Moment za aguero ambazo hata yeye binafsi hawezi sahau ni msimu wa 2011/2012 kwenye game na QPR.....
Huu ni msimu ambao nadhani project ya sheikh mansour ilikuwa inaanza huku Robert mancin akiwa kwenye ubora wake ,ni msimu ambao city ilikuwa inafanya sajili kubwa kubwa huku ikionesha project nzuri na endelevu .........
ilikuwa city iliyokuwa inasajili wachezaji mastar ,kina Silva ,dzeko ,ballotel ,aguero ,nasri ,robiho,vicent kompany,....Walitua city
ballotel na utukutu wake wote ile game na QPR alikorofishana na mchezaji mmoja wa QPR aisee nilijua ballotel anaenda kula red ,lakin huwezi Amin ballotel alitulia ,na akawa mpole yule mchezaji akala umeme pekee yake ...!
Huwezi Amin ballotel katika historian yake ya mpira pale city hakuwa kutoa assit ,lakin siku hiyo ndio assit aliyotoa kwa aguero na kumaliza game ....
Ni msimu ambo united hawatakuja kusahau kwenye historia ya mpira ,kwani ile siku man UTD walikuwa wameshashinda game vs sanderland huku wakisubili kombe la epl kulichukua , wakiwa wanajiandaa na sherehe [emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28].....
Ndege iliyokuwa imebeba kombe ilikuwa ipo angani haijui la kufanya iende OT au etihadi !!!! ...lakin rubani alikuwa ameshapigiwa simu apeleke kombe OT ,.....
Wakati man city tukiwa tunatapatapa hapa na pale ,90min ,zimeishia ,zikaongezwa tatu .....2min zikaisha ...3min ikafika ........daaaa muda huo tunawachezea nusu uwanja , QPR wamepaki bus hatari ,ingekuwa kibongo bongo tungesema wale jamaa wametumwa [emoji28][emoji28][emoji28][emoji28][emoji28]...mpira unatoka nje ,nasri anakimbilia haraka ,anaurudisha uwanjani ,zinapigwa pass hapa na pale ,ndani ya box ,fans wote wa city wamenyanyuka hawaelewi kinachotokea kabisa uwanjan ......super Mario ballotel anatoa assit ya kwanza kwa aguero kwenye angle ngumu ,aguero anaweka kamban ....90+3min ...aguerooooooooooooo!
City tunachukua epl kwa mara ya kwanza .....
Mancin ndio akavunja utawala wa furgason pale epl ,kuanzia hapo city ilianza kutoa kipigo cha mbwa Koko msimu unavoanza huku mansour akizidi kuimalisha management ,mara pep guardiola akatua Etihad .....!
Unajua Nini kilifuata , furgason ndio alikuwa akitawala pale England ,na ulikuwa huwezi sema chochote kuhusu united ,mpaka leo pep anazidi kutembeza kichapo ...mpaka Sasa united hawaamin kuwa wameshatolewa kwenye mbio za kuchukua epl Kwan tumebaki wanaume wawili tu Liverpool na city kwa Sasa .....Toka kipindi hicho tumebeba epl mara 5 kuzidi timu zote za england ....
2011-2012 -epl
2013-2014.
2017-2018.
2018-2019.
2020-2021....yote haya kachukua Sergio Kun aguero
And we are attacking the title 2021/2022...
This is our city
View attachment 2045440