The SGR War: Wakati Kenya wakisuasua, Uganda wameamua kujenga SGR. Hii ni fursa kwa SGR ya Tanzania. Is it viable? Tuichangamkie?

Atakuwa anazunguka na ule wimbo wa "Tanzania ni donor country" kichwani mwake.

Ahaaa ahaaa, halafu kuna watu walikuwa wanaamini hayo maneno ya kuwa sisi tutakuwa donor country, na waandishi kama kina Paskali walikuwa serious wanaandika hayo maneno kwenye notebook zao!
 
Acha kupotosha watu wewe dogo,mradi wa bomba la mafuta umechelewa sababu ya makubaliano kati ya Total na serikali ya uganda kuchukua muda mrefu. Kwani mafuta yameanza kuchimbwa huko Uganda?

Sisi tunanufaika bomba kupita hapa Tanzania ili mafuta yasafirishwe,sasa unaanza kuleta lawama hata mafuta hayajaanza kuchimbwa,unatakaka kusafirisha hewa?
 
Mbona inajulikana upo Tanzania. Ndio maana moja kwa moja watalii wanatua kIA ili kupanda mlima kilimanjaro.

Wakenya hawana akili hiyo ya kusema mlima Kilimanjaro uko Kenya. Wao wanasema fika Kenya uone mlima Kilimanjaro, na kweli ukiwa Kenya unaona mlima Kilimanjaro. Na ukitaka kupanda unapewa bei yake na protocol zake za kupandia huo mlima. Simple hivyo yaani.
 
Ile 2017 kule Chongoleani Tanga mpaka wakapatanishwa Ruge RIP na Makonda, hao wazungu wa Total walikuwepo, mbele ya marais Museveni na Magufuli tukaambiwa 2020 mradi utakuwa umekamilika. Sasa ww haya maelezo yako ya mfukoni unatoa wapi? Kama mafuta yalikuwa hayajaanza kuchimbwa, na makubaliano na Total yalikuwa bado, lile igizo pale Chongoleani lilikuwa la nini?
 
Hizi habari wadanganye wanaufipa unaowaongoza kama kamanda mkuu.

Watalii hawaji Tanzania kuona mlima kilimanjaro kama unavyofikilia zipo taratibu ambazo ni kupitia kwa mawakala wa utalii.
 
Mkuu tindo , kwanza nakiri mimi ni mywaji wa pombe, na huwa natembea sana na Joni Mtembezi alama nyeusi, uzuri wa Joni Mtembezi, hata ukilewa vipi, hauamki nazo, kwasababu, stimu yake haikai kwenye kimiminika kama bia hivyo kujaa tumboni, Joni Mtembezi ni vapour, stimu yake inaingia kwenye damu na ku evaporates kwa kupumua, hivyo unaamka fit na kusali misa ya kwanza.

Ni kweli SGR yetu kipande cha Dar-Moro kimechelewa kukamilika due to janga la Corona ambalo limeathiri kila kitu hadi upatikanaji wa fedha. Ile simu ya China, sio ilipigwa, tulipigiwa sisi!, na ombi la fedha za ku fund SGR sio ombi jipya, ni kukumbushia tuu kwasababu the original plan ilikuwa ni China kuifund SGR yote 100% kwa masharti ya kui oparates hadi deni lilipwe lote ndipo wakabidhi, na catchment area yake ilikuwa ni bandari ya Bagamoyo. Kwa vile kiukweli kabisa, sisi kama sisi, hatuna uwezo wa kuitandaza SGR Tanzania nzima, hivyo ile kanunu ya ili ule ni lazia uliwe, msije kushangaa mradi wa bandari ya Bagamoyo ukaendelea na Mchina akagharimia SGR yote iliyobakia nchi nzima.
P
 
Unaifahamu TANU kuwa baba kwa ccm sasa mtoto kurithi wewe unalialila nini humu
Bwahaaa bwahaaaa, nimecheka kwa nguvu, anayemiliki majengo ya urithi anampomcheka aliyepanga. Kwani mlipoanza mbwembwe na huo mradi wa SGR mlidhani ni kukaanga mayai?
 
Fuatilia mambo kwa ukaribu,wazungu wa Total walikuwepo Chongoleani,ila zilitokea sintofahamu ambazo zilisababisha kuchelewa kuchimba mafuta. Hivyo sisi kama Tanzania huwezi kulaumu eti mradi umecheleweshwa na serikali yetu.
 
Ni jambo jema!

Lakini sidhani kama tuna mashindano na Kenya mkuu Pascal!
Mweshimiwa kabisa , naomba uone mfano huu:

kuna kilo moja ya nyama wewe umekubali robo tatu mimi nikila nyama yote iliyobaki nitakuwa robo tuu.

Suala la ushindani katika uchumi ndio suala la kila siku kati ya nchi na nchi duniani. Ukizalisha bidhaa nyingi kuliko mwenzao ina maana mtagombea soko na mwenye kuzalisha kwa wingi ana uwezo mkubwa wa hata kushusha bei.

Kiuchumi anaye tawala sekta yeyote ile ndio mwenye sauti au mamlaka.
 
Tanzania SGR yenyewe inasuasua sasa hivi hawana pesa tena! Mwanza kwenyewe itafika lini? Magufuli ataondoka madarakani na kuiacha hata TABORA haitafika! I can bet for that!
 
Abiria pekee haiwezi kukupa faida kwenye SGR, na hata mizigo ikiwa michache bado ni tatizo kubwa, hasa wenzetu ambao pesa ya ujenzi yote ni mkopo. Unapo kopa unakuwa na tatizo zaidi: Unanyimwa uhuru kuweza kuendesha biashara nje ya makubaliano ya mkopo.
 

Nashukuru kwa maelezo yako ya hiyo John Walker.

Tuje kwenye huo upotoshaji wako wa kipande cha Dar-Moro. Unasema tatizo ni ugonjwa wa corona, huu ni uongo wa mchana kweupe, kipande cha Dar-Moro kilikuwa kiishe Nov 2019. Ugonjwa wa corona ulianza mwishoni mwa Dec 2019, hivyo bajeti ya kipande cha Dar-Moro hakina uhusiano wowote na janga la corona.

Rais wa China ndio apige simu kwetu akibembeleza nini labda? Hiyo ya China kufund hiyo project ya SGR ni makubaliano ambayo JK alikuwa kaingia na wachina, ila alipoingia Magufuli aligoma maana alisema mradi uko overestimated, hivyo akasema tutajenga kwa fedha zetu za ndani maana sisi ni matajiri. Mradi hawakupewa tena wakandarasi wa kichina, akapewa Mturuki. Tunaojua ukweli tulisema Tanzania haina fedha za ndani 10t za kujenga huo mradi, nyie wazalendo mkaamini, leo hii kipande tu cha Dar-Moro ndio inabidi uuongope kuwa sababu ni Corona. Kwa taarifa yako hapa tulipokwama, huo mradi wa Bagamoyo utaanza tena kwa masharti mabaya kuliko ilivyokuwa enzi za JK.

Nikushauri Paskali wakati mwingine kaa kimya tu, hivi hujajifunza kuwa ccm imejaa matapeli? Unakumbuka kabla ya Magufuli kuingia madarakani ule wimbo wa uchumi wa gas, unakumbuka zile data za profesa Muhongo? Leo yako wapi? Wakati tumeanza mambo ya porojo za uchumi wa gas tulianza na Mozambique hapo, leo Msumbiji wanaendelea na ujenzi ya gas plant ya $20b mradi mkubwa kuliko wa bandari ya Bagamoyo uliokuwa uwe wa $10b. Sisi sasa hivi tumeachana na umeme wa gas uliokuwa uzalishe 5,000MW, tumerudi kwenye umeme wa maji utakaozalisha 2,115MW kwa 6.5t! Je tungeweka tu 3t kwenye umeme wa gas ambapo bomba tayari liko hapa Dar na uzalishaji umeanza tusingepata hizo 2,115MW? Saa hii unaanzisha mada za kujichoresha za SGR wakati miaka mitatu 300km tu bado. Toka nje ya box kaka, hoji mambo ya msingi, haya mapambio hayakutoi.
 
Tanzania SGR yenyewe inasuasua sasa hivi hawana pesa tena! Mwanza kwenyewe itafika lini? Magufuli ataondoka madarakani na kuiacha hata TABORA haitafika! I can bet for that!
Unafahamu pesa tuliyokwisha lipa au ubwabwaja tu
 
We hujamuelewa Pascal umejipu kwa pupa anazungumzia mzigo.Hata huku Meter gauge ya TRC kwenda Arusha na Moshi imejaa mpaka Jan huko sembese SGR ya huko.
 
Fuatilia mambo kwa ukaribu,wazungu wa Total walikuwepo Chongoleani,ila zilitokea sintofahamu ambazo zilisababisha kuchelewa kuchimba mafuta. Hivyo sisi kama Tanzania huwezi kulaumu eti mradi umecheleweshwa na serikali yetu.

Kama mkataba wa mradi ulikuwa bado haujafikiwa, lile igizo la kuzindua mradi lilikuwa la nini pale Tanga mbele ya marais wawili, na hao wazungu wa Total? Serikali yetu haiwezi kuchelewesha chochote maana ilikuwa haitoia hata shilingi zaidi ya eneo la kijiografia kupitisha bomba. Japo kulikuwa na upotoshwaji wa wazi kuonyesha kuwa ni mkataba wa Tanzania na Uganda. Wakati ule tulikuwa tunasikia sifa za wazi zilizojaa propaganda kumsifu Magufuli kuwa ni sehemu ya mafanikio yake, tulisema wazi sifa zile ni za upotoshaji.
 
Mkuu tindo , kwanza hoja iliyo mezani ni SGR, bomba la mafuta ni something else, ila kwa vile mimi na Total ni dam dam, nitakuelimisha kidogo kuhusu kuchelewa kwa mradi huu, has nothing with us, mradi huu kwanza umechelewa na Uganda kwa kampuni ya Tullow kushindwa kuelewana na Total kuhusu mgawanyo wa mapato, hili limemalizika, Total imeinunua kampuni ya Tullow 100%, sasa mambo yanaendelea. Ila kitakachochelewesha mradi kuanza, ni kitu kinachoitwa "price elasticity of demand", wakati ule barrel la crude oil ilikuwa $ 60 sasa ni $ 16 per barrel, hivyo sasa wasoma trends wana soma kwa makini economic projections kama price itakuja ku stabilize in a near future, ndipo ujenzi uanze, vinginevyo kwa bei hiyo ya $ 16 per barrel, haiwezi kulipa gharama za extraction, treatment and transport, itakuwa ni hasara, hivyo the final ivestment decision bado haijasainiwa!.
P
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…