The 2019 NBA Playoffs


Kwenye ushabiki, usichukulie kama kila comment kwamba mtu ana maanisha, no.

Ila ni kwamba kila dongo unaloona karibu unamrushia adui.

Ila kimoyomoyo inakuwa unajua ukweli ni upi!
 
Hongera kwa raptors!
Walistahili huu ubingwa bila kujali gsw wamepatwa na nini. Kiufundi,mbinu za nick nurse zilifanya kazi vizuri kuliko za steve kerr.
Bench palyers wa raptors waliisaidia timu point nyingi ukilinganisha na benchers wa gsw. Hapa inabidi kerr alifanyie kazi hili.
 
Yes hii iko hivyo, sasa wamejikuta wanataka sympathy kutoka kwa kila mtu.

Wakiambiwa hii ni basketball siyo mchezo wa netball wanalia lia. Curry anacheza kama netball.

Nadhani Kawhi kawaonesha jinsi basketball inavyochezwa.
Samahani Broh...
Performance ya Kahwi kwenye hizi finals ipo hivi:
Game 1: 23 pts
Game 2: 34 pts
Game 3: 30 pts
Game 4: 36 pts
Game 5: 26 pts
Game 6: 22 pts
Average pts per game: 28 pts

Tukija upande wa Curry performance kwenye hizi finals ilikuwa hivi:
Game 1: 34 pts
Game 2: 23 pts
Game 3: 47 pts
Game 4: 27 pts
Game 5: 31 pts
Game 6: 21 pts
Average pts per game: 30 pts

Kwa performance za hawa watu wawili nisaidieni,huenda mimi kuchelewa kwangu kuanza kufuatilia huu mchezo kunanifanya mimi nishindwe kuwa mchambuzi mzuri wa huu mchezo...
1) Performance hii ya Curry ni ndogo..?
2) Kipi kinafanya performance ya Kahwi ionekane bora kuliko ya Curry..?
3) Kama GSW wangeshinda,still Kahwi angekuwa finals MVP,kwa kulinganisha performance zao..?
4) Kama Kwa performance Hii still Curry anaonekana kuwa "garbage" when it comes to championship games,unafikiri nini kinapungua kwenye performance za Curry kwenye finals,especially this year championship games..?

Sorry kwa gazeti..!
 

You are not true to yourself, right?

Any day any time, hakuna timu ya kuifunga GSWs kama ikiwa haina majeruhi.

Leo tu kama Klay asingeumia game ilikuwa inaenda kwa GSWs.

Personally najua injuries ndizo zimetupa ubingwa Haters.
 
You are not true to yourself, right?

Any day any time, hakuna timu ya kuifunga GSWs kama ikiwa haina majeruhi.

Leo tu kama Klay asingeumia game ilikuwa inaenda kwa GSWs.

Personally najua injuries ndizo zimetupa ubingwa Haters.
Nimemaanisha mkuu Don Clericuzio ,hongereni na mlistahili sana tu. Bench letu ni dogo/dhaifu ukilinganisha na la mpinzani.

Mfano mzuri ni livingston kwenye hii series hakuwa na impact kabisa,he should have filled klay's shoes if he was in his best form.
 

Mkuu mimi niko kishabiki, usidhani kila nachoponda namaanisha.

Anyway, let's get to business:
Kwenye performance za hao watu weka stats za Assists, Rebounds, Steals na Blocks.

Hii itakusaidia kupata all round player au two way player (means effective on defense and offense) kati yao hao wawili.

Tukija chini hapo:-
  1. Performance ya Curry ni nzuri kiasi, hizi finals alikuwa mzuri kupita finals zote alizocheza.
  2. Kawhi anambiti Curry kwa sababu kwamba yeye ni 2-way player, anaweza kucheza defense na anafunga vile vile. Curry ana disadvantage ya umbo kiasi kwamba kupambana na bigmen kwenye D ni ngumu. Kawhi alishawahi kuwa DPOY na always anakuwa kwenye NBA Defense Teams, Curry hajawahi kuingia hata mara moja.
  3. Angeweza kuchukua, lakini hii ni myth, ni kujadili kitu ambacho hakina uhalisia.
  4. Performance hii ilikuwa ni nzuri, unajua punda anayekaribia kufa teke lake linaumiza kuliko yule mzima? Maana yake ni kwamba Curry amepafomu sana kwa sababu ilikuwa ni kujaribu kujiokoa na kifo.
Pamoja mkuu.
 

Ukiwa na First Team ambayo wote ni All Stars ni ngumu kuwa na bench kubwa kwa sababu ya Salary Caps. Mishahara mingi inakuwa imechukuliwa na starters, unajikuta unabaki na bench ambalo ni average.
 
Mkuu,hiyo point namba 2 nadhani ni sababu za kimaumbile na si kiufundi hivyo hutakiwi kumuhukumu kwa hilo. Hebu nijuze ni mchezaji gani mwenye kimo kama chake anayefanya vizuri defensively.
Curry ni finals material ndio maana NN alimwekea defense ya watu 2 kila alipopata mpira,same as kawhi kwa gsw.
 

To me, Curry is not NBA Finals Material until when he becomes NBA Finals MVP.

My materiality threshold to him is Finals MVP.
 
Ukiwa na First Team ambayo wote ni All Stars ni ngumu kuwa na bench kubwa kwa sababu ya Salary Caps. Mishahara mingi inakuwa imechukuliwa na starters, unajikuta unabaki na bench ambalo ni average.
Don, you've just explained NBA league situation in as simple term as a 5 year old can understand. Word, mate.
 
Na mnaniweza kwelikweli yaani..!
Ukitaka povu linitoke,uwakandie Eminem na Steph Curry,I'm half Stan to these guys..!
Kama kule kwenye uzi wenu wa Liverpool,kuna jamaa ukitaka kumtibua basi wewe mkandie Henderson..!

Ushabiki kwenye hii michezo ni kitu cha ajabu sana, hakuna anayetaka mchezaji wake pendwa au timu iwe criticised.

Wengine kama mimi huwa nachagua weak point natafuta points za kuitetea.

Nikiona adui anaanza kuwa emotional najua huyu tayari.
 
Mfano mzuri ni livingston kwenye hii series hakuwa na impact kabisa,he should have filled klay's shoes if he was in his best form.
Unataka kumwonea tu Livingston! Na uzee wote huo? He had a deadly jumper kabla ya injury iliyomwaribia hadi leo.
 
Na mnaniweza kwelikweli yaani..!
Ukitaka povu linitoke,uwakandie Eminem na Steph Curry,I'm half Stan to these guys..!
Kama kule kwenye uzi wenu wa Liverpool,kuna jamaa ukitaka kumtibua basi wewe mkandie Henderson..!
Hahaha there we share our appreciation for Em
 
Mkuu BAK naangalia First take kuna jamaa anasema kwamba People are afraid to criticize Steph Curry cause he is a golden boy. Anasema Steph can not close out games, he can't take the final shot. Anasema he scored the most meaningless 47 points in game 3 [emoji16]. Naomba msaada wako ku upload hiyo clip mkuu BAK cc Dan Clericuzio. Its exactly what you have been saying @DonClericuzio [emoji16]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…