This is why all mama mean nothing to some people!

This is why all mama mean nothing to some people!

mkuu pole sana

najua unaumia sana lakini amini kunavitu hutokea kwa watu usichotegemea kutendwa na binadamu yoyote .. ila nakuomba sana endelea kumheshimu na umpe heshima yake kama mzazi
 
Kokutona,i dont have family,also hii haijaniathiri lolote,so nitakua mzazi na baba mwema sana kwa wanangu!

Great to hear that. Uwe baba mwema kwa wanao, na mume mwema pia kwa mkeo, ili akupende pia na akutunzie wanao vema. Kuavoid ya mama yako yasijekurudia.
I can feel you have great heart. Jipe mda wa kuheal the pain uliyonayo.
 
W of S,ninachema mimi pia ni mtazamo wangu pia,pia sio sahihi kwa watoto kujua kwamba wazazi wanagombana kwani inaathiri watoto,but ugomvi unapowakumba watoto hapo ndo unapokuwa ishu,maoni au mtazamo wangu sio "msaafu" unaweza ukakosolewa,cha msingi unakosolewa namna gani.Na kama mkosoaji atatumia vigezo hafifu nitamjulisha.Yes maisha ndivyo yalivyo that's why we are here now!
 
Eiyer,ninachosema ni kua kuna mambo watu wanapitia kwenye mahusiano wasiyomuambia yeyote! Ni kama baba yenu ambavyo nae haongei ubaya wa mama hata kama upo. Wanawake wangapi humu baba zao hawajui chembe ya struggles zao? Japo mama yako angejaribu kuwa na mahusiano nanyi walau baba yake angeona. Msamehe, ukiwa baba mwema bila kuwa mume mwema unaweza kurudia historia ya baba yako. Kinyongo ulicho nacho kwa mama kitakufanya usimpe raha mkeo na kumfanya hata akukimbie. Kumsamehe mama kutakuweka huru.
King'asti my dear,faham hakuna matatizo aliyokua anayapata kwa baba,babu mzaa mama ndo shahidi,hata kama mfano yalikuwepo hata kututafuta?Hata kutujulia hali?Baba hakuwahi kumkataza hata mara chache alizokuja wakati mwingine aliletwa na baba!
 
Usijali Kokutona,kwanza siwezi kubadili yaliyopita,so lazima nijifunze kupitia hayo ili nijekua mwanadamu mwema kwa wengine!
 
King'asti my dear,faham hakuna matatizo aliyokua anayapata kwa baba,babu mzaa mama ndo shahidi,hata kama mfano yalikuwepo hata kututafuta?Hata kutujulia hali?Baba hakuwahi kumkataza hata mara chache alizokuja wakati mwingine aliletwa na baba!
Pole sana.

Mimi nakubaliana na wewe kuwa kuna wamama wana roho za kikatili sana siku hizi, haijalishi mume kamtenda kwa kiasi gani, kama mama ana ugomvi na baba hapo watoto wanahusika vipi? Sijawahi ona mwanamke anakimbia watoto, nijuavyo mimi wengi huwa wanaendelea kubaki kwenye ndoa zenye mateso ukimuuliza atakwambia navumilia kwasababu ya wanangu/mwanangu. Yakimshinda sana atakimbia na wanae/mwanae...


Muulize vizuri huyo mama yako labda ana sababu za msingi zilizopelekea yeye kuwakimbia...


Mimi ukiniuliza nani kama mama ntakujibu hakuna manake nimelelewa na mama pekee baada ya baba kufariki (rip baba). Kwako wewe hakuna kama baba manake hukuwahi kushuhudia/kupata malezi ya mama yako.


Huu msemo wa nani kama mama kadri siku zinavyoenda unazidi kupoteza maana. Kuwa mama sio kubeba mimba na kuzaa jamani, nani kama mama ni pamoja na malezi na upendo tunaowapa hao watoto wetu.

Sio mtu uzae utelekeze watoto/mtoto afu uje hapa useme nani kama mama!
 
Babu Aspirin usijali nitafuata mfano wa baba,nitakua baba mwema sana kwa wanangu!!
Hili ndilo neno la Mungu. Wathibitishie kina mama kuwa hata sisi wanaume tunaweza kulea.

Nani kama BABA?
 
King'asti,najua maana ya kusamehe,nimeshamsamehe,yamepita,wala simchukii,sina kinyongo chochote nae,sitaweza kumtendea baya yoyote nitakae muoa kwani sikulelewa hivyo na baba,nataraji nitakaemuoa atakua na furaha sana!
 
Sweetlady,sidhani kama ni muhimu kuyatafuta yaliyopita,cha kuangalia ni kua tunajifunza nini kupitia hayo!
 
Pole sana,naomba unielewe sikulazimishi kunielewa nikiwa kama mwanamke kumbuka kua MAMA ni mama tu na hakuna atakae chukua nafasi yake
hujui nini kilimsibu mpaka akatoweka siamini kama aliwaacha bila sababu ya msingi,au jaribu kukanae chini umulize kila suali linalokukera ndani ya moyo wako lazima atakua na sababu, kuto kuja kwenye msiba wa Mzee wako pia hakumfanyi wewe umchukie sababu walisha achana juuyakua alikua mzazi mwenzie,na usisahau labda alikua na majukumu najua una uchungu kulelewa na mzazi mmoja wakati mama yuko hai niamani atakua na sababu yakufanya alio yafanya nenda kamuone Mama kaanae chini muongea am sure mtayamaliza kwa salama na amani.

Hakuna sababu yoyote ya msingi ya kumfanya mama atoweke na kuacha wanae bila hata kuwa anaenda kuwaona mpaka alazimishwe. Kuna wanawake ni wajinga sana wakishaolewa basi akili zao zote zinahamia kwa hao wapenzi/waume zao wala hawajali watoto waliowaacha eti madai yao wanatafuta furaha, unaacha kuwafurahisha watoto uliowaleta duniani wewe mwenyewe eti unafurahisha mtoto wa mwanamke mwingine kha!

Ukishamleta mtoto duniani lazima uhakikishe unamlea vyema kwani kuzaa huwa hakulazimishwi unaamua mwenyewe.

Aisee,

Situation yako imenitia huzuni kwa kiasi fulani. But kumbuka hakuna kama Mama are you sure huyo unayemwita Baba yako (RIP) alikuwa ni Baba yako kabisa siongei kwa ubaya tafadhali nielewe. But mama huwezi singiziwa hata kidogo, unajua kuna kitu hutokea usimlaumu sana mama yako hujui ni kwa sababu gani walitengana na baba yako na nini kilimtia hasira kiasi hicho. Mpaka akawa anawachukia watoto wake but acha nikwambie ukweli hata kama unasema hataki kuwaona but ukweli uko pale pale mama hapo alipo huwa anasikia uchungu na kuwakumbuka watoto wake asikwambie mtu bana. "UCHUNGU WA MWANA AUJUAE MZAZI"

Kha dena uchungu gani alionao huyu mama? hapana bana huyu hakustahili kuitwa mama asee tabu zote hizi za mimba halafu uzae mtoto umtelekeze?

Kweli nimeamini unamchukia mama yako, japo ulisema humchukii.

Kumchukia mama wa hivi ni haki yake kabisa
 
Hili ndilo neno la Mungu. Wathibitishie kina mama kuwa hata sisi wanaume tunaweza kulea.

Nani kama BABA?
Asprin itafika mahali nani kama mama itapoteza maana, watu wamezoea kutamka tu kwa kufuata mkumbo.


Nani kama mama haina maana kwa mtu ambaye mama amemtelekeza bila malezi, haijalishi alibeba ujauzito kwa miezi tisa. Hivyo hivyo nani kama baba haina maana kwa mtu ambaye hajayapata malezi ya baba yake...


Mimi naamini malezi aliyoyapata mtu kwa hao wazazi wawili ndiyo yatampelekea aamue nani kama mama/baba.
 
Kweli babu ODM hakuna kama Baba!Huo ndo ukweli mchungu ambao kuna watu hawautaki!
 
Maty,thanx,sometime ukweli lazima usemwe,uwe mchungu au la,utasemwa tu!
 
Kweli babu ODM hakuna kama Baba!Huo ndo ukweli mchungu ambao kuna watu hawautaki!
Ni kweli kabisa kwa upande wako..je vipi na waliokimbiwa na baba zao? Wakalelewa na mama tu?
 
Sweelady,na wao nao ni hivyohivyo hakuna tofauti hapo.Adhabu ni ileile!
 
Ok sweetlady,upendeleo hakuna.Madhara ni yaleyale!
 
Hi natumai mu wazima!Hey plz woman don't get angry with me!Natumia mimi mwenyewe kama mfano;Nilizaliwa pamoja na ndugu zangu wawili hivyo tukawa wa3,wakati tukio linatokea mimi ndo nilikuwa mdogo kuliko wengine,mama yetu alitutelekeza jioni na kwenda kuolewa na mwanaume mwingine,wakati huo my Late father(may his soul rest in peace)alikua amesafiri kikazi,toka siku hiyo sikumwona mama mpaka nilipotimiza umri wa miaka 13,tuliishi na baba bila ya baba kuoa coz hakutaka mapema tuteseke,mama alipokuja alituona kwa dakika chache tena kwa kulazimishwa na baba,Alipoondoka sikumwona mpaka nilipotimiza miaka 25 alipolazimishwa na marehem babu(apumzike kwa amani)ambae ni baba yake,tulikuja kuonana tena hosptl wakati babu anaumwa na hapo ni baada ya miaka mi3,mara ya mwisho nilimuona mwaka jana nilipoamua kwenda kumwona,kumbuka kwenye msiba wa baba hakuja,to be hornest with u,i don't feel anything for her!Pia sijui umuhimu wake,wala sijui mapenzi ya mama.Napenda nieleweke kua simchukii,najua yeye ni mama yangu,alinizaa na alininyoshesha,lakini haza ni majukumu yake!Hajawahi kunishawishi kwa njia yoyote kuwa yeye ni mama!Sasa kama huyu aliesikia uchungu kwaajili yangu yupo hivi,nitaona vipi umuhimu wa akina mama?Je kama mimi tupo wangapi?JE NI NANI KAMA BABA,I LOVE HIM MUCH,I WISH HE COULD BE HERE!

Pole sana na umenikumbusha machungu
Hata mimi yalinikuta,mama aliona ndoa yake ni vyema zaidi kuliko mimi aliyenizaa nje ya ndoa.....Hakuthamini kuwa nilimwitaji wala hakujali uchungu aliyonipa kwa vitendo vyake.Nilipata upendo kutoka kwa baba wa kambo kuliko hata kwake.Alitugawa kwenye mafungu nami nilibaki pekeyangu coz ckuwa mtoto wa ndoa ile.kupokea vichapo na matusi ya hapa na pale hata yaliyo juu ya umri wangu.Ilibidi ndugu zake wanichukue na kunilea.
Hakutaka kunieleza baba yangu ni nani akidai kuwa amefariki na hafahamu ndugu zake.
Mimi ni mdada lakini for sure miaka michache iliyopita nilikuwa namchukia sana mama yangu....But baada ya kugundua kuwa atleast saffering alizonipa zimenifanya niwe mchakalikaji wa kujitafutia life{not dependat} nikapata nafasi ya kumpatia nafasi yake tena maishani mwangu.
For the life she is in she real needs me now more than ever and I am glad to help her.
Think twice na umsamehe Mama yako
 
Back
Top Bottom