The Greatest JF intelligent man

Sasa hapa utapata nafasi ya kuongea na watu walioishi na Nyerere na kwenda Ikulu na kumuomba tausi mmoja tumchukue tuende naye nyumbani, na Nyerere akalifikiria jambo hilo na kucheka.

Watu ambao tumempiga ngumi mtoto wa Mwinyi darasani, kwa sababu kaja na kuturingishia shilingi moja mpya yenye picha ya baba yake na wengine tulikuwa hatufagilii mtu kujifanya mtoto wa rais darasani, tukamwambia "kama baba yako rais ni huko huko nyumbani kwenu, hapa darasani, wote wanafunzi sawa, chukua ngumi hiyoo".

Na wala hatukufanywa kitu na Mwalimu yeyote.

Egalitarianism. Look that up if you do not know the meaning.

Hizo ndizo enzi hizo ninazosema Nyerere alijenga a semblance of a classless society.

Sasa ukimlaumu mzee wa watu kashatangulia mbele ya haki, ukimlaumu kwamba alitaka kuwa confuse elite class kwa Kiingereza, nitakuona humjui Nyerere. Kwa sababu Nyerere kiukweli kabisa alitaka kujenga a classless society. Kama alishindwa ni kwa sababu ya dynamics za kiuchumi na kisiasa, si kwa sababu ya kukosa nia.

Sasa nikiona unataka kumlaumu huyu babu - ambaye ana mengi sana ya kulaumiwa- kwa sababu ya kwamba alitaka ku confuse elite class, wakati yeye mwenyewe hakuamini katika elitism, nakuona hujamuelewa bado. Labda tuliokuwapo enzi zake tukueleweshe.

Leo mtoto wa kapuku akimpiga ngumi mtoto wa rais kama nilivyompiga mimi mtoto wa Mwinyi sijui itakuwaje!

Uzuri wa JF ni kwamba kuna vijana wanamsoma Nyerere kama legend aliyefariki na wengine tushamuomba Nyerere tuchukue tausi Ikulu tuwapeleke nyumbani wakati hatujui kwamba tausi ni nyara za taifa ambazo hazitakiwi kuchukuliwa nje ya mamlaka ya Ikulu.
 
Nimemwambia kwamba Mama yangu, Mr. Sozigwa, Miss Wickens na Mwalimu Nyerere walifanya kazi Ikulu ya Nyerere pamoja.

Na bado ana assume kwamba nimesoma middle school na Nyerere?

Is this chap being poetic or what?
 
Nimemwambia kwamba Mama yangu, Mr. Sozigwa, Miss Wickens na Mwalimu Nyerere walifanya kazi Ikulu ya Nyerere pamoja.

Na bado ana assume kwamba nimesoma middle school na Nyerere?

Is this chap being poetic or what?

Si ajabu atakuwa ni dogo wa 90s huyo.

Na ukianza kuongelea mambo ya tausi wa ikulu sidhani hata wanaelewa unachokiongelea.
 
Mea culpa!
You are on "Anger Management" tour as part of a mental health outreach initiative.

4 weeks.

Upon a successful completion, seeing that you are bent on hygiene, you will get a $200 reward towards a hygiene product of your choice (cologne house etc).

Failure to do so will not only chalk you up as an unreliable polymer, but one that is also not fun.

Almost a failed Scott academic living out his life in a grotesque stupor of a thinly disguised hedonism, that is really very a very accomplished nihilism.

Which is it now?
 

Hahahaa....I don't even know what to say.

Your jawbreaking, sesquipedalian-ish vocab is blinding.

It's like I'm reading a piece of prose right out of the New England Journal of Medicine.

I can't hang with you, man. I'm not Alan Dershowitz nor Michael Eric Dyson and I'm far from brother Cornel West....
 
He's just a translator, We can see him brilliant or intelligence just because we don't have a habitual of reading different article or books, But for the people who interested on reading it's nat a big deal for them, All in All he's good on planning Stories and all audiences we are enjoying good writing from Him, keep it up
 
Nimemwambia kwamba Mama yangu, Mr. Sozigwa, Miss Wickens na Mwalimu Nyerere walifanya kazi Ikulu ya Nyerere pamoja.

Na bado ana assume kwamba nimesoma middle school na Nyerere?

Is this chap being poetic or what?
Mkuu nimekuelewa hujasoma middle school. Pia sidhani wote waliosoma middle school walisoma na Nyerere.
Nimekuelewa na shukrani kwa gist of info. Kuhusu Nyerere, na watoto wa AHMwinyi.
 
Stepping aside from him, and centering on that "translator" idea.

Kuna watu nishagombana nao hapa kwa sababu nimewaambia kwamba hawawezi kubishana na mimi kwa sababu nimesoma kazi za Lord Bertrand Russell na wao wameishia kwenye kazi za Lord Jesus.

Kwa sababu hawajui Kiingereza!

Si kwa sababu Kiingereza ni usomi au kina upawa zaidi ya Kiswahili, hasha, nishasema hpo juu Kiingereza kama lugha ni dhalili ukikilinganisha na Kiswahili.

Lakini kimepata kuwa, kwa sababu moja au nyingine, kibiashara, kishistoria, kisiasa etc, kuwa kama alivyosema Nyerere, "Kiswahili cha dunia". Kuna mambo ambayo Kiswahili hata maneno yake hatuna, yameandikwa Kiswahili.

Unapotaka kumueleza mtu katika Kiswahili kwamba huna "multiverse" au "boson particle", utatumia maneno gani?

Sasa kwa mtu asiyejua Kiingereza, hata ukimtafsiria "Hegelian dialectic" kama televisehni ya Zanzibar enzi hizo kwa kusema "Mapinduzi Daima" (wangapi wanakumbuka hili?) utakuwa ushamvusha mto mkubwa wa kufikiri mambo yako bila mapinduzi.
 

Kiswahili ni lugha nzuri na iliyo tamu sana.

Na ni moja ya lugha zilizo rahisi kujifunza.

Tatizo moja kubwa nilionalo mimi ni ukosefu wa taasisi imara za kukikuza.

Baadhi ya watu hudai Kiswahili hakijitoshelezi kimsamiati kama ambavyo Kiingereza kinavyojitosheleza.

Hiyo dhana sikubaliani nayo. Ni dhana potofu.

Kiingereza kimeazima maneno hadi kwenye Kiswahili! Huko kwenye Kilatini ndo usiseme kabisa.

Kila mwaka taasisi za lugha ya Kiingereza huingiza maneno mapya kwenye kamusi zake.

Kwenye Kiswahili sijawahi kuliona hilo.

Sasa kwa mfano kama maneno flani ya Kiingereza hayapo kwenye Kiswahili kwa nini tusiyaazime na tukayaswalihisha tu ili nasi tuwe nayo?

Mbona mengine tumeyaswalihisha? Polisi tumeliswalihisha...hospitali tumeliswalihisha.....shule tumeliswalihisha...na mengineyo mengi tu tumeyaswalihisha.

Sioni kwa nini tusiyaswalihishe na hayo mengine ambayo hatunayo kwenye msamiati kwa sasa.

Waingereza hadi neno 'safari' wameliazima na kuliingiza hadi kwenye kamusi zao.

Hata sisi naamini tunaweza kufanya hivyo hivyo kwa yale ambayo tunaona hatunayo.
 
Kuna wahafidhina wanasema kuswahilisha kama ulivyokuita (kutohoa) ni kuchafua Kiswahili.
 
Kuna wahafidhina wanasema kuswahilisha kama ulivyokuita (kutohoa) ni kuchafua Kiswahili.

Actually kuswalihisha ni neno kabisa la Kiswahili.

Hao wahafidhina basi watakuwa ni wajinga wa lugha ya Kiswahili maana Kiswahili ni mseto wa lugha kadhaa na maneno yake mengi yametoka kwenye lugha zingine.

Polisi, rais, wilaya, dunia, shule, baba, kwa mfano tu, ni maneno yaliyoazimwa na kuswalihishwa.

Sasa hao wahafidhina sijui wanazungumzia Kiswahili gani hicho!!
 
Najua, najua.

Wanasema kwamba Kiswahili kimejawa na maneno ya kutohoa (au kwa Kiswahili kingine Kuswahilishwa) mpaka asili yenyewe inapotea.

Na huu mjadala si wa Kiswahili tu.

Kwa yeyote aliyekisoma Kiingereza cha ndani cha kina Churchill na hata zamani zaidi, atajua na kuona hawa kama walikuwa na nafasi ya kutumia neno lenye mizizi ya "old English" au neno jipya la kutohoa kutoka Kilatini, walichagua neno la "Old English".

Kwa hivyo huu si mjadala mpya wa Kiswahili tu.

Hata Kiingereza kilishakuwa na mjadala huu.

Wangapi wanajua hilo?
 
andika kiswahili boya wewe mwenzio kaandika kiswahili.......sasa mtu anakuongelezea kichagga we unamjibu kikurya dah the most intelligent man in JF hahahahaha
 
Si ajabu atakuwa ni dogo wa 90s huyo.

Na ukianza kuongelea mambo ya tausi wa ikulu sidhani hata wanaelewa unachokiongelea.
Kuhusu tausi wa ikulu. Umenikumbusha mbali sana. Tulipata kuishi jirani na mtu aliyesemekana kuwatunza hao tausi wa ikulu.
 
Kuhusu tausi wa ikulu. Umenikumbusha mbali sana. Tulipata kuishi jirani na mtu aliyesemekana kuwatunza hao tausi wa ikulu.

Wakati nipo dogo nilikuwa naenda hapo kucheza na au niseme kuwatazama huku nikimsubiri maza atoke kazini turudi nyumbani.

Nilikuwa nawaona ni kivutio kizuri sana.

Siku hizi sijui hata kama wapo tena.
 
Mkuu nilipata nafasi ktk harakati zangu kujadili nguli mmoja wa social linguistics duniani hiyo kauli ya Nyerere

"Kingereza ni Kiswahili cha dunia"

Aliniambia Nyerere in UK land while speaking that, and he could have said differently when in Africa.
 
Taasisi hazina meno. Tataki (udsm) wanajitahidi kidogo wametafsiri vitabu kadha wa kadha shida inakuja utumizi wa kiswahili uko limited sana ktk elimu. Siku itakapotumika kama lugha ya kufundishia sekondari itakuwa vizuri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…