The Miracle Of The Sun/Muujiza Wa Jua - 13 October 1917

The Miracle Of The Sun/Muujiza Wa Jua - 13 October 1917

P h a r a o h

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2024
Posts
785
Reaction score
1,413
images (53).jpeg
maxresdefault.jpg
The_crowd_looking_at__the_Miracle_of_the_Sun__occurred_during_the_Our_Lady_of_Fatima_apparitio...jpg
Tarehe 17 October 1917, maelfu ya watu takriban watu 70,000, walishuhudia jua likifanya kitu kisicho cha kawaida,

waliweza kuliangalia kwa takriban dakika 15 bila kuumia macho,
waliokua wanaliona walisema lilikua linatoa mwanga kwa rangi tofauti tofauti, pia lilionekana kama linazunguka,
huku likionekana kuisogelea dunia na baadae likarudi katika umbali wake wa kawaida.

Ilikuaje takriban watu 70,000 wakusanyike siku hiyo kuliangalia jua ?

- kila kitu kilianzia kwa watoto watatu:-
Jacinta Marto,
Fransisco Marto,
na binamu

yao Lúcia dos santos

images (57).jpeg


Hawa watoto ni ndugu, Jacinta alikua na miaka 07, kaka yake Fransisco 09, na binamu yao Lucia 10.

siku moja walipokua wanachunga tarehe 13 may 1917 waliona kitu kilicho washangaza...
mkubwa wao ( Lucia ) akawaambia wasiende kutangaza wakirudi nyumbani.

walipofika nyumbani yule mdogo ( Jacinta) akashindwa ku kaa kimya akamwambia mama yake...
leo tulivokua tunachunga tulimuona bibi mzuri anang'aa, mzuri amevaa nguo nyeupe
ametuambia tuwe tunasali Rozali na atakua anakuja kila mwezi.

kama ilivyokua kawaida ilikua ni kitu ambacho hakiingii akilini unapo ambiwa habari kama hiyo, na ikizingatiwa ni watoto ndo wanaoleta hadithi hizo, mama yao aliwapuuzia,

tarehe 13 june 1917 wakaenda tena pale kama walivyo ambiwa yule bibi yao walio muona siku ile ( Bikira Maria )akawatokea tena kama alivyo waahidi waje siku hii,
hii siku akawaonyesha maono jinsi Jehanamu palivyo

aka ahidi kuwachukua wale ndugu wawili, Jacinta na Fransisco Marto ( wote wawili wakafariki miaka miwili baadae )
akamwambia Lucia atabaki duniani muda mrefu ili kusambaza ujumbe wake ( Lucia aliishi hadi mwaka 2005 )

hizi habari zilivyozidi kusambaa, hawa watoto wakapata umaarufu zaidi na upinzani pia vitisho n.k... kutoka kwa wasio amini

Tarehe 13 july 1917
Bikira maria akawatokea tena hii siku akawaambia kuhusu vita ya kwanza ya dunia na kuwaambia wasali zaidi Rozari kuombea amani na vita ya kwanza itaisha muda sio mrefu
( kipindi hiko vita ya kwanza ya dunia ilikua ikiendelea )
pia akawaambia watu wasipo mrudia Mungu itatokea vita kubwa zaidi ya hiyo ( vita ya pili ya dunia ) ambayo pia kabla haija anza dunia itapewa ishara.

Tarehe 13 August 1917
walikua gerezani siku hii, walifungwa ili wahojiwe kwasababu habari hizi zilisambaa mno, kwahiyo waliwekwa ndani kwa muda wakiwa wanahijiwa

Tarehe 13 September 1917
siku hii watu wengi waliwafuata ili na wao wakamuone Bikira Maria atakapo watokea,
lakini Bikira Maria alikua anaonekana na wale watoto watatu,
wengi wao hawakuweza kumuona

Bikira Maria akahaahidi kujidhihirisha kwa watu wote mwezi ujao yaani tarehe 13 October 1917

kwa miezi hiyo mitano habari zikikua zimeshasambaa sana watu wa karibu na wengine wa mbali walikuja ili kuisubiri tarehe 13 mwezi wa 10

Tar 13 October 1917
zaidi ya watu 70,000 waliokusanyika wakimsubiri Bikira Maria,
wakaanza kushuhudia Jua likifanya mambo yasiyo ya kawaida,

Jua lilishuhudiwa kwa takriban dakika 15 likizunguka, likitoa miale ya rangi tofauti likishuka kuikaribia dunia na baadae kurudi lilipokua.
muda wote huo watu waliweza kuliangalia bila kuumia macho.

kushuhudiwa huko na maelfu ya watu kukafanya tukio hilo lijulikane kwa kasi dunia nzima.

April, 4 1919 - Fransisco Marto alifariki
February, 20 1920 - Jacinta Marto alifariki

Mwaka 1930 baada ya tafiti za kanisa Catholic, kanisa likautambua rasmi huo muujiza na kuanza harakati za kuwatangaza Jacina na Fransisco kua watakatifu,

Mwaka 1938 January 25 hadi 26 Jua lilikua likitoa rangi ya tofauti ( aurora borealis )
kitu kilicho ibua hofu kwa watu wengi sana siku mbili mfululizo
images (58).jpeg


1939 vita ya pili ya dunia ikaanza wakakumbuka ule mwanga wa jua ulikua ni ishara waliyoambiwa watapewa ( hii vita ya pili ilikua kubwa sana ikahusisha hadi matumizi ya mabomu ya atomic yaliyo lipua Hiroshima na Nagasaki )

Baada ya kanisa kuwatambua:-

September 12, 1951 walitaka kuhamisha mabaki ya miili yao kwenda kuizika upya Kanisani,
waliikuta miili yao ipo vile vile kama ilivyozikwa miaka 32 iliyopita. haijaharibika kabisa.

Lúcia dos Santos alifariki February 13, 2005

Muujiza wa Jua ndio muujiza ulioshuhudiwa na watu wengi zaidi tariban 70,000 hadi 100,00 wanakadiriwa kushuhudia siku hiyo,

ukishuhudiwa na waandishi wa habari, watu wasio amini na wanao amini,

umebaki kuwa Supernatural phenomenal iliyo ripotiwa mara nyingi zaidi.
 
Nakumbuka enzi hizo school nikiingia kwenye pepa nikipiga salamu Maria zangu 3 pepa likirudi ni Banda juu ya mlima yaan A ya 99.9 yaan hio 0.1 basi tu teacher kaona aibu kunipa 100 chini ya 100 na teacher anatangaza kabisa pepa langu ndio litakua marking scheme yake na ananiambia niwafundishe waliokula misuaki, wakiuliza Siri ya Mafanikio nikiwaambia nilipiga salamu Maria kabla pepa wanacheka, wajomba na wapwa zangu tusiache kusali rozali kuna maajabu usifikiri uongo
 
Saa 9 HII Wewe kunja Goti umuombe MUNGU Muda huu wanasema mbingu zinakua zimefunguka ukiomba chochote Muda huu unatapa,

Ps: Muda huu ndio Muda ambao hata Wezi wakiiba huku wanamuomba Mungu hawakamatwi Muda huu walinzi wamelala wamechoka kukaa Macho
Let do it mkuu...
Sometimes unaweza ukawa wewe umesema kawaida kumbe something sent 2 me through you...

Ngoja nkae hapa nipige at ikhiras tatu mkuu 🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏🙏
 
Nakumbuka enzi hizo school nikiingia kwenye pepa nikipiga salamu Maria zangu 3 pepa likirudi ni Banda juu ya mlima yaan A ya 99.9 yaan hio 0.1 basi tu teacher kaona aibu kunipa 100 chini ya 100 na teacher anatangaza kabisa pepa langu ndio litakua marking scheme yake na ananiambia niwafundishe waliokula misuaki, wakiuliza Siri ya Mafanikio nikiwaambia nilipiga salamu Maria kabla pepa wanacheka, wajomba na wapwa zangu tusiache kusali rozali kuna maajabu usifikiri uongo
Nguvu za Mungu ni dhahiri....Kuna kabila fulani Afrika wanamcha Mungu sana.....ingawa ni walevi hupata kubarikiwa kiuchumi.
 
Nakumbuka enzi hizo school nikiingia kwenye pepa nikipiga salamu Maria zangu 3 pepa likirudi ni Banda juu ya mlima yaan A ya 99.9 yaan hio 0.1 basi tu teacher kaona aibu kunipa 100 chini ya 100 na teacher anatangaza kabisa pepa langu ndio litakua marking scheme yake na ananiambia niwafundishe waliokula misuaki, wakiuliza Siri ya Mafanikio nikiwaambia nilipiga salamu Maria kabla pepa wanacheka, wajomba na wapwa zangu tusiache kusali rozali kuna maajabu usifikiri uongo
Safi sana. hadi Chuo ulikuwa unapiga hayo mabanda??? Au baada ya kukua ulipunguza imani ukaona unajumudu?? Na sasa upo kwa kazi gani???

Hakina imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo. Huu ushuhuda wako unanikumbusha jambo langu fulani enzi hizo nipo O-Level. Niliomba kwa imani nikapewa kile kile. Sema baada ya kuanza kufukunyua mambo mengi kwa kutaka kujiongeza ufahamu imani yangu imepungua sana. Nakazana kabla ya uzeeni niwe nimerudia imani ya kale niliyokuwa nayo.
 
Safi sana. hadi Chuo ulikuwa unapiga hayo mabanda??? Au baada ya kukua ulipunguza imani ukaona unajumudu?? Na sasa upo kwa kazi gani???

Hakina imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo. Huu ushuhuda wako unanikumbusha jambo langu fulani enzi hizo nipo O-Level. Niliomba kwa imani nikapewa kile kile. Sema baada ya kuanza kufukunyua mambo mengi kwa kutaka kujiongeza ufahamu imani yangu imepungua sana. Nakazana kabla ya uzeeni niwe nimerudia imani ya kale niliyokuwa nayo.
Mpaka Chuo huko kwengineko ni privacy yangu
 
Back
Top Bottom