SEHEMU YA KUMI ...... MWISHO
Mickey akapigwa na mshangao, kila alivyokuwa akimwangalia Stacie alishindwa kuelewa sababu iliyomfanya msichana huyo kuwa hivyo. Wakati mwingine akahisi vibaya kwamba msichana huyo alikuwa gaidi na hivyo alitaka kuulipua uwanja huo lakini wakati mwingine, alilitupilia mbali wazo lake na kuendelea na mambo yake.
Kwa kuwa alikuwa maarufu duniani kote, hata hapo nchini Uholanzi ilikuwa kero kwake, kila aliyemuona, alimfuata na kutaka kupiga naye picha huku wengine wakitaka kupewa ushauri juu ya biashara walizokuwa nazo, kwa kifupi, Mickey alichukia kuwa maarufu.
“Can you help me?” (Unaweza kunisaidia?) ilisikika sauti ya msichana mmoja, kimuonekano, alionekana kuwa miongoni mwa watu waliokuwa na mafanikio, wale waliopitia njia mbalimbali na ngumu mpaka kufanikiwa.
“What can I help you?” (Naweza kukusaidia nini?)
“My name is Candy, I’m enterprenuer, I have been passing through many problems in my business,” (Ninaitwa Candy, mimi ni mjasiriamali, ninimepitia matatizo mengi katika biashara zangu) alisema msichana yule.
Akabaki akizungumza na yule mwanamke. Alimueleza ukweli kwamba alikuwa na biashara nyingi na kubwa lakini kwa kipindi kirefu amekuwa akipata hasara kwani hakujua ni kwa namna gani angeweza kuzizuia fedha zake kutumika kwa kiwango kikubwa kama ilivyokuwa.
Kwa kuwa alikuwa mtu aliye na kiu ya kuwasaidia watu ili wanufaike na kile kiasi walichokuwa wakikipata, Mickey akaanza kumshauri mwanamke yule mpaka alipohakikisha kwamba alielewa kila kitu.
Hawakukaa sana hapo Uholanzi, baadae wakatakiwa kupanda ndege ya Shirika la Ndege la Qatar Airways kwa ajili ya kuendelea na safari yao mpaka Qatar. Kutoka hapo mpaka Qatar, walichukua masaa kumi, ndege ikaanza kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Hamad uliopo nchini humo katika Jiji la Doha na kisha kuchukuliwa na kupelekwa katika hoteli moja ya nyota tano.
Mickey alibaki akiyaangalia mandhari ya jiji hilo. Idadi ya watu haikuwa kubwa lakini ulikuwa moja ya mji uliokuwa safi huku kukiwa na majengo makubwa yalioufanya kupendaza na kuvutia mno.
Walipofika katika Hoteli ya Sultan Adesh, akateremka na kupelekwa katika chumba alichotakiwa kukaa. Mickey hakutulia, kila muda alikuwa kazini, kitu cha kwanza kabisa kukifanya kilikuwa ni kuchukua kompyuta yake ya mapajani na kuiunganisha na internet na kuanza kuangalia vitu alivyotaka kuviangalia muda huo.
Hakuchukua muda mrefu kuangalia vitu hivyo, akapitiwa na usingizi kwani tayari muda ulisomeka kwamba ni saa saba usiku.
****
Waarabu walitumia wiki nzima kumtangaza Mickey kwamba angeweza kufika nchini Qatar kwa ajili ya kutoa semina kubwa iliyohusu ujasiriamali. Walimjua, waliufahamu uwezo wake kwani hata kile kitabu alichokuwa amekitoa, walikinunua na kilionekana kuyabadilisha maisha yao kibiashara.
Kitendo cha kusema kwamba mtu huyo angeweza kufika Qatar, kiliwafanya matajiri wengi kutamani kuhudhuria huku kiingilio kikiwa kikubwa, zaidi ya riyal milioni moja ambayo ilikuwa ni sawa na milioni tano za Kitanzania.
Tiketi za kutosha zaidi ya elfu mbili zikaandaliwa na ndani ya siku mbili, tiketi zote zikawa zimekwisha huku watu wengine wakilalamikia kukosa, Hakukuwa na cha kufanya, kwa sababu mtu huyo angeweza kwenda mpaka Dubai, wale waliokosa tiketi basi wangekuwa na fursa ya kwenda huko kwa ajili ya kumsikiliza mhamasishaji huyo.
“What if Qaar Shalbaab come?” (Itakuwaje Qaar Shabaab wakija?) aliuliza jamaa mmoja.
“Impossible, we have enough security in here,” (Haiwezekani, tuna ulinzi wa kutosha mahali hapa) alisema jamaa mwingine.
Qaar Shalbaab lilikuwa moja ya makundi ya kigaidi yaliyokuwa yakiogopwa sana duniani. Kundi hili lililokuwa nchini Afghanistan, lilikuwa miongoni mwa yale makundi yaliyokuwa yakishambulia sehemu mbalimbali katika nchi za kiarabu kwa kutumia mabomu na hata kujitoa mhanga kwa kujilipua na mabomu waliyokuwa wakiyavaa miilini mwao.
Hawakuwa watu wazuri, kundi hili la kigaidi lililojificha katika Milima ya Tora Bola nchini humo lilikuwa likiongozwa na mtu aliyesadikiwa kuwa na roho mbaya kuliko watu wote duniani, huyu aliitwa Tawfaq Majid.
Wanawake wengi wa Kiarabu walikuwa wakivamiwa katika makazi yao na kubakwa huku wengine wakiteswa kwa kufanyiwa mambo ya kikatili. Wasichana wadogo wakaogopa kwenda shuleni kwani shule nyingi zilikuwa zikivamiwa na watoto wa kike kupigwa huku sheria kuu ya kundi hilo ikisema kwamba mtoto wa kike hakutakiwa kupata elimu.
Japokuwa sheria za nchi za Kiarabu kuwa ngumu, lakini kundi hilo lilizifanya sheria hizo kuwa ngumu zaidi. Kila siku msimamo wao ulikuwa mmoja kwamba nchi za Kiarabu zilitakiwa kukaliwa na Waarabu tu na hakutakiwa kuingia Mzungu yeyote ndani ya nchi hizo.
Mauaji hayakukoma katika nchi nyingi za Kiarabu, Wazungu wengi walikuwa wakiuawa kwa kuchinjwa hadharani jambo lililowafanya Wamarekani kuwa na chuki kubwa na kiongozi wa kundi hilo, Tawfaq Majid.
Huyo ndiye mtu aliyekuwa akitafutwa kipindi hicho, kichwa chake kilikuwa na thamani ya zaidi ya dola milioni mbili, zaidi ya shilingi bilioni nne za Kitanzania. Hakukuwa na mtu aliyekuwa akifahamu kama mtu huyo alikuwa akipatikana katika milima hiyo.
Mashirika mbalimbali ya kijasusi duniani likiwepo shirika la kijasusi lenye uwezo mkubwa dunia, ISI (Inter Services Intelligence) kutoka nchini Pakistan, yalifanya kila liwezekanalo kumpata kiongozi huyo au hata watu waliotoka katika kundi hilo lakini hawakufanikiwa.
Kila siku watu walizidi kuuawa, idadi ya watu waliokuwa wakijitoa mhanga ilizidi kuongezeka jambo lililozua hofu kubwa duniani. Hakukuonekana kuwa watu waliokuwa na nguvu za kuwatafuta watu hao ambao walizidi kuwa hatari kadiri siku zilivyozidi kwenda mbele.
Mataifa yote ya Kiarabu yalilichukia kundi hili lililoshikilia msimamo wake kwamba watoto wa kike hawakutakiwa kwenda shule na wala nchi za Kiarabu hazikuwa kambi za Wazungu.
“Nina wasiwasi nao,” alisikika jamaa mmoja.
“Kwa nini?”
“Wanaweza kuja kuanzisha vurugu, inabidi kuwe na ulinzi mkali hapa,” alisema jamaa huyo.
Hicho ndicho kilichofanyika, kwa sababu ndani ya ukumbi huo kulitarajiwa kuwa na watu wenye fedha zao, tena wengine wakiwa viongozi wa nchi, ulinzi mkubwa ukaimarishwa, hakukuwa na mtu yeyote aliyeruhusiwa kuingia na aina yoyote ile ya chuma huku wanawake waliokuwa wakivaa majuba wakichunguzwa kwa umakini kwa kuvuliwa nguo hizo katika vyumba maalum ili kuwaepuka wale waliojivisha mabomu kwa ajili ya kujilipua.
Siku ambayo semina hiyo ilitakiwa kuanza, ndiyo ambapo kundi hilo lililokuwa chini ya Tawfaq lilihisiwa kufanya shambulio ndani ya ukumbi huo huku lengo lao likiwa ni kumuua Mickey aliyekuja kwa ajili ya kazi ya upelelezi huku akitumia kivuli cha ujasiriamali.
Saa 4:05 asubuhi siku ya semina hiyo, tayari Mickey alikuwa amesimama mbele ya ukumbi huo, watu wengi walikuwa mbele yake kwa ajili ya kumsikiliza. Hakuonekana kuwa na wasiwasi, alizungumza huku akionekana kujiamini kwa kila neno alilokuwa akilitamka.
Watu walikuwa makini kumsikiliza, kila neno alilokuwa akilizungumza, lilionekana kuwa ‘nondo’ vichwani mwa watu, wengi wakajikuta wakitingisha vichwa vyao kutoka juu kwenda chini.
Ilipofika saa sita mchana, watu wakapata muda wa mapumziko, hapo, walikunywa na kula, kila kona, walikuwa wakimzungumzia Mickey, alionekana kuwa na uwezo mkubwa wa kuyafafanua yale aliyokuwa akiyazungumza, baada ya nusu saa, semina ikaendelea kama kawaida.
“Mbona nasikia kelele, kuna nini?” aliuliza jamaa mmoja, alikuwa karibu na mlango wa kuingilia ukumbini humo.
“Kuna mwanamke anataka kuingia, hebu njoo kwanza,” alisema jamaa mwingine, alitoka huko mlangoni na kuja kuwaita wenzake.
Malumbano yalikuwa yakiendelea baina ya walinzi hapo mlangoni na mwanamke aliyefika mahali hapo huku akiwa amevaa juba jeusi jeusi na hijabu kichwani. Alitaka kuingia kinguvu, japokuwa walinzi walikuwa wakimzuia, lakini alikuwa akilazimisha jambo lililozua hofu kubwa kwa kila mtu aliyekuwa hapo mlangoni.
“Twende kule...” alisema mlinzi mmoja.
“Wapi?” aliuliza mwanamke yule.
“Kwenye chumba maalum.”
“Kufanya nini?”
“Kukupekua, hivyo ndivyo tunavyofanya kwa kila mwanamke anayetaka kuingia ndani.”
“Haiwezekani.”
“Haiwezekani nini?”
“Kwenda huko.”
“Basi napo hautakiwi kuingia humu,” alisema mlinzi.
“Hapana! Nitaingia tu.”
Bado mwanamke yule alikuwa aking’ang’ania kuingia ndani ya ukumbi ule pasipo kukaguliwa. Hawakujua sababu iliyomfanya kukataa lakini kosa kubwa walilolifanya, mashine ya kuchunguzia kama mtu alikuwa na kitu cha chuma au silaha yoyote ilikuwa ndani ya jengo lile, umbali kadhaa kutoka katika chumba kile kikubwa kilichokuwa kikifanyikia semina ile.
Walinzi walijitahidi kumzuia mwanamke yule lakini naye alikuwa mbishi, hakutaka kukubaliana nao, aliendelea kubishana nao, lakini huku kila mmoja akiwa hajui ni kitu gani kilichotokea, ghafla, mwanamke yule akaanguka chini, kichwa chake kilikuwa kimefumiliwa kwa risasi, damu zilizokuwa zikimtoka kichwani, zikaanza kutapakaa katika sakafu, kila mmoja akaogopa, walipoangalia huku na kule, hakukuwa na mtu aliyeshika bunduki, kila mmoja akachanganyikiwa!
Hawakujua ni nani aliyekuwa amempiga risasi, wao walishtukia akiwa chini huku damu zikiendelea kumtoka, tukio hilo, liliwashangaza mno!
****
Wamarekani waliamua kutilia umakini katika kumlinda mtu wao, alikuwa mtu maalum ambaye walihakikisha kwamba angekamilisha kazi zote walizokuwa wamemuagiza katika nchi za Uarabuni.
Kila alipokuwepo, tayari ulinzi mkubwa ulikuwa umekwishawekwa hivyo alitakiwa kufanya kila kitu kwa kujiaminisha lakini mwisho wa siku walitaka kupata kile walichokuwa wakikitata.
Kitendo cha kuwa ndani ya ukumbi ule wa semina, tayari Wamarekani walikwishadumisha ulinzi wao kwa kutamani kumlinda mtu huyo kwa kitu chochote kibaya ambacho kingeweza kumtokea.
Nje ya hoteli hiyo, sehemu mbalimbali hasa maghorofani na hata kwenye vioo vya hoteli zilizokuwa karibu na eneo hilo, Wamarekani kutoka C.I.A walikuwa wamejaza titi madirishani huku wakiwa na bunduki zao zilizowekwa vyombo vya kuzuia mlio wa risasi, bunduki zenye nguvu zijulikanazo kama Riffle, bunduki maalumu zilizokuwa zikitumika na wadunguaji (snipers)
Mara baada ya kumuona mwanamke wa Kiarabu aliyevaa juba jeusi akizozana na walinzi waliokuwepo mlangoni, wakahisi kwamba kulikuwa na tatizo lililokuwa limetokea. Walichokifanya ni kuziweka vizuri ‘earphone’ zao ili kusikika mwanamke yule alikuwa akizungumza nini.
“Who is she?” (Ni nani?) aliuliza jamaa mmoja, alikuwa ameiweka vizuri bunduki yake huku akiwa amekwishamlenga mwanamke yule, alikuwa akizungumza na mwenzake aliyekuwa ghorofa nyingine.
“I don’t know,” (Sijui)
“Should I shoot her down?” (Nimpige risasi?)
“No! Just wait,” (Hapana! Subiri kwanza)
Bado walinzi waliendelea kuzozana na mwanamke yule kwamba ilikuwa ni lazima aende katika chumba maalum kwa ajili ya kupekuliwa ili aonekane kama alikuwa mtu salama au la, yeye hakutaka, aliendelea kusisitiza kwamba ilikuwa ni lazima kupita pasipo kukaguliwa.
“Just shoot her down,” (Mpige risadi tu)
Ulikuwa ni uamuzi ulioonekana kuwa sahihi, alichokifanya mwanajeshi yule wa Kimarekani ni kumpiga risasi mwanamke yule, risasi ya kichwa ilimpiga na kumwangusha chini na hapohapo kupoteza maisha hapohapo. Walinzi wale walipomwangalia vizuri kwa ndani, alikuwa amevalia kikoi kilichokuwa na mabomu kadhaa ya kujitoa mhanga.
Mickey aliendelea kutoa masomo ya ujasiriamali katika sehemu mbalimbali katika nchi za Kiarabu, tofauti na Wamarekani wengine, Mickey akatokea kupendwa na kuaminika zaidi ya mtu yeyote kitu kilichowapelekea Waarabu wengi kutaka mtu huyo aendelee kuishi nchini mwao.
Japokuwa alionekana mtu mwenye busara ambaye alizungumza taratibu mpaka kumuelewa, lakini hakukuwa na aliyegundua kwamba huyo Mickey alikuwa miongoni mwa watu wenye roho mbaya waliowahi kutokea katika Shirika la Kijasusi la C.I.A.
Hiyo ilikuwa ni safari yake ya kwanza, baada ya kumaliza semina yake iliyomchukua wiki nne, akarudi nchini Marekani ambapo moja kwa moja akaamua kumuoa msichana wake wa siku nyingi, Elizabeth Kenz na kuanza kuishi pamoja ambapo baada ya mwaka mmoja, wakapata mtoto wa kiume waliyemuita kwa jina la Victor.
Maisha yalikuwa mazuri, japokuwa aliishi na mume wake lakini hakuna hata siku moja Elizabeth aligundua au kuhisi kwamba mume wake, Mickey alikuwa jasusi wa Kimarekani aliyekuwa akiua watu kadiri alivyoagizwa.
Ilipofika mwaka 1993, Mickey akatumwa tena kwenda nchini Iran, lengo kubwa la kutumwa nchini humo lilikuwa ni kupeleleza ni kwa namna gani jeshi la Marekani lingeweza kupenya na kuingia katika nchi mbili, Iraq na Syria.
Hilo, kwake wala halikuwa tatizo, kwa sababu alikuwa mtu makini kwa kila alichokuwa akikifanya, akaelekea huko. Kitu cha kwanza kabisa alichokifanya mara baada ya kuwasili nchini humo ni kwenda katika kambi ya Wamarekani iliyokuwepo katika Mji wa Badhiir, pembezoni mwa nchi ya Iran upande wa Mashariki, sehemu ambayo iliaminika kama imelaaniwa kutokana na ardhi yake kuwa kavu kila wakati.
Alipofika huko, akakaribishwa na kuambiwa kwamba baada ya wiki moja kazi ilitakiwa ifanikiwe na hivyo kurudisha majibu mazuri nchini Marekani. Kwa kuwa alijiamini sana, siku iliyofuata, akaanza zoezi lake la kusafiri kwa kutumia ngamia jangwani ili aweze kufahamu ni sehemu gani jeshi lao lingeweza kupita ili kuingia katika nchi hizo.
Safari haikuwa nzuri, ilikuwa yenye kuchosha, alipita jangwa kwa jangwa, jua lilikuwa kali lakini yote hayo alivumilia kwa kuwa aliamini kwamba anafanya kazi kwa ajili ya nchi yake. Alitembea na ngamia yule mpaka alipofika katika sehemu iliyokuwa na mahema kadhaa, hapo, wakatokea Waarabu wawili waliokuwa na bunduki na kuanza kumsogelea.
“You American?” (Wewe ni Mmarekani?) aliuliza Mwarabu mmoja aliyetumia Kingereza cha kujifunza.
“Yes! Where Am I?” (Ndiyo! Nipo wapi hapa?) aliuliza Mickey.
Waarabu hao waliposikia kwamba mtu aliyesimama mbele yao alikuwa Mmarekani, miongoni mwa watu waliokuwa wakiwachukia, wakamuweka chini ya ulinzi na kumuingiza ndani. Mickey hakuonekana kuwa na wasiwasi, zaidi ya Waarabu kumi walisimama mbele yake na kuanza kuzungumza nao kwa kutumia Lugha ya Kiarabu aliyokuwa akiifahamu vizuri kitu kilichowafanya Waarabu wale kujiona kuwa na thamani, kitendo cha Mmarekani kuzungumza Kiarabu, wakajiona kuwa juu.
Mickey akaanza kuwaelezea kwamba alifika mahali hapo kwa kuwa alikuwa safarini kuelekea nchini Iraq hivyo hakujua ni njia ipi angeweza kupitia, njia ingemfanya kuwa nyepesi kuingia nchini humo pasipo kugundulika.
Alipoulizwa sababu zaidi, aliwaambia kwamba alikuwa mjasiriamali aliyekatazwa kuingia nchini humo ila kwa sababu asilimia kubwa ya watu waliokuwa wakiishi Iraq walikuwa masikini, alitaka kuzungumza nao na kuwaambia namna ambavyo wangeweza kufanya na hatimae kupata utajiri na kuwa wafanyabiashara wakubwa.
Maneno yake, sura yake ya huruma, tabasamu lake likawafanya Waarabu wale wamuamini kwa asilimia mia moja kwani hakuwa mgeni kwao hivyo kumwambia njia za panya zote ambazo zilikuwa zikitumika, alitakiwa kuzitumia hizo kwa ajili ya kufika nchini humo.
“Nashukuru, natakiwa kurudi sasa,” aliwaambia Waarabu gao.
“Kurudi wapi?”
“Mjini.”
“Hauendi Iraq?”
“Nilitaka nifahamu kwanza, nina semina na Wairan, baada ya hapo ndiyo nitaondoka. Mmebarikiwa kuwa na mafuta mengi, ila bado hamjajua ni kwa jinsi gani mnaweza kufanikiwa kupitia mafuta hayo,” alisema Mickey.
Kwa muda wa masaa matano ambayo alikaa nao tayari akaonekana kuwa rafiki yao, wakaanza kucheka naye huku wakimwambia mambo mengi kuhusu nchi nyingi za Kiarabu.
Mickey hakutaka kukaa sana, alichokifanya ni kuondoka na kurudi Badhiir ilipokuwa kambi ya Wamarekani. Alipofika huko, akawaambia kila kitu kilichokuwa kimetokea, mpaka njia ambayo walitakiwa kuitumia jambo lililoonekana kuwa rahisi kufanyika, hivyo Mickey alionekana kuwa msaada kwao.
“You are the man......You are the man,” (Wewe mwanaume...Wewe mwanaume) alisema mwanajeshi mmoja huku akitumia msemo uliomaanisha kumpa sifa mtu, msemo uliotumika sana nchini Marekani hasa kwa vijana wa mtaani.
Usiku wa siku hiyo, Mickey akaanza kupanga mipango yake ya kusonga mbele, alitaka kuelekea upande uliokuwa na nchi ya Syria kwa ajili ya kukamilisha kazi zake alizokuwa amepangia.
Kitu kilichomshtua kutoka katika lindi la mawazo ya mipango yake, ni pale alipoanza kusikia kelele za wanawake zikitokea sehemu kulipokuwa na mahema yaliyotengwa.
Kwanza akashtuka, hiyo ilikuwa ni kambi pekee ya Wamarekani nchini Uarabuni ambayo haikuwa na mwanamke yeyote yule, sasa hizo sauti za wanawake zilikuwa ni za wakina nani.
Hakutaka kubaki hapo, alichokifanya, akachukua bunduki zake na kwenda kule kulipokuwa na mahema yale. Sauti za wanawake waleziliendelea kusikika kwa ukaribu zaidi, alipolifungua hema lile, akapigwa na mshtuko, zaidi ya wanawake kumi wa Kiarabu walilazwa chini na wanajeshi wa Kimarekani waliokuwa na kazi moja tu, kuwabaka kwa zamu huku wanajeshi wengine wakiwa pembeni na bunduki zao, kwa kila kilichokuwa kikiendelea, walikishangangilia.
Moyo wa Mickey ukabadilika, hasira kali zikamkaba kooni, hakuamini kile alichokuwa akikiona mbele yake. Ni kweli alikuwa mwanaume mwenye roho mbaya hasa linapokuja suala la kuua lakini kitendo cha kushuhudia wanawake wakibakwa, kilimkera moyoni mwake. Akageuka na kutaka kuondoka.
“Hey man! Where are going? Come and
JamiiForums' Community Engagement Guidelines | Mwongozo wa Ushiriki kwenye Mijadala these young slut girls,” (Hey mwanaume! Unakwenda wapi? Njoo ufanye mapenzi na wanawake hawa wadogo na wachafu) alisema mwanajeshi mmoja huku akimvuta Mickey.
“Let me go,” (Niache niondoke) alisema Mickey huku sauti yake ikisikika kama ya mtu mwenye hasira kali.
Mwanajeshi yule akamuachia Mickey ambaye akaanza kupiga hatua mpaka kwenye hema lile, alipofika, akajilaza kitandani.
Kadiri alivyokuwa akizisikia kelele za wanawake wale, hasira zilizidi kumpanda, akajikuta akianza kuwachukia wanajeshi wale. Ilipofika saa saba usiku, tena kelele zile zikizidi kuongezeka, alichokifanya ni kuchukua bunduki zake zilizokuwa ndani ya begi na kuanza kurudi kule kulipokuwa na mahema yale. Hakukuwa na kitu kingine alichokuwa akikifikiria zaidi ya kuwaua wanajeshi wote, kitendo cha kubakwa kwa wanawake wale, alikichukia kwani alijua haikuwa kazi ambayo iliwapelekea wanajeshi wale kupelekwa katika nchi za Kiarabu.
Alipolifikia hema lile kubwa, akaingia ndani, bunduki zilikuwa mikononi. Hakuwa Mickey yule aliyekuja kipindi cha nyuma, alikuwa amebadilika, hasira kali ilimkaba kooni, alichokuwa akikitaka ni kuwaua wanajeshi wote waliokuwa mule ndani ya lile hema, aliwahesabu harakaharaka, walikuwa kumi na tano.
Aliyesimama mbele yao alikuwa Mickey, yuleyule jasusi kutoka C.I.A, jasusi aliyejulikana zaidi kwa mauaji makubwa aliyokuwa akiyafanya kila alipoambiwa kwamba mtu fulani alitakiwa kuuawa.
Aliwaangalia wanajeshi, kelele za wanawake wale zilimfanya kushikwa na hasira zaidi, paji lake la uso lilitawaliwa na ndita, hakutaka kusikia kitu chochote kwa wakati huo, kile alichokuwa akikitaka ni kuwapiga risasi tu.
Hawakujua kwamba huyu Mickey aliyeingia alikuwa tofauti na yule wa kipindi kilichopita, sasa hivi, alikuwa na hasira mithiri ya mbwa mwitu aliyechokozwa hivyo hakutaka kusikia kitu chochote kile. Akazikoki bunduki zile na kuwanyooshea.
“Paaa...paaaa....” ilisikika milio kadhaa ya risasi ndani ya hema lile, wanajeshi wote kumi na tano wakaanguka chini na kufa hapohapo.
Hali ilionekana kuwa ya hatari mahali hapo, damu zilitapakaa katika kila eneo ndani ya hema lile, wanawake wale wa Kiarabu wakabaki wakilia, hawakuamini kama mtu yule angeweza kuwaua wanajeshi wale na kuwaacha hai wao.
“You are free, you can go home now,” (Mpo huru, mnaweza kwenda nyumbani sasa) alisema Mickey na kutoka hemani mule.
Moyo wake ukaridhika, alichokifanya ni kuondoka mahali hapo huku akijiandaa kutoa ripoti ya uongo juu ya kilichokuwa kimetokea hapo Badhiir.
****
‘Fifteen soldiers were killed in Iran’ (Wanajeshi kumi na tano wauawa Iran) kilikuwa kichwa cha habari kilichopita katika Kituo cha Televisheni cha CNN cha nchini Marekani. Ilikuwa moja ya taarifa iliyomsisimua kila Mmarekani huku wengi wao wakiwa hawaamini kama waliweza kuwapoteza wanajeshi wengi namna hiyo tena kwa wakati mmoja.
Maswali mengi yakaanza kumiminika vichwani mwa watu kwamba ilikuwaje wanajeshi hao wauawe kwa pamoja tena ndani ya hema huku wakiwa wamekaa karibukaribu namna ile.
Swali hilo na maswali mengine yaliyokuwa yakiulizwa na watu yakakosa majibu. Walichokifanya C.I.A ni kuwasiliana na Mickey ili kutaka kufahamu ni kitu gani kilichokuwa kimetokea mpaka wanajeshi hao kuuawa katika kambi waliyomwambia aende huko.
Hawakutaka kupewa majibu kupitia simu, walichomwambia ni kwamba alitakiwa kwenda nchini Marekani ambapo huko, wakamuweka chini na kuanza kuzungumza naye huku ndani ya chumba hicho kukiwa na watu zaidi ya ishirini.
“Nini kilitokea?” aliuliza kiongozi wa shirika hilo, bwana Powell.
“Sifahamu. Siku ya tukio, sikuwa hapo Badhiir, nilikwenda kukamilisha majukumu yangu, na bahati nzuri nikakamilisha kila kitu, tena kwa mafanikio makubwa,” alisema Mickey.
“Ulipoondoka, uliiacha kambi katika hali nzuri?”
“Naweza kusema hivyo kwani hakukuwa na dalili za kutokea kwa adui yeyote yule,” alisema Mickey.
“Kipi unahisi kinaweza kuwa chanzo cha watu hawa kuuawa?”
“Sijajua, ila nilipowaacha, kulikuwa na kundi la wanawake kambini, nahisi, hao ndiyo waliosababisha kila kitu,” alisema Mickey.
Kilichofanyika, upelelezi ulitakiwa kufanyika zaidi ili kujua ni kitu gani kilichokuwa kimetokea. Watu makini walioaminika katika kufanya upelelezi wakaelekea huko, wakaingia mpaka kwenye kambi hiyo na kukaa huko kwa muda wa wiki moja lakini hawakufanikiwa kupata chochote kile.
Siku iliyofuata, zaidi ya Wamarekani mia tatu walikuwa barabarani huku wakiwa na mabango yaliyosema kwamba ilitakiwa wanajeshi wote waliokuwepo katika nchi za Uarabuni warudishwe nchini kwani kuwepo huko kulimaanisha kwamba wanajeshi wengi wangeendelea kuuawa.
Alichokifanya Bush baba ni kuongeza jeshi zaidi nchini humo, hakutaka kusikia kitu chochote kile kuhusu kuwarudisha wanajeshi wake nchini Marekani. Alikuwa na hasira mno na Waarabu, hakutaka watu hao waendelee kuishi, kuna wakati alitamani awe Mungu ili awapoteze wote kwani uwepo wao mbele ya macho yake ilikuwa chukizo kubwa kwake.
Wamarekani walipiga kelele lakini hakukuwa na kilichobadilika, waliandamana mno tena katika majimbo yote nchini humo lakini hakukuwa na utekelezaji wowote ule, msimamo wa rais huyo ulikuwa mmoja tu kwamba ilikuwa ni lazima wanajeshi waongezwe nchini humo kwa ajili ya kuongeza nguvu.
“Kwa nini wasiwaruhusu wanajeshi wetu warudi? Haya mambo ya kivita, huwa siyapendi sana,” alisema Elizabeth huku akionekana kuumizwa na kile kilichokuwa kikiendelea.
“Sijajua ila kama ningekuwa mwanajeshi, nisingeweza kwenda, sisi wengine ambao hata hatujui kushika bunduki, tunaweza kufa kwa presha,” alisema Mickey.
“Hata kule mitaani haukuwahi kushika bunduki?”
“Hapana! Nilikwishawahi kuziona wakiwa nazo watoto wenzangu, lakini sikuwahi kushika hata siku moja, ninazihofia mno,” alisema Mickey huku akijifanya kuogopa kushika bunduki.
Elizabeth aliendelea kupigwa upofu, hakujua kama mume wake ndiye alikuwa nyuma ya kila kitu kwa kuwaua wanajeshi wale. Alipoambiwa kwamba alikuwa muoga kushika bunduki, akayaamini maneno hayo kwani hakuwahi kumuona mume wake akishika bunduki na hata alipomshauri kwamba amiliki bunduki kutokana na umaarufu wake, alimkatalia.
Miongoni mwa watu ambao Elizabeth alikuwa akiwaona kwamba ni waoga namba moja duniani, wa kwanza alikuwa mume wake. Wakati mwingine alijifanya kuogopa mpaka kutazama filamu za kutisha au kila alipokuwa akiangalia filamu zilizojaa mauaji makubwa, alikuwa akikunja sura yake kama mtu aliyeumizwa mno.
Siku zikaendelea kukatika. Kadiri Mickey alipotumwa nchini Marekani, aliendelea kuua kificho hasa pale alipowaona wanajeshi wenzake wakiendelea kuwabaka wanawake wa Kiarabu.
Mwaka 2009 wakati Barack Obama alipokuwa akichukua ofisi na kuwa rais wa Marekani, ndicho kilikuwa kipindi Mickey alitumwa nchini Iran kwa ajili ya kuhakikisha kwamba anawachonganisha watu wa taifa hilo na Iraq kutokana na mtafaruku mkubwa wa mafuta uliokuwa ukiendelea.
Alipofika huko, kama kawaida, tabia za wanajeshi kubaka wanawake wa Kiarabu ilikuwa ikiendelea na hakuacha kuua, aliendelea kuwamaliza wanajeshi wa Marekani kwani kwake, kitendo cha kubakwa kwa mwanamke kilionekana chukizo kubwa kuliko hata kuua.
Ilipofika mwaka 2010, hapo ndipo tetesi zilipoanza kusikika kwamba Mickey, jasusi aliyekuwa akitumainiwa kwa kupewa ‘mission’ nyingi ndiye aliyehusika katika kuwamaliza wanajeshi wengi wa Kimarekani kwa kuwaua kwa sababu tu walikuwa na tabia ya kuwabaka wanawake wa Kiarabu, wakuu wa C.I.A wakakasirika, hasira zao zikawaka dhidi ya Mickey.
Nao wakataka kumuua, yaani ni sawa na kuukata mti ulioupanda mwenyewe na kuumwagilia kila siku. Japokuwa alikuwa mtu muhimu, hawakuwa na jinsi, ili kuokoa maelfu ya wanajeshi wa Kimarekani, ilikuwa ni lazima kumuua Mickey. Ripoti ya ombi la kuuawa, likapitishwa na bwana Powell kusaini. Kilichosubiriwa ni kazi tu kufanyika.
Zoezi la kumuua Mickey halikuwa jepesi hata mara moja, alifanya kazi kama jasusi wa C.I.A kwa kipindi kirefu mno hivyo mbinu zote walizokuwa wakizitumia majasusi alikuwa akizifahamu.
Kuna kipindi walitaka kumuua hotelini huku mmoja wa majasusi akijifanya mfanyakazi wa hoteli hiyo ambaye alikuwa bize akikihudumia chumba chake, kitu cha ajabu, siku ambayo alitaka kummaliza, hakuweza kumuona tena, alikuwa amekwishaondoka zake hotelini hapo.
C.I.A hawakuchoka, bado waliendelea kusisitiza kwamba Mickey alitakiwa kuuawa haraka iwezekanavyo. Kila kitu walichokuwa wakikifanya, alikigundua hivyo walipata wakati mgumu mno.
Mpaka nchi ya Marekani inaweka historia ya kutawaliwa na mtu mweusi, Barack Obama, bado walikuwa wakiendelea kumtafuta Mickey ili wamuue lakini ikashindikana kabisa.
“Nataka tufanye kitu,” alisema Mickey, alikuwa akizungumza na mwanaume mmoja aliyeonekana kufanana naye kuanzia umbo, yaani urefu na mwili.
“Kitu gani?”
“Nitakulipia dola milioni tano endapo tu utakubali kufanya kile ninachokitaka,” alisema Mickey.
“Kitu gani?”
“Nataka uwe mimi.”
“Niwe wewe? Kivipi?”
Mickey akaanza kumfafanulia kwamba alitaka kutengeneza sura ya bandia inayofanana na yeye na kisha kumgawia jamaa huyo ambaye angekuwa mbadala wake na angeshughulika katika kila kitu alichokuwa akikifanya, yaani aonekane kama Mickey.
Japokuwa ilikuwa kazi kubwa lakini malipo yake yakamfanya kuvutiwa na kutaka kuifanya kazi hiyo. Kiasi cha dola milioni tano ambazo zilikuwa ni zaidi ya shilingi bilioni kumi, kilimpagawisha mwanaume huyo aliyeitwa Stefan.
Baada ya kukubaliana kwa kila kitu, Mickey akaanza kufanya mawasiliano na mtaalamu wa kutengeneza sura za bandia, Chung Lu, mwanaume kutoka nchini China. Akafika nchini Marekani na kuonana na Mickey ambapo akapewa maelezo juu ya nini kilitakiwa kufanyika.
Baada ya kupewa maelekezo yote, siku iliyofuata, wote watatu wakawa ndani ya chumba maalumu ambapo humo ndipo kulipofanyika mchakato wa kutaka kutengeneza sura ya bandia na kuvishwa Stefan.
Mchakato mzima ulichukua masaa nane, sura iliyofanana na Mickey ikatengenezwa na kisha kuvarishwa Stefan huku sura nyingine ya Stefan ikitengenezwa na kuvarishwa Mickey. Huo ndiyo ulikuwa mchezo alioamua kuucheza na hakutaka kujali kuhusu chochote kile.
Kesho yake, akachukua kila kilichokuwa chake, kuanzia simu yake, kadi zake zote zikiwepo za benki, magari yake na kumuachia.
Hata Stefan alipoanza kuishi na Elizabeth, mwanamke huyo hakuweza kugundua kitu chochote kile. Kuanzia sauti, muonekano mpaka baadhi ya tabia bado mwanaume huyo alionekana kuwa kama Mickey.
Mara kwa mara Mickey alikuwa akiendelea kufika nyumbani hapo na kujifanya kuwa rafiki mkubwa wa Stefan. Japokuwa kila alipokuwa akimwangalia mke wake akiwa amekumbatiana na Stefan alijisikia wivu lakini hakuwa na jinsi, alijua alichokuwa akikifanya hivyo alivumilia kwa kila kitu.
Katika kipindi ambacho Mickey alitakiwa kwenda nchini Tanzania, tayari C.I.A walikuwa wamekwishaandaa mpango mkubwa wa kumuua hivyo walijiandaa vilivyo. Siku ambayo Stefan alipokuwa akielekea huko huku akiwa na muonekano wa Mickey, hakugundua kwamba kulikuwa na mpango kabambe wa kumuua.
Mickey mwenyewe hakutaka kubaki nchini Marekani, alitaka kufuatilia kila kitu kilichokuwa kikiendelea. Mpaka kipindi ambacho Stefan alipigwa risasi, Mickey alikuwa uwanjani hapo akishuhudia na kuona kwamba hiyo ilikuwa nafasi yake ya kuuawa kama ilivyokuwa imepangwa.
Dunia nzima ikaingiwa na majonzi, kila mtu akalaumu kwa nini Mickey alikuwa ameuawa na wakati alikuwa mhamasishaji mkubwa duniani na alifanya kila kitu alichoweza kuwakwamua watu kutoka katika umasikini mkubwa waliokuwa nao.
C.I.A wakafurahia pasipo kufahamu kwamba mtu waliyekuwa wamemuua hakuwa Mickey bali alikuwa Stefan aliyevaa sura ya bandia ya Mickey.
Elizabeth alilia usiku na mchana, kifo cha mumewe kilimuuma mno, hakula wala hakulala, kila alipokuwa akikaa na kumfikiria mume wake, alizidi kuumia moyoni wake.
“I will avenge, I will kili a person who murded my father,” (Nitalipa kisasi, nitamuua yule aliyemuua baba yangu) alisema Victor huku akionekana kuwa na hasira.
Mwaka mmoja baadae, Mickey akajitokeza kwa mke wake huku akiwa na muonekano wa Stefan. Elizabeth alipomuona, hakujua kama ni mume wake bali alijua kwamba ni rafiki mkubwa wa marehemu mume wake.
“Kuna siri nzito nataka kuongea nawe,” alisema Mickey huku sauti yake ikiwa imebadilika kabisa.
“Siri gani?”
“Kuhusu mume wako,” alisema Mickey, hapohapo Elizabeth akaanza kububujikwa na machozi kwani picha ya mume wake ikaanza kumrudia tena.
“Amefanyaje?”
“Naomba tukaongelee chumbani, hii ni siri nzito mno,” alisema Mickey.
“Kuongelea chumbani?”
“Ndiyo!”
“Hapana. Hakuna mtu anayeruhusiwa kuingia chumbani kwangu, haiwezekani!”
“Lakini hili ni muhimu kwako.”
“Hapana. Nimesema haiwezekani, tena naomba uondoke,” alisema Elizabeth huku akiwa amekwishabadilika, tayari machozi yale yalikuwa yamekwishaloanisha mashavu yake. Taswira ya mume wake ilijirudia vema kichwani mwake.
****
Ilionekana kuwa ngumu sana kwa Mickey kuzungumza na mkewe kuhusu kile kilichokuwa kimetokea mpaka kufikia siku hiyo. Muda wote Elizabeth alikuwa akilia tu kwani kwa jinsi alivyokuwa akimpenda mume wake, na vile ambavyo Mickey mwenye sura ya Stefan alivyomkumbusha, aliumia mno.
Alitamani kumwambia hapohapo kwamba yeye ndiye alikuwa mume wake lakini hakuona aanzie wapi, alichokifanya ni kuondoka huku akimuachana mke wake katika hali hiyo.
Huko, kitu cha kwanza kabisa alichokifanya ni kuwasiliana na mtoto wake, Victor na kuomba kukutana naye kwa kuwa alikuwa na mambo mengi aliyotaka kumwambia kuhusu baba yake, yaani yeye mwenyewe.
Kwa kuwa kijana huyo alikuwa nchini Ujerumani, akaomba kukutana naye baada ya wiki moja, kweli, baada ya wiki moja, Victor alikuwa mbele yake, akaanza kuzungumza naye.
Victor alibaki kimya akimsikiliza Mickey, hakugundua kama alikuwa baba yake, alichokifahamu ni kwamba mtu huyo alikuwa rafiki mikubwa wa baba yake.
Kitu alichokifanya Mickey ni kumuhadithia Victor tangu siku ile alipokuwa amezaliwa, vitu alivyokuwa akivifanya kama mtoto na kumuonyeshea picha nyingi za kipindi hicho. Victor akapigwa na mshangao, alijiuliza kwamba ilikuwaje rafiki wa baba yake awe na vitu vingi namna hiyo na wakati hata baba yake hakuwa navyo? Kila alichojiuliza, alikosa majibu.
“Where did you get them?” (Umevipata wapi?) aliuliza Victor.
“I had them since you were a baby boy,” (Nilikuwa navyo tangu ulipokuwa mtoto mdogo) alisema Mickey.
“My dad has never shown me all of these,” (Baba hakuwahi kunionyeshea hivi vyote) alisema Victor huku akichukua simu ile na kuanza kuziangalia picha zile.
“I know! But let me tell you the truth,” (Najua! Ila acha nikwambie ukweli)
“What truth?” (Ukweli upi?)
“I am your father,” (Mimi ni baba yako)
“What?” (Nini?)
“Shiiiii”
Mickey akamtuliza Victor, alionekana kama mtu aliyeshtuka sana hivyo akamwambia atulie na kisha angemwambia kila kitu kilichokuwa kimeendelea. Kwanza Victor hakuonekana kuamini, ilikuwaje mwanaume huyo aseme kwamba alikuwa baba yake na wakati alifahamu fika kwamba baba yake alikuwa Mickey.
Aliendelea kujiuliza zaidi labda mama yake alikuwa ametembea nje ya ndoa na mwisho wa siku mwanaume huyo kumpa mimba na hivyo kupata mtoto ambaye ndiye yeye, kila alichokuwa akijiuliza, alikosa jibu.
“Haiwezekani, baba yangu ninamjuua, mama hawezi kumsaliti baba na kutembea na wewe,” alisema Victor huku akionekana kuchanganyikiwa.
“Mimi ni nani?”
“Nakujua wewe kama rafiki yake baba yangu.”
“Sawa. Twende tukatembee, nitakwambia kila kitu.”
Walichokifanya ni kutoka hapo mgahawani walipokuwa na kwenda kutembea katika eneo kubwa la Bustani ya Livingston iliyokuwa hapo New York, pembezoni mwa Mghahawa wa KFC.
Huku, Mickey akaanza kumuhadithia mtoto wake kila kitu kilichokuwa kimetokea katika maisha yake tangu siku ya kwanza alipojiunga na CIA, wanajeshi walipowabaka wasichana wa Kiarabu na kuamua kuwaua mpaka mpango mzima uliofanywa kwa ajili ya kummaliza.
Victor alibaki akishangaa, hakuamini kile alichokuwa amekisikia kutoka kwa baba yake, hapohapo, akajikuta akimkumbatia kwa furaha kwani baada ya kuumia kwa kipindi kirefu kwa kudhani kwamba baba yake alikuwa ameuawa nchini Tanzania na C.I.A, mwisho wa siku akakutana naye tena na kumwambia kwamba alikuwa mzima na aliyeuawa hakuwa yeye.
Siku hiyohiyo wakaelekea nyumbani, huko, akamwambia mama yake kile kilichotokea, bi Elizabeth akajikuta akibubujikwa na machozi na hata Mickey alipoamua kuwatembelea tena, akajikuta akimkumbatia kwa furaha.
Hawakutaka kuchelewa, baada ya miezi miwili, Elizabeth akatangaza kwamba alitaka kuolewa na rafiki wa mume wake, Stefan pasipo dunia kujua kwamba huyo bwana harusi ndiye alikuwa mume wake wa ndoa.
Mickey akamuoa tena Elizabeth na maisha kuanza tena. Akaachana na C.I.A, akawa mwanaume huru aliyeanzisha biashara nyingi na kuuendelezea ubilionea aliokuwa nao.
Kwa nchini Tanzania, mara baada ya kupewa maelezo juu ya mauaji yaliyokuwa yametokea kwamba yalikuwa chini ya Marekani, Gideon akaachiwa huru na kurudi nchini Malawi ambapo huko akaendeleza upelelezi wake mpaka kumtia mikononi bwana Timoth.
Mpaka ilipofikia mwaka 2013, bwana Mickey, huku akiwa chini ya jina la Stefan, akafanikiwa kupata mtoto wake wa pili wa kike aliyempa jina la Lindsey.
MWISHO
TOA MAONI YAKO
CHANZO : BURE SERIES