The Best FIFA Football Awards 2019: Messi atwaa tuzo ya Mchezaji bora, Klopp awa Kocha bora

Greatest Of All Time

JF-Expert Member
Joined
Jan 1, 2017
Posts
23,620
Reaction score
52,790
Saa 2 za Usiku kwa Masaa ya Afrika ya Mashariki, kutakuwa na hafla ya utoaji wa tuzo ya Mchezaji bora wa FIFA kwa mwaka 2019 pale jijini Milan nchini Italy.

Pia hafla hiyo itaambatana na utoaji wa tuzo ya mchezaji bora kwa wanawake.

Vilevile kutakuwa na tuzo ya goli bora la mwaka, kocha bora wa mwaka pamoja na kikosi bora cha mwaka.

Kwa mchezaji bora wa mwaka 3 bora ni Messi, Ronaldo na Van Dijk ambaye anapigiwa chapuo kubwa ya kuibuka na tuzo hiyo.

Mimi ningepata nafasi, kura yangu ningempa Van Dijk. Wewe kura yako ungempa nani?

Tukutane pale Milan nchini Italy kuanzia saa 2 usiku kwenye king'amuzi cha Dstv.




 
Kaliodou koulibaly.
 
Bernado Silva amebeba - EPL, FA CUP, LEAGUE CUP na hilo kombe la UEFA ulilolisema tena yeye akiwa ndie mchezaji bora wa mashindano nani anastahiki zaidi?
dah mkuu haya mambo kwanza tuwaachie wenyewe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…