Thamani ya Legacy dhidi ya Pata potea ya 2025

Thamani ya Legacy dhidi ya Pata potea ya 2025

Nilimpenda sana huyu mama SSH
Nilimsifia sana!
Nilimwona mwokozi wetu mkuu!
Nimekata tamaa nae, washauri wake (ie mawaziri) wanampeleka shimoni!
Haukuwa peke yako na hauko peke yako. Kwa hakika wengi tumebakia tumeduwaa na midomo wazi.
 
Anashindwa nini kuwatoa kama kweli anajua tatizo ndo hilo

Tofauti ya misuli hapo yawezekana si bure:

IMG_20220820_172058_204.jpg
 
Mama Samia alikuwa na muda wote wa kutuwekea misingi imara ya Tanzania mpya yenye haki kamili. Tukawa na Tanzania isiyokuwa na malalamiko. Sote tukajisikia kuwa na haki sawa.

Ajabu na kweli mzuka uliompitiliza wa 2025 umempiga upofu. Haoni wala hasikii.

Haya matozo yanayopigiwa kelele kila kona hata hayamfikirishi? Chawa wake wangapi nguli hawaonekani tena mitandaoni hata kumjibia hoja?

Amepima kuona kama akikwama 2025 au atakapotoka madarakani atakuwa na sifa au hata kuacha legacy gani?

Angeshukuru kwa minne aliyopata na kujielekeza kwenye kuliweka taifa mikononi mwa watu, hata mitano mingine ya haki mbona ingemfuata tu?

Yetu macho, ngoja tuone.
Matatizo hayajawahi kuisha Tanzania na duniani pia. Rais Samia anafanya anayoweza na asiyoweza hakuna haja ya kupoteza muda.
 
Matatizo hayajawahi kuisha Tanzania na duniani pia. Rais Samia anafanya anayoweza na asiyoweza hakuna haja ya kupoteza muda.
Tunayo matatizo makubwa zaidi ya kikatiba yenye kuhitaji ufumbuzi wa haki sasa. Majirani zetu Kenya hapo wamepiga hatua mno.

Makelele unayoyasikia na tozo ni mwendelezo ule wa sera za walamba asali dhidi ya wengine.

Yako mengi ...
 
Kwamba aachane na washauri sio?..awe jeshi la mtu mmoja asiyeshaurika ..Kwa logic yako hii kumbe jpm alikuwa sahihi..kumbe washauri wa nchi hii ni tatizo
Usipopima ushauri unaopewa lazima uingie kwenye shida, wahenga walisema "akili za kuambiwa changanya na zako".
 
Mama Samia alikuwa na muda wote wa kutuwekea misingi imara ya Tanzania mpya yenye haki kamili. Tukawa na Tanzania isiyokuwa na malalamiko. Sote tukajisikia kuwa na haki sawa.

Ajabu na kweli mzuka uliompitiliza wa 2025 umempiga upofu. Haoni wala hasikii.

Haya matozo yanayopigiwa kelele kila kona hata hayamfikirishi? Chawa wake wangapi nguli hawaonekani tena mitandaoni hata kumjibia hoja?

Amepima kuona kama akikwama 2025 au atakapotoka madarakani atakuwa na sifa au hata kuacha legacy gani?

Angeshukuru kwa minne aliyopata na kujielekeza kwenye kuliweka taifa mikononi mwa watu, hata mitano mingine ya haki mbona ingemfuata tu?

Yetu macho, ngoja tuone.
Subiria mda utaongea wewe konokono WA kienyeji.
 
Shaka akiwa Tabora amesema dunia yote inamkubali Mwigulu, sasa naona hiki kikundi cha hawa vijana walevi ni tatizo jipya la wakati huu tuliopo.
 
Tunayo matatizo makubwa zaidi ya kikatiba yenye kuhitaji ufumbuzi wa haki sasa. Majirani zetu Kenya hapo wamepiga hatua mno.

Makelele unayoyasikia na tozo ni mwendelezo ule wa sera za walamba asali dhidi ya wengine.

Yako mengi ...
Kwa hiyo ukipata Katiba kama ya Kenya utakuwa umetatua matatizo yote
 
Kwa hiyo ukipata Katiba kama ya Kenya utakuwa umetatua matatizo yote
Kupungua kwa tatizo moja out of our way? Kwani wewe hukupata kusikia ni heri ya nusu shari?
 
Shaka akiwa Tabora amesema dunia yote inamkubali Mwigulu, sasa naona hiki kikundi cha hawa vijana walevi ni tatizo jipya la wakati huu tuliopo.

Kuna na mwamba mmoja kamsimisha kazi naye kakomaa. Kama nchi kuna shehena kubwa ya wajinga.
 
Kwanza huyo Mama hakutakiwa kuwa Rais in the first place kwa sababu hana uwezo, in knowledge and in practice. Hili liko wazi kwa sababu maamuzi yake anawategemea CHAWA zaidi kuliko akili zake mwenyewe. Chawa kama machemba, kipara au huyu aliyenyooshewa bastola si watu sahihi kwa sababu siyo watu wenye fikra kuhusu Tz miaka 50 ijayo.. hawa ni wachumia tumbo tu..
 
Ngoja tusubiri tuone kama hiyo 2025 atafanikiwa kwenye hiyo dhamira yake.

Ila kwangu mimi niseme tu big No kwa huyu Bi Mkubwa. Siwezi kumpigia kura ya ndiyo.

Kama ana jeshi na tume ya uchaguzi anateua yeye, hahitaji kura hata moja kukaa madarakani. Machafuko tu ndio yataturudisha kwenye mstari.
 
Hutaki kulipa tozo na Kodi halafu unataka maendeleo, kwa Taarifa yako ni kuwa mataifa unayooona yameendelea yalipitia njia hii tupitayo, walitozana Kodi kuzijenga nchi zao, walijifunga mikanda ili kuijenga kesho yao iliyo Bora

Njia ya kupata maendeleo siyo mteremko Wala Tambalale Wala mtelezo, Ni Kama dawa chungu ambayo ukimaliza kuinywa unapona, Sasa hatuwezi tukasema usinywe dawa kwa kuwa Ni chungu wakati tunajuwa hutapona, hii ndio dawa ya kuondoa umaskini, ndio dawa ya kuijenga nchi yetu ikapendeza na kuwa ya mfano


lazzima tujifunge mikanda, lazima tujibane kidogo, lazima tupunguze kidogo katika vipato vyetu ili kupeleka katika kuijenga Tanzania yetu tutakayo jivunia sote
 
Kwanza huyo Mama hakutakiwa kuwa Rais in the first place kwa sababu hana uwezo, in knowledge and in practice. Hili liko wazi kwa sababu maamuzi yake anawategemea CHAWA zaidi kuliko akili zake mwenyewe. Chawa kama machemba, kipara au huyu aliyenyooshewa bastola si watu sahihi kwa sababu siyo watu wenye fikra kuhusu Tz miaka 50 ijayo.. hawa ni wachumia tumbo tu..
Acha dharau unachomzidi ni mapumbu tu ndiyo unaringia. Ungekuwa wewe ndiyo una knowledge usingekuwa hapa JF unalialia hapa
 
Kuna na mwamba mmoja kamsimisha kazi naye kakomaa. Kama nchi kuna shehena kubwa ya wajinga.
Yaani ndugu yangu ukiona nchi inaishia kuwa na taifa la vijana wengi kuishia kuishia kuwa ' machawa na wengine eti kushinda siku nzima kujadili sijui 'madili', mara kujadili bongofleva, kubet na kufanya uchuuzi barabarani, au soga za Simba/Yanga ,badala ya kujadili, kuona na kupanga njia na mikakati sahihi ya leo na kesho ya maendeleo endelevu, kwa mustakabali wa Taifa lao, sasa kwa kweli matokeo yake ndio haya.utaona na safari bado ni ndefu aiseee........... kazi iendelee.
 
Back
Top Bottom