The Greatest Man in Universe: Kijana mdogo aliyefanya makubwa na kuacha alama akiwa na umri mdogo

The Greatest Man in Universe: Kijana mdogo aliyefanya makubwa na kuacha alama akiwa na umri mdogo

Pamoja na kuishi bila shari na mtu akasalitiwa na bwana Yuda Eskariote na wenzake wachache kisha Pilato akatoa hukumu ya akasulubiwa akafa kisha akapaa mbinguni

Mwandishi ni pepo au nani.

mbona humalizii maandiko.

Kwenye uzi wako unasema alikufa.;


hapa tena unasema alikufa then akapaa mbinguni,


SEMA WALIMSURUBISHA, AKAFA, AKAFUFUKA NA KUPAA MBINGUNI.


unakosea wapi nduguuuuu!
 
Mwandishi ni pepo au nani.

mbona humalizii maandiko.

Kwenye uzi wako unasema alikufa.;


hapa tena unasema alikufa then akapaa mbinguni,


SEMA WALIMSURUBISHA, AKAFA, AKAFUFUKA NA KUPAA MBINGUNI.


unakosea wapi nduguuuuu!
Huwezi kukosoa kwa hekima?
 
Huwezi kukosoa kwa hekima?
Ok sorry! Very sorry.


Ila mbona umeandika vizuri sana . Umekosa tu kitu hicho halafu hata unapowajibu wengine ni kama sio mtafiti kwa sababu ya kutokukamilisha nguzo za ujio wa Yesu Kristo.

Msingi mkubwa wa Yesu unapomuelezea ni muhimu kuaininisha alizaliwa sio kwa kawaida, alikufa sio kwa kawaida na alilifufuka na kicha akapaa mbinguni.

unajua unapomtaja Yesu (unataja ukombozi yaani Kuzaliwa,kufa na kufufuka kwake).
 
Ok sorry! Very sorry.


Ila mbona umeandika vizuri sana . Umekosa tu kitu hicho halafu hata unapowajibu wengine ni kama sio mtafiti kwa sababu ya kutokukamilisha nguzo za ujio wa Yesu Kristo.

Msingi mkubwa wa Yesu unapomuelezea ni muhimu kuaininisha alizaliwa sio kwa kawaida, alikufa sio kwa kawaida na alilifufuka na kicha akapaa mbinguni.

unajua unapomtaja Yesu (unataja ukombozi yaani Kuzaliwa,kufa na kufufuka kwake).
Upo sahihi kiongozi wangu.. nikiri hapa kua nimekosea kutotaja matendo matati haya makuu aliyoyafanya Kristo, lakini msingi wa mada hii ni kumzungumzia yesu yule ambae ni mtu. (To the matter of fact nimekosea kutitaja utatu huo )
 
Karma mimi nilikua namweliezea Yesu yule mwanadamu ila angalia watu walivyonipiga mawe.. sijui hawaelewi sentesi.. Mungu aliyejifanya mtu
 
Salute
Mnamo mwaka wa 4BC jijini Galilaya katika kitongoji kiitwacho Nazareth kulikuwa na familia ya Bw. Joseph na mkewe Maria; walipata mtoto wa kiume wakamwita Jina Yeheshua au Yesu.

Ilikua ni moja ya kaya ya kimaskini, Bw. Joseph alikua anajishughulisha na shughuli za uchakataji wa mbao yaani useremala pia mkewe Bi. Maria alikuwa anajihusisha na shughuli ndogo ndogo za mikono. Yesu alifundishwa kusoma na kuandika tu maana wazazi wake hawakuweza kumudu gharama za kumpeleka shule zaidi, lakini alisoma pia masomo ya dini kwa walimu wa kiebrania waitwao “Rabi”. Kijana huyu alikuwa akisaidiana na baba yake kufanya shughuli za uchakataji mbao.

Alipotimiza miaka 30 kijana huyu ndio nyota yake ya mafanikio ilipoanza kung’aa, alianza kazi zake za kufundisha watu kama “Rabi” mambo mbalimbali yahusiyo falsafa ya maisha. Alifundisha kwa muda wa miaka mitatu tu, so alipokua na miaka 33 alifariki dunia kwa kuwambwa msalabani na dola ya Rumi iliyokua inatawala nchi nyingi kipindi hicho.

Kosa lake lilikua ni uhaini kwa kujiita mfalme wakati nchi hiyo ilikuwa ina mtawala ambaye ni Herode na Gavana Pilato wakiwa chini ya mtawala Kaisari Tiberius, pia kuweka maandamano yasiyo na kibali.

Japo aliishi miaka 33 na kufanya kazi yake kama rabi kwa mmuda wa miaka 3 aliweza kufanya mengi makubwa ambapo mpaka leo hii ulimwengu hautamsahau kamwe. Japo kafariki takribani miaka 2000 iliyopita lakini kila siku wafuasi wake wanazidi kuongezeka, hapo zamani kulikuwa na watu mashuhuri na maarufu wengi sana waliofanya mambo mengi kama vile Mose, Imhotep, Caesar Augustus, Archimedes, Pharaoh Rammiress II, Socrates, Spartacus, Leonidas, Plato, Alexander the Great, Aristottle, Ibrahim, Nebucadnezar na wengineo wengi. Lakini kijana mdogo sana ndani ya miaka mitatu tu aliweza kuvunja rekodi za watuwote hao mashuhuli na kubaki yeye ndiyo kinara.

Miaka imepita lakini mpaka leo hakuna mtu ambaye ameweza kuvunja rekodi yake, anafahamika kama mwanafalsafa, mtabiri na mwanasayansi nguli aliyewahi kuishi na hatokuja kutokea kama yeye.

Vitabu vyenye mafundisho yake ndio vinaongoza kuuza kuliko vyote, ni binaadamu ambae jina lake linazidi kukua kila siku badala ya kufifia japo ni miaka 2000 imepita. Wafuasi wake wengi wamekuja kuwa ni watu mashuhuri na wanafalsafa wakubwa kama vile Paulo, Thomas aquinus, Francis of Assis, Ignatus Luyola, St Luke, Francis Xvery, John Paul II, nk.

Kaacha miongozo ambayo ilikuja kutengeneza taasisi kubwa yenye nguvu na washirika wengi ambayo ni Catholics. Inaonyesha watu wengi mashuhuri duniani wamepita kwenye taasisi hii au ni wafuasi wa mafundisho ya huyu kijana mdogo. Yeye ndiyo binaadamu zaidi maarufu ulimwenguni. Kaacha historia ambayo haiwezi vunjwa maisha yote maana jina lake limeshindwa kufutika. Hebu fikiria kama alifanya mambo yake kwa muda wa miaka 33 tu ila umaarufu wake unazidi kukua na wafuasi wanazidi kuongezeka siku baada ya siku.

Wakuu mimi kiukweli namuonea sana wivu huyu kijana, haiwezekani kwa muda wa miaka 20+ niliyoishi hapa duniani sijawahi kufanyiwa Happy birthday, sidhani kama kuna mtu mwingine tofauti na mama anayekumbuka siku yangu ya kuzaliwa. Lakini kijana mdogo aliyekufa miaka mingi sana iliyopita karibia dunia nzima wanajua siku ya kuzaliwa kwake na hua wanasherhekea nyumbani huwa wanapika wali kabisa na kuchinja yule mbuzi mnene tuliemchunga muda mrefu halafu mimi first born kwenye kumbukumbu yangu ya kuzaliwa sijawahi pewa hata andazi.

Kinachoniumiza zaidi najua siku nikifa tu watu watanisahau mara tu baada ya kutandua msiba wangu, sitakumbukwa na yoyote kama yesu tunavyomkumbuka labda nyie wa huku JF mtanikumbuka kwa posts zangu.

Kiukweli mimi sikubali, kwanini Yesu atushinde watu wote wakati alikuwa binadamu sawa kama sisi? Tunakosea wapi? Kweli tumeshindwa kuvunja rekodi zake nasi basi tukumbukwe hata kwa muda wa miaka 10? Lakini je, huyu kijana mdogo alifanyaje hadi akaweza kufanya mambo makubwa yote haya ndani ya muda mdogo?

Maneno yote huko juu ni kuonyesha jinsi huyu kijana alivyoweza fanaya mambo mengi ndani ya muda mchache lakini kubwa la msingi ni kujua je aliwezaje? Alitumia nini?

Yesu aliwezaje?

Ukichunguza utajua kabisa huyu mtu alikuwa ana vitu anafanya ili kutimiza mipango yake hiyo yenye matokeo makubwa. Yesu alitumia vitu vitatu ili kufanya yote hayo. Kwanza kabisa alikua anajtambua (nilishaliongelea hili), pili alikuwa anafahamu kusudi lake (nitaliongelea hili panapo majaliwa) tatu alijali muda kuliko kitu chochote. Yes! Hapa ndiyo kwenye kiini cha mada yetu; Time Management. Jinsi nidhamu nzuri ya matumizi ya muda inaweza kukuletea mafanikio makubwa.

Japo Yesu hakuwa na elimu kubwa lakini alijitambua na alitambua kusudi lake mapema mno ndiyo maana alitumia muda wake vizuri sana akaweza kufanya mambo mengi makubwa. Alithamini muda wake alifanya kazi yake kwa nidhamu ya hali ya juu muda ukiwa ndio silaha yake kuu.

Kuna mtu aliwahi muuliza The Godfather Mwl. Julius Nyerere kwamba anawezaje kufanya mambo mengi kama vile kuhudhuria vikao, kuwa na familia yake, kuandika vitabu na makala kwenye magazeti, kuongoza nchi, kufanya ziara n.k kwa wakati mmoja? Nyerere alisema yeye anaheshimu muda. Muda wa kula anakula tu, muda wa kikako anakua kikaoni, kutembea anatembea tu, muda wa kulala analala tu n.k n.k

Najua humu wengi wetu hili ni ngumu sana. Unakuta mtu yupo anatembea kwenda mahali fulani lakini muda huohuo anasimama kuchat, muda wa kulala yeye anasoma kitabu, muda wa kusoma yeye anakula, muda wa kula ndiyo kwanza anaanza kuongea na simu, muda wa kazi yeye anaingia JF, muda wa kutafuta watoto yeye anapiga stori na mwenzi wake.

In short, muda hatuuthamini hasa huku kwetu Afrika, ndiyo maana Wachina wanatuendesha sana na tunaona kuwa wanatunyayasa huko makazini maana wao wamekulia kwenye malezi ya kufanya kitu kutokana na muda unaruhusu kufanya nini, sasa ile silka yao wakiileta huku twaona hawa watu wapo kama mashetani.

Kijana amka jali muda wako ulionao. Kwani nyie wenzangu hamumuonei wivu huyo jamaa huko juu aliyefanya mambo mengi ndani ya muda mfupi? Moja kati ya utajiri mkubwa binaadamu alionao ni muda.

Kama umefanikiwa kuwa na leo basi wewe ni tajiri mkubwa, leo hii ndio muda wako amka ukafanye yale unayotamani kufanya. Usisubiri kesho, kesho haipo siku zote ipo leo tu! Achana na kupoteza muda wako kwa kwenda location kupiga picha za kupost Facebook upate like 300, unadhani siku ukifa kuna mtu atakukumbuka kwa kuacha picha zenye like nyingi na quality nzuri huko FB? Sahau hili.

Yesu alijitambua mapema ndiyo maana aliweza fanya mambo makubwa, jitambue kijana mwenzangu hautakumbukwa kwa kuweza kutaja kikosi kizima kinachocheza ligi daraja la tatu huko Italy au England. Tumia muda wako huu ulionao leo kwa kufanya mambo yatakayoacha alama isiyofutika hapa duniani.

Huyo ndio Yesu the Greatest man, hakuna mtu mwingine kama yeye, hakuna atakayeweza kuvunja rekodi zake alizoacha sana tunaweza fuata matendo yake ili kufanya mambo makubwa kwenye maisha ila kumpita tuache legacy kubwa kuliko yeye haitawezekana kamwe.

Tujali muda jamani, ipo siku tutajutia huu muda tuanaopoteza kufuatilia mwanamke mmoja miezi sita halafu kila siku unatumia zaidi ya masaa 4 kuwasiliana nae wakati muda huo ungefanya mambo mengi ya msingi ndani ya miezi hiyo 6 yakamfanya huyo mwanamke akajileta mwenyewe.

Utajiri wetu mkubwa sisi watoto wa maskini ambao tunaweza kuutumia kupunguza kiwango cha umaskini kwenye familia zetu kama Yesu alivyofanya kwenye familia yetu ni MUDA. Jali muda utakutunza uzeeni.

JE WEWE BINAFSI NI NANI UNAONA NI GREATEST MAN ALIYEFANYA VITU VIKUBWA AMBAE TWAWEZA KUJIFUNZA KUPITIA YEYE?
Ahsanteni.
Like & Share

Da’Vinci
El maestro.
Yesu aka Yeheshua au Joshua alikuwa msomi wa ngazi ya digrii ya juu sana. Licha kwamba alizaliwa kama binadamu mwingine Roho yake ilikuwa kamilifu, wanazuoni wa elimu ya nyota na tabiri (Mamajusi) kutoka mashariki ya mbali walitabiri uzaliwaji wake, ambao ndio waliwajulisha Wayahudi juu ya matajio ya kuzaliwa kwa Roho tukufu ya Yesu katika nchi ya wayahudi, walipitiliza pale waliposema atakuwa Mfalme kitu kilicho mchonganisha na Mtawala wa wayahudi wakati huo Helode, kumtambulisha kuwa atakuwa mfalme kwao haikuwa makosa kwani kwa tamaduni zao huko mashariki ya mbali huwa mwenye high spiritual attainment ndio alikuwa anakuwa kiongozi, waliona kuwa kwa ukuu wa utukufu wa Roho ya Yesu waliona alifaa hata kutawala dunia nzima, wasijue kuwa itaibua mtafaruki mkubwa kwenye utawala wa Helode mpaka kuibuka njama za kutaka kumuuwa. Helode aliwapa zawadi wampelekee mtoto Yesu ili baada aweze ku trace mahali alipo ili aje kumuuwa. Akitegemea kuwa wale Mamajusi baada ya kumuona na kumkabidhi zawadi wangerudi kwake na kumhabarisha alipo Mtoto Yesu.

Waligundua njama za Helode hivyo hawakurudi kwa Helode bali waliwataharisha wazazi wa mtoto Yesu na kuwashauri wamtoroshe, lakini pia walingia makubaliano na wazazi kuwa Yesu anahitaji kuelimishwa na wao juu ya kusuduo au sababu za kuzaliwa wake, hivyo wamtaka Joseph, awapelekee mtoto pindi afikapo umri wa kwenda shule na wao watamsomesha bure katika chuo chao. Yesu akiwa mtoto alitoroshewa Misri, baada ya kifo Helode walirudi na kama ilivyokuwa kwa taratibu za wayahudi mtoto alipelekwa kusomea dini ya kiebrania kwa ma Rabi (kama ilivyo kwa waisilamu mtoto huenda Madrasa). Yesu alikuwa muelewa kiasi cha kuwabishia walimu wake. Alipofika miaka 12 historia inonyesha Yesu alitoweka na kurudi tena akiwa na miaka 30 akiwa na elimu ( spiritual knowledge ya ngazi ya juu ya kimashariki) ambayo ilipingana kabisa na ile ya Kiebrania. Alishindwa hata kuhudumu kwenye Masinagogi, alifundisha vitu vilivyopingana na mila na desturi za kiyahudi, waliokuwa wanaishi kwa kufuata amri kumi za Mungu walizopewa na Nabii Musa.

Mapingano ya Mafundisho yake na Mafalisayo na Makuhani yaliopelekea kuwa kama muhaini;-

1. Kwenye Amri kumi kuna amri inayotoa katazo la kutokuitaja jina la Mungu, Yesu alijitanabaisha kuwa yeye ni Mwana wa Mungu. Haikuwaingia akilini kuwa mtoto waokuwa wanamuona akimsadia baba yake kama selemala msaidizi eti baada kutoweka kwa muda na kurudi ghafla anajimwambafai kuwa ni mwana wa Mungu wanapaswa kumuheshimu na kumuogopa, kwanza walimchukulia kama mtu aliyechanganyikiwa na kuwa ni kichaa wakamdharau.

2. Wakati kuna katazo la kutofanya kazi yeye alitenda matendo ya uponyaji siku ya sabato.

3. Aliweza fanyafujo mahekaluni kama kupindua meza na kuwatawanya waumini mahali wao walipatambua kuwa ni patakatifu.

4. Katika makutano na mafundisho yake hakuwa na mfumo Dume. Wayahudi wanaamini dhambi imeletwa na Eva(Hawa) hivyo mwanamke alitengwa hata kwenye ibada, au jumuishi mbalimbali, hakusikilizwa na hakutakiwa hata kutoa mchango wake wa mawazo, wanawake walitengwa kabisa na ukikuta myahudi anaongea na mwanamke basi ujue ni ndugu yake yaani mkewe, dada, shangazi au binamu. Yesu hakufanya hivyo alikuwa huru kuongea na mwamke yeyote. Kumbuka alivyokutwa akiongea na yule mwanamke msamaria pale kisimani wanafunzi wake walishituka. Alikuwa na wanafunzi wanawake pia kama Mary Magdalene ambaye inasemekana alikuwa mke wake.

5. Hakuwa mbaguzi, wayahudi walijiona ni taifa teule hivyo wakuwa wanajitenga na makabila mengine, katika wanafunzi wake kulikuna wengine wasio wayahudi.

6. Yesu alidharau sheria na mila kandamizi za kiyahudi, kama kupiga mwanamke aliyefumaniwa mawe hadi kufa na au lazima ya kufanya tohala. Licha ya yeye kufanyiwa tohala akiwa kachanga, aishasikika akiwaambia wayahudi waliotaka kusibitisha kuwa tohala ina umuhimu gani kwenye mila yao, aliwaambia kama tohala ingelikuwa kitu muhimu na lazima sana basi Baba yangu yaani Mungu angewatahili mkiwa mimba tumboni mwa mama zenu kitu ambacho kilikuwa ni kama dharau kwa wayahudi.

7. Uwezo wa kufanya miujiza na mafundisho yake kufuata njia ya uzima wa milele yaliwavutia sana watu, mpaka makuhani walipungukiwa kabisa waumini na sadaka kupungua lakini pia Yesu alikuwa kama mamlaka ya rufani, akiyapinga na kuyapa changamoto maaumuzi mengi waliofanywa wanasheria (mafalisayo) watu walipenda kupata second opinion kutoka kwa Yesu. Hivyo akasabisha mkanganyiko wa hatari ya watu waliozoea kujiona muhimu kudharauliwa yaani Makuhani, Mafalisayo na Watoza ushuru, na kupelekea kuonekana ni muhaini. Akajengewa mashitaka kwa watawala na kuamriwa kuhukumiwa kwa kosa la uhaini na kupata adhabu ya juu.

Kwahiyo sio kweli kwamba yesu alikuwa hana elimu, pia familia yake haikuwa masikini, umasikini ulikwisha siku alipozaliwa kutokana za zawadi kutoka kwa Mamajusi na Helode. Kumbuka zawadi kuubwakati huo ilikuwa vipande vya dhahabu.

Hongera kwa kupenda kujielimisha kweni mengi umeongea karibu na ukweli.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yesu aka Yeheshua au Joshua alikuwa msomi wa ngazi ya digrii ya juu sana. Licha kwamba alizaliwa kama binadamu mwingine Roho yake ilikuwa kamilifu, wanazuoni wa elimu ya nyota na tabiri (Mamajusi) kutoka mashariki ya mbali walitabiri uzaliwaji wake, ambao ndio waliwajulisha Wayahudi juu ya matajio ya kuzaliwa kwa Roho tukufu ya Yesu katika nchi ya wayahudi, walipitiliza pale waliposema atakuwa Mfalme kitu kilicho mchonganisha na Mtawala wa wayahudi wakati huo Helode, kumtambulisha kuwa atakuwa mfalme kwao haikuwa makosa kwani kwa tamaduni zao huko mashariki ya mbali huwa mwenye high spiritual attainment ndio alikuwa anakuwa kiongozi, waliona kuwa kwa ukuu wa utukufu wa Roho ya Yesu waliona alifaa hata kutawala dunia nzima, wasijue kuwa itaibua mtafaruki mkubwa kwenye utawala wa Helode mpaka kuibuka njama za kutaka kumuuwa. Helode aliwapa zawadi wampelekee mtoto Yesu ili baada aweze ku trace mahali alipo ili aje kumuuwa. Akitegemea kuwa wale Mamajusi baada ya kumuona na kumkabidhi zawadi wangerudi kwake na kumhabarisha alipo Mtoto Yesu.

Waligundua njama za Helode hivyo hawakurudi kwa Helode bali waliwataharisha wazazi wa mtoto Yesu na kuwashauri wamtoroshe, lakini pia walingia makubaliano na wazazi kuwa Yesu anahitaji kuelimishwa na wao juu ya kusuduo au sababu za kuzaliwa wake, hivyo wamtaka Joseph, awapelekee mtoto pindi afikapo umri wa kwenda shule na wao watamsomesha bure katika chuo chao. Yesu akiwa mtoto alitoroshewa Misri, baada ya kifo Helode walirudi na kama ilivyokuwa kwa taratibu za wayahudi mtoto alipelekwa kusomea dini ya kiebrania kwa ma Rabi (kama ilivyo kwa waisilamu mtoto huenda Madrasa). Yesu alikuwa muelewa kiasi cha kuwabishia walimu wake. Alipofika miaka 12 historia inonyesha Yesu alitoweka na kurudi tena akiwa na miaka 30 akiwa na elimu ( spiritual knowledge ya ngazi ya juu ya kimashariki) ambayo ilipingana kabisa na ile ya Kiebrania. Alishindwa hata kuhudumu kwenye Masinagogi, alifundisha vitu vilivyopingana na mila na desturi za kiyahudi, waliokuwa wanaishi kwa kufuata amri kumi za Mungu walizopewa na Nabii Musa.

Mapingano ya Mafundisho yake na Mafalisayo na Makuhani yaliopelekea kuwa kama muhaini;-

1. Kwenye Amri kumi kuna amri inayotoa katazo la kutokuitaja jina la Mungu, Yesu alijitanabaisha kuwa yeye ni Mwana wa Mungu. Haikuwaingia akilini kuwa mtoto waokuwa wanamuona akimsadia baba yake kama selemala msaidizi eti baada kutoweka kwa muda na kurudi ghafla anajimwambafai kuwa ni mwana wa Mungu wanapaswa kumuheshimu na kumuogopa, kwanza walimchukulia kama mtu aliyechanganyikiwa na kuwa ni kichaa wakamdharau.

2. Wakati kuna katazo la kutofanya kazi yeye alitenda matendo ya uponyaji siku ya sabato.

3. Aliweza fanyafujo mahekaluni kama kupindua meza na kuwatawanya waumini mahali wao walipatambua kuwa ni patakatifu.

4. Katika makutano na mafundisho yake hakuwa na mfumo Dume. Wayahudi wanaamini dhambi imeletwa na Eva(Hawa) hivyo mwanamke alitengwa hata kwenye ibada, au jumuishi mbalimbali, hakusikilizwa na hakutakiwa hata kutoa mchango wake wa mawazo, wanawake walitengwa kabisa na ukikuta myahudi anaongea na mwanamke basi ujue ni ndugu yake yaani mkewe, dada, shangazi au binamu. Yesu hakufanya hivyo alikuwa huru kuongea na mwamke yeyote. Kumbuka alivyokutwa akiongea na yule mwanamke msamaria pale kisimani wanafunzi wake walishituka. Alikuwa na wanafunzi wanawake pia kama Mary Magdalene ambaye inasemekana alikuwa mke wake.

5. Hakuwa mbaguzi, wayahudi walijiona ni taifa teule hivyo wakuwa wanajitenga na makabila mengine, katika wanafunzi wake kulikuna wengine wasio wayahudi.

6. Yesu alidharau sheria na mila kandamizi za kiyahudi, kama kupiga mwanamke aliyefumaniwa mawe hadi kufa na au lazima ya kufanya tohala. Licha ya yeye kufanyiwa tohala akiwa kachanga, aishasikika akiwaambia wayahudi waliotaka kusibitisha kuwa tohala ina umuhimu gani kwenye mila yao, aliwaambia kama tohala ingelikuwa kitu muhimu na lazima sana basi Baba yangu yaani Mungu angewatahili mkiwa mimba tumboni mwa mama zenu kitu ambacho kilikuwa ni kama dharau kwa wayahudi.

7. Uwezo wa kufanya miujiza na mafundisho yake kufuata njia ya uzima wa milele yaliwavutia sana watu, mpaka makuhani walipungukiwa kabisa waumini na sadaka kupungua lakini pia Yesu alikuwa kama mamlaka ya rufani, akiyapinga na kuyapa changamoto maaumuzi mengi waliofanywa wanasheria (mafalisayo) watu walipenda kupata second opinion kutoka kwa Yesu. Hivyo akasabisha mkanganyiko wa hatari ya watu waliozoea kujiona muhimu kudharauliwa yaani Makuhani, Mafalisayo na Watoza ushuru, na kupelekea kuonekana ni muhaini. Akajengewa mashitaka kwa watawala na kuamriwa kuhukumiwa kwa kosa la uhaini na kupata adhabu ya juu.

Kwahiyo sio kweli kwamba yesu alikuwa hana elimu, pia familia yake haikuwa masikini, umasikini ulikwisha siku alipozaliwa kutokana za zawadi kutoka kwa Mamajusi na Helode. Kumbuka zawadi kuubwakati huo ilikuwa vipande vya dhahabu.

Hongera kwa kupenda kujielimisha kweni mengi umeongea karibu na ukweli.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ahsante sana mkuu...
Maelezo yako yako bomba sana..Hongera
 
You categorized jesus as a MAN?
He was a Man with God's Spirit that why he was referred God as His Father. And He as Son of God. Creation is the Game where God pray by Himself following rules set by God Himself.

Ili aje Dunian kwa Mwanadamu basi itabidi aache utukufu wake azaliwe kama mwanadamu na anapitia yote ayapitiayo mwanadamu haijalishi umungu wake, iliatimize yale yaliyomleta hutanguliza watao mwongoza ili at point in time apate God realization au ajitambue.

Kwa hiyo mtoa maada hakuwa amekosea, walioishi nae walimuona ni binadamu wa kawaida wenye mitazamo tofauti, kuna waliomthamini na walimdharau na kumdhihaki pia. Kwani kimwili hakutofautiana nao alikuwa na mahitaji sawa na wao. Iko dhana ya kutaka kumtukuza kimwili ambayo ni potofu, utukufu wake ni wa kiroho, mwili hauwezi kuwa mtukufu kwani unamapungufu, ni Roho tuu ukiondoa unafsi inaweza kukamilika na kuweza pata Umoja mtakatifu (Oneness) na kuwa na Mungu kwa Mungu. Rohoni unakuwa ( to be) wakati mwili unaishi wakati fulani kwa muda fulani, hauwezi kuwa mahala pote wakati wowote. Mwili uko limited in time with space.

Kwa kuwa alikuwa mwilini basi alikuwa limited na time na space na hivyo hakuwa perfect so he was a person.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
He was a Man with God's Spirit that why he was referred God as His Father. And He as Son of God. Creation is the Game where God pray by Himself following rules set by God Himself.

Ili aje Dunian kwa Mwanadamu basi itabidi aache utukufu wake azaliwe kama mwanadamu na anapitia yote ayapitiayo mwanadamu haijalishi umungu wake, iliatimize yale yaliyomleta hutanguliza watao mwongoza ili at point in time apate God realization au ajitambue.

Kwa hiyo mtoa maada hakuwa amekosea, walioishi nae walimuona ni binadamu wa kawaida wenye mitazamo tofauti, kuna waliomthamini na walimdharau na kumdhihaki pia. Kwani kimwili hakutofautiana nao alikuwa na mahitaji sawa na wao. Iko dhana ya kutaka kumtukuza kimwili ambayo ni potofu, utukufu wake ni wa kiroho, mwili hauwezi kuwa mtukufu kwani unamapungufu, ni Roho tuu ukiondoa unafsi inaweza kukamilika na kuweza pata Umoja mtakatifu (Oneness) na kuwa na Mungu kwa Mungu. Rohoni unakuwa ( to be) wakati mwili unaishi wakati fulani kwa muda fulani, hauwezi kuwa mahala pote wakati wowote. Mwili uko limited in time with space.

Kwa kuwa alikuwa mwilini basi alikuwa limited na time na space na hivyo hakuwa perfect so he was a person.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hukukosea kujiita msafiri lazaro.. you so smart mam. Hongera
 
He was a Man with God's Spirit that why he was referred God as His Father. And He as Son of God. Creation is the Game where God pray by Himself following rules set by God Himself.

Ili aje Dunian kwa Mwanadamu basi itabidi aache utukufu wake azaliwe kama mwanadamu na anapitia yote ayapitiayo mwanadamu haijalishi umungu wake, iliatimize yale yaliyomleta hutanguliza watao mwongoza ili at point in time apate God realization au ajitambue.

Kwa hiyo mtoa maada hakuwa amekosea, walioishi nae walimuona ni binadamu wa kawaida wenye mitazamo tofauti, kuna waliomthamini na walimdharau na kumdhihaki pia. Kwani kimwili hakutofautiana nao alikuwa na mahitaji sawa na wao. Iko dhana ya kutaka kumtukuza kimwili ambayo ni potofu, utukufu wake ni wa kiroho, mwili hauwezi kuwa mtukufu kwani unamapungufu, ni Roho tuu ukiondoa unafsi inaweza kukamilika na kuweza pata Umoja mtakatifu (Oneness) na kuwa na Mungu kwa Mungu. Rohoni unakuwa ( to be) wakati mwili unaishi wakati fulani kwa muda fulani, hauwezi kuwa mahala pote wakati wowote. Mwili uko limited in time with space.

Kwa kuwa alikuwa mwilini basi alikuwa limited na time na space na hivyo hakuwa perfect so he was a person.

Sent using Jamii Forums mobile app
Nimekuelewa.
 
Back
Top Bottom