Thamani kubwa iliyobebwa na samaki

Thamani kubwa iliyobebwa na samaki

Hamza Nsiha

JF-Expert Member
Joined
Jul 25, 2022
Posts
221
Reaction score
197
Ni matumaini yangu ulishawahi kusikia makundi mbalimbali ya vyakula kipindi unasoma elimu ya msingi. Ambapo ulijifunza kuwa kuna Kabohaidreti/wanga, protini, fati, vitamini na madini asilia.

Katika kundi la protini ulisoma kuwa, ni vyakula vinavyosaidia katika ukuaji wa mwili pamoja na kutengeneza kinga za mwili. mfano uliweza kuona vyakula kama vile nyama, maharage, samaki n.k.

Tafiti nyingi zinaonesha kuwa samaki imebeba virutubisho vingi ambavyo baadhi yake ni fati au mafuta yaitwayo (Omega-3- polyunsaturated fatty acids).

Mafuta haya ni muhimu zaidi katika ukuaji/afya ya ubongo (brain development) hivyo huongeza ufanisi wa ubongo katika utendaji kazi pia katika afya ya moyo ambapo husaidia kupunguza magonjwa mbalimbali ya moyo.

Ili kupata virutubisho hivyo ni lazima utumie njia thabiti ambayo ni "Uokaji" au "Uchemshaji" wa samaki suala ambalo ni mtihani kidogo katika jamii zetu. Kwa kufanya hivyo utaweza kuvuna virutubisho hivyo pamoja na virutubisho vya Vitamini D.


Je! Mimi na wewe tunatumia njia gani hasa katika uandaaji wa Samaki kabla ya kumtia kinywani?

Hata kama unakula kwa mama n'tilie unaweza kujiunga na mdahalo huu pia.
 
Ni matumaini yangu ulishawahi kusikia makundi mbalimbali ya vyakula kipindi unasoma elimu ya msingi. Ambapo ulijifunza kuwa kuna Kabohaidreti/wanga, protini, fati, vitamini na madini asilia.

Katika kundi la protini ulisoma kuwa, ni vyakula vinavyosaidia katika ukuaji wa mwili pamoja na kutengeneza kinga za mwili. mfano uliweza kuona vyakula kama vile nyama, maharage, samaki n.k.

Tafiti nyingi zinaonesha kuwa samaki imebeba virutubisho vingi ambavyo baadhi yake ni fati au mafuta yaitwayo (Omega-3- polyunsaturated fatty acids).

Mafuta haya ni muhimu zaidi katika ukuaji/afya ya ubongo (brain development) hivyo huongeza ufanisi wa ubongo katika utendaji kazi pia katika afya ya moyo ambapo husaidia kupunguza magonjwa mbalimbali ya moyo.

Ili kupata virutubisho hivyo ni lazima utumie njia thabiti ambayo ni "Uokaji" au "Uchemshaji" wa samaki suala ambalo ni mtihani kidogo katika jamii zetu. Kwa kufanya hivyo utaweza kuvuna virutubisho hivyo pamoja na virutubisho vya Vitamini D.


Je! Mimi na wewe tunatumia njia gani hasa katika uandaaji wa Samaki kabla ya kumtia kinywani?

Hata kama unakula kwa mama n'tilie unaweza kujiunga na mdahalo huu pia.
Kama samaki ina hivyo virutubisho vya kusaidia ukuaji bora wa ubongo..mbona watu wa pwani ambao samaki ndio chakula chao kikuu wana akili ndogo sana tena za hovyo?..je una weza prove vipi uhalali wa hiyo hicho kirutubisho omega cha ubongo.

#MaendeleoHayanaChama

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Kama samaki ina hivyo virutubisho vya kusaidia ukuaji bora wa ubongo..mbona watu wa pwani ambao samaki ndio chakula chao kikuu wana akili ndogo sana tena za hovyo?..je una weza prove vipi uhalali wa hiyo hicho kirutubisho omega cha ubongo.

#MaendeleoHayanaChama

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
Je, wanafuata njia stahiki katika uandaaji maana mikoa hii kwa asilimia kubwa ndio mikoa inayosifika katika mapishi ya vyakula mbalimbali ni vigumu sana kukuta watu wanachemsha tu samaki badala ya kurost na viungo kede kede.........tazama mikoa ya Kanda ya Ziwa unaweza kuprove hili.........Mwanza, Shinyanga, Kagera n.k
 
Kama samaki ina hivyo virutubisho vya kusaidia ukuaji bora wa ubongo..mbona watu wa pwani ambao samaki ndio chakula chao kikuu wana akili ndogo sana tena za hovyo?..je una weza prove vipi uhalali wa hiyo hicho kirutubisho omega cha ubongo.

#MaendeleoHayanaChama

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
Kuhifadhi juzuu 30 na kusoma bila kuangalia hzo sio akili kama rahisi hifadhi agano la kale halafu usome bila kuangalia kila unachoambiwa we sema hawataki shule lakini sio uongee huo utopolo wako hapo juu.
 
Back
Top Bottom