The three musketeers

The three musketeers

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
''THE THREE MUSKETEERS''
Hiyo picha hapo chini nzuri sana muonekano wake.

Inawaonyesha viongozi wakiwa katika ukakamavu na fikra nzito.
Walikuwa wanafikiri nini?

Lakini linaloweza kumfikirisha mtu katika hii picha anaependa kuhangaisha kichwa chake ni historia za viongozi hawa.
Wanasema chini ya kila paa la nyumba kuna historia.

Hakika.
Kila picha ukiiangalia hutokosa cha kujifunza.

Picha hii inanikumbusha kitabu cha Alexandre Dumas, "The Three Musketeers."
Huyu Alexandre Dumas alikuwa Mfaransa mwandishi bingwa wa vitabu.

Kitabu chake kingine mashuhuri ni "The Count of Monte Cristo."
Ndani ya vitabu hivi kuna mengi yanayofanana na harakati za siasa kama zinavyochezwa Afrika.

Kuanguka na kunyanyuka.
Picha hii imenifikirisha kidogo asubuhi hii.

Lakini sifa zote zimwendee mpigaji wa picha hii.
Hii ni moja ya zile picha zinazokataa kufa.

Itatazamwa baada ya miaka 100 na mtazamaji atajiuliza, "Hawa walikuwa nani na nini historia yao?"

Itapendeza kama viongozi hawa wataandika tawasifu zao.

In Shaa Allah na ikiwa wataandika kila mmoja wao katika kitabu chake asikose kuweka picha hii.

Picha huzungumza maneno 1000.

May be an image of 3 people, people standing and outdoors
 
Hahahahah wewe Mzee mchochezi Sana eti Three Musketeers,
Nimekusoma vema Sana,hiyo team Moja Hatari Sana Katika chama Cha kijani
Wana mizizi mirefu Sana mithili ya mitende Kwenye Oasis za jangwa la Sahara!
😁😁😁😁
 
hiyo Picha ina watu wanne, hao watatu walikuwa ni kama wajinga, hapo ni kama wametekwa, wamejikuta wanaendelea kufanya kitu ambacho wameishajua wamekosea lakini hawawezi kuacha, hizo unazodhani ni nyuso za fikra, zilikuwa ni nyuso za majuto
 
Kinana alimshobokea Mwendazaka na kumfanyia kampeni ya kufa mtu mpaka akashinda,
Duh..lakini alivyo kuja kumtema kama takataka na kuleta genge lake ambalo sasa ndio linafyekelewa mbali... na trust me.... halitakaa lirudi tena maana ni walikuwa wakuja wote kwenye chama chao....
 
Kinana alimshobokea Mwendazaka na kumfanyia kampeni ya kufa mtu mpaka akashinda,
Duh..lakini alivyo kuja kumtema kama takataka na kuleta genge lake ambalo sasa ndio linafyekelewa mbali... na trust me.... halitakaa lirudi tena maana ni walikuwa wakuja wote kwenye chama chao....

Alitimiza wajibu wake kama GS,hakukuwa na shobo hapo.
Hii picha inaonyesha jinsi gani hawa Makomredi walijawa na Simanzi.
Baada ya kazi ya msingi ya kuhakikisha mgombea anashinda kwa namna yoyote kukamilika,ndipo taswira ya anguko lao ilipotanabahi dhahiri.
Wote walijua kuwa Chama kimeshaharibika,na wakosaji ni wao.

Pombe aliwaacha Uchi CCM wasijue la kumfanya,Idara ya Maadili na Usalama ya Chama ilifanya Blunder kubwa kumpitisha Mgonjwa wakijua wazi gharama ambayo Chama ingekwenda kulipa!
Ndani ya Miezi michache ya Utawala wa Rais Samia,Nchi imepumua.Propaganda za kumtukuza Pombe zilishika hatamu,Wananchi walikwisha ku Buy-in.Hofu ilitanda kubwa.
Mungu ni mwenye Kupenda haki,Pombe hakustahili kuongoza Taifa la watu waungwana kama sisi,Bora alivyomtwaa akaongoze askari wa Motoni.
 
Back
Top Bottom