Mdakuzi
JF-Expert Member
- Apr 6, 2012
- 4,294
- 6,872
Na Herieth Makwetta
Mwanamuziki Hamis Mwinyijuma, maarufu Mwana FA amepata wakati mgumu kwa kulazimishwa na mashabiki kutaja jina la Lady Jay Dee baada ya kuliruka jina hilo alipokuwa akiimba wimbo wa Mabinti ambao ndani yake kuna jina la Lady Jay Dee.
Tofauti na ilivyozoeleka katika wimbo wa Mabinti, kwa mara ya kwanza Mwana FA aliruka jina la mwanamuziki Lady Jay Dee 'Anaconda' hali iliyowafanya mashabiki wamtake arudie tena na kutenda haki.
Mwana FA alisita kwa muda na baadaye aliamua kuurudia wimbo huo na ilipofikia kipengele cha kumtaja Jide aliimba kwa kumtaja, hali iliyoufanya ukumbi ulipuke kwa shangwe na mashabiki kumtaka arudie tena na tena.
Kutokana na hilo FA aliamua kufunguka, "Tunaishi na watu hivyo lazima mtagongana, hata mapacha wanakosana na kusameheana, lakini wakati mwingine shida inawafanya mnapata," alisema Mwana FA.
Awali shoo ilitangazwa kuwa ingekuwa ya watu 400 tu. Lakini mpaka inafika saa nne kasoro usiku, muda uliotangazwa kuanzwa kwa shoo hiyo watu waliokuwa wamefika walikuwa 250 tu.
Saa nne kamili mwanamuziki Hamis Mwinyijuma, Mwana FA alikanyaga 'red carpet' akiwa na mbunifu wa mavazi Sheria Ngowi, na baada ya kuchukuliwa picha kadhaa alianza kuelekea nje ya ukumbi katika sehemu waliyosimama watu wakipata chakula na vinywaji, watu walizidi kufurika lakini kila aliyeingia alikuwa alwatan kidogo.
Waliendelea kuwasili mastaa na shoo inaanza mashabiki wanaanza kuingia ukumbini saa tano kamili baada ya kupata chakula na vinywaji nje, huku muziki wa taratibu ukipigwa na bendi ya muziki wa dansi ya Njenje.
Mashabiki wanaendelea kubadilishana mawazo mpaka inapotimu saa tano na robo usiku, ambapo Mwana FA anapanda jukwaani.
Chanzo: Gazeti la Mwananchi
Mwanamuziki Hamis Mwinyijuma, maarufu Mwana FA amepata wakati mgumu kwa kulazimishwa na mashabiki kutaja jina la Lady Jay Dee baada ya kuliruka jina hilo alipokuwa akiimba wimbo wa Mabinti ambao ndani yake kuna jina la Lady Jay Dee.
Tofauti na ilivyozoeleka katika wimbo wa Mabinti, kwa mara ya kwanza Mwana FA aliruka jina la mwanamuziki Lady Jay Dee 'Anaconda' hali iliyowafanya mashabiki wamtake arudie tena na kutenda haki.
Mwana FA alisita kwa muda na baadaye aliamua kuurudia wimbo huo na ilipofikia kipengele cha kumtaja Jide aliimba kwa kumtaja, hali iliyoufanya ukumbi ulipuke kwa shangwe na mashabiki kumtaka arudie tena na tena.
Kutokana na hilo FA aliamua kufunguka, "Tunaishi na watu hivyo lazima mtagongana, hata mapacha wanakosana na kusameheana, lakini wakati mwingine shida inawafanya mnapata," alisema Mwana FA.
Awali shoo ilitangazwa kuwa ingekuwa ya watu 400 tu. Lakini mpaka inafika saa nne kasoro usiku, muda uliotangazwa kuanzwa kwa shoo hiyo watu waliokuwa wamefika walikuwa 250 tu.
Saa nne kamili mwanamuziki Hamis Mwinyijuma, Mwana FA alikanyaga 'red carpet' akiwa na mbunifu wa mavazi Sheria Ngowi, na baada ya kuchukuliwa picha kadhaa alianza kuelekea nje ya ukumbi katika sehemu waliyosimama watu wakipata chakula na vinywaji, watu walizidi kufurika lakini kila aliyeingia alikuwa alwatan kidogo.
Waliendelea kuwasili mastaa na shoo inaanza mashabiki wanaanza kuingia ukumbini saa tano kamili baada ya kupata chakula na vinywaji nje, huku muziki wa taratibu ukipigwa na bendi ya muziki wa dansi ya Njenje.
Mashabiki wanaendelea kubadilishana mawazo mpaka inapotimu saa tano na robo usiku, ambapo Mwana FA anapanda jukwaani.
Chanzo: Gazeti la Mwananchi