wehu tuu
halafu wanatudharau sie walimu masikini yarabi
llooohh
acheni hizo wadada na wamama wote
umalaya sio dili wala nini!
oneni sasa mnajidhalilisha tu!na mnadhalilika pia
hongereni vidume vyote mnaowamega hawa wasiojielewa...!!
hapa mwalimu mwenzangu sijakuelewa. Hapa nani anamdhalilisha nani? Kimsingi huyu mwanaume na hawa wanawake wote wamefanya mambo yao. Na msamiati wa kudhalilika hauko kichwani kwa yeyote kati yao. Unadhani kuna mwanamke yeyote miongoni mwa hawa amedhalilika? Wote wamefikia malengo yao isipokuwa yule wa Watu8 (nae angempata watu8 yeye ndo angestahili hongera kwa kufikia lengo lake).
Binti anayetumia mtego wa ucha Mungu kawanasa wote wale, na wengine kawalia hela na papuchi kawanyima; sioni mahali asipojielewa.
Mama mtu mzima aliyeonekana na busara za kutoa ushauri naye kapanga mkakati kijana akajitokeza hadharani akifikiri anaenda kupewa ushauri wa kumaliza tatizo lake la kisaikolojia. Kijana akanasa kwenye mtego wa mama. Huyu mama nae hajielewi? Kijana mwenyewe kasema hakutegemea lakini ndo hivyo aliwekwa kati akaliwa utamu na hela.
Kimsingi hapa ni ile habari ya kuuziana cheni feki kwa hela feki. Mtu anaazimia kutafuta hela ili ajithibitishe kwamba yeye ni kidume! Binafsi huwa sioni tofauti ya kimtazamo kati ya mwanamke na mwanaume anayemvulia nguo mwenzie. Wanawake tuna mengi sana ya kusema kuhusu hawa wanaume. Sema ndo majukwaa yetu saluni na vibarazani. Na kama wanaume wangejua huwa tunaongea nini kuhusu wao nakwambia kuna wanaume wangeshapoteza nguvu za kiume kwa sononi. Wanawake nao huwa wanaambiana mambo yao na kupanga mikakati ya kusaidiana. Mmoja akishafanikiwa anapeleka feedback. Unaskia "...shosti, siwezi kukusimulia....nenda na wewe ujionee..." Wanachora ramani, shosti naye anaenda. Shosti akitoka tu mlangoni anachukua simu na kutua yaliyomkaba kooni kwa mwenzie.."heee! shostiiiii....hapa sijui nicheke maana nahisi nitajikojolea, ngoja nije huko huko. Wakikutana sasa! Wanaanza kumchambua mkaka wa watu kuanzia maumbile mpaka utekelezaji. Mkaka naye saa hizo yuko Hisaje anajigamba kwa wenzie jinsi alivyoweza kuwala mtu na shosti wake bila wao kujua!! hahahaaaa....
Moyo wa mtu ni kiza kinene. Yaani mwanamke anataka hela yako au mwili wako, anajiwekea mkakati wa kukufanya ujipinde ili ufikie kiwango anachotaka, unaenda kutafuta hela hata kwa kuiba, unaenda kwake unapatwa halafu unakuja kujitapa hadharani kuwa umepata. Siwezi kumpa mwanaume kama huyu hongera kwa kufanyana na hawa wanawake, maana itakuwa namaanisha kuwa hawa wanawake ni wajinga, walikuwa hawataki, lakini kwa ujanja wa huyu kaka wamepatikana wakati ukweli ni kuwa walikuwa wanataka ila mwanzoni mwanaume huyu hakuwa amekidhi viwango. Alipokidhi alikubaliwa.
Mimi ni mwanamke, na huwa najiskia vibaya kidogo pale unapokuta kwa mfano katika biblia ni mwanaume tu anaonywa dhidi ya mbinu za mwanamke; anaonywa asimpe mwanamke/kahaba nguvu zake ; anaonywa dhidi ya mwanamke mtu mzima anayemdanganya kuwa mumewe kasafiri au kafa waende nyumbani kwake,anaonywa kwa kila jinsi asitumie nguvu zake, muda na fedha zake kwa mwanamke. Halafu unamkuta mahali anajisifia jinsi anavyokiuka haya maonyo. Mi nawapa hongera madume na majike yote yanayojiheshimu. Wasiojiheshimu siwahukumu maana ukamilifu si asili yetu. Mara nyingi hujikuta tukifanya mambo tusiyotaka lakini tunazidiwa nguvu. Tumeona huyu kaka kuna wakati aliona anataka kuacha na akatafuta ushauri ili aache, ila bila kujua akaenda kuomba ushauri kwa nyani kuhusu visa vya ngeder. All in all, he is not happy ila kama kuongea kunafariji, why not? Pengine ndo maungamo yanaanza.