Duh kweli Rweyemamu msanii, anashangaa nini sasa, anadhani kwa yeye kuwa na uhakika wa mshahara wake wa mwezi + marupurupu + ulinzi akiwa na sehemu nzuri ya kulala ndiyo kila mtanzania? a wapi na kwa wadanganyika wengine sivyo hivyo mambo ni tofauti can you immagine fedha hakuna za kununulia madawati lakini za kumfadhili TOSS kusimamia wizi wa kura Tarime zipo halafu eti Kurugenzi ya mawasiliano haijalisemea hili KUGUSWA TU kakutana na wanahabari, naamini hii ni rasharasha tu, mvua bado wajipange maana hali si nzuri kwa wananchi kama wanavyodhania wao.
Natoa hoja.
Unajuwa ukiwa raisi wa watu...Then movement yako ni rather from down up na si top down.
Halafu eti walisubiri kumwambia kuhusu mawe hadi alipofika huko anakokwenda.
Kwanini hawakumpigia simu? Ama alikuwa amelala ndani ya gari yake?
Sasa huko anakopita ni wananchi anatembelea ama miti?
Huyu Rais inakuwa vipi anafanya ziara kama Bush?
Ama hata Rais wa nje?
Kwasababu hizo haraka haraka ambazo wanazifanya kwenye ratiba yake ni kumwonyesha hali ambazo si halisi..Sasa waligunduwa anaweza kuona kwenye gazeti na angewauliza ni vipi hawakumwambia...MPENI REALITY..NA YEYE NI MUHIMU ATAFUTE REALITY KWA KUJUWA HALI HALISI YA WANANCHI HUKO MITAANI.....MAMBO NI MBAYA NA HUKU MAFISADI WANA MABILIONI WANAYAITA "VIJISENTI" NA HUKU KUKIWA NA RUMOURS KWAMBA WANAJITAPA KUWA WAO NDIYO WENYE NCHI.
Kwani JK hachungulii humu?
Kwanza alitakiwa alale hapo kijijini kwa mwananchi mmojawapo watakayemchaguwa ama popote penye ulinzi wa kutosha na si kusema mambo ya ratiba...Ratiba gani isiyokuwa ya kukutana na wapiga kura ziarani?
Nyie washauri wa JK mwelezeni ukweli na mumwonee huruma huyu mtu jamani.
Nilishawahi kusema huko nyuma urais wa Tanzania ni kazi ngumu..Wengine wanadhani ni urahisi..Mwalimu mwenyewe kama si mambo ya chama kimoja angekumbana na mengi tu...Na bado pia alikumbana na mambo mengi lakini usalama wa Taifa ulikuwa ni usalama wa chama tawala....Hivyo unawekwa kizuizini ukileta za kuleta....This is now a new era.
Watu hawajifunzi kutokana na historia...Hamkumbuki hata chini ya chama kimoja bado kulikuwa na vugu vugu la uasi na kupinduliwa kwa serikali?
Wakati huu wa vyama vingi wananchi ni wazi wataonyesha frustrations zao kwa namna nyingi ambazo hazijawahi kutokea chini ya fikra "Sahihi" za mwenyekiti wa chama chenye kushika hatamu