Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
OkSEHEMU YA KUMI ...... MWISHO
Mickey akapigwa na mshangao, kila alivyokuwa akimwangalia Stacie alishindwa kuelewa sababu iliyomfanya msichana huyo kuwa hivyo. Wakati mwingine akahisi vibaya kwamba msichana huyo alikuwa gaidi na hivyo alitaka kuulipua uwanja huo lakini wakati mwingine, alilitupilia mbali wazo lake na kuendelea na mambo yake.
Kwa kuwa alikuwa maarufu duniani kote, hata hapo nchini Uholanzi ilikuwa kero kwake, kila aliyemuona, alimfuata na kutaka kupiga naye picha huku wengine wakitaka kupewa ushauri juu ya biashara walizokuwa nazo, kwa kifupi, Mickey alichukia kuwa maarufu.
“Can you help me?” (Unaweza kunisaidia?) ilisikika sauti ya msichana mmoja, kimuonekano, alionekana kuwa miongoni mwa watu waliokuwa na mafanikio, wale waliopitia njia mbalimbali na ngumu mpaka kufanikiwa.
“What can I help you?” (Naweza kukusaidia nini?)
“My name is Candy, I’m enterprenuer, I have been passing through many problems in my business,” (Ninaitwa Candy, mimi ni mjasiriamali, ninimepitia matatizo mengi katika biashara zangu) alisema msichana yule.
Akabaki akizungumza na yule mwanamke. Alimueleza ukweli kwamba alikuwa na biashara nyingi na kubwa lakini kwa kipindi kirefu amekuwa akipata hasara kwani hakujua ni kwa namna gani angeweza kuzizuia fedha zake kutumika kwa kiwango kikubwa kama ilivyokuwa.
Kwa kuwa alikuwa mtu aliye na kiu ya kuwasaidia watu ili wanufaike na kile kiasi walichokuwa wakikipata, Mickey akaanza kumshauri mwanamke yule mpaka alipohakikisha kwamba alielewa kila kitu.
Hawakukaa sana hapo Uholanzi, baadae wakatakiwa kupanda ndege ya Shirika la Ndege la Qatar Airways kwa ajili ya kuendelea na safari yao mpaka Qatar. Kutoka hapo mpaka Qatar, walichukua masaa kumi, ndege ikaanza kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Hamad uliopo nchini humo katika Jiji la Doha na kisha kuchukuliwa na kupelekwa katika hoteli moja ya nyota tano.
Mickey alibaki akiyaangalia mandhari ya jiji hilo. Idadi ya watu haikuwa kubwa lakini ulikuwa moja ya mji uliokuwa safi huku kukiwa na majengo makubwa yalioufanya kupendaza na kuvutia mno.
Walipofika katika Hoteli ya Sultan Adesh, akateremka na kupelekwa katika chumba alichotakiwa kukaa. Mickey hakutulia, kila muda alikuwa kazini, kitu cha kwanza kabisa kukifanya kilikuwa ni kuchukua kompyuta yake ya mapajani na kuiunganisha na internet na kuanza kuangalia vitu alivyotaka kuviangalia muda huo.
Hakuchukua muda mrefu kuangalia vitu hivyo, akapitiwa na usingizi kwani tayari muda ulisomeka kwamba ni saa saba usiku.
****
Waarabu walitumia wiki nzima kumtangaza Mickey kwamba angeweza kufika nchini Qatar kwa ajili ya kutoa semina kubwa iliyohusu ujasiriamali. Walimjua, waliufahamu uwezo wake kwani hata kile kitabu alichokuwa amekitoa, walikinunua na kilionekana kuyabadilisha maisha yao kibiashara.
Kitendo cha kusema kwamba mtu huyo angeweza kufika Qatar, kiliwafanya matajiri wengi kutamani kuhudhuria huku kiingilio kikiwa kikubwa, zaidi ya riyal milioni moja ambayo ilikuwa ni sawa na milioni tano za Kitanzania.
Tiketi za kutosha zaidi ya elfu mbili zikaandaliwa na ndani ya siku mbili, tiketi zote zikawa zimekwisha huku watu wengine wakilalamikia kukosa, Hakukuwa na cha kufanya, kwa sababu mtu huyo angeweza kwenda mpaka Dubai, wale waliokosa tiketi basi wangekuwa na fursa ya kwenda huko kwa ajili ya kumsikiliza mhamasishaji huyo.
“What if Qaar Shalbaab come?” (Itakuwaje Qaar Shabaab wakija?) aliuliza jamaa mmoja.
“Impossible, we have enough security in here,” (Haiwezekani, tuna ulinzi wa kutosha mahali hapa) alisema jamaa mwingine.
Qaar Shalbaab lilikuwa moja ya makundi ya kigaidi yaliyokuwa yakiogopwa sana duniani. Kundi hili lililokuwa nchini Afghanistan, lilikuwa miongoni mwa yale makundi yaliyokuwa yakishambulia sehemu mbalimbali katika nchi za kiarabu kwa kutumia mabomu na hata kujitoa mhanga kwa kujilipua na mabomu waliyokuwa wakiyavaa miilini mwao.
Hawakuwa watu wazuri, kundi hili la kigaidi lililojificha katika Milima ya Tora Bola nchini humo lilikuwa likiongozwa na mtu aliyesadikiwa kuwa na roho mbaya kuliko watu wote duniani, huyu aliitwa Tawfaq Majid.
Wanawake wengi wa Kiarabu walikuwa wakivamiwa katika makazi yao na kubakwa huku wengine wakiteswa kwa kufanyiwa mambo ya kikatili. Wasichana wadogo wakaogopa kwenda shuleni kwani shule nyingi zilikuwa zikivamiwa na watoto wa kike kupigwa huku sheria kuu ya kundi hilo ikisema kwamba mtoto wa kike hakutakiwa kupata elimu.
Japokuwa sheria za nchi za Kiarabu kuwa ngumu, lakini kundi hilo lilizifanya sheria hizo kuwa ngumu zaidi. Kila siku msimamo wao ulikuwa mmoja kwamba nchi za Kiarabu zilitakiwa kukaliwa na Waarabu tu na hakutakiwa kuingia Mzungu yeyote ndani ya nchi hizo.
Mauaji hayakukoma katika nchi nyingi za Kiarabu, Wazungu wengi walikuwa wakiuawa kwa kuchinjwa hadharani jambo lililowafanya Wamarekani kuwa na chuki kubwa na kiongozi wa kundi hilo, Tawfaq Majid.
Huyo ndiye mtu aliyekuwa akitafutwa kipindi hicho, kichwa chake kilikuwa na thamani ya zaidi ya dola milioni mbili, zaidi ya shilingi bilioni nne za Kitanzania. Hakukuwa na mtu aliyekuwa akifahamu kama mtu huyo alikuwa akipatikana katika milima hiyo.
Mashirika mbalimbali ya kijasusi duniani likiwepo shirika la kijasusi lenye uwezo mkubwa dunia, ISI (Inter Services Intelligence) kutoka nchini Pakistan, yalifanya kila liwezekanalo kumpata kiongozi huyo au hata watu waliotoka katika kundi hilo lakini hawakufanikiwa.
Kila siku watu walizidi kuuawa, idadi ya watu waliokuwa wakijitoa mhanga ilizidi kuongezeka jambo lililozua hofu kubwa duniani. Hakukuonekana kuwa watu waliokuwa na nguvu za kuwatafuta watu hao ambao walizidi kuwa hatari kadiri siku zilivyozidi kwenda mbele.
Mataifa yote ya Kiarabu yalilichukia kundi hili lililoshikilia msimamo wake kwamba watoto wa kike hawakutakiwa kwenda shule na wala nchi za Kiarabu hazikuwa kambi za Wazungu.
“Nina wasiwasi nao,” alisikika jamaa mmoja.
“Kwa nini?”
“Wanaweza kuja kuanzisha vurugu, inabidi kuwe na ulinzi mkali hapa,” alisema jamaa huyo.
Hicho ndicho kilichofanyika, kwa sababu ndani ya ukumbi huo kulitarajiwa kuwa na watu wenye fedha zao, tena wengine wakiwa viongozi wa nchi, ulinzi mkubwa ukaimarishwa, hakukuwa na mtu yeyote aliyeruhusiwa kuingia na aina yoyote ile ya chuma huku wanawake waliokuwa wakivaa majuba wakichunguzwa kwa umakini kwa kuvuliwa nguo hizo katika vyumba maalum ili kuwaepuka wale waliojivisha mabomu kwa ajili ya kujilipua.
Siku ambayo semina hiyo ilitakiwa kuanza, ndiyo ambapo kundi hilo lililokuwa chini ya Tawfaq lilihisiwa kufanya shambulio ndani ya ukumbi huo huku lengo lao likiwa ni kumuua Mickey aliyekuja kwa ajili ya kazi ya upelelezi huku akitumia kivuli cha ujasiriamali.
Saa 4:05 asubuhi siku ya semina hiyo, tayari Mickey alikuwa amesimama mbele ya ukumbi huo, watu wengi walikuwa mbele yake kwa ajili ya kumsikiliza. Hakuonekana kuwa na wasiwasi, alizungumza huku akionekana kujiamini kwa kila neno alilokuwa akilitamka.
Watu walikuwa makini kumsikiliza, kila neno alilokuwa akilizungumza, lilionekana kuwa ‘nondo’ vichwani mwa watu, wengi wakajikuta wakitingisha vichwa vyao kutoka juu kwenda chini.
Ilipofika saa sita mchana, watu wakapata muda wa mapumziko, hapo, walikunywa na kula, kila kona, walikuwa wakimzungumzia Mickey, alionekana kuwa na uwezo mkubwa wa kuyafafanua yale aliyokuwa akiyazungumza, baada ya nusu saa, semina ikaendelea kama kawaida.
“Mbona nasikia kelele, kuna nini?” aliuliza jamaa mmoja, alikuwa karibu na mlango wa kuingilia ukumbini humo.
“Kuna mwanamke anataka kuingia, hebu njoo kwanza,” alisema jamaa mwingine, alitoka huko mlangoni na kuja kuwaita wenzake.
Malumbano yalikuwa yakiendelea baina ya walinzi hapo mlangoni na mwanamke aliyefika mahali hapo huku akiwa amevaa juba jeusi jeusi na hijabu kichwani. Alitaka kuingia kinguvu, japokuwa walinzi walikuwa wakimzuia, lakini alikuwa akilazimisha jambo lililozua hofu kubwa kwa kila mtu aliyekuwa hapo mlangoni.
“Twende kule...” alisema mlinzi mmoja.
“Wapi?” aliuliza mwanamke yule.
“Kwenye chumba maalum.”
“Kufanya nini?”
“Kukupekua, hivyo ndivyo tunavyofanya kwa kila mwanamke anayetaka kuingia ndani.”
“Haiwezekani.”
“Haiwezekani nini?”
“Kwenda huko.”
“Basi napo hautakiwi kuingia humu,” alisema mlinzi.
“Hapana! Nitaingia tu.”
Bado mwanamke yule alikuwa aking’ang’ania kuingia ndani ya ukumbi ule pasipo kukaguliwa. Hawakujua sababu iliyomfanya kukataa lakini kosa kubwa walilolifanya, mashine ya kuchunguzia kama mtu alikuwa na kitu cha chuma au silaha yoyote ilikuwa ndani ya jengo lile, umbali kadhaa kutoka katika chumba kile kikubwa kilichokuwa kikifanyikia semina ile.
Walinzi walijitahidi kumzuia mwanamke yule lakini naye alikuwa mbishi, hakutaka kukubaliana nao, aliendelea kubishana nao, lakini huku kila mmoja akiwa hajui ni kitu gani kilichotokea, ghafla, mwanamke yule akaanguka chini, kichwa chake kilikuwa kimefumiliwa kwa risasi, damu zilizokuwa zikimtoka kichwani, zikaanza kutapakaa katika sakafu, kila mmoja akaogopa, walipoangalia huku na kule, hakukuwa na mtu aliyeshika bunduki, kila mmoja akachanganyikiwa!
Hawakujua ni nani aliyekuwa amempiga risasi, wao walishtukia akiwa chini huku damu zikiendelea kumtoka, tukio hilo, liliwashangaza mno!
****
Wamarekani waliamua kutilia umakini katika kumlinda mtu wao, alikuwa mtu maalum ambaye walihakikisha kwamba angekamilisha kazi zote walizokuwa wamemuagiza katika nchi za Uarabuni.
Kila alipokuwepo, tayari ulinzi mkubwa ulikuwa umekwishawekwa hivyo alitakiwa kufanya kila kitu kwa kujiaminisha lakini mwisho wa siku walitaka kupata kile walichokuwa wakikitata.
Kitendo cha kuwa ndani ya ukumbi ule wa semina, tayari Wamarekani walikwishadumisha ulinzi wao kwa kutamani kumlinda mtu huyo kwa kitu chochote kibaya ambacho kingeweza kumtokea.
Nje ya hoteli hiyo, sehemu mbalimbali hasa maghorofani na hata kwenye vioo vya hoteli zilizokuwa karibu na eneo hilo, Wamarekani kutoka C.I.A walikuwa wamejaza titi madirishani huku wakiwa na bunduki zao zilizowekwa vyombo vya kuzuia mlio wa risasi, bunduki zenye nguvu zijulikanazo kama Riffle, bunduki maalumu zilizokuwa zikitumika na wadunguaji (snipers)
Mara baada ya kumuona mwanamke wa Kiarabu aliyevaa juba jeusi akizozana na walinzi waliokuwepo mlangoni, wakahisi kwamba kulikuwa na tatizo lililokuwa limetokea. Walichokifanya ni kuziweka vizuri ‘earphone’ zao ili kusikika mwanamke yule alikuwa akizungumza nini.
“Who is she?” (Ni nani?) aliuliza jamaa mmoja, alikuwa ameiweka vizuri bunduki yake huku akiwa amekwishamlenga mwanamke yule, alikuwa akizungumza na mwenzake aliyekuwa ghorofa nyingine.
“I don’t know,” (Sijui)
“Should I shoot her down?” (Nimpige risasi?)
“No! Just wait,” (Hapana! Subiri kwanza)
Bado walinzi waliendelea kuzozana na mwanamke yule kwamba ilikuwa ni lazima aende katika chumba maalum kwa ajili ya kupekuliwa ili aonekane kama alikuwa mtu salama au la, yeye hakutaka, aliendelea kusisitiza kwamba ilikuwa ni lazima kupita pasipo kukaguliwa.
“Just shoot her down,” (Mpige risadi tu)
Ulikuwa ni uamuzi ulioonekana kuwa sahihi, alichokifanya mwanajeshi yule wa Kimarekani ni kumpiga risasi mwanamke yule, risasi ya kichwa ilimpiga na kumwangusha chini na hapohapo kupoteza maisha hapohapo. Walinzi wale walipomwangalia vizuri kwa ndani, alikuwa amevalia kikoi kilichokuwa na mabomu kadhaa ya kujitoa mhanga.
Mickey aliendelea kutoa masomo ya ujasiriamali katika sehemu mbalimbali katika nchi za Kiarabu, tofauti na Wamarekani wengine, Mickey akatokea kupendwa na kuaminika zaidi ya mtu yeyote kitu kilichowapelekea Waarabu wengi kutaka mtu huyo aendelee kuishi nchini mwao.
Japokuwa alionekana mtu mwenye busara ambaye alizungumza taratibu mpaka kumuelewa, lakini hakukuwa na aliyegundua kwamba huyo Mickey alikuwa miongoni mwa watu wenye roho mbaya waliowahi kutokea katika Shirika la Kijasusi la C.I.A.
Hiyo ilikuwa ni safari yake ya kwanza, baada ya kumaliza semina yake iliyomchukua wiki nne, akarudi nchini Marekani ambapo moja kwa moja akaamua kumuoa msichana wake wa siku nyingi, Elizabeth Kenz na kuanza kuishi pamoja ambapo baada ya mwaka mmoja, wakapata mtoto wa kiume waliyemuita kwa jina la Victor.
Maisha yalikuwa mazuri, japokuwa aliishi na mume wake lakini hakuna hata siku moja Elizabeth aligundua au kuhisi kwamba mume wake, Mickey alikuwa jasusi wa Kimarekani aliyekuwa akiua watu kadiri alivyoagizwa.
Ilipofika mwaka 1993, Mickey akatumwa tena kwenda nchini Iran, lengo kubwa la kutumwa nchini humo lilikuwa ni kupeleleza ni kwa namna gani jeshi la Marekani lingeweza kupenya na kuingia katika nchi mbili, Iraq na Syria.
Hilo, kwake wala halikuwa tatizo, kwa sababu alikuwa mtu makini kwa kila alichokuwa akikifanya, akaelekea huko. Kitu cha kwanza kabisa alichokifanya mara baada ya kuwasili nchini humo ni kwenda katika kambi ya Wamarekani iliyokuwepo katika Mji wa Badhiir, pembezoni mwa nchi ya Iran upande wa Mashariki, sehemu ambayo iliaminika kama imelaaniwa kutokana na ardhi yake kuwa kavu kila wakati.
Alipofika huko, akakaribishwa na kuambiwa kwamba baada ya wiki moja kazi ilitakiwa ifanikiwe na hivyo kurudisha majibu mazuri nchini Marekani. Kwa kuwa alijiamini sana, siku iliyofuata, akaanza zoezi lake la kusafiri kwa kutumia ngamia jangwani ili aweze kufahamu ni sehemu gani jeshi lao lingeweza kupita ili kuingia katika nchi hizo.
Safari haikuwa nzuri, ilikuwa yenye kuchosha, alipita jangwa kwa jangwa, jua lilikuwa kali lakini yote hayo alivumilia kwa kuwa aliamini kwamba anafanya kazi kwa ajili ya nchi yake. Alitembea na ngamia yule mpaka alipofika katika sehemu iliyokuwa na mahema kadhaa, hapo, wakatokea Waarabu wawili waliokuwa na bunduki na kuanza kumsogelea.
“You American?” (Wewe ni Mmarekani?) aliuliza Mwarabu mmoja aliyetumia Kingereza cha kujifunza.
“Yes! Where Am I?” (Ndiyo! Nipo wapi hapa?) aliuliza Mickey.
Waarabu hao waliposikia kwamba mtu aliyesimama mbele yao alikuwa Mmarekani, miongoni mwa watu waliokuwa wakiwachukia, wakamuweka chini ya ulinzi na kumuingiza ndani. Mickey hakuonekana kuwa na wasiwasi, zaidi ya Waarabu kumi walisimama mbele yake na kuanza kuzungumza nao kwa kutumia Lugha ya Kiarabu aliyokuwa akiifahamu vizuri kitu kilichowafanya Waarabu wale kujiona kuwa na thamani, kitendo cha Mmarekani kuzungumza Kiarabu, wakajiona kuwa juu.
Mickey akaanza kuwaelezea kwamba alifika mahali hapo kwa kuwa alikuwa safarini kuelekea nchini Iraq hivyo hakujua ni njia ipi angeweza kupitia, njia ingemfanya kuwa nyepesi kuingia nchini humo pasipo kugundulika.
Alipoulizwa sababu zaidi, aliwaambia kwamba alikuwa mjasiriamali aliyekatazwa kuingia nchini humo ila kwa sababu asilimia kubwa ya watu waliokuwa wakiishi Iraq walikuwa masikini, alitaka kuzungumza nao na kuwaambia namna ambavyo wangeweza kufanya na hatimae kupata utajiri na kuwa wafanyabiashara wakubwa.
Maneno yake, sura yake ya huruma, tabasamu lake likawafanya Waarabu wale wamuamini kwa asilimia mia moja kwani hakuwa mgeni kwao hivyo kumwambia njia za panya zote ambazo zilikuwa zikitumika, alitakiwa kuzitumia hizo kwa ajili ya kufika nchini humo.
“Nashukuru, natakiwa kurudi sasa,” aliwaambia Waarabu gao.
“Kurudi wapi?”
“Mjini.”
“Hauendi Iraq?”
“Nilitaka nifahamu kwanza, nina semina na Wairan, baada ya hapo ndiyo nitaondoka. Mmebarikiwa kuwa na mafuta mengi, ila bado hamjajua ni kwa jinsi gani mnaweza kufanikiwa kupitia mafuta hayo,” alisema Mickey.
Kwa muda wa masaa matano ambayo alikaa nao tayari akaonekana kuwa rafiki yao, wakaanza kucheka naye huku wakimwambia mambo mengi kuhusu nchi nyingi za Kiarabu.
Mickey hakutaka kukaa sana, alichokifanya ni kuondoka na kurudi Badhiir ilipokuwa kambi ya Wamarekani. Alipofika huko, akawaambia kila kitu kilichokuwa kimetokea, mpaka njia ambayo walitakiwa kuitumia jambo lililoonekana kuwa rahisi kufanyika, hivyo Mickey alionekana kuwa msaada kwao.
“You are the man......You are the man,” (Wewe mwanaume...Wewe mwanaume) alisema mwanajeshi mmoja huku akitumia msemo uliomaanisha kumpa sifa mtu, msemo uliotumika sana nchini Marekani hasa kwa vijana wa mtaani.
Usiku wa siku hiyo, Mickey akaanza kupanga mipango yake ya kusonga mbele, alitaka kuelekea upande uliokuwa na nchi ya Syria kwa ajili ya kukamilisha kazi zake alizokuwa amepangia.
Kitu kilichomshtua kutoka katika lindi la mawazo ya mipango yake, ni pale alipoanza kusikia kelele za wanawake zikitokea sehemu kulipokuwa na mahema yaliyotengwa.
Kwanza akashtuka, hiyo ilikuwa ni kambi pekee ya Wamarekani nchini Uarabuni ambayo haikuwa na mwanamke yeyote yule, sasa hizo sauti za wanawake zilikuwa ni za wakina nani.
Hakutaka kubaki hapo, alichokifanya, akachukua bunduki zake na kwenda kule kulipokuwa na mahema yale. Sauti za wanawake waleziliendelea kusikika kwa ukaribu zaidi, alipolifungua hema lile, akapigwa na mshtuko, zaidi ya wanawake kumi wa Kiarabu walilazwa chini na wanajeshi wa Kimarekani waliokuwa na kazi moja tu, kuwabaka kwa zamu huku wanajeshi wengine wakiwa pembeni na bunduki zao, kwa kila kilichokuwa kikiendelea, walikishangangilia.
Moyo wa Mickey ukabadilika, hasira kali zikamkaba kooni, hakuamini kile alichokuwa akikiona mbele yake. Ni kweli alikuwa mwanaume mwenye roho mbaya hasa linapokuja suala la kuua lakini kitendo cha kushuhudia wanawake wakibakwa, kilimkera moyoni mwake. Akageuka na kutaka kuondoka.
“Hey man! Where are going? Come and JamiiForums' Community Engagement Guidelines | Mwongozo wa Ushiriki kwenye Mijadala these young slut girls,” (Hey mwanaume! Unakwenda wapi? Njoo ufanye mapenzi na wanawake hawa wadogo na wachafu) alisema mwanajeshi mmoja huku akimvuta Mickey.
“Let me go,” (Niache niondoke) alisema Mickey huku sauti yake ikisikika kama ya mtu mwenye hasira kali.
Mwanajeshi yule akamuachia Mickey ambaye akaanza kupiga hatua mpaka kwenye hema lile, alipofika, akajilaza kitandani.
Kadiri alivyokuwa akizisikia kelele za wanawake wale, hasira zilizidi kumpanda, akajikuta akianza kuwachukia wanajeshi wale. Ilipofika saa saba usiku, tena kelele zile zikizidi kuongezeka, alichokifanya ni kuchukua bunduki zake zilizokuwa ndani ya begi na kuanza kurudi kule kulipokuwa na mahema yale. Hakukuwa na kitu kingine alichokuwa akikifikiria zaidi ya kuwaua wanajeshi wote, kitendo cha kubakwa kwa wanawake wale, alikichukia kwani alijua haikuwa kazi ambayo iliwapelekea wanajeshi wale kupelekwa katika nchi za Kiarabu.
Alipolifikia hema lile kubwa, akaingia ndani, bunduki zilikuwa mikononi. Hakuwa Mickey yule aliyekuja kipindi cha nyuma, alikuwa amebadilika, hasira kali ilimkaba kooni, alichokuwa akikitaka ni kuwaua wanajeshi wote waliokuwa mule ndani ya lile hema, aliwahesabu harakaharaka, walikuwa kumi na tano.
Aliyesimama mbele yao alikuwa Mickey, yuleyule jasusi kutoka C.I.A, jasusi aliyejulikana zaidi kwa mauaji makubwa aliyokuwa akiyafanya kila alipoambiwa kwamba mtu fulani alitakiwa kuuawa.
Aliwaangalia wanajeshi, kelele za wanawake wale zilimfanya kushikwa na hasira zaidi, paji lake la uso lilitawaliwa na ndita, hakutaka kusikia kitu chochote kwa wakati huo, kile alichokuwa akikitaka ni kuwapiga risasi tu.
Hawakujua kwamba huyu Mickey aliyeingia alikuwa tofauti na yule wa kipindi kilichopita, sasa hivi, alikuwa na hasira mithiri ya mbwa mwitu aliyechokozwa hivyo hakutaka kusikia kitu chochote kile. Akazikoki bunduki zile na kuwanyooshea.
“Paaa...paaaa....” ilisikika milio kadhaa ya risasi ndani ya hema lile, wanajeshi wote kumi na tano wakaanguka chini na kufa hapohapo.
Hali ilionekana kuwa ya hatari mahali hapo, damu zilitapakaa katika kila eneo ndani ya hema lile, wanawake wale wa Kiarabu wakabaki wakilia, hawakuamini kama mtu yule angeweza kuwaua wanajeshi wale na kuwaacha hai wao.
“You are free, you can go home now,” (Mpo huru, mnaweza kwenda nyumbani sasa) alisema Mickey na kutoka hemani mule.
Moyo wake ukaridhika, alichokifanya ni kuondoka mahali hapo huku akijiandaa kutoa ripoti ya uongo juu ya kilichokuwa kimetokea hapo Badhiir.
****
‘Fifteen soldiers were killed in Iran’ (Wanajeshi kumi na tano wauawa Iran) kilikuwa kichwa cha habari kilichopita katika Kituo cha Televisheni cha CNN cha nchini Marekani. Ilikuwa moja ya taarifa iliyomsisimua kila Mmarekani huku wengi wao wakiwa hawaamini kama waliweza kuwapoteza wanajeshi wengi namna hiyo tena kwa wakati mmoja.
Maswali mengi yakaanza kumiminika vichwani mwa watu kwamba ilikuwaje wanajeshi hao wauawe kwa pamoja tena ndani ya hema huku wakiwa wamekaa karibukaribu namna ile.
Swali hilo na maswali mengine yaliyokuwa yakiulizwa na watu yakakosa majibu. Walichokifanya C.I.A ni kuwasiliana na Mickey ili kutaka kufahamu ni kitu gani kilichokuwa kimetokea mpaka wanajeshi hao kuuawa katika kambi waliyomwambia aende huko.
Hawakutaka kupewa majibu kupitia simu, walichomwambia ni kwamba alitakiwa kwenda nchini Marekani ambapo huko, wakamuweka chini na kuanza kuzungumza naye huku ndani ya chumba hicho kukiwa na watu zaidi ya ishirini.
“Nini kilitokea?” aliuliza kiongozi wa shirika hilo, bwana Powell.
“Sifahamu. Siku ya tukio, sikuwa hapo Badhiir, nilikwenda kukamilisha majukumu yangu, na bahati nzuri nikakamilisha kila kitu, tena kwa mafanikio makubwa,” alisema Mickey.
“Ulipoondoka, uliiacha kambi katika hali nzuri?”
“Naweza kusema hivyo kwani hakukuwa na dalili za kutokea kwa adui yeyote yule,” alisema Mickey.
“Kipi unahisi kinaweza kuwa chanzo cha watu hawa kuuawa?”
“Sijajua, ila nilipowaacha, kulikuwa na kundi la wanawake kambini, nahisi, hao ndiyo waliosababisha kila kitu,” alisema Mickey.
Kilichofanyika, upelelezi ulitakiwa kufanyika zaidi ili kujua ni kitu gani kilichokuwa kimetokea. Watu makini walioaminika katika kufanya upelelezi wakaelekea huko, wakaingia mpaka kwenye kambi hiyo na kukaa huko kwa muda wa wiki moja lakini hawakufanikiwa kupata chochote kile.
Siku iliyofuata, zaidi ya Wamarekani mia tatu walikuwa barabarani huku wakiwa na mabango yaliyosema kwamba ilitakiwa wanajeshi wote waliokuwepo katika nchi za Uarabuni warudishwe nchini kwani kuwepo huko kulimaanisha kwamba wanajeshi wengi wangeendelea kuuawa.
Alichokifanya Bush baba ni kuongeza jeshi zaidi nchini humo, hakutaka kusikia kitu chochote kile kuhusu kuwarudisha wanajeshi wake nchini Marekani. Alikuwa na hasira mno na Waarabu, hakutaka watu hao waendelee kuishi, kuna wakati alitamani awe Mungu ili awapoteze wote kwani uwepo wao mbele ya macho yake ilikuwa chukizo kubwa kwake.
Wamarekani walipiga kelele lakini hakukuwa na kilichobadilika, waliandamana mno tena katika majimbo yote nchini humo lakini hakukuwa na utekelezaji wowote ule, msimamo wa rais huyo ulikuwa mmoja tu kwamba ilikuwa ni lazima wanajeshi waongezwe nchini humo kwa ajili ya kuongeza nguvu.
“Kwa nini wasiwaruhusu wanajeshi wetu warudi? Haya mambo ya kivita, huwa siyapendi sana,” alisema Elizabeth huku akionekana kuumizwa na kile kilichokuwa kikiendelea.
“Sijajua ila kama ningekuwa mwanajeshi, nisingeweza kwenda, sisi wengine ambao hata hatujui kushika bunduki, tunaweza kufa kwa presha,” alisema Mickey.
“Hata kule mitaani haukuwahi kushika bunduki?”
“Hapana! Nilikwishawahi kuziona wakiwa nazo watoto wenzangu, lakini sikuwahi kushika hata siku moja, ninazihofia mno,” alisema Mickey huku akijifanya kuogopa kushika bunduki.
Elizabeth aliendelea kupigwa upofu, hakujua kama mume wake ndiye alikuwa nyuma ya kila kitu kwa kuwaua wanajeshi wale. Alipoambiwa kwamba alikuwa muoga kushika bunduki, akayaamini maneno hayo kwani hakuwahi kumuona mume wake akishika bunduki na hata alipomshauri kwamba amiliki bunduki kutokana na umaarufu wake, alimkatalia.
Miongoni mwa watu ambao Elizabeth alikuwa akiwaona kwamba ni waoga namba moja duniani, wa kwanza alikuwa mume wake. Wakati mwingine alijifanya kuogopa mpaka kutazama filamu za kutisha au kila alipokuwa akiangalia filamu zilizojaa mauaji makubwa, alikuwa akikunja sura yake kama mtu aliyeumizwa mno.
Siku zikaendelea kukatika. Kadiri Mickey alipotumwa nchini Marekani, aliendelea kuua kificho hasa pale alipowaona wanajeshi wenzake wakiendelea kuwabaka wanawake wa Kiarabu.
Mwaka 2009 wakati Barack Obama alipokuwa akichukua ofisi na kuwa rais wa Marekani, ndicho kilikuwa kipindi Mickey alitumwa nchini Iran kwa ajili ya kuhakikisha kwamba anawachonganisha watu wa taifa hilo na Iraq kutokana na mtafaruku mkubwa wa mafuta uliokuwa ukiendelea.
Alipofika huko, kama kawaida, tabia za wanajeshi kubaka wanawake wa Kiarabu ilikuwa ikiendelea na hakuacha kuua, aliendelea kuwamaliza wanajeshi wa Marekani kwani kwake, kitendo cha kubakwa kwa mwanamke kilionekana chukizo kubwa kuliko hata kuua.
Ilipofika mwaka 2010, hapo ndipo tetesi zilipoanza kusikika kwamba Mickey, jasusi aliyekuwa akitumainiwa kwa kupewa ‘mission’ nyingi ndiye aliyehusika katika kuwamaliza wanajeshi wengi wa Kimarekani kwa kuwaua kwa sababu tu walikuwa na tabia ya kuwabaka wanawake wa Kiarabu, wakuu wa C.I.A wakakasirika, hasira zao zikawaka dhidi ya Mickey.
Nao wakataka kumuua, yaani ni sawa na kuukata mti ulioupanda mwenyewe na kuumwagilia kila siku. Japokuwa alikuwa mtu muhimu, hawakuwa na jinsi, ili kuokoa maelfu ya wanajeshi wa Kimarekani, ilikuwa ni lazima kumuua Mickey. Ripoti ya ombi la kuuawa, likapitishwa na bwana Powell kusaini. Kilichosubiriwa ni kazi tu kufanyika.
Zoezi la kumuua Mickey halikuwa jepesi hata mara moja, alifanya kazi kama jasusi wa C.I.A kwa kipindi kirefu mno hivyo mbinu zote walizokuwa wakizitumia majasusi alikuwa akizifahamu.
Kuna kipindi walitaka kumuua hotelini huku mmoja wa majasusi akijifanya mfanyakazi wa hoteli hiyo ambaye alikuwa bize akikihudumia chumba chake, kitu cha ajabu, siku ambayo alitaka kummaliza, hakuweza kumuona tena, alikuwa amekwishaondoka zake hotelini hapo.
C.I.A hawakuchoka, bado waliendelea kusisitiza kwamba Mickey alitakiwa kuuawa haraka iwezekanavyo. Kila kitu walichokuwa wakikifanya, alikigundua hivyo walipata wakati mgumu mno.
Mpaka nchi ya Marekani inaweka historia ya kutawaliwa na mtu mweusi, Barack Obama, bado walikuwa wakiendelea kumtafuta Mickey ili wamuue lakini ikashindikana kabisa.
“Nataka tufanye kitu,” alisema Mickey, alikuwa akizungumza na mwanaume mmoja aliyeonekana kufanana naye kuanzia umbo, yaani urefu na mwili.
“Kitu gani?”
“Nitakulipia dola milioni tano endapo tu utakubali kufanya kile ninachokitaka,” alisema Mickey.
“Kitu gani?”
“Nataka uwe mimi.”
“Niwe wewe? Kivipi?”
Mickey akaanza kumfafanulia kwamba alitaka kutengeneza sura ya bandia inayofanana na yeye na kisha kumgawia jamaa huyo ambaye angekuwa mbadala wake na angeshughulika katika kila kitu alichokuwa akikifanya, yaani aonekane kama Mickey.
Japokuwa ilikuwa kazi kubwa lakini malipo yake yakamfanya kuvutiwa na kutaka kuifanya kazi hiyo. Kiasi cha dola milioni tano ambazo zilikuwa ni zaidi ya shilingi bilioni kumi, kilimpagawisha mwanaume huyo aliyeitwa Stefan.
Baada ya kukubaliana kwa kila kitu, Mickey akaanza kufanya mawasiliano na mtaalamu wa kutengeneza sura za bandia, Chung Lu, mwanaume kutoka nchini China. Akafika nchini Marekani na kuonana na Mickey ambapo akapewa maelezo juu ya nini kilitakiwa kufanyika.
Baada ya kupewa maelekezo yote, siku iliyofuata, wote watatu wakawa ndani ya chumba maalumu ambapo humo ndipo kulipofanyika mchakato wa kutaka kutengeneza sura ya bandia na kuvishwa Stefan.
Mchakato mzima ulichukua masaa nane, sura iliyofanana na Mickey ikatengenezwa na kisha kuvarishwa Stefan huku sura nyingine ya Stefan ikitengenezwa na kuvarishwa Mickey. Huo ndiyo ulikuwa mchezo alioamua kuucheza na hakutaka kujali kuhusu chochote kile.
Kesho yake, akachukua kila kilichokuwa chake, kuanzia simu yake, kadi zake zote zikiwepo za benki, magari yake na kumuachia.
Hata Stefan alipoanza kuishi na Elizabeth, mwanamke huyo hakuweza kugundua kitu chochote kile. Kuanzia sauti, muonekano mpaka baadhi ya tabia bado mwanaume huyo alionekana kuwa kama Mickey.
Mara kwa mara Mickey alikuwa akiendelea kufika nyumbani hapo na kujifanya kuwa rafiki mkubwa wa Stefan. Japokuwa kila alipokuwa akimwangalia mke wake akiwa amekumbatiana na Stefan alijisikia wivu lakini hakuwa na jinsi, alijua alichokuwa akikifanya hivyo alivumilia kwa kila kitu.
Katika kipindi ambacho Mickey alitakiwa kwenda nchini Tanzania, tayari C.I.A walikuwa wamekwishaandaa mpango mkubwa wa kumuua hivyo walijiandaa vilivyo. Siku ambayo Stefan alipokuwa akielekea huko huku akiwa na muonekano wa Mickey, hakugundua kwamba kulikuwa na mpango kabambe wa kumuua.
Mickey mwenyewe hakutaka kubaki nchini Marekani, alitaka kufuatilia kila kitu kilichokuwa kikiendelea. Mpaka kipindi ambacho Stefan alipigwa risasi, Mickey alikuwa uwanjani hapo akishuhudia na kuona kwamba hiyo ilikuwa nafasi yake ya kuuawa kama ilivyokuwa imepangwa.
Dunia nzima ikaingiwa na majonzi, kila mtu akalaumu kwa nini Mickey alikuwa ameuawa na wakati alikuwa mhamasishaji mkubwa duniani na alifanya kila kitu alichoweza kuwakwamua watu kutoka katika umasikini mkubwa waliokuwa nao.
C.I.A wakafurahia pasipo kufahamu kwamba mtu waliyekuwa wamemuua hakuwa Mickey bali alikuwa Stefan aliyevaa sura ya bandia ya Mickey.
Elizabeth alilia usiku na mchana, kifo cha mumewe kilimuuma mno, hakula wala hakulala, kila alipokuwa akikaa na kumfikiria mume wake, alizidi kuumia moyoni wake.
“I will avenge, I will kili a person who murded my father,” (Nitalipa kisasi, nitamuua yule aliyemuua baba yangu) alisema Victor huku akionekana kuwa na hasira.
Mwaka mmoja baadae, Mickey akajitokeza kwa mke wake huku akiwa na muonekano wa Stefan. Elizabeth alipomuona, hakujua kama ni mume wake bali alijua kwamba ni rafiki mkubwa wa marehemu mume wake.
“Kuna siri nzito nataka kuongea nawe,” alisema Mickey huku sauti yake ikiwa imebadilika kabisa.
“Siri gani?”
“Kuhusu mume wako,” alisema Mickey, hapohapo Elizabeth akaanza kububujikwa na machozi kwani picha ya mume wake ikaanza kumrudia tena.
“Amefanyaje?”
“Naomba tukaongelee chumbani, hii ni siri nzito mno,” alisema Mickey.
“Kuongelea chumbani?”
“Ndiyo!”
“Hapana. Hakuna mtu anayeruhusiwa kuingia chumbani kwangu, haiwezekani!”
“Lakini hili ni muhimu kwako.”
“Hapana. Nimesema haiwezekani, tena naomba uondoke,” alisema Elizabeth huku akiwa amekwishabadilika, tayari machozi yale yalikuwa yamekwishaloanisha mashavu yake. Taswira ya mume wake ilijirudia vema kichwani mwake.
****
Ilionekana kuwa ngumu sana kwa Mickey kuzungumza na mkewe kuhusu kile kilichokuwa kimetokea mpaka kufikia siku hiyo. Muda wote Elizabeth alikuwa akilia tu kwani kwa jinsi alivyokuwa akimpenda mume wake, na vile ambavyo Mickey mwenye sura ya Stefan alivyomkumbusha, aliumia mno.
Alitamani kumwambia hapohapo kwamba yeye ndiye alikuwa mume wake lakini hakuona aanzie wapi, alichokifanya ni kuondoka huku akimuachana mke wake katika hali hiyo.
Huko, kitu cha kwanza kabisa alichokifanya ni kuwasiliana na mtoto wake, Victor na kuomba kukutana naye kwa kuwa alikuwa na mambo mengi aliyotaka kumwambia kuhusu baba yake, yaani yeye mwenyewe.
Kwa kuwa kijana huyo alikuwa nchini Ujerumani, akaomba kukutana naye baada ya wiki moja, kweli, baada ya wiki moja, Victor alikuwa mbele yake, akaanza kuzungumza naye.
Victor alibaki kimya akimsikiliza Mickey, hakugundua kama alikuwa baba yake, alichokifahamu ni kwamba mtu huyo alikuwa rafiki mikubwa wa baba yake.
Kitu alichokifanya Mickey ni kumuhadithia Victor tangu siku ile alipokuwa amezaliwa, vitu alivyokuwa akivifanya kama mtoto na kumuonyeshea picha nyingi za kipindi hicho. Victor akapigwa na mshangao, alijiuliza kwamba ilikuwaje rafiki wa baba yake awe na vitu vingi namna hiyo na wakati hata baba yake hakuwa navyo? Kila alichojiuliza, alikosa majibu.
“Where did you get them?” (Umevipata wapi?) aliuliza Victor.
“I had them since you were a baby boy,” (Nilikuwa navyo tangu ulipokuwa mtoto mdogo) alisema Mickey.
“My dad has never shown me all of these,” (Baba hakuwahi kunionyeshea hivi vyote) alisema Victor huku akichukua simu ile na kuanza kuziangalia picha zile.
“I know! But let me tell you the truth,” (Najua! Ila acha nikwambie ukweli)
“What truth?” (Ukweli upi?)
“I am your father,” (Mimi ni baba yako)
“What?” (Nini?)
“Shiiiii”
Mickey akamtuliza Victor, alionekana kama mtu aliyeshtuka sana hivyo akamwambia atulie na kisha angemwambia kila kitu kilichokuwa kimeendelea. Kwanza Victor hakuonekana kuamini, ilikuwaje mwanaume huyo aseme kwamba alikuwa baba yake na wakati alifahamu fika kwamba baba yake alikuwa Mickey.
Aliendelea kujiuliza zaidi labda mama yake alikuwa ametembea nje ya ndoa na mwisho wa siku mwanaume huyo kumpa mimba na hivyo kupata mtoto ambaye ndiye yeye, kila alichokuwa akijiuliza, alikosa jibu.
“Haiwezekani, baba yangu ninamjuua, mama hawezi kumsaliti baba na kutembea na wewe,” alisema Victor huku akionekana kuchanganyikiwa.
“Mimi ni nani?”
“Nakujua wewe kama rafiki yake baba yangu.”
“Sawa. Twende tukatembee, nitakwambia kila kitu.”
Walichokifanya ni kutoka hapo mgahawani walipokuwa na kwenda kutembea katika eneo kubwa la Bustani ya Livingston iliyokuwa hapo New York, pembezoni mwa Mghahawa wa KFC.
Huku, Mickey akaanza kumuhadithia mtoto wake kila kitu kilichokuwa kimetokea katika maisha yake tangu siku ya kwanza alipojiunga na CIA, wanajeshi walipowabaka wasichana wa Kiarabu na kuamua kuwaua mpaka mpango mzima uliofanywa kwa ajili ya kummaliza.
Victor alibaki akishangaa, hakuamini kile alichokuwa amekisikia kutoka kwa baba yake, hapohapo, akajikuta akimkumbatia kwa furaha kwani baada ya kuumia kwa kipindi kirefu kwa kudhani kwamba baba yake alikuwa ameuawa nchini Tanzania na C.I.A, mwisho wa siku akakutana naye tena na kumwambia kwamba alikuwa mzima na aliyeuawa hakuwa yeye.
Siku hiyohiyo wakaelekea nyumbani, huko, akamwambia mama yake kile kilichotokea, bi Elizabeth akajikuta akibubujikwa na machozi na hata Mickey alipoamua kuwatembelea tena, akajikuta akimkumbatia kwa furaha.
Hawakutaka kuchelewa, baada ya miezi miwili, Elizabeth akatangaza kwamba alitaka kuolewa na rafiki wa mume wake, Stefan pasipo dunia kujua kwamba huyo bwana harusi ndiye alikuwa mume wake wa ndoa.
Mickey akamuoa tena Elizabeth na maisha kuanza tena. Akaachana na C.I.A, akawa mwanaume huru aliyeanzisha biashara nyingi na kuuendelezea ubilionea aliokuwa nao.
Kwa nchini Tanzania, mara baada ya kupewa maelezo juu ya mauaji yaliyokuwa yametokea kwamba yalikuwa chini ya Marekani, Gideon akaachiwa huru na kurudi nchini Malawi ambapo huko akaendeleza upelelezi wake mpaka kumtia mikononi bwana Timoth.
Mpaka ilipofikia mwaka 2013, bwana Mickey, huku akiwa chini ya jina la Stefan, akafanikiwa kupata mtoto wake wa pili wa kike aliyempa jina la Lindsey.
MWISHO
TOA MAONI YAKO
CHANZO : BURE SERIES
Ok![]()
SIMULIZI HII IMEKAMILIKA
IMEANDIKWA NA : NYEMO CHILONGANI
CHANZO : BURE SERIES
SEHEMU YA KWANZA
Matangazo yalikuwa yamebandikwa kila kona ndani ya Jiji la Dar es Salaam yaliyokuwa yakihusu ujio wa mjasiriamali mkubwa, Potter Mickey aliyejulikana duniani kote kutokana na mafundisho yenye nguvu ya kuwafanya watu kujishughulisha na biashara na mwisho wa siku kufanikiwa.
Huyu alikuwa mjasiriamali mwenye nguvu kubwa ya ushawishi, mjasiriamali aliyejitengenezea jina kubwa duniani kote kutokana na masomo yake yaliyoleta mabadiliko makubwa katika jamii.
Mickey alikuwa miongoni mwa watu mashuhuri duniani, kazi yake kubwa ilikuwa ni kuwahamasisha watu wengi kuweka nguvu kubwa katika biashara na hatimae kufanikiwa kwa kiasi kikubwa.
Japokuwa alikuwa Mmarekani lakini hakuwa mtu wa kutulia tu nchini mwake, leo alikuwa Afrika Kusini, wiki ijayo Uingereza, mara Urusi na sehemu nyingine duniani zikiwepo nchi za Kiarabu.
Ingawa lilikuwa ni jambo gumu kwa Waarabu kuwaruhusu Wamarekani kuingia nchini mwao kiholela lakini kwa bwana Mickey lilikuwa jambo jepesi sana, kila alipotaka kuingia katika nchi hizo zilizokuwa katika Umoja Waarabu wa Emirate, aliruhusiwa bila tatizo lolote lile.
Alizunguka kuanzia Dubai, Fujairah, Abu Dhabi, Ajman na sehemu nyingine katika nchi zilizokuwa katika umoja wa Kiarabu wa Emirate, huko kote alikuwa akihubiri kuhusiana na namna ambavyo mtu anaweza kufanya ili kufanikiwa katika biashara zake.
Mbali na nchi hizo, pia Mickey alitembelea nchi zilizokuwa Asia kama Iran, Iraq, China na sehemu nyingine, kote huko bado alikuwa akihubiri kuhusu ujasiriamali katika kufanikiwa.
Mickey alipendwa, mahubiri yake yalimfurahisha kila mtu aliyekuwa akimsikiliza, mara kwa mara alikuwa akipokea mialiko kutoka katika nchi za Kiarabu, wote walikuwa wakinufaishwa na mahubiri yake na hivyo kuyatumia katika biashara zao za mafuta.
Baada ya kuzunguka katika nchi za Kiarabu kwa kipindi kirefu, bwana Mickey akahama na kuhamia barani Ulaya, kama kawaida yake bado mahubiri yake yalikuwa gumzo kwa kila mtu aliyeyasikia.
Aliendelea kuwasisitizia watu kwamba paundi moja waliyokuwa nayo ambayo ilikuwa ni kiasi kidogo cha fedha kingeweza kuyabadilisha maisha yao na kuwagawia mabilioni ya paundi.
Kwa maneno yake ya harakaharaka, ilionekana kuwa ngumu sana lakini alipokuwa akifafanua namna ambavyo hiyo paundi moja ilivyotakiwa kutumika na kuzalisha mabilioni, kila mtu alibaki akishangaa na kukubaliana naye.
“This is the man of God,” (Huyu ni mtu wa Mungu) alisikika jamaa mmoja akiwaambia wenzake.
“Yes! His words change me positively from one step to another” (Ndiyo! Maneno yake yamenibadilisha kutoka hatua moja kwenda nyingine) alisema jamaa mwingine.
Kila alipokwenda, Mickey aliacha sifa kubwa, watu walikuwa wakimpenda huku wengi wakimuita mhamasishaji wa utajiri kwa masikini bila kuwa na ubaguzi wowote ule. Sifa zake hizo ndizo zilizomfanya kupokea mialiko mingi katika nchi nyingine nyingi.
Kila alipokuwa akienda, aliongozana na mkewe, Elizabeth ambaye alionekana kuwa mtu muhimu kuliko wengine. Kupitia mafundisho yake, akajikuta akijiingizia kiasi kikubwa cha fedha, vitabu vya ujasiriamali kama Think like A Businessman, Walking With Success vilimuingizia fedha nyingi ambazo alizitumia kuwasaidia watu waliokuwa na matatizo mbalimbali kama umasikini na wagonjwa.
Baada ya kuzunguka duniani kwa kipindi kirefu, akahitaji muda wa kupumzika, akili yake ilichoka, hakutaka tena kusafiri na kwenda sehemu nyingine kufanya mafundisho yake, kwa wakati huo, alihitaji kuipumzisha akili yake tu.
Kichwa chake kikalifikiria Bara la Afrika, sehemu ambayo ilikuwa na vivutio vingi. Alichokifanya ni kufungua kompyuta yake ili kuangalia ni nchi gani alitakiwa kwenda kwa ajili ya mapumziko hasa katika majira ya joto kama hayo, akaichagua nchi ya Tanzania.
“We are going to Tanzania once again” (Tunakwenda Tanzania kwa mara nyingine) alisema Mickey, alikuwa akimwambia mke wake, Elizabeth.
“What am I suppose to do?” (Natakiwa kufanya nini?) aliuliza Elizabeth.
“You have to tell Victor that we are going to meet with him there,” (Unatakiwa kumwambia Victor kwamba tunakwenda kukutana naye huko) alisema bwana Mickey.
“No problem.” (Hakuna tatizo)
Victor alikuwa mtoto wao aliyekuwa akisoma katika Chuo cha Mississippi nchini Marekani. Kama alivyokuwa baba yake, hata naye alikuwa akisomea mambo ya biashara ili baadae aje kuwa mfanyabiashara mzuri na mhamasishaji kuhusu ujasiriamali.
Uwezo wake chuoni haukuwa mdogo, Victor alikuwa akifaulu sana masomo yake, alikuwa miongoni mwa watu waliokuwa wakifanya vizuri kabisa katika masomo yote. Kila siku alikuwa akitumia dakika ishirini kuwaambia wanachuo wengine ni kwa namna gani walitakiwa kuyabadilisha maisha yao na mwisho wa siku kuwa mabilionea.
Kama alivyokuwa baba yake, naye alitokea kupendwa na kuwa mhubiri mzuri kuhusu mambo ya biashara kiasi kwamba wanachuo wengine walisema kwamba Victor alikuwa zaidi ya baba yake.
Ingawa alipanga kuja Tanzania kupumzika na mkewe lakini mara baada ya maprofesa wa Chuo Kikuu kusikia kwamba bwana Mickey alikuwa akija ndani ya nchi hiyo, wakaandaa tamasha lake kwa ajili ya mafundisho ya ujasiriamali kwa ajili ya wanachuo wa chuo hicho.
“Kuna kazi nimepewa,” alisema bwana Mickey.
“Kazi gani?”
“Natakiwa kwenda kuwafundishi wanachuo kuhusu ujasiriamali.”
“Wapi? Uarabuni kama kawaida?”
“Hapana. Hukohuko Tanzania tunapokwenda.”
“Mmmh! Lakini hiki si ndiyo kipindi chetu cha mapumziko mpenzi!”
“Najua hilo, lakini haina jinsi, sijawahi kufundisha nchini Tanzania, mara nyingi tumekuwa tukienda kule na kupumzika, naomba uniruhusu tu nifanye kitu kama hicho,” alisema Mickey kwa sauti ya upole.
“Mpenziiiiiii...”
“Naomba uniruhusu, siku mbili tu.”
“Lakini kw.....”
“Si zaidi ya siku mbili mpenzi, naomba uwape nafasi watu wengine nao watajirike.”
“Sawa. Ila niahidi, siku mbili!”
“Nakuahidi.”
Mickey akamsogelea mke wake, Elizabeth na kumkumbatia. Alikuwa akifanya mambo mengi katika maisha yake lakini mengi aliyokuwa akiyafanya, ilikuwa ni lazima kumshirikisha mkewe. Alimpenda mwanamke huyo, alimthamini na kumjali kwa kila kitu.
Ingawa alikuwa na ndugu, marafiki lakini mke wake ndiye alikuwa kila kitu, kila nchi aliyokwenda kufundisha ilikuwa ni lazima aende na mke wake huyo aliyekuwa mtu muhimu kuliko watu wote katika maisha yake.
Baada ya wiki moja safari ya kwenda nchini Tanzania ikaanza. Ndani ya ndege, kila mmoja alionekana kuwa na furaha, kila wakati walikuwa wakikumbatiana tu, hakukuwa na kitu ambacho kwao kilionekana kuwa cha thamani kama kuwa karibu.
Waliishi pamoja kwa miaka thethini na tano, walizoeana na mapenzi yao kukua kadiri siku zilivyozidi kwenda mbele, hawakuwa watu wa kugombana mara kwa mara, kila mmoja alipokuwa akifanya kosa, alikubali kwamba alikosea na aliomba msamaha.
Baada ya wiki moja, safari ya kuelekea nchini Tanzania ikaanza. Ilikuwa ni safari ndefu na yenye kuchosha lakini baada ya masaa ishirini na tano, ndege ya Shirika la Ndege la American Airlines ilikuwa ikitua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere.
Hali ya hewa ilikuwa ni ya joto sana, kwa kuwa safari hiyo ilihusiana na ufundishaji wa ujasiriamali chuoni, maprofesa walikuwa uwanjani hapo kwa ajili ya kuwapokea. Mapokezi yalifanyika vizuri, walipoona kila kitu kimekamilika, wakawachukua na kuelekea hotelini kwa ajili ya mapumziko kabla ya kuanza kwa semina ya ujasiriamali iliyokuwa ikitangazwa sehemu zote jijini Dar es Salaam kwa kubandika matangazo mbalimbali.
****
Wanachuo wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam walikuwa wamejiandaa kwa ajili ya kusikiliza mafundisho juu ya namna ya kuwa bilionea kutoka kwa mhamasishaji mashuhuri aliyekuwa akifanya ziara zake mbalimbali duniani, bwana Potter Mickey.
Kila mmoja alikuwa na kiu ya kufanikiwa, kitendo cha kuambiwa kwamba shilingi elfu moja waliyonayo inaweza kuwafanya kutajirika na kuwa na mabilioni ya shilingi, kuliwachanganya watu.
Siku iliyofuata, wanafunzi wengi walikuwa wamekusanyika katika Jengo la Nkurumah kwa ajili ya kumsikiliza mhamasishaji huyo aliyetarajiwa kuingia chuoni hapo muda mchache ujao.
Idadi hiyo kubwa ya watu waliokuwa wamekusanyika ndani ya jengo hilo, liliufanya ukumbi huo kuwa mdogo kwani si wanachuo peke yao waliokuwa mahali hapo bali hata watu wengine kutoka sehemu nyingine walikuwa ndani ya jengo hilo.
Vitabu vyake vya ujasiriamali vya bwana Mickey viliendelea kuuzwa ukumbini, kila mtu alitaka kuwa navyo, kutoa shilingi elfu ishirini kwa ajili ya kuwa na vitabu hivyo viwili wala haikuonekana kuwa tatizo hata kidogo.
Baada ya dakika thelathini, bwana Mickey akafika chuoni hapo huku akiwa na mkewe. Watu wakaanza kushangilia, kuonekana tu ndani ya chuo hicho, tayari watu wakapata matumaini mapya, wale wasiokuwa na fedha wakajiona kuanza kupata utajiri.
“Daah! Huyu jamaa ni noma sana, unajua nilianza kufuatilia mafundisho yake kwa njia ya vitabu toka mwaka juzi, jamaa anatisha, amenifanya na mimi kuwa mtu miongoni mwa watu kwa kuwa na biashara nyingi,” alisikika mwanachuo mmoja, alikuwa kijana lakini mwenye biashara nyingi.
“Kumbe ulipata ujuzi kutoka kwa huyu jamaa?” aliuliza mwanachuo mmoja.
“Ndiyo! Yaani ukimsikiliza na kuvisoma vitabu vyake, utapenda.”
“Hebu ngoja na mimi nimsikilize, naweza kupata kitu,” alisema jamaa huyo.
Siku hiyo, watu walijifunza mambo mengi kuhusiana na biashara, kila neno alilokuwa akilizungumza bwana Mickey, lilionekana kuwa msingi mkubwa kwa wanachuo waliokusanyika mahali hapo.
Alijua kuzungumza na watu, kadiri alivyoendelea kuongea na ndivyo ambavyo watu walitamani aendelee kuzungumza zaidi na zaidi. Alionekana ni mtu mwenye mafanikio makubwa ambaye alikuwa akitaka kuwaona watu wakifanikiwa na kuwa mamilionea wakubwa duniani.
Hakutaka kuwaona watu wakiwa masikini, aliamini kwamba kila mtu duniani alikuwa na uwezo mkubwa wa kupata fedha kwa kufanya biashara, hivyo nafasi hiyo alikuwa akiitumia vilivyo kwa kuwaambia watu ni kwa namna gani walitakiwa kuanza na kiasi kidogo cha fedha walichokuwa nacho.
Siku hiyo, kila mtu akaonekana kumuelewa bwana Mickey ambaye alikuwa akizungumza hatua kwa hatua kama ambavyo mtu anaweza kumuhadithia mtoto mdogo kitu fulani. Baada ya kufanya semina hiyo kwa saa moja na nusu, akamaliza na kuomba kuondoka.
“Nitakwenda kuwa tajiri, nipe miaka miwili,” alisema mwanachuo mmoja.
“Mawazo yako ni kama mimi, pia nitakwenda kuwa tajiri mkubwa,” alisema jamaa mwingine.
Maneno yake yakawatia watu hamasa, kila mmoja alijiona kuwa na uwezo mkubwa wa kufanya biashara na kufanikiwa na mwisho wa siku kuwa mfanyabiashara mkubwa nchini, yaani ilikuwa ni sawa na mtu aliyeangalia filamu za mapigano za kina Jackie Chan na mwisho wa picha, akitoka nje kujiona kuwa na uwezo wa kupigana kama mcheza filamu huyo.
Siku hiyo bwana Mickey na mkewe wakarudi hotelini ambapo wakafanya mambo yao na kujiandaa kwa ajili ya siku ya pili na ya mwisho ya semina hiyo iliyotakiwa kufanyika palepale chuoni ili waendelee na ishu zao za mapumziko kama walivyotarajia.
Siku hiyo ilipofika, bwana Mickey akaonekana kuwa tofauti kabisa, hakuwa na furaha kama siku iliyopita, kila wakati alionekana mtu wa mawazo kupita kawaida kitu kilichomtia hofu mke wake, bi Elizabeth.
“Kuna nini?”
“Hakuna kitu mke wangu!”
“Hapana, niambie kuna nini, umebadilika sana!”
“Sijajua kwa nini, lakini kiukweli hakuna kitu, endapo kungekuwa na kitu, nisingeweza kukuficha mke wangu!” alisema bwana Mickey.
Japokuwa aliambiwa na mume wake kwamba hakukuwa na kitu chochote kibaya lakini moyo wake haukuonekana kuridhika hata kidogo, naye akajikuta akiingia katika huzuni.
“Unakumbuka kwamba Victor anaingia leo usiku?” aliuliza bi Elizabeth.
“Yeah! Nakumbuka sana kipenzi. Tutakwenda kumpokea na vitu vingine viendelee, kwanza tumalize hii semina,” alisema bwana Mickey.
Siku hiyo ya pili na ya mwisho ndiyo ilionekana kuwa balaa. Watu walifurika mara mbili ya siku iliyopita, zaidi ya watu elfu moja walihitaji kumsikia mhamasishaji huyo kutoka nchini Marekani.
Ukumbi wa Nkurumah ukawa mdogo kiasi kwamba kwa haraka sehemu ikabadilishwa na kupelekwa katika uwanja wa mpira chuoni hapo ili kila mtu apate nafasi ya kumsikiliza mtu huyo.
“Hapa poa sasa, hewa safi na ukitaka hata juu ya mti unakaa, full kujiachia tu,” alisema jamaa mmoja.
Kutokana na sehemu hiyo kuwa na miti mingi, wapo wanachuo ambao walipanda juu ya miti na kuanza kumsikiliza bwana Mickey aliyekuwa akiongea kwa uchungu wa kuwataka watu watoke pale walipokuwa na kusonga mbele.
Siku hiyo alizungumza mambo mengi ambayo yote yalionekana kuwa faida kwa kila mtu aliyekuwa akimsikiliza.
“One day my father gave me fifty cent that changed my life forever. I know, it is very difficult to believe me but let me tell you what I did. I asked myself abo.....” (Siku moja baba yangu alinipa senti hamsini iliyobadilisha maisha yangu milele. Najua ni vigumu mno kuniamini lakini acha nikwambie kile nilichokifanya. Nilijiuliza kuh....) alisema bwana Mickey lakini hata kabla hajamaliza sentensi yake, ukasikika mlio wa risasi mahali hapo.
“Paaaaaa.....” mlio mkubwa wa risasi ukasikika, bwana Mickey akaangua chini, damu zikaanza kumtoka kichwani kwake, kama alivyokuwa ameanguka, aliishia hivyohivyo na hakuweza kuutingisha mwili wake.
Watu waliokuwa mahali hapo, mara baada ya kusikia mlio wa risasi ile, wakaanza kukimbia hovyo, wale waliokuwa juu ya miti, ghafla wakajikuta wakiwa chini bila kujua wameshukaje na kuanza kukimbia.
Lilikuwa ni moja ya tukio lililoogopesha, mlio wa risasi uliokuwa umesikia, haukuonekana kuwa wa kawaida, ulikuwa na sauti kubwa kiasi kwamba baadhi ya watu walihisi kwamba lilikuwa bomu.
Kila mmoja akakimbia na ni bi Elizabeth peke yake ndiye aliyekuwa amebaki mahali hapo, aliuhisi mwili wake ukiwa umepigwa ganzi, picha aliyokuwa akiiona kwamba mume wake alikuwa chini, damu zilikuwa zikimtoka kichwani baada ya risasi kupenya kwenye paji la uso wake na kutokea nyuma, ilikuwa ni moja ya picha yenye kutisha ambayo hakuwahi kuiona maishani mwake.
Hapohapo akaanza kumkimbilia mume wake pale chini, hakukuwa na wa kumsaidia, kila mtu alikuwa amekimbia kuyaokoa maisha yake.
“Mickey...Mickey...please wake up, dont’t leave me alone, wake up my husband...wake up and look at me....” (Mickey...Mickey...tafadhali amka, usiniache peke yangu, amka mume wangu...amka na uniangalie...) alisema bi Elizabeth huku akilia kama mtoto.
Aliushika mwili wa mume wake pale chini, hakuwa akiamini kile kilichokuwa kimetokea, wakati mwingine alifikiri kwamba alikuwa ndotoni na baada ya dakika chache angeamka na kujikuta akiwa kitandani, chumbani na mumewe lakini ukweli ulibaki palepale kwamba hakuwa kwenye maisha ya njozi, kila kilichokuwa kikitokea, kilitokea katika maisha halisi.
Baada ya dakika tano kuona kwamba kila kitu kilikuwa shwari, wale watu waliokuwa wamekimbia wakaanza kujikusanya mahali hapo ili kuona ni kitu gani kilikuwa kimetokea.
Bi Elizabeth alikuwa jukwaani, bado alikuwa ameushika mwili wa mume wake huku akilia kama mtoto, muda wote alikuwa akimtaka aamke kwani hakuwa akiamini kama alikuwa amefariki dunia.
“Kuna nini?” aliuliza jamaa mmoja, alikuwa akiangalia huku na kule, hakuwa akijiamini.
“Mmmh! Sijui, mimi nilisikia paaa, baada ya hapo nikajikuta nipo barabarani,” alisema jamaa mwingine.
“Hivi ilikuwa risasi au bomu?”
“Mmmh! Wala sijui!”
Bi Elizabeth alikuwa akiendelea kulia, moyo wake ulikuwa kwenye maumivu makali, bado hakuwa akiamini kile kilichokuwa kimetokea, kila aliyekuwa akimwangalia mahali hapo, alimuonea huruma, wala hazikupita dakika nyingi, akaanguka chini na kupoteza fahamu, hakujua ni kitu gani kiliendelea baada ya hapo.
****
Mwili wa bwana Mickey ulikuwa chini, damu zilikuwa zimetapakaa katika jukwaa lile, watu walibaki wakishangaa tu kana kwamba hawakuwa wakifahamu ni kitu gani kilichokuwa kikiendelea mahali hapo.
Maprofesa wakapiga hatua mpaka katika jukwaa lile, pembeni ya mwili wa bwana Mickey kulikuwa na mke wake ambaye alipoteza fahamu kutokana na mshtuko mkubwa alioupata baada ya kushuhudia mume wake kipenzi akiwa amepigwa risasi mbele ya macho yake.
Gari la mtu binafsi likasogezwa na kumchukua bi Elizabeth na kuondoka naye huku wakiuacha mwili wa bwana Mickey palepale ulipokuwa. Ndani ya dakika kadhaa, polisi wakafika na baadhi ya watu kutoka katika kitengo cha upelelezi, walichokifanya ni kuupiga picha mwili ule na kuchukua vipimo vyote ambavyo walitakiwa kuvichukua, baada ya hapo, wakauchukua na kuondoka nao.
Ilikuwa ni taarifa iliyoshtua mno, hakukuwa na mtu aliyeamini kama kweli mhamasishaji huyo kutoka nchini Marekani alikuwa ameuawa nchini Tanzania. Taarifa hizo ziliendelea kusambazwa na ndani ya kipindi kichache tu, dunia nzima ikafahamu kile kilichokuwa kimetokea katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Dunia nzima ikaanza kuilalamikia Tanzania kwa kutokuwa makini katika kudumisha ulinzi wa nchi yao, kitendo kilichokuwa kimetokea kilimsikitisha kila mtu na kuendelea kuilaumu nchi hiyo.
Marekani haikutaka kukaa kimya, wakatoa tamko ambalo walitaka litelekezwe mara moja na nchi ya Tanzania kwamba muuaji aliyemuua bwana Mickey anapatikana na kufikishwa katika vyombo vya sheria.
“Kimenuka!”
“Kuna nini?”
“Umewasikia wakina Obama huko?”
“Wamesemaje?”
“Wamesema wanataka kumjua muuaji, sijui kama ataweza kupatikana.”
Tamko la Marekani walilokuwa wamelitoa likaanza kuwa gumzo, kila mtu alilizungumzia kitu ambacho kwa kiasi kikubwa kikaleta hofu katika serikali ya Tanzania. Magazeti yakaandika sana kuhusu agizo hilo lililotakiwa kufanyiwa kazi mara moja na ripoti kutolewa.
“Mmesikia kilichosemwa?” aliuliza kamanda wa jeshi la polisi, bwana Kizota.
“Tumesikia.”
“Tunahitaji kumpata huyu mtu, iwe isiwe, ni lazima apatikane. Naliacha jukumu hili kwenu, nataka ndani ya siku mbili, muuaji ajulikane, na ndani ya wiki moja, muuaji huyo apatikane! Mmenielewa?” aliuliza kamanda Kizota.
“Tumekuelewa mkuu.”
Taarifa zikapelekwa mpaka katika kitengo cha upelelezi, TISS (Tanzania Internal Security Service) ambapo huko wakaandaa watu wawili kwa ajili ya kupeleleza na kujua ni mahali gani mtu huyo alipokuwa.
Mtu mmoja miongoni mwa wale waliokuwa wamechaguliwa aliitwa Martin Subian, alipewa jukumu la kumjua mtu huyo, alikuwa akiishi wapi na mtu wa pili ambaye naye alichaguliwa katika jukumu hilo la kumtafuta muuaji alikuwa ni Mathias Jonathan, kazi yake kubwa ilikuwa ni kumpata mtu huyo na kumtia nguvuni.
Siku iliyofuata, asubuhi na mapema Martin akaanza safari ya kuelekea chuo kikuu kwa lengo la kupata taarifa zote zilizokuwa zikimhusu mtu huyo, alikuwa nani, alikuwa katika eneo gani alipokuwa akimpiga risasi bwana Mickey na kwa nini alifanya hivyo.
Alipofika chuoni, moja kwa moja akaunganisha mpaka kwa Professa Ahmed Mitimingi na kuanza kuzungumza naye. Kwa kumwangalia Martin, hakuonekana kama alikuwa kijana shupavu, mwenye nguvu, alionekana kuwa hohehahe ambaye hata kama ungemuona basi ungeweza kusema kwamba una uwezo mkubwa wa kupambana naye na ukampiga.
“Ninaitwa Martin Subian kutoka TISS,” alisema Martin huku akitoa kitambulisho chake na kumkabidhi Professa Mitimingi. Akakichukua na kukiangalia, aliporidhika, akamtaka kuendelea kuzungumza.
“Ninataka kufahamu eneo alilouliwa bwana Mickey,” alisema Martin.
“Hakuna tatizo, twende.”
Wawili hao wakainuka na kutoka nje, hakukuwa na mtu aliyegundua kwamba mtu aliyekuwa akiongozana na Profesa Mitimingi alikuwa mtu hatari kwa kupambana na watu hata kama walikuwa watano.
Alionekana nadhifu, suti nyeusi lakini kiunoni alikuwa na bunduki iliyofichwa ambapo kama hali ingechafuka bunduki hiyo ingeingia katika matumizi wakati wowote ule. Hawakuchukua muda mrefu, wakafika uwanjani hapo.
“Hapa ndipo alipouawa.”
“Sawa. Jukwaa lilikuwa wapi na aligeukia wapi?” aliuliza Martin.
“Twende nikupeleke jukwaa lilipokuwa.”
Wakaendelea kupiga hatua mpaka sehemu kulipowekwa jukwaa lile, bado alama za vyuma vilivyokuwa vimechimbwa kwa chini zilionekana. Martin akasimama sehemu ile na kuangalia upande ambao bwana Mickey alikuwa akiangalia.
Muda wote huo Martin alikuwa kimya, alikuwa akiangalia huku na kule huku akionekana kujifikiria kitu. Kichwa chake kikianza kuivuta picha ya bwana Mickey, aliikumbuka vilivyo kwamba risasi ilipenya katika paji lake la uso na kutokea kichogoni.
Alisimama usawa mzuri na kuanza kuangalia sehemu ambayo ilikuwa ni nyepesi kwa mpigaji kupiga risasi ile.
“Bunduki iliyotumika ni Rifle yenye uwezo mkubwa wa kumpiga hata mtu aliyekuwa umbali wa mita mia mbili, ni bunduki iliyotengenezwa nchini Urusi ambayo mara nyingi hutumiwa na watu watunguaji wajulikanao kama snipers,” alisema Martin huku akiangalia kila kona maeneo hayo.
“Umejuaje?”
“Hakuna bunduki inayoweza kupiga umbali mrefu kama Rifle, hii ni bunduki iliyotengenezwa mahususi kwa ajili ya maadui wanaokaa kwa umbali mkubwa, na hii ndiyo iliyotumika mahali hapa,” alijibu Martin.
“Kulikuwa na watu wengi mahali hapa, sasa inawezekana vipi mpigaji kuwa karibu na mlengwa?”
“Mpigaji alikuwa mbali na ndiyo maana nilisema alitumia bunduki hii kwa kuwa ilikuwa na uwezo wa kupiga kitu kilichokuwa hata umbali wa mita mia mbili. Kama bwana Mickey alisimama hapa na kupigwa risasi upande huu, ina maana mpiga alisimama kule,” alisema Martin.
“Mmh! Huku kote kulijaa watu!”
“Najua, atakuwa alisimama kule porini. Unapaona?”
“Napaona, ila sidhani.”
“Twende nikuonyeshee.”
Wakatoka mahali hapo na kuelekea katika kichaka kilichokuwa umbali wa mia mia moja. Baadhi ya wanachuo walikuwa wakiwaangalia tu. Kila walipokuwa wakipiga hatua, waliwafuatilia kwa ukaribu pasipo kujulikana.
Prosefa Mitimingi na Martin wakafika katika kichaka kile kile kidogo na kuingia ndani. Martin akasimama na kuanza kuangalia kule kulipowekwa jukwaa, alipaangalia kwa umakini, alipoona amekosea, akasimama pembeni kidogo, alipoona hajakaa sawa, akaelekea pembeni kidogo mpaka alipojiona amekaa sawa na sehemu ile aliyosimama bwana Mickey kule jukwaani.
“Mpigaji alikuwa mahali hapa,” alisema Martin maneno yaliyomfanya Profesa Mitimingi kushtuka.
“Umejuaje?”
“Subiri.”
Martin akainama chini na kuanza kuyaangalia majani vizuri. Hali ya utofauti ilionekana katika majani yale. Majani ya upande mwingine yalikuwa yamesimama lakini majani ya pale alipokuwa ameinama yalikuwa yamelala kuonyesha kwamba kulikuwa na mtu aliyalalia.
“Unaona...majani yamelala, kuna mtu alikuwa mahali hapa, bila shaka ndiye huyo muuaji,” alisema Martin.
“Mmmh.”
“Subiri.”
Martin akaanza kutafuta kitu mahali pale, hakutulia, kila wakati alikuwa akipekua huku na kule, alionekana kuwa bize kupita kawaida. Wala haukuchukua muda mrefu, akakuta ganda la risasi likiwa mahali hapo, akalichukua na kuanza kuliangalia, Professa Mitimingi alikuwa kimya akimwangalia.
“Nini hicho?”
“Hili ni ganda la risasi, lisome lilivyoandikwa,” alisema Martin huku akimpa ganda lile na kuliangalia, liliandikwa Rifle 07T, bunduki kali iliyotoka nchini Urusi.
Kila kitu alichokuwa akikisema Martin mahali pale, Professa Mitimingi alikuwa akishangaa na kujikuta akimkubali kijana huyo kwamba alitoka TISS. Waliendelea kukaa kule huku akiambiwa vitu vingi, baada ya hapo, wakarudi ofisini.
“Nadhani nimekuonyeshea mengi na kukufundisha mengi, nahitaji kitu kimoja kutoka kwako,” alisema Martin.
“Kitu gani?”
“Kumjua mtu aliyepiga risasi hiyo.”
“Mmmh! Ni vigumu kufahamu.”
“Ulikuwepo wakati wa tukio?”
“Ndiyo! Nilikuwepo.”
“Hukumuona?”
“Hapana, sikumuona.”
“Hapana! Hebu vuta kumbukumbu, kumbuka vizuri, kumbuka kuanzia mwanzo mpaka mwisho,” alisema Martin.
“Kweli sikuweza kumuona.”
“Hapana. Hebu jaribu kukumbuka, vuta picha, kumbuka kuhusu kichaka kile, jaribu kukumbuka, nahisi nitapata picha. Kumbuka vizuri.”
Profesa Mitimingi akabaki kimya, ni kweli alijitahidi kuvuta picha zaidi, kila alipokuwa akikumbuka, hakukumbuka kumuona mtu kama huyo.
“Unasema ulikuwa jukwaani?”
“Ndiyo!”
“Hebu kumbuka vizuri, hakuna mtu aliyekwenda kule kichakani? Kumbuka, vuta kumbukumbu,” alisema Martin.
Prosessa akabaki kimya, alionekana kujifikiria kitu. Alijitahidi kukumbuka kila kitu kilichotokea siku ile katika uwanja ule. Alivuta kumbukumbu, alizivuta zaidi na zaidi mpaka akaonekana kushtuka.
“Mmmh!” alibaki akiguna.
“Niambie umekumbuka nini.”
“Kuna mtu alikwenda katika pori lile kukojoa, namkumbuka sana, alikuwa akiishikashika zipu ya suruali yake, mgongoni alibeba begi,” alisema Professa.
“Unamfahamu mtu huyo?”
“Mmmh! Hapana.”
“Bado! Jaribu kukumbuka.”
“No! Kuna mtu nilimuona akielekea kule, lakini sikuwa nikimfahamu kabisa, nilipomuona akiishikashika zipu ya suruali yake, niligundua kwamba alitaka kukojoa, nilitaka kumtuma mtu akamwambie kwamba hairuhusiwi kukojoa vichakani, sasa sijui kwa nini nilipuuzia,” alisema Professa Mitimingi.
“Umesema alibeba begi, alibeba begi rangi gani?”
“Lilikuwa jekundu, sikumbuki lilikuwa la aina gani.”
“Sawa. Kidogo maelezo yako yanaweza kufaa. Alivaa nguo za aina gani?’
“Nakumbuka ilikuwa jinzi nyeusi na fulana nyekundu.”
“Hivyo tu?”
“Hapana, alikuwa na kofia nyeupe,” alijibu professa.
“Sawa.
Professa akabaki akijiuliza, ni kwa jinsi gani Martin alikuwa amemwambia akumbuke kitu fulani mpaka kumfahamu mtu aliyeingia ndani ya kichaka kile na wakati hakuwa akikumbuka kitu chochote kile, mpaka hapo, alijipa uhakika kwamba mtu aliyesimama mbele yake alikuwa hatari sana na hakuwa na mchezo hata kidogo.
“Umejuaje kama ningeweza kukumbuka?”
“Hakuna siri. Kwenye tukio lolote linalotokea jukwaani, wale watu waliokaa mbele ambao wanawaona watu wengi, ni lazima muuaji au mtu aliyefanya tukio fulani walikuwa wakimuona ila walimpuuzia, ndiyo inavyotokea kila siku. Hata ukimfuata mtu mwingine aliyekuwa jukwaani siku ile, atakwambia kwamba alimuona ila alipuuzia na ndicho kilichotokea kwako!” alisema Martin.
“Mmmh! Ni hatari sana. Kwa hiyo nini kinafuata?”
“Kumtafuita mtu huyo aliyevalia jinzi nyeusi, begi jekundu na kofia nyeupe.”
“Tunampataje?”
“Ni kazi nyepesi sana. Ila jua huyo mtu si Mtanzania.”
“Mmmh!”
“Ndiyo. Kwa sisi Watanzania hakuna mtu anayeweza kuitumia Rifle vizuri mpaka awe komandoo, ni moja ya bunduki zinazosumbua sana. Kama umeona mtu kaitumia na mpigo mmoja tu aliweza kumuua mhusika, jua huyo si Mtanzania, atakuwa mtu wa nje ya Tanzania, na kama ni Mtanzania, jua kwamba atakuwa komandoo kitu ambacho hakiniingii akilini,” alisema Martin.
“Mmmh! Sasa utampata vipi?”
“Ni kitu chepesi sana, kama kumsukuma mlevi mlimani, usiwe na wasiwasi, nataka kuonana na rais wa chuo hiki,” alisema Martin.
“Unadhani atakusaidia?”
“Ndiyo. Asilimia mia moja.”
“Hakuna tatizo.”
ITAENDELEA