The Manchester City (The Citizens) | Special Thread

Maoni yangu binafsi kama SHABIKI wa Man City
1) KDB kama mchezaji muhimu:

Kwanza ni lazima nikili kuwa mechi ya leo dhidi ya SPURS itakuwa ngumu sana, ugumu huo unakuja kutokana na matokeo ya mechi ya kwanza na ubora wa Pochettino.
Hivyo kutokana na ugumu wa mechi ya leo inahitajika De Bruyne awe katika kiwango chake kile tulichokizoea (De Bruyne ndio mchezaji mwenye ufunguo wa matokeo yatakayotupeleka hatua ya nusu fainali), wanachotakiwa kufanya wachezaji wengine wa City ni kumpa ushirikiano mzuri mzungu chuma (De Bruyne), na hii ndio maana halisi ya neno timu.

2) Muda David Silva kupumzika:
Kama umekua mfuatiliaji mzuri wa mechi za Man City basi bila shaka utakubaliana na mimi kuwa kiwango cha mchawi huyu wa soka kimeshuka sana, nafikiri ni muda umeanza kupingana nae. Kutokana na kushuka kwa David Silva nafikiri mechi ya leo ilikuwa ni wakati muafaka kwa Pep Guardiola kumtumia Bernardo Silva kwenye nafasi ya David Silva.

3) Ni mechi ya Pep kuanza kumuamini Sane:
Kasi ya Sane itasababisha matatizo makubwa sana kwa mabeki wa Spurs, pia Sane ana rekodi nzuri sana katika mechi ambazo ameanza katika uwanja wa Etihad.

4) Danilo acheze nafasi ya beki wa kushoto:
Kutokana na Zinchenko kuwa majeruhi bas itakua vyema sana kama nafasi yake itazibwa na Danilo. Kwanini Danilo na sio Mendy? Danilo amecheza mechi nyingi msimu huu kulinganisha na Mendy, pia aina ya uchezaji wa Mendy inaweza kuigharimu timu (Ni mzito sana).

5) No Mahrez, No Gundogan:
Kama ningekuwa na uwezo wa kuonana uso kwa macho na Pep, basi ningempigia hata magoti kumuomba hao watu wasiwe kwenye kikosi cha kwanza cha mechi ya leo, hawaaminiki kabisa hao wahezaji. Ila kwa jinsi PEP anavyompenda Gundogan, sitoshangaa nikimuona kwenye kikosi cha kwanza.

6) KIKOSI CHANGU CHA LEO:
Ederson
Walker, Kompany/Stones, Laporte, Danilo
Fernandinho
De Bruyne, Bernardo
Sterling, Aguero, Sane

MWISHO; No Otamendi please...!!!πŸ˜”πŸ˜”πŸ˜”
 
Mkuu yan tupo pamoja kabisa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hiyo namba nne upo sahihi.
 
"Ahsante sana Guardiola kwa kuwaanzisha Gundogan na David Silva,tutafanyaje sasa,wakati wewe ndio MTU wa mwisho katika kufanya maamuzi ya nani acheze na nani asicheze!?"

Nitakuja kucheki matokeo baada ya kipindi cha kwanza..!
 
Mkongwe...
Hapa nilipo nakisubiri kikosi cha kwanza kwa hamu,yaani nikiona jina la Mahrez au Gundogan basi nitacheki matokeo baada ya dakika 45 za kwanza,baada ya hapo ndio nitaamua kama niingie online kuendelea kuangalia au nilale zangu tu..!
Hahahha mm nipo maeneo nasubiri game

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mechi ni ngumu sio nyepesi kabisa....

Mungu bariki Man City
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…