Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
THE STANDARD OF THE REASONABLE MAN’’ (KIWANGO CHA FIKRA YA MTU WA KAWAIDA): MJADALA WA UTEUZI WA MKURUGENZI WA TUME YA UCHAGUZI ZANZIBAR
Lord Denning wanasheria wanamjua sana kwa hukumu zake.
Lord Denning kamueleza ‘’Reasonable Man yaani, ‘’Mtu wa Kawaida,’’ ni mtu gani.
Lord Denning kamweleza kwa kiwango ambacho hakimpi shida mtu yeyote kumtambua mtu huyu ni nani.
Kiwango hiki cha utambuzi kinamweleza mtu huyu na mimi hapa nitaleta maelezo katika mazingira ya hapa kwetu kuwa, ‘’Mtu wa Kawaida,’’ ni yule mwananchi katika barza ya kahawa mtaani mahali kama Manzese Uzuri au Magomeni Makuti na kweninge mfano wa huo ambae kwa kuongeza kusema si msomi, la hasha, ni mtu wa kawaida tu pengine ana ubao wake sokoni anauza nazi au ana genge mtaani anauza nyanya.
Huyu ndiye ‘’Mtu wa Kawaida.’’
Unapotoa uamuzi kwa jambo lolote kupima uamuzi uko sawa au tenge tumia kiwango cha mwananchi huyu wa kawada kuamua.
Tumia ubongo wa mwananchi huyu mkazi wa barza ya kahawa kupima yote usomayo na kusikia katika mjadala wa uteuzi wa Mkurugenzi wa ZEC.
PICHA: Kulia ni Lord Denning.
Lord Denning
Lord Denning wanasheria wanamjua sana kwa hukumu zake.
Lord Denning kamueleza ‘’Reasonable Man yaani, ‘’Mtu wa Kawaida,’’ ni mtu gani.
Lord Denning kamweleza kwa kiwango ambacho hakimpi shida mtu yeyote kumtambua mtu huyu ni nani.
Kiwango hiki cha utambuzi kinamweleza mtu huyu na mimi hapa nitaleta maelezo katika mazingira ya hapa kwetu kuwa, ‘’Mtu wa Kawaida,’’ ni yule mwananchi katika barza ya kahawa mtaani mahali kama Manzese Uzuri au Magomeni Makuti na kweninge mfano wa huo ambae kwa kuongeza kusema si msomi, la hasha, ni mtu wa kawaida tu pengine ana ubao wake sokoni anauza nazi au ana genge mtaani anauza nyanya.
Huyu ndiye ‘’Mtu wa Kawaida.’’
Unapotoa uamuzi kwa jambo lolote kupima uamuzi uko sawa au tenge tumia kiwango cha mwananchi huyu wa kawada kuamua.
Tumia ubongo wa mwananchi huyu mkazi wa barza ya kahawa kupima yote usomayo na kusikia katika mjadala wa uteuzi wa Mkurugenzi wa ZEC.
PICHA: Kulia ni Lord Denning.
Lord Denning