Pele ni king kwa mtazamo wako, ni sawa kabisa bro. Kwa mtazamo wangu, Ronaldo is the King.
Moja, mafanikio yake yako wazi. Na wakali wangu wengine wote wanamkubali, kuanzia Zidane, Ronaldinho, Messi, Nesta, mpaka kina Benzema n.k.
Mbili na muhimu zaidi, career yake na changamoto za majeruhi alizopitia, bado alipambana ambapo karibu kila mtu alisema haiwezekani, akarudi na kutawala. Hapa kuna mafunzo na inspirations kimaisha kwa ujumla.
Tatu, nadhani naongea kwa niaba ya kila mpenda soka duniani, wote huwa tunajiuliza ingekuwa vipi Ronaldo asingekumbwa na hayo majeruhi?? Moja ya vitu ntakavyomuomba Sir G in the next life, ni anionyeshe tu career ya Jamaa bila hayo majanga, nione angefika wapi.
Ya mwisho, nimesikia tu Pele alichoweza kufanya na kuona mara chache. Kwa upande mwingine, nimeona yote aliyofanya Ronaldo.