Ila nyie jamaa... tupeni striker mmoja majirani zenu. [emoji16]
Hahaha!...mbaya zaidi ata huyu haaland tuliyenaye, mlipigiwa simu na CEO wa molde F.C ya Norway bwana John-Vick wakati huo Ole alikuwa ndo kocha wao na haaland alikuwa bado hajaenda ata kule Salzburg.
Mkaambiwa kuna mtoto huku ni striker yupo vizuri sanaaa, mkadharau bana na hamkwenda ata kumuangalia sasa. muda mwingine mnafurahisha sana UNITED a.k.a History FC na makombe yenu yale mlobeba tokea 1907/1908, 1911 kipindi icho ata offside hakuna..😂😂😂😂😂
Nasio huyo tu ata Alvarez mwenyewe mliambiwa mkatuma Scout wenu wakamwona vyema mkasema mtarudi ila cha ajabu hamkurudi tena. Na mliambiwa £16m tu....nahisi nyie ndo mkafanya hadi sie City tushushiwe bei ya Alvarez hadi kuuziw £14m...maana RiverPlate walihisi huenda bei ya dogo ipo juu ndo maana hamkurudi tena 😆😆😆
POOR UNITED...TATIZO MNAVIMBAGA SANA KUJIONA NYIE NDO WABABE WA ENGLAND...KUMBE MMEBAKI KWENYE MAKARATASI TU YA HISTORIA HUKU NYAKATI ZIKIWAACHA NA HAZIRUDI NYUMA TENA..."In Short GLORY DAYS ARE OVER"
Wakati huo mkijikuta Sio kila mchezaji ana hadhi ya kuchezea kwenu united...sisi City tulichukua kila aliyekuwa tayar kucheza kwetu ili mradi tusiondoke ligi kuu tu, ila chakushangaza upepo umebadilika sahivi ndo mnawatafuta wachezaji wa hadhi yenu alafu wanawakataa Sasa( Reference: F. De Jong).
Na kauli zenu zilivyokuwaga za kishujaa sasa...muangalie babu apo 2009 anatoa kauli #KAVU...Afu juzi tu apo etihad mmepigwa 6 akabadilika adi rangi usoni....shenz!, anajiuliza imekuwaje wakati sisi City sio favourite wa kushinda kwenye DERBY???