The Only Thing We Have to Fear is Fear itself

The Only Thing We Have to Fear is Fear itself

duuuh hii imetolewa recycle bin?

Usitaharuki Mkuu!
Hamna cha dust wala recycle bin hapa JF.
Hii ni maktaba kubwa sana na kuna watu wakubwa zaidi au mithili...
Wanaonufaika zaidi na JF ni wanaosoma zaidi na kuitembelea kurasa zote.
 
I support You Mh. Mbowe in every Move, you deserve respect and support for those Tanzanians who need Justice.

Tuache Njaa, tuache unafiki. Tuikomboe Tanzania dhidi ya Ukoo wa Panya.

Viva Chadema!
 
TIME HAS REACH
LET GETOUT NOW AND SPEAK FREELY,
FEAR SHOULD NOT GET A CHANCE IN OUR LIVELHOOD, FEAR AND DOUBTNESS HAS BECAME MAJOR ISSUE AMONG MOSTLY TANZANIAN HEARTS, LET THROW OUTAWAY OLD ENGINE,AND PUT NEW MODERN WHICH GOES WITH REAL MEAN TiME,BLESSED BE TANZANIA
 
Hujui kuwa Mbowe ni member wa JF.

Alikuwa ctive sana wakati yuko shule UK.
ZeMarcopolo sio wewe ambaye huwa unasema Mbowe hakusoma unaweza kutuambia huko UK alikwenda kusoma secondary?

Halafu acha uongo wa ki-CCM alikuwa active wakati ID yake ina post 2 tu.
 
Salaam Wana Jambo.

Kwanza kabisa naomba niwapongeze wale walioanzisha forum hii kama sehemu ya matumizi ya uhuru wao binafsi. Aidha, niwapongeze kwani forum hii ni sehemu ya harakati muhimu ya kujadili mustakabali wa nchi yetu.

Nimesoma maoni, pongezi, malalamiko, hofu, ushauri na mambo mengine kadhaa katika forum hii. Nimejadiliwa mara kadhaa katika hoja tofauti. Nawapongeza wote waliochangia mada zilizonihusu hata kama wamenipinga au kuzusha. Nitoe pongezi zaidi kwa wale walioonyesha kuipenda nchi yetu na kuitakia mema kwa mijadala mbalimbali.

Leo naandika kwenye forum hii kwa mara ya kwanza. Siyo kusudio langu kujibu hoja zinazonihusu moja kwa moja. Aidha, siyo nia yangu kuingia kwenye malumbano ya aina yeyote na wachangiaji. Naheshimu sana uhuru na mawazo ya wote hata kama kwa makusudi au bahati mbaya yanapotosha. Binadamu tunatofautiana katika fikra, uelewa na malengo.

Siasa na uongozi wa Taifa letu vina mahusiano ya moja kwa moja na maisha yetu ya kila siku.Tanzania ni nchi yetu sote. Hatuna sababu ya kufanya masihara na siasa wala viongozi wetu wote. Walio madarakani na wale wenye nia hiyo.

Mara nyingi, binadamu ni wepesi wa kulaumu na kuhukumu. Tunapenda kadhalika, kudai haki pengine bila kutafakari kwa kina tumetekeleza wajibu wetu kwa kiasi gani.

Tupende tusipende, Tanzania ina kilio. Wote tusipojiuliza na kutekeleza wajibu wetu, kila mtu na nafasi yake kukabiliana na msiba huu, kamwe kilio hakitaisha. Muda wetu wa kuishi maisha haya ni mfupi sana na kila mmoja wetu anastahili kujiuliza amechangia nini katika wajibu wa kumaliza msiba huu?

Naamini, tatizo kubwa la kwanza la kukabiliana nalo nchini mwetu ni WOGA na HOFU. Naamini Wana Jambo forum wengi ni watu wenye uelewa wa kutosha. Kwa nchi yetu iliyo hoi kielimu na hata kiuwezo, hawa ni watu wa "kutumainiwa" na familia zao na hivyo nchi yao kwani familia ni sehemu ya nchi. Napenda kuamini ni sehemu ya "cream" ya Taifa letu nanyi kwa kutoa mawazo yenu, mmekuwa sehemu ya harakati.

Nasikitika, wengi wa wana forum wanatumia majina yasiyo ya kweli. Sina hakika kama siyo ishara ya woga! Na kama wasomi, waelewa, wenye upeo wanakuwa hivyo, Watanzania wa kawaida wategemewe wawe vipi? "Authenticity" ya tunayoyaandika inafifishwa na hali hii?

CHANGAMOTO: KWA KUFICHA MAJINA YETU UJASIRI WETU WA KUHOJI, KULAUMU NA KUHUKUMU UNAPINGANA NA DHAMIRA YA HARAKATI? HARAKATI NA WOGA VINAENDANA? WOGA UNAWEZA KUOKOA TAIFA?

By concealing our identity, are we truly living to our motto which says "Where we dare talk openly?"

"The only thing we have to fear is fear itself" - President Franklin Delano Roosevelt, Washington DC, 4th March 1953

Nawashukuru na naomba kutoa hoja!!

Freeman Mbowe

KWANZA KARIBU MWENYEKITI, PILI NAOMBA SOMA MAWAZO WANGU KUHUSIANA NA ISHU YA MWIGAMBA NA MIENENDO YETU YA KUTUMIA MITANDAO YA KIJAMII.



Tuhuma alizozitoa Mwigamba dhidi ya chama nimezisoma vizuri JF, nasikitika kwa kiongozi wa nyadhifa yake kutumia mtandao wa kijamii kuyasema yale mbaya zaidi kwa kutumia jina la bandia. Wenzetu waliokuwa kwenye vikao vya maamuzi wanakikosoa chama kwa kutumia mitandao, je, sisi tusiokuwa kwenye hivyo vikao tutatumia nini?

Vijana wengi waCHADEMA tumekilaani na kukoseshwa raha na kitendo cha Mwigamba, pamoja na hayo, hoja alizokuja nazo hadharani Mwigamba si za kubezwa hata kidogo. Tulaani kwa upande mmoja na tujikite kwenye maudhui ya hoja zake kwa upende wa pili.

Tunaomba viongozi wetu wakuu wa CHADEMA waangalie namna wanavyopokea mawazo mapya, namna wanavyowasikiliza wachache, namna ya kutekeleza maamuzi ya wengi(wengi wape) na namna ya kutekeleza maamuzi na maagizo ya vikao vikubwa vya kichama. Moja ya hoja ya Mwigamba kuwa vikao na maamuzi yake haviheshimiwi na viongozi wakuu aliowataja, sitaki kuamini kuwa hizo kasoro alishawahi kuzisema kwenye vikao sema tu hao viongozi kama alivyosema hawasikilizi maamuzi ya vikao, kama hawasikilizi maamuzi ya vikao wataweza kumsikiliza mtu mmoja anaye wakosoa? kama ndivyo basi hii ndio sababu iliyopelekea kutoka hadharani.

Huenda namna ya hizo nilizozianisha hapo juu zikawa hazifanywi katika namna ya kuridhisha na kupendeza, kama ndivyo, majukwaa ya ndani ya chama yatakuwa yananyima fursa ya kupokea mawazo mapya na kukosoa utendaji wa ofisi za viongozi wakuu. CHADEMA ijitathimini kwa hili, isiishie kumchukulia hatua za kinidhamu tu Mwigamba bila kuzifanyia kazi hoja alizokuja nazo hadharani.

Nimefurahi kusikia kuwa ametakiwa kudhithibitisha tuhuma alizozitoa dhidi ya viongozi wakuu wa chama, natoa rai kama tuhuma hizi zikithibiti basi Dr.Slaa, Mbowe, Zitto, Arfi na viongozi kama hao wa upande wa Zanzibar wajiuzulu nyadhifa zao. Wabaki kama wanachama wa kawaida na tuingize uongozi mwingine, uongozi utakaokuja kuendeleza mazuri ya watu hao na kuacha mabaya ya watu hao.( kama hayo mabaya yapo na yakithibiti). Endapo haya mambo yakithibiti na wasipojiuzulu basi itakuwa ni ndoto kwa CCM kutoka ikulu na ni ndoto kwa CHADEMA kuingia ikulu.

Kama Mwigamba akishindwa kuthibitisha hizi tuhuma alizozitoa dhidi ya viongozi wakuu wa chama, asiishie kuvuliwa uongozi tu, lakini pia afukuzwe uanachama na ikibidi ashitakiwe mahakamani kutokana kitendo hichi kibaya na kichafu ili iwe fundisho kwa watu wote wenye tabia kama hii ambao bado hawajajulikana, kwa kufanya hivi hao wengine ambao bado hawajulikana wanaweza kuacha tabia hii kwa kuchelea kukutwa na kitakachompata Mwigamba. Nafikiri hii ndio itakuwa njia ya pekee ya kulinda nidhamu na heshima ya chama mbele ya wanachama na watanzania kwa ujumla ambao kimsingi ndio wanunuaji wa sera zetu. Tukilea ujinga huu watatokea wengi wa kutuvuruga kisa tu waliona Mwigamba kapewa adhabu ndogo au onyo la kulaza ukope.

Hata hivyo sisi tulio nje ya ya vikao tunaweza kujiuliza operesheni ya M4C imepotelea wapi? Au tumeicha mara baada ya kutokea tukio la Iringa na vurugu za gesi Mtwara? Hivi ni kweli CCM wanatuandalia matukio bila kujua? Je, wakiacha kuandaa hayo matukio kisa tu Mwigamba kawashutua ndio CHADEMA bai bai? Pia tunaweza kujiuliza uchaguzi wa chama utafanyika lini ikiwa ilisemekana hadi desemba mwaka huu uchaguzi ungekuwa umekwisha malizika kwa ngazi zote, tunajiuliza hili la uchaguzi nalo limepotelea wapi? Hizi ni baadhi ya hoja chache alizokuja nazo Mwigamba hadharani. Je, sisi wanaCHADEMA tuishie kuona usaliti wa Mwigamba bila kuzingatia hoja hizi? Kwanini viongozi wasizijibu hoja za Mwigamba?

Kwa vyovyote vile watazijibu, wakati Mwigamba akithibitisha hizi tuhuma, subira ndio kila kitu katika hili, kama katakiwa kuthibitisha na kwa vyovyote vile nasi twakiwa kusubiri, kama ndivyo huu wimbo wa usaliti usaliti unapata uhalali gani katika kipindi hichi cha kusubiri? Na wale wanawalaumu Mbowe na viongozi wenziwe waliotajwa katika bandiko la Mwigamba pia wanapata uhalali gani wa kufanya hivyo ikiwa bado Mwigamba hajathibitisha katika vikao halali na uthibitisho huo kukubalika? Tuvute subira kwani siku zote ndio huvuta heri, kinyume chake labda tunataka maamuzi ya chama juu ya hili yazingatie mbwembwe zetu badala ya uthibitisho wenyewe.

Pamoja na hayo, Mwigamba kama aliona mawazo yake hayasikilizwi na kutekelezwa, na kama aliamini mawazo yake ni sahihi na yako kwaajili ya kujenga chama, basi ni vema MOSI angejiuzulu; hakuna umuhimu wa kufanya kazi na watu usiowaamini na kuwakubali au wasiokusikiliza au wanaokubeza. Pili, angetoka hadharani, tena si kwakutumia jina bandia, bali angetumia jina lake halisi, angetangaza kujiuzulu kwake na mapungufu aliyoyasema angeyataja kama sababu ya kujiuzulu huko.

Kitendo cha kuusifia uongozi wa Dr.Slaa na Mh.Mbowe kwenye kikao halali cha chama, na kisha kwa kutumia jina la bandia akawa anaukandia huo uongozi kama vile hakuusifia muda fupi uliopita kwa wakati ule, ni usaliti kwa uzalendo wake kwa chama, usaliti kwa weledi wake ambao wengi wetu tunaujua na mwisho ni usaliti kwa uanaume wake; kwani hatutaraji kwa mwanaume kusema vitu sahihi na anavyoviamini kwa kutumia jina la bandia kisa tu asijulikane. Nitaendelea kumlaumu Mwigamba kwa hili haijalishi alichokisema ni sahihi au la!

Halafu hili suala la viongozi na wanachama kutumia mitandao vibaya na bila ridhaa ya CHADEMA yenyewe limekuwa kama vile limeota mizizi fulani vilee. Kipindi fulani tulishuhudia Naibu Katibu mkuu wa CHADEMA akitupiana maneno na wajumbe wa kamati kuu kisa tu namba yake lilikuwa kwenye tamko la wajumbe hao walilolitoa kwa niaba ya chama, wengine tunajiuliza, kama lile lilikuwa tamko la chama lililobarikiwa na kamati kuu iweje Naibu Katibu mkuu alipinge hadharani ikiwa na yeye ni mjumbe wa kamati kuu ikiwa kimsingi na kikatiba yeye ni zao la tamko? Nimelitaja hili kwa lengo la kuonesha hii tabia ya kutumia mitandao ya kijamii kwa namna mbaya na chafu kwa Mwigamba si wa kwanza na limbuko.

Pia tulishuhudia vijana wakimtuhumu Zitto kuwa ni msaliti na mengi yalisemwa, vijana waliokuwa wanasema Zitto msaliti ni wanachama na wanajulikana vizuri, lakini hadi leo hii na kwa vyovyote vile hawajaitwa kuthibitisha usaliti wa Zitto na wanaendelea hadi sasa katika mitandao kumuandama Zitto. Hotuba aliyoitoa Zitto katika mkutano wa CHADEMA Tabora hivi karibuni aliwaasa vijana waache kuwagombanisha viongozi wakuu wa chama, alisema vijana wanashinda kwenye mitandao kugombanisha viongozi, kwa vyovyote vile Zitto alisema hivi huku akizingatia mambo yanayofanywa na baadhi ya vijana kwenye mitandao. Hili la Mwigamba ni matokeo ya CHADEMA kushindwa kuwadhibiti baadhi ya vijana wa CHADEMA wanaotumia mitandao kukichafua chama na inaonekana mwindelezo tu wa tabia za watu kudhani kuwa CHADEMA iko kwenye mitandao ingawa kiukweli CHADEMA iko kwenye mioyo ya wananchi.

HITIMISHO:
Mara nyingi tunaambiwa wagawe kisha watawale. CCM inafanya kila hali kuhakikisha Viongozi wa CHADEMA na wanachama wao wanakuwa wanagawanyika ili wapate kutushinda na kututawala kwa muda mrefu watakavyo. Tunavyowakosoa viongozi wetu hadharani, kwa vyovyote vile CCM watajifanya kama vile wanaunga mkono ule upande unaokosolewa, lengo la kufanya hivyo ili wale wanaokosoa waone wale wanaowakosoa kuwa ni wasaliti kisa tu wanaungwa mkono na CCM. Hivyo sitoshangaa kuona CCM wakimuunga mkono Mwigamba kama vile wanavyojifanya wanamuunga mkono Zitto.

Hitimisho langu linalenga kwa sisi wanaCHADEMA tulio nje ya vikao vikubwa vya maamuzi, tuwaunge mkono viongozi wetu wote, kukiwa na ulazima wa kuwakosoa, basi tufanye hivyo kwa kuzingatia hoja na kwa kufuata utaratibu(kinyume chake vurugu na usaliti); kwa kufanya hivyo tutaweza kujadili hoja kwa kuzingatia maudhui ya hoja yenyewe na si kwa kuzingatia wasifu wa mtoa hoja ambao hausiani na hoja yake(upo wasifu wa mtoa hoja wenye kuhusiana na hoja yake) lakini kubwa tutaweza kujitoa kwenye ulimwengu wa macho ya nazi na ushabiki wa kichamchunga.

Hitimisho langu linalenga kutukumbusha kuwa hakuna wakati ambao CHADEMA yahitaji mshikamano na utangamano kama wakati wa sasa; wakati ambao CCM imeshagundua iko chumba cha wagonjwa mahututi na inajiandaa kisaikolojia kwa kushindwa uchaguzi ujao(Rejea hotuba ya Kikwete aliyoitoa tar 24 mjini Dodoma). Ili tuwe na mshikamano na huo utengamano ni lazima viongozi wakuu wa chama wakaonesha njia na kuwadhihirishia umma kuwa wao ni wamoja na hakuna matatizo miongoni mwao na wawatake watu wasiamini kuwa wao viongozi wakuu na migogoro kama watu wanaoshinda kwenye mitandao wanavyojaribu kuaminisha umma kuwa CHADEMA iko na migogoro. Tusipofanya hivyo, CCM itajiandaa kisaikolojia kwa kupokea ushindi badala ya kujindaa kupokea kipigo toka kwa CHADEMA.

Hitimisho langu linalenga kuwa si kila mwanaCHADEMA anayeikosoa CHADEMA na viongozi wake ni msaliti na katumwa na CCM hata kama huyo mkosoaji anaungwa mkono na CCM(Zingatia sababu za CCM kuwaunga mkono wakosoaji wa CHADEMA waliomo ndani ya CHADEMA), bali ifike mahala tukubali kuwa chama kimekua kikubwa na kina watu wengi na kila mmoja wetu yuko na uwezo wake wa kufikiri na kuyatazama mambo, kwa kuzingatia hilo, ni sahihi msimamo yetu na maoni yetu kutofautiana kama vile uwezo wa kufikiri kwetu unavyotafautiana. Ni hivi, lile ambalo waliona "sahihi" kwa uwezo wako wa kufikiri na mwingine kwa uwezo huo huo anaweza kuliona "si sahihi" kwa hivyo kuheshimiana, kusikilizana na kufuata mawazo ya wengi yaliyozingatia hoja za wachache ndio kila kitu katika maisha ya seti kuu iitwayo chama cha siasa, kinyume chake ni vurugu kama si udikteta uliodhahiri.

Hitimisho langu lanalenga kutoa waasa kwa vijana, kwa kuanzia mimi niliyeandika haya na kwa wenzangu wote, tusimamie misingi ya chama na tujenge hiyo misingi kwenye mioyo yetu, tuwe wanachama wa kumaanisha na si wanachama kadi au vumbi. Wanachama wa CHADEMA wa kumaanisha ni wale ambao hata kama Dr.Slaa akirudi CCM wao wataendelea kuwa CHADEMA, haturajii kwa mwanachama wa kumaanisha kuingia CCM kisa tu Zitto Kabwe kajiunga na CCM. Mwanachama aliye na msingi wa CHADEMA katika moyo wake hawezi kuwakosoa viongozi wake kinyume na taratibu na katu hawezi kuwatetea viongozi wake wabadhirifu kisa tu yuko na mahaba na hao viongozi.

BILA CHADEMA IMARA MAFISADI WATATAMBA MCHANA WA JUA UTOSI.

MIMI NA WEWE TUIFANYE KUWA IMARA.


MwanaCHADEMA.

 
andiko refu lakini lenye mchanganuo wenye afya kuhusu mustakabali wa chadema!

KWANZA KARIBU MWENYEKITI,
PILI NAOMBA SOMA MAWAZO WANGU KUHUSIANA NA ISHU YA MWIGAMBA NA MIENENDO
YETU YA KUTUMIA MITANDAO YA KIJAMII.




Vijana wengi waCHADEMA tumekilaani na kukoseshwa raha na
kitendo cha Mwigamba, pamoja na hayo, hoja alizokuja nazo hadharani
Mwigamba si za kubezwa hata kidogo. Tulaani kwa upande mmoja na
tujikite kwenye maudhui ya hoja zake kwa upende wa pili.

Tunaomba viongozi wetu wakuu wa CHADEMA waangalie namna
wanavyopokea mawazo mapya, namna wanavyowasikiliza wachache, namna ya
kutekeleza maamuzi ya wengi(wengi wape) na namna ya kutekeleza maamuzi
na maagizo ya vikao vikubwa vya kichama. Moja ya hoja ya Mwigamba kuwa
vikao na maamuzi yake haviheshimiwi na viongozi wakuu aliowataja,
sitaki kuamini kuwa hizo kasoro alishawahi kuzisema kwenye vikao sema
tu hao viongozi kama alivyosema hawasikilizi maamuzi ya vikao, kama
hawasikilizi maamuzi ya vikao wataweza kumsikiliza mtu mmoja anaye
wakosoa? kama ndivyo basi hii ndio sababu iliyopelekea kutoka hadharani.

Huenda namna ya hizo nilizozianisha hapo juu zikawa hazifanywi
katika namna ya kuridhisha na kupendeza, kama ndivyo, majukwaa ya
ndani ya chama yatakuwa yananyima fursa ya kupokea mawazo mapya na
kukosoa utendaji wa ofisi za viongozi wakuu. CHADEMA ijitathimini kwa
hili, isiishie kumchukulia hatua za kinidhamu tu Mwigamba bila
kuzifanyia kazi hoja alizokuja nazo hadharani.

Nimefurahi kusikia kuwa ametakiwa kudhithibitisha tuhuma
alizozitoa dhidi ya viongozi wakuu wa chama, natoa rai kama tuhuma
hizi zikithibiti basi Dr.Slaa, Mbowe, Zitto, Arfi na viongozi kama hao
wa upande wa Zanzibar wajiuzulu nyadhifa zao. Wabaki kama wanachama wa
kawaida na tuingize uongozi mwingine, uongozi utakaokuja kuendeleza
mazuri ya watu hao na kuacha mabaya ya watu hao.( kama hayo mabaya yapo
na yakithibiti). Endapo haya mambo yakithibiti na wasipojiuzulu basi
itakuwa ni ndoto kwa CCM kutoka ikulu na ni ndoto kwa CHADEMA kuingia
ikulu.

Kama Mwigamba akishindwa kuthibitisha hizi tuhuma alizozitoa
dhidi ya viongozi wakuu wa chama, asiishie kuvuliwa uongozi tu, lakini
pia afukuzwe uanachama na ikibidi ashitakiwe mahakamani kutokana
kitendo hichi kibaya na kichafu ili iwe fundisho kwa watu wote wenye
tabia kama hii ambao bado hawajajulikana, kwa kufanya hivi hao wengine
ambao bado hawajulikana wanaweza kuacha tabia hii kwa kuchelea
kukutwa na kitakachompata Mwigamba. Nafikiri hii ndio itakuwa njia ya
pekee ya kulinda nidhamu na heshima ya chama mbele ya wanachama na
watanzania kwa ujumla ambao kimsingi ndio wanunuaji wa sera zetu.
Tukilea ujinga huu watatokea wengi wa kutuvuruga kisa tu waliona
Mwigamba kapewa adhabu ndogo au onyo la kulaza ukope.

Hata hivyo sisi tulio nje ya ya vikao tunaweza kujiuliza
operesheni ya M4C imepotelea wapi? Au tumeicha mara baada ya kutokea
tukio la Iringa na vurugu za gesi Mtwara? Hivi ni kweli CCM
wanatuandalia matukio bila kujua? Je, wakiacha kuandaa hayo matukio kisa
tu Mwigamba kawashutua ndio CHADEMA bai bai? Pia tunaweza kujiuliza
uchaguzi wa chama utafanyika lini ikiwa ilisemekana hadi desemba mwaka
huu uchaguzi ungekuwa umekwisha malizika kwa ngazi zote, tunajiuliza
hili la uchaguzi nalo limepotelea wapi? Hizi ni baadhi ya hoja chache
alizokuja nazo Mwigamba hadharani. Je, sisi wanaCHADEMA tuishie kuona
usaliti wa Mwigamba bila kuzingatia hoja hizi? Kwanini viongozi
wasizijibu hoja za Mwigamba?

Kwa vyovyote vile watazijibu, wakati Mwigamba akithibitisha hizi
tuhuma, subira ndio kila kitu katika hili, kama katakiwa kuthibitisha
na kwa vyovyote vile nasi twakiwa kusubiri, kama ndivyo huu wimbo wa
usaliti usaliti unapata uhalali gani katika kipindi hichi cha kusubiri?
Na wale wanawalaumu Mbowe na viongozi wenziwe waliotajwa katika bandiko
la Mwigamba pia wanapata uhalali gani wa kufanya hivyo ikiwa bado
Mwigamba hajathibitisha katika vikao halali na uthibitisho huo
kukubalika? Tuvute subira kwani siku zote ndio huvuta heri, kinyume
chake labda tunataka maamuzi ya chama juu ya hili yazingatie mbwembwe
zetu badala ya uthibitisho wenyewe.

Pamoja na hayo, Mwigamba kama aliona mawazo yake hayasikilizwi
na kutekelezwa, na kama aliamini mawazo yake ni sahihi na yako
kwaajili ya kujenga chama, basi ni vema MOSI angejiuzulu; hakuna
umuhimu wa kufanya kazi na watu usiowaamini na kuwakubali au
wasiokusikiliza au wanaokubeza. Pili, angetoka hadharani, tena si
kwakutumia jina bandia, bali angetumia
 
Hakuna kitu kinachonipita akili yangu kama kutojibu hoja kwa kujifanya kujibu hoja! Maneno ya kebehi na dharahau yanaweza kuvutia hisia lakini hayashindi hoja. Je upinzani wa Tanzania jinsi ulivyosasa unaweza kukabidhiwa nchi nzima kuiongoza? Jibu langu ni HAPANA HAPANA HAPANA!! Je CCM jinsi ilivyosasa inaweza kuongoza nchi yetu jibu ni NDIYO NDIYO NDIYO! Je CCM na matatizo yake yote na mapungufu yake yanayoweza kujaza vitabu inastahili kupewa uongozi wa nchi jibu ni HAPANA HAPANA HAPANA, Je upinzania namapungufu yake yanayoweza kujaza juzuu wanastahili kupewa uongozi wa nchi jibu ni HAPANA HAPANA HAPANA!! Nitafafanua.

Chama cha Mapinduzi ni chama ambacho kimelewa madaraka na viongozi wake wengi wamebweteka na vyeo vyao na kutokana na chama hicho kukita katika kila kona ya maisha ya Watanzania basi viongozi hao hawaoni haja ya kulitumikia Taifa letu jinsi ile inapaswa! Pamoja na hayo yote, CCM imeweza kufanya mambo ambayo Watanzania wanayathamini licha ya kujua udhaifu mkubwa wa Chama hicho. Unafikiri viongozi wote wasomi walioko CCM hawajui udhaifu wa chama chao au ni sisi wewe kwenye Jambo Forum ambao ndio tuna akili zaidi kuliko Mtanzania yeyote?

Wengi wa wanachama wa CCM ambao wamepima upinzani na chama tawala wamechagua chama tawala. CCM inafanyiwa mabadiliko toka ndani, toka viongozi waliopo ndani, na toka wanachama waliondani. Hawasubiri wakosoaji walio nje kujiunga nacho ndio waanze kufanye mabadiliko!! CHADEMA, CUF, TLP na wenzao hawawezi kusubiri watu wajiunge nacho ndio waanze mabadiliko!!

Kuna watu wanajifanya wanajua historia hapa, bila ya shaka wanaijua historia ile inayowafaa wao na matakwa yao! Martin Luther King Jr hakuwa mwanasiasa, na kilichomsukuma sio haja ya kuwa na cheo cha kisiasa. Alisukumwa na imani yake!! Soma maandiko yake ya "Barua toka Jela ya Birmingham"!

Wanamtolea mfano Abraham Lincoln, nani aliwaambia Lincoln alikuwa mpinzani wakati alipotia sahihi "tangazo la kuwekwa huru" kwa watumwa kusini mwa Marekani? Je unajua hata tangazo lake halikuwafungua watumwa wote? Lincoln, alifanya mabadiliko hayo akiwa Rais wa Marekani! Kwa kifupi, kama kuna mtu anayeweza kuleta mabadiliko makubwa katika Tanzania si Mbowe, si Lipumba, si Mrema, ni Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania!

Mmemtaja Mandela, Mandela alileta mabadiliko makubwa zaidi alipokuwa kifungoni au alipotolewa nje? Nitawaacha mfikiri nina maana gani hapo!

Quarz anadai ati siwezi kuwa mkosoaji tu na sitoi masuluhisho ya aina yoyote. Inaonekana hujafuatilia maandishi yangu. Mimi ni mkosoaji mkubwa wa serikali ya Kikwete, nilipigia kelele suala la Mahita kabla ya watu wengi kulipigia kelele, niliungana na wengine kupigia kelele suala la Richmond bila haya (na nikaitisha kuondolewa kwa Msabaha), nilipigia kelele mambo mengi ambayo wasikilizaji wangu wanayajua! Leo nikisimama na kusema kuwa licha ya kelele zangu CCM bado ni chama pekee kinachoweza kuongoza Tanzania watu wanadhani nimejigeuka! Hata kidogo. Mimi sina maslahi katika Upinzani, sina maslahi na CCM (sio mwanachama). Maslahi pekee niliyonayo ni yale yanayohusu Tanzania nzima na siyo chama au kikundi fulani cha watu! Ni kwa sababu hiyo siwezi kutetea kuikabidhi hatima ya Tanzania kwa watu wasio na nia wala uwezo wa kuongoza Taifa alimradi ati ni wapinzani na wao pia wanaichukia serikali ya CCM. Nina madhaifu mengi, lakini ujinga wa kisiasa sio mojawapo!

Nimetoa mapendekezo ni nini upinzani ufanye ili ujiweke mahali pazuri pa kushinda watu wanadhani ninawaletea husuda! Kama wao wanasubiri watu wajiunge nao ndio waanze kujiimarisha, basi waendelee kusubiri!! Anzeni kujiimarisha wenyewe msisubiri hisani ya CCM! CCM haina mpango wa kuwaimarisha wala haina nia ya kuona mmeungana!! Papa mkaange kwa mafuta yake!

Kuhusu hilo la kunitakia nifie huku huku niliko, wala halinitishi kwani nikifa au nikiwa hai mimi ni mali ya bwana, na nitakufa kama Mtanzania, kama nitafia kwenye ardhi ya wazazi wangu au ugenini!! Anyway, nakutakia wewe na wenzio muishi maisha marefu na ya afya, na muweze kuitumikia nchi yetu kwa kujituma zaidi kuliko wale ambao wamefanya hivyo hadi sasa.

Wabillah Tawfiq!

Mwanakijiji, niseme ukweli kabisa na kukubali sana hicho unachokisema,,,nimefuatilia maandishi yako mengi na umetoa ushauri mara nyingi kwa upinzani na hata kwa serikali yetu, nina amini bila hata kusema wewe mwenyewe, umesukumwa kutoa ushauri huu kwa kutimiza wajibu wako kama mtanzania. Mungu hatokuuliza umeifanyia nini Tanzania bali atakulipa vinono bi maana hana sababu ya kuuliza.

Ni vema vyama vya upinzani pamoja na chama chetu cha CHADEMA vifikirie dhamira yao kuutumikia umma ni ya kweli au ni ya urongo, lazima waifikirie ile dhamira yao ya kuitoa CCM madarakani, kwani kwa vyovyote vile utitiri huu wa vyama vya siasa, kutokufika kwa wananchi vyama hivi vya siasa na kushindwa kwa vyama hivyo mara zote kuitoa CCM madarakani toka mfumo wa vyama vingi ulivyorudishwa tena mwaka 1992 ni kiashiria tosha kuwa vyama hivi havina dhamira ya dhati ya kushika dola.

Nafikiri na kama sitakosea majuma mawili yaliyopita kulitolewa utafiti unaonesha kuwa asilimia kubwa ya watu wasiokuwa na elimu ya chuo ndio wanaoukubali uongozi wa KIKWETE, na kwa Tanzania wengi sana hatuna hiyo elimu ya chuo na wengi wa Tanzania hao tunaishi vijijini. Kiukweli watanzania wengi hawajafikiwa na vyama vya upinzani na asilimia kubwa ya wanachama na wapenzi wa vyama vya upinzani wameingia kwenye vyama hivyo kwa kuongozwa na ushabiki wao kwa wanasiasana si kwa kuongozwa na dhamira ya kutaka kuleta mabadiliko kupitia vyama hivyo.

Mfano: Dr Slaa na timu yake ya M4C walifika Katika vijiji vya Morogoro na kufungua misingi na matawi huko, alipoondoka huku nyuma kukawa hakuna watu wa kuwafundisha wale wanachama 30 wanaounda MSINGI (ngazi chini kabisa katika CHADEMA) falsafa na itikadi ya CHADEMA, kwa hiyo hawa watu 30 huwezi kuwaita wanaCHADEMA bali utawaita ni wafuasi Dr.Slaa, au Zitto, au Mbowe au wa viongozi wengine wanaofanya operesheni mbalimbali za kichama zenye kujumuisha na ufungzi wa matawi na misingi mipya, kiukweli wanakuwa wafuasi wa hao watu kwakuwa viongozi hao walipoondoka mara ya operesheni kupita katika eneo lao hao wanachama wapya hawakupata semina ya kufundishwa chama. Nilishawahi kuandika kipindi fulani kuwa Mnyika akihamia CCM tunaweza kulikosa jimbo la Ubungo, kwasababu tuna wanachama mashabiki na si wanachama wa kumaanisha. Wanachama wa ushabiki, Mnyika anaweza kuhama nao na watakuwa ndio msingi wa kura zake jumlisha na za CCM.

Ukitaka kuamini tuna wanaCHAMA mashabiki na si wanaCHADEMA, jaribu kutazama mienendo ya wanaCHADEMA humu JF kukiwekwa uzi kuhusu Zitto au Dr.Slaa au Mbowe, utajua ni mwanaCHADEMA gani akiusoma huo UZI ataupinga na nani atauunga mkono kwa kutazama tu maudhui ya UZI husika. Hawa ndio wanachama ambao CHADEMA inajivunia nayo ambao kiukweli si wanachama wake bali ni wanachama wa watu.

Ofisi za jimbo na kata ndizo zenye jukumu la kuhakikisha kuwa M4C ikipita na kuleta wanachama wapya zenyewe ziwafunde hao wanachama, lakini watendaji wa ofisi hizi(makatibu) hawana mishahara wala posho hivyo muda mwingi wanatumia kuhemelea familia zao badala ya kujenga chama na kwa hivyo hawapati muda wa kutoa semina kwa wanachama katika matawi yaliyopo kwenye majimbo yao. Hii ndio maana wanachama tulioletwa na vumbi la helkopta hatujui chochote zaidi ya kumshabikia yule tuliyevutiwa naye katika kuikandia CCM katika ile siku ya helkopta ilipotua mara ya kwanza kwenye kijiji chetu na kubahatika kuiona kwa macho yetu.

Kwakuwa simu za mchina mashallah nazo siku hizi hazisemi urongo na kwakuwa wakina KABANG, CHEKA BOMBASTIKI, EPIC NATION na ILE YA YATOSHA hawatutupi kimtindo fulani, hivyo basi matlai ya vumbi la helkopta tunayaleta mitandaoni kwa kushabikia kila asemacho mtu kama vile huyo ni mungu na/au kupinga kila asemacho mtu kama vile huyo mtu ni shetani. Tangu lini shetani hupatia mbele ya mja si kama kwa shetani huyo kutega mitego yake? Tangu lini Mungu hukosea si kama kwa mja huyo mwenye kusema Mungu kakosea anataka kujitoa mwenyewe kwenye mtandao wa kupendwa na Mungu? Hawa ndio wanachama wa vyama vya upinzani, na wanachama namna hii ni rahisi kurubuniwa na CCM na nirahisi kuvihujumu vyama vyao bila wenyewe kujua.

Hapa naweza kusema kuwa, kwa wale wananchi wa vijijini waliongia kwenye vyama vya upinzani wengi wao hawazijui falsafa na itikadi ya vyama hivyo, CHADEMA imeshindwa kuwafundisha wanachama wake hata wakijue na vyama vingine pia vimeshindwa kufanya hivyo. Wanachama hawa vanavipenda vyama vyao si kwasababu vyama vyao vina jawabu juu ya kero za maji, elimu na huduma nyingine kwenye vijiji watokavyo bali wanavipenda vyama vyao kwasababu ndani ya vyama vyao kuna viongozi wanajua kukemea ufisadi na kuishambulia CCM na serikali bila woga. Kwa kufanya hivyo wanakuwa wanachama wa watu badala ya kuwa wanachama wa chama husika. Wanzabar wanaipenda CUF kwasababu Seif haoni haya kusema Muungano ni sawa na ukoloni, Seif akienda CHAUSTA lazima CUF Zanzibar itapwaya na CHAUSTA kuja juu.

Hapa naweza kusema kuwa wananchi wengi wa vijijini wanachojua wao na wanachokipenda ni kuamka asubuhi kuenda shamba na watoto zao wameenda shule, wanakula chakula, wanakunywa maji na usiku wanalala kwa amani na utulivu bila kububudhiwa na panya au pimbi. Wanapenda hivi bila kuzingatia ni umbali gani mtoto wao wanatembea kufuata hiyo elimu, ni ubora gani wa hiyo elimu, na hata hawazingatii pia ubora wa hapo wanapolala kwa amani na utulivu. Mtanzania huyu hajui kuwa ni wajibu wa serikali kuboresha hayo na ni wajibu wake kuitoa na kuingiza serikali madarakani. Mtanzania wa namna hii ukimuuliza swali hili, "Hivi kwa maoni yako uongozi wa Kikwete ni mzuri?", Jibu lake atakalokupa ni kuwa ungozi wa Kikwete ni mzuri. Watanzania hawa vyama vya upinzani hatujawafikia na ndio hao walioifanya ile tafiti iseme watanzania wengi waliokuwa hawana elimu ya chuo wanaridhishwa na uongozi wa Kikwete.

Hapa naweza kusema kuwa, wanachama wengi wa vyama vya upinzani walipo vijijini na mijini hawajui falsafa, itikadi na sera za vyama vyao, kwa kuongezea, kitendo cha ushabiki na kitendo cha wanachama hao kutolipa ada za uanachama tangu siku ile alipopewa kadi ya bure au ya kununua mwenyewe(huenda pia alinunua kwa ushabiki tu) ni kiashiria tosha kuwa mwanachama huyo si mwanachama wa kumaanisha bali mwanachama vumbi. Kama waamini juu ya chama kwanini usilipie ada ya uanachama kwa wakati? kwanini usiamini juu ya misingi ya ujenzi wa tasisi badala yake unaamini juu ya kumjenga mtu? Vyama venye nia ya dhati ya kuingia ikulu na kutumikia umma haviwezi kuwa na wanaCHAMA wa namna hii, kwani tunategemea wanaCHAMA ndio kura za msingi, lakini wanachama wa namna hii huwezi kuwategemea kwani lowassa na kundi lake ni rahisi kuwarubuni lakini pia yule wanayemuamini katika chama akihama nao pia uhama. Hivi Maalim Seifu arudi CCM au Zitto ajiunge na CCM wafikiri wataenda huko wenyewe?

Hapa naweza kusema kuwa viongozi wa majimbo wa vyama vya siasa pindi timu za makao makuu wakianzisha uperesheni ya ujenzi wa chama basi viongozi hawa wa majimbo na kushirikiana na wa kata watoe semina kwa wanaCHAMA wapya, lakini pia ofisi za majimbo zijiwekee utaratibu wa kutoa elimu ya uraia na kujitambua katika kata, vijiji na mitaa ambayo iko kwenye jimbo husika ili kuwafikia watanzania kwa ujumla wao haijalishi ni wanachama wa vyama vingine au hawana chama kabisa, kwa kufanya hivi watanzania hawa watajua wao kama raia wana haki gani toka kwa serikali yao na wanajibu gani kwa nchi yao, kinyume chake kila uchaguzi tutakuwa tuna lalamika tunaibiwa kumbe watu wengi wenye kadi za vyama vyetu vya upinzani hawaendi kupiga kura pamoja na kwamba walijiandikisha kupiga kura. Sasa ikiwa chama kimeshindwa kumshawishi mwanachama wake kwenda kupiga kura, je, kitaweza kumshawishi mwanachama wa chama kingine au asiyekuwa na chama akipigie chama hicho kura? Jibu la swali hili weka kapuni kama wewe ni mnafiki.

Pia natoa rai kwa wale wanachama wa kweli wa vyama hivi vya upinzani, kwa mfano CHADEMA kwa kuzingatia kuwa chama hakina chanzo cha mapato himilivu na chenye kutumainiwa na kutegemwa, basi katika maeneo yetu tunayotoka tunaweza tukaanzisha kautaratibu ambacho wenyewe wanachama wa jimbo husika au kata husika tunakubaliana kwa hiyari bila kulazimishwa na kwa sharti la yeyote miongoni mwetu asifungwe kwa hilo, kautaratibu wa kuwafikiria makatibu wa maeneo yetu kwa kuanzisha japo ka mchango cha kila mwezi ili fedha hizi tuwape wale wanaofanya kazi katika ofisi za chama kwa niaba yetu. Mfano mtu unatumia 500 ngapi kwa mwezi? je, mkijiamulia kwa kwa mwezi kila mmoja wenu achangie jero?

Pia natoa rai, pamoja na kwamba ruzuku ni ndogo kwa vyama vya siasa na mapato mengine pia hayatoshelezi lakini ni vema hii ruzuku ika gawanywa kwa majimbo na mapato mengine yangegawanywa kwa majimbo yote pamoja na udogo wake. Niko na imani mgawanyo huu mdogo unaweza kupewa nguvu na michango ya hiyari ya wanachama katika majimbo husika. Zingatia hapo juu nimependekeza kila mwezi mwanachama anaweza kuombwa kuchangia tsh 500/= Kama makatibu wakifanya kazi nzuri wanachama hawatajutia michango yao, kwani chama kinahitaji kuhudumiwa na si chama kituhudumie. CHAMA kitatuhumie mara baada ya chama hicho kushika dola na kitafanya hivyo kwa kuteleza ilani ya uchaguzi na si vinginevyo.

Pia natoa rai kwa vyama vya upinzani kuangalia namna na njia mbadala ya kuongeza mapato badala ya kutegemea ruzuku toka serikalini. Ruzuku iko kisheria, lakini ni wazimu si kama ujuha kwa chama cha upinzani kutegemea kuingia ikulu kwa kutegemea fedha za ruzuku katika kuendesha harakati zake. Kwa mfano humu kwenye mitandao vijana huwa wanaweka picha zilizotengezwa zenye kuonesha mabasi yenye alama na nembo nzuri za CHADEMA, kwanini CHADEMA na vyama vingine vya upinzani visifikirie kuanzisha miradi kama hiyo kama taratibu zinaruhusu vyama kuwa na vitega uchumi wa vya namna kama hiyo? Ukweli uko wazi vyama maskini haviwezi kuitoa CCM hata TANU ilikuwa na fedha(ingawa fedha hizo zilitokana na wanachama na si biashara) ndio maana ikaweza kutuleta uhuru. Kwani Nyerere alienda UN kwa ungo? na alizungukuka nchini kwa miguu? Je, wakati anazunguka familia yake ilikuwa inakaa njaa? Tuache utani, fedha ni muhimu, nidhamu kaitka fedha ni muhimu na kujitolea pia ni muhimu, naam, yote haya ni muhimu.

HITIMISHO:
Nimeandika mengi na hili nisiharibu mambo na kwa kuchelea kutoka nje ya mada niliyokuwa naiandikia naoma nihitimishe kwa kutoa rai kwa vyama vyote vya upinzani kuangali namna ya itakayowezesha uchaguzi ujao tunasimamisha mgombea mmoja wa urais na kuangalia namna ya kuweza kufanya mashirikiano ya kutoa elimu ya uraia na kujitambua kwa watanzania wote hususani waliopo vijijini kwani huko ndiko walipo watanzania wengi. Ile aibu ya zaidi ya nusu waliojiandikisha kupiga kura uchaguzi uliopita hawakujitokeza kupiga kura isijirudie tena uchaguzi ujao, kinyume chake tutashindwa uchaguzi ujao pamoja na kwamba tutafanya chini ya katiba mpya; sasa sijui tutasingizia nini?? Manake nyumba ya mwanasiasa kama nyumba ya mganga, naam, haishiwi nyimbo.

Njano5
0784845394
 
Mhh! inatia moyo,hongeleni viongozi wa CHADEMA ndoto zenu hakika zinatimia karibuni.
 
Wakuu,

Hii post iliwekwa mwaka 2006 tuliichangia kipindi hicho.Sasa wengine wasidhani ni mpya
 
Wakuu,

Hii post iliwekwa mwaka 2006 tuliichangia kipindi hicho.Sasa wengine wasidhani ni mpya

Ni kweli Ben, wakati mwingine ama niseme kabisa hizi public figure ni alama muhimu sana kwenye mabadiliko tofauti tofauti ya taifa, kuna wakati watu hujisahau kwa kutojua walichokuwa wakikiamini kabla, kwa hivyo machapisho yao hutumika kuwakumbusha!

Jana kama una kumbu kumbu nzuri wakati bi hawa ghasia akichangia mjadala kwenye bunge maalum la katiba alisema yafuatayo, namnukuu..
"Wanajifanya wazalendo huku wanakesha wakiwatukana wazee wetu waasisi wa taifa.."
BAADA YA MUDA,
"Huyu mzee Warioba ni kimbelembele. Ktk hadidu za rejea aliambiwa asiguse muungano, lakini kwa kujifanya muelewa akaugusa na mbaya zaidi ya kutaka kuuvunja. Halafu hata baada ya kuwasilisha rasimu bado akawa anajipeleka peleka kwenye vyombo vya habari. Kamati ilikua na wajumbe zaidi 30, lakini yeye tu ndo kiherehere wa kuongea na media kila siku. Wengine hatuwaoni. Huyu mzee vp!?'' Ni vizuri kutunza mambo ili yatumike kama ushahihi kwa siku za mbeleni...
 
Mheshimiwa Mbowe umenikuna. Umetuthibitishia kama alivyosema Mzee ES kuwa forum hii inapitiwa na watu wazito! Ahsante sana kwa kuingia hapa. It has boosted the profile of the forum, but of course, of our party as well! Najua hakuna kiongozi wa CCM anayeweza kuthubutu kutumbukia humu. Kwanza wale jamaa wana allergy na kusoma. They just dont even read! Chinga waamushe hao wenzako waanze kutafuta maarifa katika maandishi!

Sasa tuwaonye akina Nungwi kuwa hapa hakuna nafasi ya longolongo, hoja zenye akili tu zinatakiwa. Sio blabla na propaganda ya kutetea mambo ambaye hayateteeki.

Nyongezea katika majibu ya kutumia pen names: Binadamu tunahlika wakati mwingine wa kuangalia 'nani amesema badala ya amesema nini'. Kwa hiyo tuliona ili to-focus kwenye hoja tukakubaliana tangu enzi za BCS kwamba tutumie pen names. Ila nakuhakikishia sio kwa sababu ya woga hata kidogo. Hatukuogopi maana mambo mengi humu ndani hatuzushi hata kidogo.

JJ: ni vizuri kwamba kuna kesi Dar kuhusu ubunge wa EAC. Lakini unajua kinachokosekana katika siasa za upinzani TZ na hasa katika CHADEMA ni militarism. We need millitant politics. Hii ya Zitto peke yake anapiga kelele wakati wengine wanaendelea na business as usual inaturudisha nyuma. Bado hatujawatia jambajamba CCM. Na ukiona CCM wanatusifia kuwa ni chama cha wastaraabu, ujue hatujafanya kazi yetu vizuri. Kuna mambo mengi ya ku-capitalise on. Inasikitisha kwamba wabunge wetu hawakulibebea bango suala la Richmond katika bunge lilipita. Hatuku-capitalise pia katika tatizo la wamachinga na wewe kama Mkurugenzi wa Vijana nafikiri hili linakuhusu moja kwa moja. In short, we must miliitarise our political party. Hawa jamaa ni mafia hasa, watatusogeza hadi uchaguzi watakuwa hawajafanya kitu lakini na sisi pia tutakuwa hatuna cha kuonesha kwamba wa are an alternative. Safari njema Dar.

Dk Kitila,umerudi chadema!!!1??????????? tafadhali nijibu au mwenye jibu anipe!
 
Mheshiwa Mbowe;

Ni kweli bandiko hili lilibandikwa kwa mara ya kwanza mwaka 2006, lakini mimi leo ndiyo natambua kuwa kumbe Mh. Mbowe ni mwana Forum katika forum hii.Na mimi nikupongeze kama ambavyo wenzangu wengi wamekupongeza na kama ulivyosema kama kuna jambo ambalo litahitaji kutolewa maelezo,basi usisite kuja kulitolea maelezo ikiwa kama njia ya kujadilana na kueleweshana.

Aidha kwa sasa Mh. Mbowe,unafahamu na tunafahamu wote kuwa Bunge la Katiba linaendelea na wewe kama sehemu ya wajumbe msiokubaliana na namna ambavyo wenzenu wa upande wa pili yaani CCM na wale 201 (wengi) walioteuliwa na Mwenyekiti wa CCM walivyouteka mchakato mzima,mmetoka ndani ya jengo hilo.Nadhani mmefanya vile kama njia ya kuupinga mchakato mzima,kwamba hautatoa Katiba ya Wananchi...well,mimi sina tatizo lakini nina mambo muhimu nataka kufahamu kutoka kwako

Kwanza kabisa,dakika hii niandikapo haya naangalia Bunge hilo "live" na nawaona hawa jamaa namna wanavyochangia na kiukweli wanasema wanakwenda kuipata katiba(iwe kwa mvua au jua)jambo ambalo ndilo limewapeleka hapo Dodoma pasipo uwepo wenu. Na kiukweli karibu wote wanaosimama na kuchangia ni waongo wa kiwango cha juu sana na nadhani hii ikiwa ni kama sehemu ya mkakati na propaganda ya kuwavuta ambao wanaowaunga mkono ninyi UKAWA, na ninyi hampo humo kutetea hoja zenu na huku nje uraiani kwa wananchi wenu tayari Jeshi la polisi na usalama wa Taifa wameshaagizwa kutowapa nafasi yoyote ya kuongea na wananchi,mmeshawekewa vikwazo. Na kuna mama mmoja kutoka Katavi,amesema anawakilisha walimu na kasema kuwa walimu wote wamemtumia text msg na simu yake imejaa txt msg hizo zikisema kuwa wao wanataka serikali mbili!!

Je, ni kweli hili linawezekana wakapitisha Rasimu ya mwisho pasipo uwepo wenu? Na wakitoka na Rasimu ya katiba ambayo ndiyo itakayokuja kwetu wananchi kwa ajili ya kupigiwa kura ya kukubaliwa au kukataliwa (kura ya maoni),mtahakikishaje kuwa Rasimu hiyo haipiti kwa sababu haikuwa shirikishi kama mnavyosema ninyi mnaotetea maoni ya wananchi?

Najua kabisa nafasi ya pekee kwa nyie mnaotetea "KATIBA YA WANANCHI" (jambo ambalo hata mimi nakubaliana na ninyi ) ni KURA YA MAONI. Vipi mmejiandaaje kukabiliana nao kwa sababu nguvu wanayoitumia humo bungeni ya kuhonga wajumbe wenye mawazo tofauti na wanounga mkono Rasimu ya Katiba kama ilivyoandaliwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba chini ya Jaji Joseph Warioba,kutisha wasiokubaliana na mawazo yao nk,nk ndiyo wakayoitumia kwa wananchi wapiga kura kwa kutumia usalama wa Taifa,polisi,Tume ya Uchaguzi na mfumo mzima wa serikali iliyo chini yao. Mmejiandaaje kukabiliana na hali hii kuzuia wananchi wasitekwe na fikra hizi za watawala kuwashawishi wananchi kuikubali Katiba ya watawala?
 
Guys,For God's sake.Tumetoa tahadhari hii ID ilipost karibia miaka 8 iliyopita na tulijadiliana sana hapa wengine muda huu wamebadili ID miongoni mwao my seniors nawajua ,hatusemi hapa.Someni Tarehe ambayo mtu alipost basi.Ah !
 
Guys,For God's sake.Tumetoa tahadhari hii ID ilipost karibia miaka 8 iliyopita na tulijadiliana sana hapa wengine muda huu wamebadili ID miongoni mwao my seniors nawajua ,hatusemi hapa.Someni Tarehe ambayo mtu alipost basi.Ah !



Kwahiyo wafanyeje?
 
Back
Top Bottom