This is unacceptable for public view!


i agree with you qm! Too graphic
 
Sasa tatizo ni hiyo idea ya kuchinja au kuiweka kwenye gazeti?

Katika hii ishu tatizo ni kuweka kwenye gazeti.

Sina tatizo na wachinjaji, kwa sababu sina ushahidi wa mazingira ya uchinjaji huo.

Kama hatuna tatizo na idea ya kuchinja, na tunapenda nyama, kwa nini kujifaragua kwamba picha hii haifai kuwekwa kwenye gazeti?

Duh kupenda nyama na kuila sio tija inayotufanya tusijali haki za wanyama inakotoka hiyo nyama. Haki iko pale pale jamani. Kuweka picha ya mnyama yoyote yule akichinjwa kwenye vyombo vya habari kunavunjwa haki za mnyama huyo.

Well, inaweza kuwa utamaduni wetu hauna tatizo na ishu kama hii. Lakini hii haihalalishi kuwa utamaduni wetu huko right. I mean, sote twajua jinsi gani utamaduni wetu unavyohitaji makeover....!!

Akija rastafarian, au animal rightists tree hugger vegetarian akasema hivyo nitamuelewa kwa sababu ana principle za kutokula nyama na ukatili kwa wanyama, je wewe ni mmoja wao?

Niwe mmoja wao au la, bado ishu iko pale pale. Na wala hakuitaji rasta, vegeterian au animal activist kuona hili. Sisi ni sehemu ya wanyama, kwa hiyo ni lazima tuwajali. What happened to "A Golden Rule?"

Mimi nafikiri, kama unataka ku protest, the issue should be mbuzi anachinjwa, na sio picha ya mbuzi anachinjwa iko front page.

Hapana.

Kwa sababu sijui mazingira ya jinsi huyo alivyochinjwa, siwezi kupotest kwenye hiyo anga. Lakini kwa sababu nimeona picha ya uchinjwaji huo iko kwenye pubulic media, ninaweza kuprotest. You have it kinyumenyume.

Kama unakula nyama halafu hutaki ijulikane nyama inatoka wapi utakuwa unasimamia obscurity tu.

Hapana tena.

Suala sio kujulikana nyama inatoka wapi au ni ya mnyama gani. Suala ni jinsi gani huyo mnyama alikuwa treated wakati wa huandaaji (uchinjwaji) wake. Kwa mara nyingine tena, umekwenda rivasi.....
 

Kazi ipo kweli kweli.

Yaani kabisa haujaona kesi yangu iko wapi?


Somo,
Kesi yangu haipo kwenye a,b,c,d zote ulizo orodhesha hapo. Kesi yangu ipo kwenye jinsi public media ilivyoweka picha ya uchinjwaji wa huyo mnyama.

Tafadhali rudi nyuma ukasome tena, halafu tuendelee.....
 
 

I'm with you QM...hiyo picha inatisha, We know that we kill animals for food but we do not want to see the graphic details. Imagine kids seeing that picture, ina weza kuwa traumatize sana sana.

In order for binadamu kula lazima hawa wanyama wa chinjwe lakini in this age of enlightment, we prefer it to be humane and in private.

Has anyone here been to a kichijio, abbatoir? It is traumatizing. It's not something you can do over and over again.

The last kicks of a dying animal is not something you want to see...Uki muona mnyama aki tokwa na uhai wake, believe you me it stays with you (maybe sio panya lakini). Whether the animal is being slaughtered or being preyed (e.g simba on a swara) or even knocked down by a car.
 

Well, tukianza kuzungumzia uuaji wa viumbe hai, then itatubidi twende zaidi ya wanyama. Kwa sababu mimea nayo ni viumbe hai, lakini tunaichuma na kuila, tunaikanyaga, kuikata, n.k.

Kwa bahati mbaya au mzuri, wanyama tunaishi kwa kulana wenyewe kwa wenyewe. Sasa ingawaje sijui kwa uhakika dini zinasemaje kuhusu uuaji wa wanyama kwa ajili ya kitoeo, sheria zilizowekwa na mnyama wa aina ya homo-sapien ziko clear kuhusu uuaji wa wanyama wa aina hii.

Kwa hiyo kwa sheria zilizowekwa na bin-adam, generally kuua mnyama (ukiondoa bin-adam mwenyewe) kwa kusudio la mboga sio ukatili. Mipaka ipo kwenye ni jinsi gani unaua mnyama huyo.

Well, hiyo kasumba ya kwamba hizi sheria ni za Western World ni mufilisi. Kwa sababu kama unajali basi utazitii hizo sheria bila ya kujali huko katika pembe ipi ya Dunia.
 
huruma,

...heri mie mla-mboga!
 
Nyama ya mbuzi tamu, anavyochinjwa sina hamu.

Kama una sense na sensitivity ya kuwa ticked off na picha ya mbuzi anavyochinjwa, kitendo cha mbuzi kuchinjwa hakikuumizi fikira?

Kama unaona mbuzi anafaa kupewa haki kwa nini usimpe haki yote? Ya kutochinjwa?

Na kama unaweza kumnyima haki ya kutochinjwa, kwa nini utake kumpa haki ya kutodhalilishwa?
 
Jamaa wanasubiria nyama kwa hamu lakini hata hawaangalii mazingira walipomchinjia huyo mbuzi. Jamani USAFI si suala kusomea digrii au diploma, is just common sense.
 
je ukiona kule machinjio ya Dodoma? Mnyama kabla hajafa tayari anachunwa ngozi!! Tusiwe over-sensitive...
 
Mlalamikaji ajue kuwa chanzo ni yeye mwenyewe kumla mbuzi; kitendo cha kula mnyama ndio violence kubwa kuliko zote; yote hayo ni kwa sababu ya binadamu kula mbuzi ( mnyama mwenzi); yaani samaki wakubwa kula samaki wadogo; sasa ktk tukio hilo tegemea violence; hayupo mnyama anayependa kukatishwa maisha; na ndio maana hupiga makelele sanan na hatujui hata sala ambazo wanatusalia kwake Muumba wao; ila i know huwa wanapeleka case kwa muumba wao; ITV wako sawa maana hiyo ndio hali halisi; binadamu tunakula wanyama wenzetu; ni hatari lazima iwekwe hadharani otherwise itakuwa sawa na kuficha ufisadi kwa sababu ulifanyika kwa uficho
 

Una maaana ya Geophrey au nani.Hata hivyo usichanganye destuli za USA na bongo,ingekuwa hivyo basi hata hapa bongo pia ingekuwa halali juma kumuoa hamis
 
Nyie mnaodai haki za mbuzi sijui wanyama sitowashangaa siku moja mkiwavisha suruali au sketi kufinya nanihii zao.Si mnajifanya mko ughaibuni wanakowaachia mbwa au paka siti ya mbele ya abiria ya gari.Shauri yenu
 
Ukiongelea haki ya wanyama unataka kusema mbuzi mwingine itatokea ataona hiyo picha ahaaaaaaaaaaaa.Ama tatizo ni nini?
Tell me this is a joke ! Kama kuitafuta IPP media ktk hivi vita vya sasa tutafute ktk mambo sio vijimambo.
Mimi nitakuunga mkono ukisema kuwa picha hiyo kwa watu wengine itakuwa ni tatizo kuona damu,ndio maana wanaeka tahadhari kwa watu wenye Obsessive-compulsive disorder (OCD) ama mwenye phobia ya kitu ambacho wanaenda kuonyesha kwenye Public Tv.Sasa sijuhi wanaweza kuwekaje kwenye still picture.
 
Hapa hatujafikia kuwa sensitive kiasi hicho, mbuzi tu. Uvunjaji wa haki za binadamu, mifugo, n.k. Basi haikupaswa kamwe kuweka/kuonyesha picha picha ya albino aliyenyofolewa viungo/kukatwa mikono. Acha mambo ya wanyama kwanza maliza tatizo la albino.
 


Animal cruelty, we have along way to go;


...Hivi, kuna anayekumbuka miaka ile, mahakamani Mtwara, mbwa alihukumiwa adhabu ya kifo kwa kosa la kuitwa IMMIGRATION?

alinyongwa/alipigwa risasi?




...vitoweo vingine bora tu uvikute mezani vishaungwa mchuzi, ...kutwa nzima anazunguka nao hivyo hao kuku, halafu eti jamaa anacheka! 🙁
 
Duuh kweli siyo sahihi,mauaji sio ya binaadamu tu bali hata kwa mbuzi,kondoo,ng'ombe etc
Please katika dunia hii ya haki za msingi kwa kila kiishimo humo NI MAKOSA TENA YA JINAI kuonyesha picha kama hiyo.
 

Violations of animal rights?! For a pet (an animal kept as a companion) au unazugumzia wanyama wote kwa ujumla? Pili hizo animal right ni kwa bongo au dunia nzima? Hivi Tanzania kuna makundi yanayotetea haki za wanyama?
Mkuu nisaidie katika hili tafadhali.
 
Unajua,wanadamu tumeshindwa kabisa kusimamia nafasi yetu tuliyopewa na Mungu,haya ndiyo matatizo.Badala yake sasa tunafuata mafundisho ya mashetani.Mawazo kwamba mnyama naye anaweza kuwa na haki ni mawazo ya mashetani kabisa ,"whether you like it or not."Kwamba sasa mnyama naye awe na haki kama mwanadamu!Mnyama hana haki yeyote.Mungu ametupa wanyama wa kila aina ili wawe chakula chetu.Sasa "how you prepare does not really matter." Nia hasa ya mafundisho hayo ni kumdhalilisha mwanadama,kumfananisha na mnyama.Kama uko makini na matukio mengi ya sasa utagundua kwamba, karibu yote yana nia moja tu, kumdhalilisha mwanadamu,kwa njia moja au nyingine ili aonekane kwamba si kitu kabisa.Angalia taabu anazosababishiwa mwanadamu tena kwa makusudi kabisa,Congo DRC,Dafur,Afghanistan,Uganda(LRA),Iraq,Zimbabwe na India hivi karibuni na mengi yaliyopita na ambayo nina hakika yanakuja.Unajua, mashetani yameshakuwa "condemed" na Mungu.Sasa yana tuonea wivu.Kwa hiyo yanatumia wanadamu wajinga wasiomjua Mungu kwa kuwadanganya kwa mbinu mbali mbali hasa za kupata fedha na mafanikio katika maisha ili kutesa wenzao.Simamia na kutetea haki za wanadamu wanaoteseka sehemu mbalimbali duniani bwana sio wanyama.Hapo nitakuona wamaana,lakini wanyama,sikuelewi.Mungu anachukizwa na mawazo hayo,epuka!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…