ilikuwa 2017 ,uefa round ya 16
Man city vs Monaco ( enzi mbape na kina fabi ,falcao wapo )
Pep kama kawaida alishinda 5-3
Tulivoenda Monaco ,ndio nikajua kuwa kocha wetu linapokuja swala na knock out stage ,basi mbinu zinamwishia ,sikutegemea kabisa kwa iyo aggregate tungeweza kutolewa uefa ...
Mbape akaweka kambani dakika ya 8 ..
Nikajua sio shida ,maana aguero ,sterling ,sane ,kdb walikuwa moto ..
Mara fabinho wayaa dakika 27 ...
Aisee sane akatuokoa ,maana aggregate ilikuwa 5-5 ...
Siku nilipomchukia otamend ,mwanaharamu yule alipuuzia Mpira wa kichwa ,ukatua kichwani mwa bakayoko na kutupia goli aggregate 6-6 ,tukatolewa kwa goli LA ugenini ...
Kilichofuata baada ya hapo ,pep kufika semi final uefa imekuwa sawa na punda kupita kwenye tundu LA sindano ...