangekuwa na jicho la kuona mbali, wangechangamkia hii kesi kwa kutengeneza muvi kali na ya kusisimua sana kuhusiana na hili sakata la Dokta na jamaa yake mbakaji.

Muhimu tu polisi na magereza, watoe ushirikiano kwenye ishu ya majengo yao, na pia kutoa wataalam wa kusaidia hiyo muvi.

Ila kwa bahati mbaya ndiyo hivyo tena! Muda huu watakuwa wanasubiria tu 2025 ifike, ili watumiwe na ccm kwenye kampeni za uchaguzi mkuu kwa malipo kiduchu.
Wanapenda sana kufanya hivyo ila tatizo linarudi kwa Watanzania. Watatumia pesa ndefu mpaka kukamilisha movie nzuri ila walaji ndio nyie mnaenda 'kuchoma' na kuuziana kwa 1,500 movie nzima.
 
Wanapenda sana kufanya hivyo ila tatizo linarudi kwa Watanzania. Watatumia pesa ndefu mpaka kukamilisha movie nzuri ila walaji ndio nyie mnaenda 'kuchoma' na kuuziana kwa 1,500 movie nzima.
Siku hizi teknolojia imebadilika. Na wenyewe wanatakiwa kuingia huko.
 
MBIO ZA UTORO ZA THABO BESTER ZAISHIA SAKAFUNI TANZANIA

Waziri Ronald Ozzy Lamola wa wizara ya katiba na vyuo vya mafunzo Afrika ya Kusini athiibithisha kukamatwa Thabo Bester nchini Tanzania na tayari mipango ya mchakato wa kisheria ili Thabo Bester awe deported kurudishwa Tanzania imeanza.

Thabo Bester akiwa na mpenzi wake wa kike Dr Nandipha Magudumana pamoja na raia mwingine wa Mozambique wamekamatwa mkoani Arusha wakiwa na hati kadhaa za kusafiria amesema Mh. Bheki Cele waziri wa Polisi wa Afrika ya Kusini.

Mbali ya kutoroka toka jela moja yenye ulinzi mkali Afrika ya Kusini alikokuwa akitumikia kesi za mauaji na ubakaji Thabo Bester pia alikuwa anaendesha biashara za kitapeli za udalali wa majumba na magari ya kifahari kwa kushirikiana girlfriend wake Dr Nandipha Magudumana.

Dr. Nandipha Magudumana aliweza wakati mmoja kufanikisha Thabo Bester kuongea kupitia mtandao wa Zoom akiwa ktk chumba cha ulinzi wa juu jela na mkurugenzi wa kampuni moja iliyopo jijini New York Marekani inayomilikiwa na bilionea Tom Motsepe.

Mkurugezi huyo alichukua hatua za tahadhari na kuomba huduma za makachero binafsi / private detective kuweza kumchunguza mtu aliyeongea naye ni nani ktk zoom ndipo alipobaini anaongea na mhalifu aliye jela nchini Afrika ya Kusini akitumikia kifungo kirefu hivyo mkurugenzi huyo kuachana naye mazungumzo ya biashara alizokuwa akizinadi pengine kwa uhakika zingekuwa haramu na za kitapeli....

Dr. Nandipha Magudumana ni msichana msomi wa elimu ya juu, ana digrii mbili za fani ya utabibu na sayansi ya Afya ambazo ni Bachelor of Health Sciences (BHSc) in Biomedical Sciences na Bachelor of Medicine and Bachelor of Surgery (MBChB), toka chuo kikuu tajwa cha University of the Witwatersrand, Johannesburg almaaruf Wits cha nchini Afrika ya Kusini.

Baada ya unaosemekana mwili wa Thabo Bester kugundulika ukiwa umeungua vibaya kiasi cha kutotambulika kati selo ya jela maarufu yenye ulinzi mkali huko Bloemfontein nchini Afrika ya Kusini, Dr. Nandipha Magudumana alitayarisha ombi la affidavit la kupewa mwili wa aliyekuwa mpenzi wake ili ukafanyiwe maziko Soweto.

Lakini katika hali ya kushangaza baadaye Thabo Bester alionekana akiwa ameongozana na Dr. Nandipha Magudumana wakifanya shopping ktk supermarket moja karibu na walipopana jumba la kifahari la kodi mbaya lililopo Sandton mitaa ya matajiri kilometa moja toka makazi ya Rais Cyril Ramaphosa, na ndipo uchunguzi kuhusu 'kifo' cha Thabo Bester ulipoanza tena.

Uchunguzi huo kwa kutumia picha za CCTV zilizowachukua wapenzi hao supermarket na pia kutaka kufahamu kwa kina vinasaba DNA vya mwili ulio uliungua vibaya jela ulikuwa ni wa nani, ulifikaje vipi ktk selo ya jela na kuzua taharuki kuwa jambazi sugu Thabo Bester ametoroka jela akiwa hai .. hatimaye wapenzi hao wawili katika uhalifu na wakiongozana na jamaa mmoja Zakaria Alberto raia wa Mozambique kunaswa nchini Tanzania.

Thabo Bester | Lamola says Bester and Magudumana were arrested in Tanzania on Friday night

Hapa nimegundua mambo kadhaa kwamba:-

1. Huyu mwanamke ambaye ni Doctor ndiyo mtu mwenye akili nyingi kuliko huyu mhalifu

2. Mwanamke huyu anafanya haya Kwa sababu tu anampenda jamaa, lakini pia ana tamaa na maisha mazuri ya kutumia akili bila kujitesa na kazi kwa mafanikio ya muda mrefu, Nigerian style

3. Walifanya kosa kubwa sana baada ya mpango wao kutimia, mhalifu alitakiwa kua mafichoni zaidi ya miaka mitano mpaka kumi ndiyo atoke nje ya nchi , kwa tamaa zao wakawahi kutumia pesa na starehe ambazo zimewaponza

4. Huyu mwanamke atatumikia kifungo ambacho ni cha wakati fulani na atakuja kutoka kwa sababu yeye si mhalifu halisi isipokua muwezeshi, ila huyu jamaa yake yamkini akifika huko S.A akapotezwa mazima.

5. Iko hatari kubwa ya ajira kwa mkuu wa gereza na maafisa wa zamu wa siku ambayo mhalifu alitoroka
 
Pamoja na hawa fugitives kukamatiwa hapa nchini, ni muhimu mno sheria zetu zikafuatwa, tusi just roll over ili kuwafurahisha SA, kwanza wajibu ilikuaje waukesha mpaka wao bila wahusika kujua, Mr.Bester ndiye pekee aliyehukumiwa, Dr.Nandipa na Mozambique citizen hawa ni illegal immigrants, wapelekwe mahakama na sheria ichukue mkondo wake, kuwa deport SA straight haitakua sawa
 
Hapa nimegundua mambo kadhaa kwamba:-

1. Huyu mwanamke ambaye ni Doctor ndiyo mtu mwenye akili nyingi kuliko huyu mhalifu

2. Mwanamke huyu anafanya haya Kwa sababu tu anampenda jamaa, lakini pia ana tamaa na maisha mazuri ya kutumia akili bila kujitesa na kazi kwa mafanikio ya muda mrefu, Nigerian style

3. Walifanya kosa kubwa sana baada ya mpango wao kutimia, mhalifu alitakiwa kua mafichoni zaidi ya miaka mitano mpaka kumi ndiyo atoke nje ya nchi , kwa tamaa zao wakawahi kutumia pesa na starehe ambazo zimewaponza

4. Huyu mwanamke atatumikia kifungo ambacho ni cha wakati fulani na atakuja kutoka kwa sababu yeye si mhalifu halisi isipokua muwezeshi, ila huyu jamaa yake yamkini akifika huko S.A akapotezwa mazima.
Sawa ila hiyo no 4 sio sahihi, Dr.Nandipa ni illegal immigrant kama wengine, ni LAZIMA ahukumiwe kwa sheria zetu za uhamiaji, Tanzania iheshimu sheria zake
 
Sorry,nilishindwa kuweka mwendelezo na pia kujibu maswali kadhaa kutokana na kubanwa na shughuli nyingine,wa South wanasema ni bora bester afungwe hukohuko tanzania kwani hawaiamini SAPS kabisa,wana mashaka kuwa anaweza kutoroshwa tena kutoka gerezani huko SA, kuna jambo nililiona tokea habari za bester kuonekana akiwa na Dr Nandipha kwenye supermarket,huku ikiaminika kuwa alishafariki kwa kujichoma moto akiwa gerezani na baadaye akafanyiwa cremation rasmi, thabo bester na Nandipha walikuwa ni wapenzi zamani,lakini waliachana muda mrefu kabla ya bester kuhukumiwa,inasemekana Dr Nandipha alikuwa akimpenda sana jambazi bester, hivyo aliposikia kuwa bester amehukumiwa altona ndiyo gap la kurudisha penzi Lao kwa gharama yoyote,ndipo alipoanza kusuka mipango ya kumtoa bester gerezani,so plan yote ya kumchomoa bester gerezani aliisuka Nandipha,hadi kuwahonga askari wa G4s waliokuwa wanaendesha gereza hilo,kununua maiti waliyoichoma moto wakidai ni ya bester, akagharimia kila kitu ikiwemo nyumba,gari,na expenses zote zitakazomfanya bester kuufurahia uhuru huo bandia,na hata baada ya picha za bester kusambaa akiwa kwenye Mall na nyingine ikimuonyesha akiwa nje ya duka jingine kubwa kusambaa,Nandipha alimhamishia bester kwenye nyumba ya kifahari aliyoipanga kwenye eneo la brooklyn huko Pretoria,baadaye tetesi zikachomoza kuhusu uwepo wa bester kwenye eneo hilo,mwandishi wa habari za kiuchunguzi aitwaye Barry roux ndiye aliyetoa hint kuhusu besters whereabouts, hivyo Dr Nandipha akalazimika kumhamisha tena bester na kumpeleka sehemu isiyojulikana!! Hadi walipokamatwa huko arusha usiku wa jana wakiwa na mtu mwingine ambaye ametambulika kama raia wa Mozambique, pia polisi wa arusha wanasema kuna mtuhumiwa mwingine mmoja ambaye alikuwa pamoja na bester ila bado hajakamatwa, hayo ndiyo mapenzi! Kuna mtu hapo juu aliuliza jinsi ambavyo bester alifanikisha uhalifu wake,bester anajulikana kama Facebook rapist!! Sababu ni hii,bester alikuwa akitumia mtandao wa Facebook kuweka matangazo ya nafasi za ajira nzuri nzuri,alikuwa akiweka na address za kuweza kuwasiliana naye ikiwa utavutiwa na ajira alizotangaza,sasa ukiwasiliana naye anakupa location ya kwenda kwa ajili ya interview na mengineyo,huku akiahidi kuwa gharama za usafiri na malazi utarudishiwa ukishafika kituoni,hapo ndipo watu walijichomeka bila kujua! Kwani baada ya kufika ulikoelekezwa ungepokelewa na bester mwenyewe,atakuonyesha sehemu ya kufikia na kula na kila kitu,sasa hapo ndipo atakuja kukupa interview, atakubaka,atakupora kila kitu,na kama Huna bahati anakuua kabisa!! Umeelewa sasa? Swali ni kuwa Dr Nandipha aliipata wapi maiti aliyoichoma kwa jina la bester? Maskini Dr Nandipha ndiyo ameshaharibu career yake kwa ajili ya mapenzi ya jambazi,muuaji na mbakaji bester, umeona kitu hapo?
Ukichunguza vizuri unaona Baster ni kama ni mtu kichaa
 
Sawa ila hiyo no 4 sio sahihi, Dr.Nandipa ni illegal immigrant kama wengine, ni LAZIMA ahukumiwe kwa sheria zetu za uhamiaji, Tanzania iheshimu sheria zake
Wala hahukumiwi hapa huyo, hao ni wahalifu ambao Serikali ya S. A itatuma maafisa wa usalama kuwafata na kurejeshwa kwao, hakuna hukumu yoyote wala kesi watakutana nayo hapa kwetu
 
Wala hahukumiwi hapa huyo, hao ni wahalifu ambao Serikali ya S. A itatuma maafisa wa usalama kuwafata na kurejeshwa kwao, hakuna hukumu yoyote wala kesi watakutana nayo hapa kwetu
Why mkuu ?,huyu raia wa Mozambique na Dr. Nandipa kosa lao hapa ni kuingia nchini kwa njia za panya, kama wasomali/Ethiopians wanavyofanya, sasa why hawa wawe tofauti?,SA lazima waheshimu sheria zetu na elewa hawa wawili hawana cases kule SA, but Mr. Bester ni tofauti maana yupo convicted kwa rapes na murder
 
Back
Top Bottom