Thamani ya kichwa cha samaki pika hivi

Thamani ya kichwa cha samaki pika hivi

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2009
Posts
42,872
Reaction score
34,363

Supu/mchuzi wa Kichwa cha Sangara

Moja kati ya mambo ninayomiss sana kuhusu my home town MWANZA A.K.A. THE ROCK CITY ni Samaki.Samaki wanaopatikana ziwa Victoria wana sifa kubwa sana kitaifa na kimataifa.Ukiishi mikoa ya

kanda ya ziwa huwezi jua thamani ya samaki hao adi utoke nje ya mkoa uwakose kwa muda.

Samaki wa maji baridi si kama wa maji chumvi,wanatofautiana ladha na zaidi ya yote wanatofautiana

aina na wingi wa virutubisho.Samaki kwa ujumla ni chanzo kikubwa cha protini na madini mwili,samaki wa maji baridi wana Omega -3 na fatty acids kidogo ukilinganisha na samaki wa maji chumvi,ata ivyo samaki

wa maji baridi ana protini nyingi na mafuta kidogo,pia anamadini mwili kama calcium,madini chuma pamoja na manganese.


Samaki hutumika kama kitoweo kwa chakula cha mchana na jioni kwa familia nyingi.Kwa wakazi wa maeneo ya ziwani samaki huliwa ata asubuhi kama kifungua kinywa kwani hupatikana kwa wingi katika maeneo hayo.


Kichwa cha sangara kina sifa ya kutoa supu au mchuzi mzito,kina mafuta na kwa ujumla ni kitamu.

Kwa miaka mingi kumekua na imani iliyojengeka kwenye makabila ya kanda ya ziwa kwamba ukila kichwa cha samaki unakua na akili nyingi.Watu wengi sana hawakubaliani na imani hii ata kidogo na mara nyingi

nimesikia watu wakiongelea vibaya au kutania juu ya imani hii.

Ukweli ni kwamba,imani yao ni ya kweli na inathibitika kisayansi.kichwa cha samaki hubeba asilimia kubwa ya madini na mafuta mengi kuliko sehem yoyote ya samaki ,mafuta hayo hubeba essential Fatty

acids(Omega -3 na omega-6) na madini mwili aina ya calcium,madini chuma,manganese.Madini haya pamoja na assential fatty acids ni virutubisho muhim sana katika ujenzi na ukuaji kwa ubongo.kilakirutubisho kina kazi yake maalum.Hivyo kwakua wakazi wa kanda ya ziwa hupata virutubisho

hivyo kwa wingi basi ubongo wao hukua vizuri na kuwapa uwezo wa kua na akili zaidi.

Ni vyema kujua kwamba ukuaji wa Ubongo wa mtoto huwa katika kiwango cha juu kabisa ndani ya miaka

miwili ya kwanza ya maisha ya mtoto,hata ivyo virutubisho hivi na vingine vingi huendelea kua muhim katika utendaji na ukuaji wakilasiku wa ubongo.Kwa upande mwingine Akili hukua na kuongezeka sawasawa na akuavyo mtoto.kumbuka tu,endapo ubongo wake ulikua vizuri na unapata virutubisho muhim

ili kuuwezesha kufanya kazi vizuri basi akili yake huwa na uwezo wa kukua na kupanuka kwa haraka zaidi.niishie hapa nisijeingilia fani ya madaktari



Nilipokwenda Mwanza kwa ajili ya christmass mwaka jana,sikufanya kosa,nilikula samaki kwa wingi,na nilianda,nikapika na kula kichwa cha sangara kwa hamu sana.Kuna namna na njia nyingi za kupika na kuanda kichwa cha samaki,nah ii ni namna moja wapo.



Vipande vya sangara tayari kwa kupika

Mahitaji

  • Kichwa cha sangara.kipasue vipande
  • Maji
  • Nyanya
  • Kitunguu maji
  • Kitunguu swaumu
  • Limao au ndimu
  • chumvi

Njia


1.Osha kichwa cha sangara vizuri,zingatia sana mashavu kwani hubeba uchafu mwingi


2.Weka samaki ndani ya sufuria zito,kisha ongeza maji adi yafunike samaki na kuzidi kidogo.


3.kisha ongezamvitunguu maji,vitunguu swaumu,nyanya na chumvi kisha bandika jikoni vichemke kwa muda mrefu na kwa moto wa wastani.moto ukiwa mkali hutapata mchuzi au supu nzuri na wakati kinatokota kichwa kitameguka meguka.


4.Chemsha adi kiive,kisha ongeza limao kabla tu ya kuepua .kama ni kwa ajili ya mtoto usiongeze limao,ila mpe juice ya chungwa baada ya kula mlo wenye samaki.

Wingi wa supu au mchuzi ni chaguo la mpishi,kama unataka supu/mchuzi mwepesi basi hakikisha

umeweka maji mengi zaidi unapoanza kuchemsha,ni vyema upima maji ya kutosha unapoanza kuchemsha ili uepuke kuongeza maji baada ya kuchemka,maji ya nyongeza siku zote huaribu ladha na ubora wa supu na hata mchuzi.


Mambo ndio kama hivyo,Kichwa cha sangara tayari kwa kula,unaweza ukanywa supu yake na kula kichwa bila kusindikiza na chakula kingine,na ukipenda unaweza kutumia kama mboga au kitoweo.

Ipe familia yako chakula bora si bora chakula.
 
Shida Ni Kwamba Ukiendekeza Kula Vichwa Vya Samaki Mchemsho Wake Ambao Ni Mtamu Sana Hukosi Kunuka Kikwapa Tena Kile Kibaya
 
Shida Ni Kwamba Ukiendekeza Kula Vichwa Vya Samaki Mchemsho Wake Ambao Ni Mtamu Sana Hukosi Kunuka Kikwapa Tena Kile Kibaya
mshana jr hiyo yako kali

Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
mshana jr hiyo yako kali

Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums

Farkhina sitanii ni kweli kabisa nilikuwa napenda kula sana michemsho ya vichwa vya samaki daily hasa pale Moroco kuna bar ilikuwa inaitwa Neema nilikuwa na rafiki yangu wakati tukiwa ofisi moja mikocheni
Baada ya muda tukaanza kunuka kikwapa kinachofanana ,binafsi sipendi kunuka napenda kunukia kuja kuchunguza nikaambiwa kama nakula vichwa vya samaki daily niache au nipunguze nikaacha kabisa pamoja na rafiki yangu !!
Farkhina huwezi amini tatizo liliisha mazima !SITANII NI KWELI KABISA na ilikuwa wayback 2004/5
 
Last edited by a moderator:
Farkhina sitanii ni kweli kabisa nilikuwa napenda kula sana michemsho ya vichwa vya samaki daily hasa pale Moroco kuna bar ilikuwa inaitwa Neema nilikuwa na rafiki yangu wakati tukiwa ofisi moja mikocheni
Baada ya muda tukaanza kunuka kikwapa kinachofanana ,binafsi sipendi kunuka napenda kunukia kuja kuchunguza nikaambiwa kama nakula vichwa vya samaki daily niache au nipunguze nikaacha kabisa pamoja na rafiki yangu !!
Farkhina huwezi amini tatizo liliisha mazima !SITANII NI KWELI KABISA na ilikuwa wayback 2004/5

Itabidi nikuamini maana kujaribu hapana mimi

Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums
 
Jamani mimi sijawahi kabisa kula kichwa cha samaki yaani.. Asante mkuu ya pishi la kichwa!
 
Farkhina sitanii ni kweli
kabisa nilikuwa napenda kula sana michemsho ya vichwa vya samaki daily
hasa pale Moroco kuna bar ilikuwa inaitwa Neema nilikuwa na rafiki yangu
wakati tukiwa ofisi moja mikocheni
Baada ya muda tukaanza kunuka kikwapa kinachofanana ,binafsi sipendi
kunuka napenda kunukia kuja kuchunguza nikaambiwa kama nakula vichwa vya
samaki daily niache au nipunguze nikaacha kabisa pamoja na rafiki yangu
!!
Farkhina huwezi amini tatizo liliisha mazima !SITANII NI KWELI KABISA na
ilikuwa wayback 2004/5

Ni kweli! Samaki, Vitunguu maji vibichi vyote vinasababisha hali hiyo na si kwapa peke yake, hata maeneo ya sirini hasa kwa jinsia ke!
 
Ahsante kwa hili pishi. Mi huwa napenda mchemsho wa sato unakuwa plain (naweka chumvi na limao tu labda na mbatata chache sana). Huwa naona sangara ana shombo sana kwa supu, mara nyingi huwa namuweka kwenye foil. labda huwa nakosea kumuandaa. Leo naenda nunua sangara nijaribu pishi lako
 
Ahsante kwa hili pishi. Mi huwa napenda mchemsho wa sato unakuwa plain (naweka chumvi na limao tu labda na mbatata chache sana). Huwa naona sangara ana shombo sana kwa supu, mara nyingi huwa namuweka kwenye foil. labda huwa nakosea kumuandaa. Leo naenda nunua sangara nijaribu pishi lako


Ukimuandaa vizuri plus viungo hutosikia shombo, ila ukikosea tu looh
 
Back
Top Bottom